Tetesi: Wabunge wanne, kuhama vyama vyao

Mi nawasikitikia wale wanaopoteza muda kwenda kuwachagua wabunge wasiojielewa
 
Kwa jinsi nimuelewavyo mkulu ni mtu wa visasi kuhama Nyarandu hakujawafurahisha japo wanamtupia vijembe kuwa ni fisadi ili hali walikuwa nae na walimkumbatia sasa anaweza kabisa kutumia pesa za walipa kodi ili awanunue wabunge wa upinzani maana siasa za ushindani haziwezi.
 
Tume itafakari wanaohama wasigombee wanaitia hasara nchi na wananchi waliowaamini
Ndo gharama ya democrasia, wacha tuingie gharama. Dawa pekee ni katiba mpya, lakini kwa kuwa Mkulu wakati wa kujinadi hakuahidi popote kuhusu katiba mpya, basi waendelee kuhama tu. Tanzania sio maskini bana!
 
Baada ya kafulila,masha na Patrobas Katambi na wengine wengi kuhama chadema.

Kumekuwepo na tetesi na habari za chini chini kuna
Vigogo zaidi wanatarajia kuhama chadema kwenda chama tawala.

Kitu kikubwa watu ambacho wanajidanganya wanadhani chadema akiondoka mtu flani au akihama mtu flani basi chama ndo kimekufa au kitapoteza mwelekeo kisiasa
Kitu ambacho sio kweli

Chadema ni taasisi na chama cha watanzania hivyo kama kuna mtu ana mipango ya kuhama ahame tuu chama kitaendelea kuwepo.

Ikumbukwe ya kwamba ndani ya chadema walikuwepo watu kama akina kaburu, jerry muro, kitila mkumbo Zitto, machali, juliana shonza,mpendazoe,slaa shibuda waliondoka chadema lakini chama bado kipoo hivyo hata mbowe, mnyika, msigwa, kubenea, mdee,sugu na wengine wengi wahamie CCM chama kitaendelea kuwepo na chama kipo kitaendelea kuwepo.

Ingekuwa chama ni mtu basi hata leo dini zisingekuwepo maana walikuwepo watu kama akina yesu na mtume muhamad leo hii hawapo duniani lakini usilamu na ukristo usingekuwepo.

Kama ukristo ungekuwa ni yesu tuu au usilamu ungekuwa ni mohamad tuu
Basi leo hii usilamu na ukristo usingekuwepo kwa maana wenye dini zao washaondoka nazo
 
Kodi zetu zinatumika kununulia wahamiaji haramu kutoka chama B kwenda chama A aka chama dola. Kama vipi bora muwanunue wananchi ili kusiwe na haja tena ya uchaguzi
 
Unafikiria kwa kutumia masaburi weee!
Kama mawazo yako ni hivyo pole yako!

Hao uliowataja akina Kaburu, Zitto, Chacha Wangwe n.k n.k walipojaribu kugusa maslahi ya chairman hasa kutangaza nia ya kugombea uchairman wa chama ndio wanageuka wasaliti kwa chama,

Hivyo basi usijidanganye kama hiyo ni taasisi wakati mwenyekiti wake kang'ang'ania uenyekiti ataki kuuchia kwa mtu mwingine.
 
Tume itafakari wanaohama wasigombee wanaitia hasara nchi na wananchi waliowaamini

Ndio CCM wajue kwamba hicho kipengele cha katiba kinachomvua mbunge ubunge wake kwasababu amehama au amefukuzwa chama ni cha hasara kwa taifa. Lakini, kwa kuwa CCM wanajali zaidi kudhibiti watu kuliko kuweka maslahi ya nchi mbele, kipengele hicho na katiba (1977) hii mbovu imeendelea kukumbatiwa.

Tubadilishe katiba ili wabunge wawe huru kuhama vyama wanapojisikia bila kulishughulisha wala kulitia hasara taifa!! Mbunge anapitishwa na chama kugombea nafasi ya ubunge, lakini anachaguliwa na wananchi (wa itikadi mbalimbali). Kwahiyo, mtu akishachaguliwa kuwa mbunge, anakuwa ni mali ya wananchi waliomchagua kwenye jimbo husika, na sio mali ya chama. Katiba ya maana na inayoendeana na wakati lazima ingetambua hili.
 
Heche na Bulaya hawakosekani hapo
 
mimi kwa sasa ningekuwa ni mbunge kupitia chama fulani ningeshahama chama fasta.
 
Habari wakuu naona kila dalili kwa wanachadema asilia wameamua kumsusia chama Mbowe baada ya kukaribisha mafisadi. Habari za kiintelijensia zikizonifikia hivi punde muda wowote kuanzia sasa Mnyika atatangaza kujiuzulu ubunge na kujivua nyazifa zote ndan ya CHADEMA na kumfuata Kafulila ili kuiendeleza vita dhidi ya ufisadi iliyozimwa na Mbowe
 
hahahahha..Hizi zako ni ramli.hazina ukweli
 
Hii ni habari njema, waache nafasi na sisi tupate vyeo tuanze kula, wenzetu wameshavimbiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…