Wabunge 19 Viti Maalum CHADEMA wafungua kesi. Bunge lasema linasubiri uamuzi wa Mahakama Kuu

Rahaaa mustarehee
 
Nchi ya ajabu Sana hii [emoji1787][emoji1787] Kuna Uzi kule jukwaa la GT kuhusu Bunge la Ndugai Na Huyu Dr kutoka dump university Kuna mdau alisema hakuta kuwa tofauti Kati ya Bunge la Ndugai na huyu Dr wa dump university.
Hao wote wana remote, spika hawezi kufanya tofauti na raisi anavyotaka.
 
Maadam jambo hili limefika mahakamani, ngoja mahakama itoe maamuzi ya mwisho wasije kusema wameonewa.

It is the last kicks of a dying horse.
Bado hamjaelewa tu mchezo ulivyo
Unajua kwa nn Spika amekimbilia kusema Hilo suala lipo mahakamani? Wanajua hadi kesi kuja kusikilizwa ni 2025
 
Sasa mawakili kaaeni mkao wa kuuwa nyoka
 
Na Msajili wa Vyama vya Siasa apitie Katiba za Vyama vya siasa nchini anone kama zina vipengele vinavyo nyima haki wanachama wao kama hicho cha CDM kinachosema, Mwanachama akikishitaki chama mahakamani kajifuta uanachama, avifanyie kazi vifutwe.
 
Ukiwahibmahakamani basi mambo yote yanasimama. Rejea kesi ya Zitto Kabwe alipofukuzwa na Chadema. Kesi ilikaa miaka miwili hadi bunge linavunjws na yeye kupata haki zake zote kama mbungr mstaafu! Hata hii inaweza kuunguruma miaka mitatu hadi 2025.

Ndio nchi ilivyo Hadi mahakama wanashiriki uonevu kisa Ni Chadema.
 
CHADEMA inaweza kufungua kesi dhidi ya wabunge 19 waliowafukuza kwenye chama chao kwamba hawawatambui, wasijitambulishe, wasitambuliwe na wasiitwe wanachama au wabunge wa CHADEMA.

Hiyo ndio kesi pekee CHADEMA wanayoweza kufungua mahakamani uamuzi ukatolewa ndani ya muda mfupi na kuna uwezekano mkubwa wa kushinda. Kesi nyingine yoyote inayohusu kutaka wabunge hao waondolewe bungeni itamalizika 2025.
 
Yaani kisheria, hata kama watakuwa wamefungua Kesi mahakamani, inabidi wake nje ya Bunge, Hadi pale shauri hilo litakapoamuliwa
Unapaswa kujua tu kuwa hao wabunge bado wanahitajika huko.
Hiyo kesi yenyewe kuja kuisha 2025.
Wangekuwa hawaitajiki wangeshaondolewa faster tu, kama spika tu aliondolewa faster tu kwa hao Wala isingeshindikana
 
Safi sana. Waende mahakamani wakashindane huko. Chadema ni chama kinachohubiri Sana HAKI na umuhimu wa kuzingatia Sheria katika maamuzi. Sasa ni Wakati wao kuishi Imani yao hiyo. Waache kulia Lia Kama last born, wakapambane Mahakamani.
 
Hii nchi ilibidi wakoloni waendelee kutawala angalau hadi mwaka 2050 pengine tungeweza kujitawala mambo madogo kama haya yanatutia aibu sana. Ndiyo maana watu wakipata upenye wanapiga hela tu vile wanajua nchi hii ni bora liende.
 

Hili Jambo lilitakiwa kufanywa mwanzoni.
 
Hii ilijulikana wazi. Mihimili ya nchi inashindana kwa ujinga. Muhimili huu ukipanda kwenye level za ujinga mwingine unapambana kufanya ujinga mkubwa zaidi
Hao kina mdee bado wanahitajika huko, wangekuwa hawaitajiki ni faster tu wangetolewa. Ndugai mwenyewe faster tu alitoleea, Sasa ndio ije kushindikana hawa kina mdee
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…