Wabongo wengi wanaoishi Marekani wana maisha magumu tofauti na wale wanaoishi nchi za Scandinavian

Wabongo wengi wanaoishi Marekani wana maisha magumu tofauti na wale wanaoishi nchi za Scandinavian

Ukihitaji salamu nenda pwani kwa waswahili,kwangu utaambulia chuya ukalishie kuku!

Bado sijafahamu ni kwanini watanzania wengi wanaoishi nchi za Marekani,Canada na Uk huwa wanamaisha magumu kupita kiasi tofauti kabisa na wale wanaoishi nchi za Scandinavian na Germany!.

Ninawafahamu jamaa kadhaa wanaoishi huko tangu zamani na hakuna walichofanya cha maana kwenye familia zao(Wazazi) hapa Tanzania,wengi huwa wanarudishwa kipindi cha matatizo tu lakini huwezi kuwaona wakiwa wanarudi kipindi cha furaha kuwasalimia ndugu zao.

Watanzania wengi wanaoishi nchi za Scandinavian huwa wamerekebisha makazi ya wazazi wao na pia huwa wamejenga nyumba za kifahari ili wanapokuwa wanakuja likizo basi hufikia huko,siyo nyumba tu bali huwa na usafiri mzuri!.

Hii ni tofauti kabisa na wabongo wanaoishi Marekani,Canada na UK,hawa huwa wanarudi makwao endapo Baba au Mama ni mgonjwa au amefariki kabisa,na huwa wakija hata vaa yao inatia mashaka!.

Huwa wanapenda kuvaa miwani mikubwa kama wachomelea welding na kujifanya kuishangaa Tanzania kana kwamba ni chooni!,Unakuta hata hela ya kuwatoa marafiki zake tu Out hawana zaidi ya kujiongelesha blah blah na masifa kibao!.Wengi wamechoka kimuonekano,Sura hazina nuru na mionekano yao imefubaa!.

Ukiwauliza wanabaki kusingizia Marekani Kodi ni kubwa na Ishu za Bills zinabana kila kona,Unabaki kumshangaa kana kwamba huko Marekani ni yeye tu ndiye Bills hupewa kubwa!.

Wabongo wengi wanaoishi Marekani na Canada waliofanikiwa huwa ni kuanzia Umri wa Miaka 50 - na Kuendelea,hawa ndiyo angalau huwa wamejenga makwao na hata hujitahidi kuprovide kwenye familia zao.

Ila hawa wenzangu na mie kuanzia miaka 25 - 45 huwa hawana cha maana zaidi ya blah blah na ngonjera kibao huku kila muda wakipiga simu na kusimanga serikali na kuwakashifu ndugu kana kwamba wanaishi kwenye vyoo!.


Wengine tunawafahamu wamekwenda huko miaka ya 90 lakini hadi leo ni kuzurura tu hawana paper!.

Any way:

Ukitaka kuona walivyo na hasira,wewe soma comments!
Kwanza wanalala Nje na kwenye vistoo ndio maana pamoja na kukaa huko USA Bado wako busy humu jf wanatamani kurudi.

Hao hao eti nao Huwa wanaenda kuwasikiliza kina Lisu,Mbowe na watu dizaini yao eti wanahutubiwa mambo ya maisha mazuri 😁😁😁😁
 
Mkuu kuna mmoja juzi katoka Marekani ni mshikaji wetu kitaani yaani jamaa kachoka utadhani alikuwa gerezani,Amefika kuona nina drive Bima(BMW) anabaki kunishangaa na kunipa masifa kibao!

hiki ndo kimefanya nimeandika uzi!
Bongo supu kuku wa buku 5 ni supu hasa,hao wa huko full mabroila harafu bei mbaya 🤣🤣
 
Hakuna sehemu yenye maisha rahisi. Narudia tena hakuna sehemu rahisi yenye maisha rahisi... Labda ubaki Bongo uwe chawa wa mama Samia ila ujue nako kuna ugumu wake. Inabidi uwe mpiga kelele kweli kweli na ujitoe akili zako.
Urahisi wa Maisha Cha kwanza ni chakula na pili nyumba.

Sasa Kwa hizo parameta 2 kipi Bora uende huko ukateseke urudi zero au ubakie bongo uwe na uhakika wa vyote?

Utapata nyumba au Ardhi huko Marekani? Eti unaenda kutafuta harafu 3/4 ya kipato kinaishia kwenye Kuendesha maisha huo si utaahira Sasa.
 
Lazima nikudharau mkuu kwasababu pamoja na kuwa nje lakini hadi Maisha nakuzidi!🤣
Usipopata maisha Afrika,huko kwingine ni Mtihani maana gharama za maisha ziko Juu.

Leo hii Lita ya mafuta ya gari ni nafuu Tanzania kuliko Nchi nyingi za Ulaya.
 
Mkuu hilo nalifahamu lakini kwa hali ya Marekani ni nchi iliyoendelea tulitegemea angalau wawe na maisha ya kuridhisha!
Kitu Kimoja watu hamfahamu ni kwamba gharama za maisha zinaendana na Maendelea,Nchi inavyozidi kuendelea na gharama za maisha zinapanda,hili ndio la msingi.
 
Umeshawahi kufika huko? Siyo kila mtu ana maisha ya kuridhisha. Na siyo kila anayeishi nchi yenye maisha mazuri naye anakuwa na maisha mazuri. Mawazo yako ni kama yale ya wazee wa vijijini wanaodhani kila mtu aliye jijini Dar ana maisha mazuri.
Ndio ukweli huu
 
Tv kubwa nchi 65 .Umenichekesha.Mimi nikajua labda una kiwanda hata cha kutengeneza vifungashio na umeajiri watu 30.Sasa TV nayo ya kulingia jamani.
Hao Jamaa ndio wabebela mabangi siku akina Mbowe au Lisu wakienda huko unategemea mtu anaejitambua na ana maisha atakuja kubeba bango eti anahutubiwa na Mbowe? Mpaka hapo unajua kabisa hao ni chokambaya wabangaizaji tuu 😁😁

Ndio maana wale wengine wanakomaa na Urais pacha huko waliko hakuna maisha 😂😂

Mwisho bongo hapa sio pa kuhama ,Ukiwa na mil.5 unapata Ardhiaekari ya kutosha.
 
Hongera. Hili la watu kujaribu kuishi maisha ya ''watu watasemaje'' ndiyo linafanya wengi wajikunyate. Halafu wengi naona wanaandika wakiwa na inferiority complex ya kujiuona wanyonge kwa watu waliwahi kuishi majuu. Nimekumbuka kijijini miaka hiyo. Kila ikifika Xmass wakati vijana wengi wanarudi likizo vijijini kulikuwa kunatokea ugomvi kati ya vijana wa kijijini na vijana wa mjini. Kisa ni vijana wa kijijini walikuwa wanadhani wanadharauliwa na vijana wa mjini. Na kejeli za ''karudi amechakaa'' zilikuwa haziishi kusemwa na vijana wa vijijini.
Hakuna Cha inferiority bwana kama huna huna tuu,Sasa wewe unaishi ughaibuni watu wanayarajia ulikimbia Hali ngumu Bongo unarudi huna tofauti na wao Sasa Kwa nini wasikuzodoe hata kama maisha ni Yako?
 
Hao Jamaa ndio wabebela mabangi siku akina Mbowe au Lisu wakienda huko unategemea mtu anaejitambua na ana maisha atakuja kubeba bango eti anahutubiwa na Mbowe? Mpaka hapo unajua kabisa hao ni chokambaya wabangaizaji tuu 😁😁

Ndio maana wale wengine wanakomaa na Urais pacha huko waliko hakuna maisha 😂😂

Mwisho bongo hapa sio pa kuhama ,Ukiwa na mil.5 unapata Ardhiaekari ya kutosha.
Mipango imegoma nini ya kufika ulipopataka ??...hii ukandiaji ni wa chuki 🤣
 
Pana vitu mnachanganya sana Nchi zilizoendelea zina fursa kuliko Nchi zetu kwa hiyo kuwa huko sio kigezo cha wewe kuendelea kama haujitumi na hujui umefata nini huko kupata mafanikio au Mtaji Nchi za Ulaya ni rahisi kuliko Nchi zetu labda ushikwe Mkono lakini Nchi zilizoendelea unaweza kujipa malengo ufanye nini baada ya muda fulani kuferi kwa baadhi ya watoto wa Mama isiwe case study ya mnachoongea maana wengi ya wanaojituma huko wapo vizuri sana na pia kwa kuwa hawatoi password kirahisi ndio maana wengi wanafurahi kudhani inawezekana asilimia kubwa wapo choka mbaya kumbe sio kweli...
Huu ujinga ndio Huwa naukataa,Nchi hizo ziko very exhausted kwenye Kila nyanja ya uchumi.

Afrika ndio Kuna fursa ingawa Changamoto ya Afrika ni mtaji na sio fursa.Binafsi uniambie nichague kazi Ulaya na Afrika nachagua Afrika
 
Mipango imegoma nini ya kufika ulipopataka ??...hii ukandiaji ni wa chuki 🤣
Kufika wapi ambako mipango imegoma? Mimi huko kwenu ntakuja kutalii mambo ikikaa sawa sio kuishi ,siwezi ishi sehemu ambayo Kila mtu ana habari zake no social cohesion kama ya Bongo.

Kiufupi sijawahi tamani kuishi Nje ya Nchi ila natamani kufika kuona kulivyo.
 
Napenda sana asili yangu na nchi yangu ila kama unajua maana ya maisha mazuri Tanzania wanayaishi viongozi tu tena wale wa ngazi za juu.
Wewe una matatizo,maisha Yako ya Daraja 3 Kwa Kila Nchi ,Sasa ukifika Marekani utaishia Daraja lipi? Hata Tanzania hapa wapo wa Maisha ya Juu,ya kati na chini kama kwingine Sasa unaposena viongozi tuu ndio wanaishi maisha mazuri kisa viongozi sio kweli,hao viongozi ni wachache kuliko wengine.

Kinachonikera hapa Tanzania ni kwamba Ukiwa na vihela Ili uwe salama inatakiwa uwe Chana tawala hata kama hutaki hii ndio kero kubwa Sasa kiasi kwamba huna uhuru wa Mali Yako.
 
Napenda sana asili yangu na nchi yangu ila kama unajua maana ya maisha mazuri Tanzania wanayaishi viongozi tu tena wale wa ngazi za juu.
Wewe una matatizo,maisha Yako ya Daraja 3 Kwa Kila Nchi ,Sasa ukifika Marekani utaishia Daraja lipi? Hata Tanzania hapa wapo wa Maisha ya Juu,ya kati na chini kama kwingine Sasa unaposena viongozi
Itapendeza zaidi HUENDA ikakuongezea kitu vile ufkiriavyo au kupunguza yale ufkiriayo/tofauti.
Nimefika Nchi za Africa kadhaa ila Nje ya Nchi Bado na Africa yote Kwa sehemu kubwa inafanana.

Huko Ulaya nk nakuona kwenye picha,video nk na pia nasoma Hali ya maisha, biashara na Uchumi lakini siwezi kutamani.kuishi huko ila kufika na ntafika before 2030 nikiwa mzima.

Nitapata exposure na experience Mpya ila siwezi tamani kuishi Kwa sababu tayari ntakuwa nimejiwekeza Afrika.
 
Back
Top Bottom