Wabunge wa Kagera wapinga Mkoa wao kumegwa na kupelekwa Chato

Wabunge wa Kagera wapinga Mkoa wao kumegwa na kupelekwa Chato

Kama Samia anahamu ya kumuenzi Magufuli kwa kuwapa mkoa "watu wake" anaweza kufanya kitu kimoja simpo

Aubadili jina mkoa wa Geita auite Chato, kisha aifanye chato kuwa ndo makao makuu ya huo mkoa wa Chato

Kagera aiache hivyohivyo, asiguse kabisa mkoa huo adhimu
Hujui hata kulikua na mkoa unaitwa West Lake Region (Mkoa wa Ziwa Magharibi)na ndio ukamegwa ukazaa Kagera na wilaya za Misenyi na Kyerwa zimejimegua Humo humo Kagera leo unabetua Midomo hamtaki kumegwa mmkea akina nani nyie.

Ukimega au kumegewa jua kuna siku utamegwaaaa tu Utake Usitake Upende Usipende. Ni hayo tu.

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Kama Samia anahamu ya kumuenzi Magufuli kwa kuwapa mkoa "watu wake" anaweza kufanya kitu kimoja simpo

Aubadili jina mkoa wa Geita auite Chato, kisha aifanye chato kuwa ndo makao makuu ya huo mkoa wa Chato

Kagera aiache hivyohivyo, asiguse kabisa mkoa huo adhimu
Na huo ndiyo ukweli, Chato iliendelezwa kwa maandalizi ya kuwa makao makuu ya "mkoa" na sasa wanataka kutimiza ahadi ya JPM aliyosema yule mzee msibani Chato. Kama Chato ipo juu kimaendeleo kwa Geita mjini ni vema rais akabadili makao makuu ya mkoa wa Geita yakawa Chato ili adhima ya wana Chato itimie.
 
Kama Chato wanataka mkoa wapeni bila kumega hata robo heka ya ardhi Kagera.

Magufuli alikuwa mkabila yaani alikaa chini na ndg zake wakapanga kumega mkoa Kagera utadhani mali yao binafsi!!! Alianza zamani kufanya hujuma zake akapewa wilaya ya Chato iliyomegwa kutoka Kagera na sasa wanataka wamege wilaya nyingine eti wapate hadhi ya mkoa.

Tutawaadabisha wote watakaojichanganya, tuko tayari kwa lolote, ukabila mmeuanzisha nasi tutamalizia liwalo na liwe.
Sikuzote unapoanzishwa mkoa lazima kuna sehemu fulan ya mikoa jiran itamegwa, kataeni kwenye vikao vyenu rasmi kuhusu jambo ilo Samia hatomega ila mkikubali huko alafu mkasema Samia akatae mtakuwa wanafiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko juu kuliko Geita ? Umefika Geita lini ? Pole sana. Usiwe unalinganisha mji wa Geita na hicho kijiji cha Chato. Chato hata hiyo Katoro haoni ndani
Na huo ndiyo ukweli, Chato iliendelezwa kwa maandalizi ya kuwa makao makuu ya "mkoa" na sasa wanataka kutimiza ahadi ya JPM aliyosema yule mzee msibani Chato. Kama Chato ipo juu kimaendeleo kwa Geita mjini ni vema rais akabadili makao makuu ya mkoa wa Geita yakawa Chato ili adhima ya wana Chato itimie.
 
Haya ni madhara ya ubinafsi na udikteta. Kama sio kupeleka mamiradi makubwa nani angehangaika na kuunda mkoa
 
Nimesema "kama" Chato ipo juu ya Geita, sijasema ipo juu. Lakini msingi wa hoja ni hao waliopanga kuiendeleza Chato ili baadaye watengeneze mkoa na kuifanya Chato makao makuu. Nia ilikuwa ya kibinafsi zaidi kuliko uhalisia. Tazama jinsi walivyojitoa Kagera kwa sababu za mtu binafsi na sasa wakaamua kutengeneza mkoa kwa sababu za mtu huyohuyo binafsi. Tazama majengo makubwa yametangulia kujengwa kabla ya kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kwanza, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa pasipo kuwa na shughuli za kupeleka ndege huko, na hiyo ni mifano michache ya hasara za uamuzi wa mtu mmoja.
 
Nimesema "kama" Chato ipo juu ya Geita, sijasema ipo juu. Lakini msingi wa hoja ni hao waliopanga kuiendeleza Chato ili baadaye watengeneze mkoa na kuifanya Chato makao makuu. Nia ilikuwa ya kibinafsi zaidi kuliko uhalisia. Tazama jinsi walivyojitoa Kagera kwa sababu za mtu binafsi na sasa wakaamua kutengeneza mkoa kwa sababu za mtu huyohuyo binafsi. Tazama majengo makubwa yametangulia kujengwa kabla ya kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kwanza, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa pasipo kuwa na shughuli za kupeleka ndege huko, na hiyo ni mifano michache ya hasara za uamuzi wa mtu mmoja.
Kabisa ndg yangu,unajengaje uwanja chato unaacha O'mukajunguti ambao unatakiwa uwe wa Africa mashariki lkn akajenga Kwa pembeni ya mwanza airport! Wenyeji wa Mushasha O'mukajunguti walishakatazwa mda mlefu wasifanye shughuli yoyote ya aridhi pale,inatia hasila na majonzi
 
Hata wapinge hadi asubuhi, atakayeamua mkoa wao umegwe ama uachwe na Chato iwe mkoa ama ibakie ilivyo ni Rais wa nchi, hizi zingine ni pre justification tu.
 
Hilo ndio tatizo. Hakuna namna njia pekee ni Mkuu wa nchi kuidhisha ili Chato iwe mkoa
Nimesema "kama" Chato ipo juu ya Geita, sijasema ipo juu. Lakini msingi wa hoja ni hao waliopanga kuiendeleza Chato ili baadaye watengeneze mkoa na kuifanya Chato makao makuu. Nia ilikuwa ya kibinafsi zaidi kuliko uhalisia. Tazama jinsi walivyojitoa Kagera kwa sababu za mtu binafsi na sasa wakaamua kutengeneza mkoa kwa sababu za mtu huyohuyo binafsi. Tazama majengo makubwa yametangulia kujengwa kabla ya kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kwanza, ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa pasipo kuwa na shughuli za kupeleka ndege huko, na hiyo ni mifano michache ya hasara za uamuzi wa mtu mmoja.
 
Sisi tulio vijijini tunaamini maendeleo yetu yapo kwenye Kata, kijiji na kitongoji.
Mahitaji yetu wilayani ni kidogo sana.

2020 vitongoji viliungwa na kufanya kitongoji kuwa kikubwa zaidi.
Kuna sehemu vitongoji vitatu viliungwa kuwa kitongoji.kimoja.
Iwapo nia ni kusogeza huduma kwa mwananchi, hapa ziisogezwa?

Baadhi ya vitongoji hivyo wakati huu haiwezekani kufanya mkutano mmoja kwa kitongoji.kizima.
Inabidi kufanya mikutano miwili hadi mitatu.
Mfano ni kitongoji cha Rwenjojo katika.kata ya Ihanda wilaya ya Karagwe au kitongoji cha Kigando kwenye kata ya Kasulo wilayani Ngara.
Mifano.ipo mingi.

Serikali haina gharama za moja kwa moja za uendeshaji wa kitongoji lakini ina gharama za uendeshaji wa wilaya na mkoa.
Tena gharama kubwa.

Naipongeza.sana.serikali.kwa kuwapa pikipiki watendaji wa.kata, maafisaelimu kata na wataalamu wa.kilimo.
Hii ina tija kubwa kwa wananchi kuliko kuunda wilaya au mkoa.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Wabunge wa Mkoa wa Kagera, Wamepinga kitendo cha kuendelea kuumega Mkoa wa Kagera. Hii imekuja baada ya Kuanzishwa Mchakato wa kufanya Wilaya ya Chato iliyopo Geita kuwa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule, alisema Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Geita (RCC) ilipendekeza wilaya tano, Chato na Bukombe mkoani Geita. Biharamulo na Ngara mkoani Kagera na sehemu ya Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma zichukuliwe kwa ajili ya kuanzisha Mkoa mpya wa Chato.

Kwa mujibu wa takwimu za sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa Wilaya ya Chato ilihesabiwa kuwa 365,127. Chato ilianzishwa mwaka 2007 kutokana na maeneo ya Wilaya ya Biharamulo, Mkoa wa Kagera, mwaka 2012 ikasogezwa katika mkoa mpya wa Geita.

Pia soma:

1). Madiwani Buchosa wakubali kuhamia Geita ili kutoa fursa kuanzishwa mkoa mpya wa Chato

2). Kuunda Mkoa wa Chato ni kupoteza historia ya Wahaya, Mkoa wa Chato hauna maslahi kwa urithi wa utamaduni wa Mtanzania

3). Prof. Tibaijuka: Chato haina sifa kuwa Mkoa

4). Kwanini Chato iwe Mkoa kutoka kwenye Mkoa mchanga wa Geita ulioundwa 2012?

5). Geita yakubali kuundwa Mkoa wa Chato; Kakonko, Biharamulo na Ngara kumegwa. Sengerema kwenda Geita..

6). Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato

7)). Rais Samia Suluhu: Mkikidhi vigezo, Chato tutaifanya kuwa Mkoa

8). Rais Samia anaweza kuanzisha mkoa mpya wa Chato endapo haya yatazingatiwa…

HOJA YA WABUNGE KUPINGA KUMEGA MKOA WA KAGERA.

1. UTANGULIZI
Sisi wabunge wa Mkoa wa Kagera kupitia Wilaya ya Muleba na Wilaya ya Bukoba Vijiiini, Mhe Charles John Mwijage wa Jimbo la Muleba Kasikazini, Mhe. Dkt, Oscar Ishengoma Kikoyo wa Jimbo Ia Muleba Kusini, na Mhe. Dkt. Jasson Samson Rweikiza tumepokea wito wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera cha tarehe 29/10/2021 tukiwa tayari tumerudi Dodoma kwa ajili ya vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge. barua za wito wa Kikao, zimeambatishwa na agenda za RCC. Agenda namba 4 ya kikao tajwa inahusu mapendekezo ya Wilaya za Biharamulo na Ngara kupelekwa mkoa pendekezwa wa Chato.

Hoja ya kuumeumega mkoa wa Kagera, inatualika kujadili faida na hasara zake kwa mkoa wa Kagera kwa kuzingatia masuala ya kijamii, kisiasa na kiuchumu. Tukiongozwa na uzalendo wetu kwa mkoa wa Kagera na utaifa wetu kwa taifa letu, kwa hali yoyote ile, pendekezo la kumega mkoa wa Kagera lina athari kubwa sana kuliko faida kwa usitawi wa Mkoa wa Kagera kihistoria, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Kwa sababu hizo, na nyingine zitakazo tolewa hapa chini, hatukubaliani na hoja ya kuumega mkoa wa Kagera.

2. CHIMBUKO LA MKOA MPYA WA CHATO
Chimbuko la kuomba mkoa wa chato halina mashiko kisiasa, kiuchumi wala kisheria. Chimbuko la mkoa wa chato linatokana na muombolezaji mmoja aitwaye Bigambo wakati wa msiba wa Hayati Magufuli. Mwombolezaji huyo alidai kusikia Hayati Magufuli akitaka Chato uwe mkoa jambo ambalo halina uthibitisho wowote kisiasa. Vigezo vya kuunda mkoa mpya hutokana na mkoa mama kutokana na ukubwa wake na/au jiografia yake kuomba kumegwa i1i kusogeza huduma kwa watu wake.

Kwa ombi hili ni tofauti sana, Wilaya ndogo na changa ya Chato iliyoanzishwa mwaka 2005 inaornba kuwa mkoa ili maeneo mengine yamegwe kuisadia kutimiza adhima yake ya kuwa mkoa jambo ambalo ni kinyume na dhana na falsafa ya uundwaji wa mikoa katika historia ya taifa hili lililoasisiwa na viongozi wetu mahiri. Geita mkoa mama, nao ni mchanga ulioanzishwa mwezi Machi mwaka 2012 ukimegwa kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kagera.

Pamoja na uchanga wake, Geita ni moja ya mikoa midogo ikiwa na kilomita za rnraba 20,054. Ukichukua ukubwa wa rniina wa Geita (20,054Km2) na Kagera (35,686Km2) kwa pamoja haifikii ukubwa wa Mkoa wa Tabora wenye ukubwa wa kilomita za mraba 76,150 au Morogoro wenye ukubwa wa kilomita za mraba 70,624. Ipo mikoa mikubwa na mikongwe iliyostahili kuleta ornbi kama hili, slyo wilaya ya Chato wala mkoa wa Geita. Kwa ukumbwa wa mkoa wa Kagera na/au Geita kuenendelea kuumega, mikoa ya Kagera na Geita itakuwa mkoa mdogo sana.

3. FAIDA
Kwa tathmini za kiuchumi, kijamii na kisiasa na kwa kuangalia jiografia ya mkoa wa Kagera kwa sasa na wilaya zinazolengwa kupelekwa hakuna faida yoyote kwa mkoa wa Kagera inayoweza kushawishi wananchi wa Mkoa wa Kagera kuridhia whlya za Biharamulo na Ngara kupelekwa mkoa pendekezwa.

4. ATHARI
Kwa kutumia vigezo vilivyotajwa hapo juu, athari kwa mkoa wa Kagera bila wilaya zake hizo mbili na kwa taifa zima la Tanzania ni kubwa sana.

4.1 KIJAMII:
(i) Mkoa wa Kagera ni muunganiko na mshikamano wilaya sabwa (7) za utawata zenye halmashauri nane. Pamoja na kuwa na wananchi wanaoweza kuhesabika kuwa makabila yanayojionyesha manne na koo nyingi sana, mapito ya mkoa huu katika historia ya kuwepo kwake yanaufanya mkoa huu kuwa jamii iliyoshikamana na imara kijamii, kisiasa na kiuchurni. Mkoa wa Kagera kwa kupakana na kuwa karibu na nchi nyingi umekuwa ukifikiwa na wageni wengi wa aina mbali mbali lakini wakati wote wana-Kagera walijiona wamoja na katika umoja huo wameweza kuhimiti matokeo yote hasi yaliyoletwa na wageni hao.

(ii) Kwa kuomba kuondoa wilaya za Ngara na Biharamulo kutasababisha mgawanyiko katika jamii na kufufua tofauti za kikabila na kikanda na koo zilizokwisha zikwa kwa siku nyingi za uhai wa mkoa huu. Pamoja na sababu nyingine, hii inatokana na ukweli kuwa wananchi wa Wilaya tano zinazobaki hawakukubaliana na hawatafurahia wilaya za Biharamulo na Nsciwa kumegwa.

(iii) Kwa taifa kuna athari kubwa za kijamii, kisiasa na kiusalama kwani mpangilio wa Wilaya tatu (3) zinazopendekezwa kuunda mkoa pendekezwa, zinawingi wa watu wenye nasaba na ushawishi wa mataifa ya jirani ambayo hayajatulia kiusalama. Mshikamano wa mkoa wa Kagera uliojengeka kwa muda mrefu uliweza kudhibiti na kumaliza nguvu athari hiyo.

4.2 KIJIOGRAFIA:
(i) Kuondoa wilaya za Biharamulo na Ngara kuna itenga Kagera inayobaki na kuinyima nafasi ya "location advantage" ya mipaka ya Kabanga na Rusumo. Ustawi wa Mkoa wa Ziwa Magharibi u;itokana na hiyo "location advantage". Katika zama hizi ambazo biashara kati ya mkoa wa Kagera na nchi jirani unaendetea kukua na kuimarika, kuzimega wilaya hizo kutaunyima mkoa wa Kagera fursa hizo za kibiashara.

(ii) Mgawanyo au kumegwa huku kunapunguza eneo la mkoa wa Kagera. Mkoa wa Kagera una ukubwa wa eneo la mraba 35,686 (KM2 35,686) ikijumuisha nchi kavu na eneo la maji ya ziwa victoria. Eneo la maji ni kilomita za mraba 10,173 na eneo la nchi kavu ni kilomita za mraba 25,513. Wilaya ya Biharamulo na Ngara ambazo ni maeneo ya nchi kavu ni kilomita za mraba 9,371. Hivyo, kumega wilaya hizo mbili, Mkoa wa Kagera utakuwa umebaki na kilomita za mraba 16,142 zinazofaa kwa kilimo utalii. ikumbukwe, Kagera si mkoa
unaotawaliwa na shughuli za huduma (Service industry) hali ambayo eneo dogo linaweza kuwa na watu wengi na shughuli nyingi za kiuchunii zinazohalalisha uwepo wa eneo la kiutawala kiasi cha mkoa. Huu ni mkoa wa wakulima, wafugaji na wavuvi hivyo kupunguza eneo Iake ni kuudhohofisha kijamii, kihistoria na kiuchumi.

(iii) Katika uhai wa mkoa huu na hasa rniaka 15 mpaka leo tumepigana sana kuwa karibu k\Ara kujenga miundombinu ya barabara. Kwa kazi inayoendelea kwenye ujenzi wa barabara mzunguko wa ndani kwa ndani kwenye mkoa itakuwa si tatizo. Kimsingi suluhisho si kumega wilaya bali kujenga na kuboresha miundombinu ya barabara, reli, afya, na uchumi.

4.3 KISIASA:
(i) Kagera bila Ngara na Biharamulo kisiasa siyo Kagera tunayoiona leo. Kufikia hatua hii ya kuwa na jamii tulivu na inayoelewana yenye mshikamano na mtazamo wa kimaendeleo haikuwa kazi rahisi, Wapo watu walihangaika kwa adhi na nyadhifa mbali mbali nao kwa kutambua mchango wao kwa Kagera si busara kuumega kila uchao.

(ii) Siasa ya Kagera ni zaidi ya mtazamo wa chama cha siasa na chama au vyama vingine. Tunazungumuza siasa kama hali au mtazamo wa jamii iliyoshuhudia na kuhimili kuanguka kwa uchumi baada ya kuvunjwa Chama cha Ushirika (BCU), Kuanguka kwa bei ya kahawa, jamii iliy()!itangulia taifa katika Vita dhidi ya Nduli ldd Amin Dada, jamii iliyopokea wimbi la wakimbizi toka nchi jirani, lakini pia jamii ambayo ilikuwa ya kwanza kupigwa na janga hatari la ukimwi.

Pia jamii hii iliyokumbwa na tetemeko kubwa la ardhi lililoaribu miundombinu na mali za watu, jamii ambayo wajasiliamali wake wengi na raia wengine walizama kwenye Mv Bukoba, ugonjwa wa Mnyauko wa r-nigomba kwa kutaja baadhi tu. Kimsingi, tafakari ya mapigo haya yaliyopata Kagera, Serikali inapaswa kuja na Mpango Maalum wa Kuikarabati Kagera (Special Economic Rehabilitation Program) ili ipone kwa ujumla wake na si kuumega vipande vipande kama inavyokusudiwa.

(iii) Athari nyingine kisiasa ni kufanya n-)aamuzi ya kumega mkoa kwa kufuata kilio cha mwombolezaji wa mkoa mwingine Bwana Bigambo alikuwa anaomboleza kama watanzania wote walivyoumia na kila mtu kusema lake kabla ya kutulizwa

View attachment 1997936View attachment 1997937View attachment 1997938View attachment 1997939View attachment 1997940View attachment 1997941
1

Kumega mega mikoa sio solution ya kuleta MAENDELEO.
Ila uwajibikaji +uzalendo ndio vitaleta maendeleo
 
kumega mega mikoa sijui wilaya ilikuwa upuuzi wa malaika wa chattle maana fikra zake zilikuwa kama za jibwa tu, akili ndogo nguvu nyingi
 
Back
Top Bottom