#COVID19 Wacheni wengine tufe. Mbona mnatulazimisha kuchanjwa wote?

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Ukimwi unaua, Malaria inaua, tb inaua. Hivi vinaua mamia kila mwaka. Hamtulazimishi kuvaa condom, kuchanjwa kama kuna chanjo, kutumia chandarua... Ila hapa tu ndo wazungu mnatulazimisha.kwa nini?

Kwa kweli nmekosa nimjibu nini huyu jamaa fala kabisa. Hataki kuchanjwa na wakati namwona mwilini ana chale kibao tu.

Nimemwambia aache ujinga aende akachanjwe. Kagoma kabisa.anasema ashagundua mchezo ulivyo.

Mimi nimemsisitizia akachanjwe aache mawazo yake hayo. Akachanjwe tujue moja. Waziri wa afya kasema kuna Watanzania million moja wanaitaka chanjo hiyo. Huyu dogo anapinga yeye ni nani? Na machale yote aliyonayo mwilini anawezaje kataa chanjo?

Nendeni mkachanjwe msitake kufa.
 
Na unatia kidole (saini) kabla hujachanjwa. Saini ni ishara kwamba kitu hicho ni hatari.

Nadhani hii itakuwa ni chanjo ya kwanza katika historia mtu anatakiwa asaini kwanza kabla hajachanjwa.
Dunia uwanja wa fujo
 
Hatudanganyiki!! Kama Rais Biden ameamua kuhonga watu wake mwenyewe ili awashawishi kuchanjwa, ni ushahidi tosha kuwa hata huku kwetu anatumia hongo!! Kwa taarifa yako hata huko Marekani zaidi ya asilimia 50 ya watu wamekataa chanjo!! Msikilize mtaalam huyu aliyebobea zkufungue macho
Your browser is not able to display this video.
 
Rais Biden wa Marekani bila aibu wala kupepesa macho ametangaza kutumia hongo ya dola 100 kwa kila Mmarekani atakayekubali kuchanjwa!! Ni ushahidi tosha kuwa hata kwenye mataifa mengine anakopeleka chanjo anatumia hongo pia!!

Katika hali ya kawaida ni rahisi Biden kuwashawishi watu wake kwenye chanjo kuliko kuwashawishi watu na viongozi wa mataifa mengine!

Kama penye urahisi ameshindwa kushawishi hadi kutumia hongo, nina uhakika kuwa kwenye mataifa mengine palipo pagumu zaidi ametumia hongo kubwa zaidi Ndiyo maana ghafla hata maprofesa ambao kwa sasa tunawaita mapropesa wameamua kula matapishi yao kwa kuyapinga maneno yao wenyewe kuhusu chanjo!

Hali kadhalika kwa baadhi ya madaktari na viongozi wengine!! Kisa, kitu kidogo!! Hivi ni viongozi wangapi wa Afrika wanaoweza kukataa rushwa ya Marekani kuwa kwa kila raia wake mmoja atakayechanjwa basi atapewa dola 100!

Akishawishi watu milioni moja atapata dola 1,000,000×100 = dola 100,000,000!
 
Na unatia kidole (saini) kabla hujachanjwa. Saini ni ishara kwamba kitu hicho ni hatari.

Nadhani hii itakuwa ni chanjo ya kwanza katika historia mtu anatakiwa asaini kwanza kabla hajachanjwa.
[emoji41][emoji41][emoji41]
Your browser is not able to display this video.
 
Huko duniani unapewa 100$ ukichanjwa, huku Bongo cjui wanasubiri nn
Huku afrika uchanjwe wewe kisha aliyekushawishi ndo anapata hiyo $100! Upo hapo! Haujashangai wapiga debe wa chanjo walivyoongezeka ghafla!! Hata maprofesa walioipinga wamegeuka kuwa mapropesa na kupigia debe chanjo!! Ila hatudanganyiki!!
 
Ukimwi unaua, Malaria inaua, tb inaua.... Hivi vinaua mamia kila mwaka. Hamtulazimishi kuvaa condom, kuchanjwa kama kuna chanjo, kutumia chandarua... Ila hapa tu ndo wazungu mnatulazimisha.kwa nini?...
Mkuu nani anataka kukulazimisha chanjo tumshitaki mahakama za kimataifa kukuingilia uhuru wako?

Waziri Mkuu kashasema kuchanja ni hiyari.

Halafu hao Watanzania bilioni moja wametoka wapi? Mnahesabu wanaoishi tu au mpaka waliokufa na ambao hawajazaliwa?
 
Tumia akili! Hiyo bilioni ni typing error alimaanisha milioni!! Halafu usizuie watu kusema, mbona wapiga debe wa chanjo wanasema ! Acha kila kambi iseme na watu waamue kulingana na walivyosikia mawazo tofauti tofati! Kwani hatujui wajanja kutumika kama chambo huku wao wakichanjana maji matupu? Hata huko nje uchafu huu ndio umetumika kurubuni watu waingie mkenge!! Ona hapa!
Your browser is not able to display this video.
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…