Wabunge wanne - Anthony Komu, Joseph Selasini, David Silinde na Wilfred Lwakatare wafutwa uanachama wa CHADEMA

Wabunge wanne - Anthony Komu, Joseph Selasini, David Silinde na Wilfred Lwakatare wafutwa uanachama wa CHADEMA

Hawa lazima wataendelea kuwa wabunge kupitia Mahakama,
Lazima watakwenda Mahakamani kupinga , mahakama itawasikiliza , itapigwa danadana hadi bunge linavunjwa
Shida ya Chadema siyo kuwaondoa bungeni bali kuwachafulia CV zao......bunge limebakiza wiki mbili tu!
 
https://millardayo.com/wabunge-wanne-chadema-watimuliwa-wametoa-kashafa-kwa-chama-video/#respond

maxresdefault-2-3-660x400.jpg


Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetanganza kuwafukuza uanachama Mbunge wa Rombo Joseph Selasini na Mbunge wa Moshi Vijijini Anthony Komu kwa kuwa wamepoteza sifa ya kuwa wanachama wa chama hicho.

“Kamati Kuu CHADEMA imeazimia Wabunge Anthony Komu na Joseph Selasini pamoja na kuwa wamejipotezea sifa ya uanachama wa CHADEMA, wameendelea kutoka kauli za kejeli, kashfa na kukiuka maagizo ya Chama, hivyo Chama kimeazimia kuwafukuza uanachama” -John Mnyika, Katibu Mkuu CHADEMA

“Mbunge David Silinde na Wilfred Rwakatare sio tu wamekiuka agizo la Chama bali wamekuwa wakijitokeza kwenye vyombo vya habari kutoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya maagizo ya Chama na Viongozi wa Chama, Kamati Kuu CHADEMA imefikia uamuzi wa kuwafuta uanachama”- MNYIKA

“Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Mariamu Msabaha, ameshiriki kukiuka maagizo ya Chama, ilitakiwa awe mfano na kwakuwa amekwenda kinyume, amevuliwa nafasi zake zote ndani ya Chama na kubaki na Ubunge na atatakiwa ajieleze kwanini asichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo”-MNYIKA

“Kuhusu Wabunge wengine ambao wamekwena kinyume na maagizo ya Chama lakini hawajaonesha utovu wa nidhamu kwa kutoa kashfa kwa Chama, watatakiwa wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo” -MNYIKA
Safi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kauli yako ina maana gani kwetu sisi watanzania Maana tunaongozwa na CCM hii hiii unayosema kuishabikia ni utaahira...wakati ndiyo iliyounda Serikali.
Hujamwelewa wala huhitaji kutoa povu. Yaani yeye anamaanisha usishabikie vyote viwili, chagua kimojawapo! Hana tatizo na mtu ambaye ana kimojawapo kati ya hivyo viwili; yeye ana tatizo na walioshika vyote viwili
 
Kabla ya 2015 CHADEMA ilikuwa taasisi ya umma ambayo ilikuwa inahamasisha umma mpaka CCM ikafikia kujivua magamba. Lakini katikati ya 2015 CHADEMA iligeuka kuwa kampuni ya mtu binafsi ikiwa na lengo la kutimiza maagazio ya mmiliki wake tu. Kwa hiyo kuhamasiha umma kukageuka kuwa ni kugoma, kuandamana na kufanya vurugu hata pale pasipokuwa na ulazima.
Mkuu una credibility kubwa humu JF sikutegemea kwenye issue serious kma hii utoe comment ya hivi!!

Ni vurugu gani waliofanya CHADEMA ? Ina maana huoni jinsi wanavyokandamizwa tofauti na pre 2015? Je huoni insubordination ya kina Silinde?
 
Mambo yanazidi kupamba moto,safari bado ni ndefu sana,kwa anaedhani safari inakaribia,akumbuke kuwa barabara siyo nzuri,anga limechafuka,bahari haijatulia.
 
Mkuu una credibility kubwa humu JF sikutegemea kwenye issue serious kma hii utoe comment ya hivi!!

Ni vurugu gani waliofanya CHADEMA ? Ina maana huoni jinsi wanavyokandamizwa tofauti na pre 2015? Je huoni insubordination ya kina Silinde?
Sidhani kama tunaweza kujadiliana hili kama hujui kuwa hivi majuzi wabunge wa CHADEMA walifanya vurugu gerezani hadi wakatiwa ndani. Cheap populist politics hazisaidii.

Tunajua kuwa wakati mwingi sana polisi wetu huwa wanatumia nguvu kubwa kuliko stahiki, lakini vile vile kuinstigate fujo kusudi ushughulikiwe na polisi halafu utafute huruma ya wananchi siyo busara na wala haisaidii mstakhbali wa nchi.

Kwa mbunge kususia vikao vya bunge bila kuoa motion to adjourn bungeni ni sawa kabisa na mimi kususia amri ya kutokuiba nikaenda kupora benki kwa nguvu; yote ni uvunjaji wa sheria na kanuni.
 
MNYIKA AMESEMA
ASUBIRI KAHAWA UMYINGIE
MAHAKAMA ITASEMA
MTAJUA CHADEMA N NGO AMA CHAMA CHA KUBET
 
Ni makosa makubwa kuendelea kuamini kwenye maisha kwamba watu wote unaoweza kufanya nao urafiki wasiwe wasaliti, Eti watu wote ambao unaweza kujenga nao Chama kusiwemo wasaliti!! Huo ni Ujinga mkubwa...
tulisema tukabezwa humu, kuwa mpaka 2020 wakati wa uchaguzi, chadema itakuwa imebaki na mwenyekiti tu hawa wote waliofukuzwa ndio waliokuwa wajenzi wa chadema 2010_2015 eti sasahivi ndio wamekuwa wasaliti.

Tabu ya Mbowe ataki kuhambiwa ukweli kuwa ndiye alialibu chadema Kwa gia yake ya angani. Sasa wanatafunana wenyewe Kwa wenyewe watamalizana. Mungu ibariki Tanzania
 
Umegeuka kuwa propaganda tool badala ya think tank.

This is too low from you!! Yaani wazee 20 waliopewa karatasi usome ndio sample size ya maoni ya wazee wa HAI zaidi ya maelfu?
If you think I am too low, the best you can do, just don't read me; it doesnt bother me at all. Elewa kuwa mimi sikupiga picha hiyo. Katika mambo kama hayo, ungeleta upande wa pili kuliko kuwa discredit watu hao bila kuwa na ushahidi wowote.

Hiyo tabia ya kudharau watu ndiyo mbaya sana katika siasa, nadhani ndiyo imekuwa sera ya siasa za CHADEMA. Mimi siwajui watu hao, ni video iliyofunguka nilipomaliza kumsikiliza Mnyika youtube, na nikawa interested nayo. Wewe tafuta video ya ku-counter madai yao tu.
 
Maamuzi magumu ni mwenyekiti kukaa pembeni ili kukiokoa chama kinyume na hapo Ni bure tu
hicho ndicho chadema pamoja na Mbowe wao hawataki kusikia kabisa, tulisema toka 2015 wakati wa Mbowe alipobadilisha gia ya angani akashindwa ilibidi ahachie madaraka ruzuku ikawa tamu, sasahivi anaanza mavuno chadema inamfia mikononi mwake hatalipa tu. Mungu ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom