Wabongo mkija majuu au ughaibuni acheni unafiki, majungu na ukora mnaliabisha Taifa lenu

Wabongo mkija majuu au ughaibuni acheni unafiki, majungu na ukora mnaliabisha Taifa lenu

Mkuu habebeki kivipi?
Mambo mengine madogomadogo ni ya kueleweshana tu, kuna watu wana ndoto za kwenda nje lakini wanakosa abc's za namna ya kufanya ili waje huko. So ni jambo la kujitoa hasa nje ya hapo unaweza kuwaona watu hawako serious.

Mfano kuna mtu ana ndoto ya kwenda kufanya kazi nje lakini hajui huko wanahitaji watu wa fani gani, skilled au unskilled n.k. Wengine hawajui hata kutofautisha passport na visa, wengine hata uhamiaji hawajawahi kusogea. Kwa hiyo nyie mliopo nje endeleeni kuwapa madini vijana wanaotaka kutoka nje kusaka fursa nzuri zaidi
Sasa mtu unamuuliza umsaidie vipi, anakuambia wewe muongo huwezi kusaidia.

Huyo mtu utamuweka katika kundi gani zaidi ya kundi la watu wasiobebeka?

Hawa watu wengine wanapenda kulalamika kuwa hawajapewa nafasi ya kusafiri kuliko wanavyopenda hiyo hiyo safari yenyewe.
 
Ila wabongo wanachomana sana. Wanawapigia hadi polisi na migration kukuchongea eti urudishwe.

Halafu kuna katabia na hulka flani ka umaskini wabongo wanayo hadi mton. Msosi mtoni siyo big deal lakini eti wanashindana kujaza friji msosi na kuringishiana unabaki kushangaa tu Wtf!
Mimi ndo maana sitaki kujuana na wabongo,mimi salaam tu basi.
 
Sasa unauliza swali halafu hutaki jibu.

Wewe ushajiwekea negative thinking kwa hiyo husaidiki.

Badala ya kutaka kujua hao wawili ilikuwaje, nimewezaje kuwasaidia, unaniita muongo.

Hata kama nilikuwa na nia ya kukusaidia, unaondoa nia hiyo.

Wewe mwenyewe una negative mentality, ndiyo maana nikasema hubebeki.

Yani wewe mwenyewe huna mentality ya kuweza, hivyo ni vigumu mtu mwingine kukusaidia.
Aliyekwambia nina negativity nani?

Mimi nataka nifike Marekani na nataka wewe Kiranga unisaidie.


Ishu ni kufika huko tu mambo mengine utaniachia mimi.

Haya twende kazi
 
Aliyekwambia nina negativity nani?

Mimi nataka nifike Marekani na nataka wewe Kiranga unisaidie.


Ishu ni kufika huko tu mambo mengine utaniachia mimi.

Haya twende kazi
Kaka kufika Marekani ni ndoto ya kila mtu anayetaka kwenda huko lakini vigezo, exposure n.k vinatofautiana kati ya mtu na mtu, so unaweza kumueleza anayetaka kukusaidia qualifications zako mfano elimu, ujuzi ulionao, documents ulizonanzo mpaka sasa i.e passport, covid 19 vaccine certificate na kiwango cha pesa ulichonacho hapo atajua ukifika kule ni kwa namna gani utamudu gharama za maisha au akubebe. Kwa kuyajua hayo yeye sasa ataweza kupima namna gani atakusaidia kukamilisha vigezo vingine kama visa au kuangalia fursa gani huko alipo itakufaa na ukifika huko utaishi vipi, yote atayajua baada ya kumwambia.

Muhimu mwenye shida awe chini aeleze nia yake na vigezo vyake then unayemuomba atajua namna ya kufix mambo ili ufanikiwe kwenda huko alipo.
 
Kaka kufika Marekani ni ndoto ya kila mtu anayetaka kwenda huko lakini vigezo, exposure n.k vinatofautiana kati ya mtu na mtu, so unaweza kumueleza anayetaka kukusaidia qualifications zako mfano elimu, ujuzi ulionao, documents ulizonanzo mpaka sasa i.e passport, covid 19 vaccine certificate na kiwango cha pesa ulichonacho hapo atajua ukifika kule ni kwa namna gani utamudu gharama za maisha au akubebe. Kwa kuyajua hayo yeye sasa ataweza kupima namna gani atakusaidia kukamilisha vigezo vyote au kuangalia fursa gani huko alipo itakufaa.

Muhimu mwenye shida awe chini aeleze nia yake na vigezo vyake then unayemuomba atajua namna ya kufix mambo ili ufanikiwe kwenda huko alipo.
Mkuu mimi elimu yangu ni form six ingawaje nilifeli.Nina leseni ya udereva class C hivyo kwenye suala la udereva niko vizuri.

Kuhusu passport ninayo,hiyo kadi ya chanjo ya covid pia ninayo,cheti ya chanjo ya homa ya manjano ninayo.

Kuhusu pesa siwezi kosa milioni 10.Hivyo ni yeye tu kunifanyia mpango niweze kufika huko
 
Kusema ukweli wabongo nje ya nchi ni wanafki sana na hawapendi kuona mwenzao anaexcel especially uwe umewakuta, ushauri ukifika ughaibuni ni mara millioni uishi na watu West Africa kuliko waswahili watakuchoma, hata demu usichukue mbogo
 
Aliyekwambia nina negativity nani?

Mimi nataka nifike Marekani na nataka wewe Kiranga unisaidie.


Ishu ni kufika huko tu mambo mengine utaniachia mimi.

Haya twende kazi
Wewe ni sawa na yule mtu aliyeota ndoto.

Halafu akaenda kwa mtafsiri wa ndoto, akitaka atafsiriwe ndoto yake.

Mtafsiri wa ndoto akamuuliza, sawa, niambie ndoto yako nikutafsirie.

Badala ya kumwambia mtafsiri wa ndoto ndoto yako akutafsirie, unampa kazi ya ziada, unamwambia mtafsiri wa ndoto kwanza akuambie umeota nini, halafu aitafsiri hiyo ndoto.

Nakupa kanuni muhimu ya kusaidiwa.

Msaidie anayetaka kukusaidia, fanya kazi yake ya kukusaidia iwe rahisi, usimuongezee mzigo wa kufanya kazi ya ziada ya kutafuta akusaidiaje. Nenda kuomba msaada ukiwa unajua unataka kusaidiwa wapi.

Juzi nilikuwa katika kikao na Profesa mmoja Mtanzania yuko US anatoa michongo ya scholarship. Tuna network ya kusaidia wanafunzi kuja kusoma US.

Alisema kitu kimoja ambacho hapendi ni mtu kuja kumwambia anataka scholarship, bila detail.

That is too general, too vague.

Alisema anataka mtu amwambie kasoma nini, kafanya mitihani gani, kakwama wapi, anahitaji msaada wapi, yani mtu fulani ambaye yeye mwenyewe kashaonesha initiative, anajua anataka kufanya nini, anahitaji msaada kufika anapotaka kufika.

Sasa, hata tukiondoa mambo ya scholarships na usomi, wewe hujaonesha initiative, uko too vague, too general, yani, hata kwa mtu ambaye hana qualification yoyote, akiniambia hivyo anakuwa kanisaidia kujua anaingia kwenye michongo gani. Kuna safari zinafanywa na watu wenye uzito mkubwa Tanzania unaweza kupata.

Tatizo wewe hata initiative ya kuniambia una kipi, au huna kipi, hujafanya.

Unakuwa kama wale wanafunzi ambao huyo rafiki yangu profesa amesema hapendi kuwasikia, wanaosema "nitafutie scholarship" tu, bila detail.

Kwa mentality hii unaweza kufika Marekani ukatamani kurudi Tanzania tu. Marekani ni nchi inayotaka specificity.
 
ata wew mwenywe ni wale wale tuu unatuletea hapa JF ili iweje badala uje utupe michngo tuje kuchukua hela unaleta nyuzi za hovyo.
 
Kaka kufika Marekani ni ndoto ya kila mtu anayetaka kwenda huko lakini vigezo, exposure n.k vinatofautiana kati ya mtu na mtu, so unaweza kumueleza anayetaka kukusaidia qualifications zako mfano elimu, ujuzi ulionao, documents ulizonanzo mpaka sasa i.e passport, covid 19 vaccine certificate na kiwango cha pesa ulichonacho hapo atajua ukifika kule ni kwa namna gani utamudu gharama za maisha au akubebe. Kwa kuyajua hayo yeye sasa ataweza kupima namna gani atakusaidia kukamilisha vigezo vingine kama visa au kuangalia fursa gani huko alipo itakufaa na ukifika huko utaishi vipi, yote atayajua baada ya kumwambia.

Muhimu mwenye shida awe chini aeleze nia yake na vigezo vyake then unayemuomba atajua namna ya kufix mambo ili ufanikiwe kwenda huko alipo.
Huyo mburula kama kashindwa kuelewa jambo dogo tu hilo, atabaki kulialia tu, wakati watu wanamuacha hapohapo.

Huyu ana uvivu wa tabia ndani kabisa katika fikra, Marekani haitaki wahamiaji wa aina yake.
 
Back
Top Bottom