Tetesi: Wachezaji watano wa Simba wasimamishwa kupisha uchunguzi kwa kichapo kikali cha goli 5 kutoka kwa Yanga

Tetesi: Wachezaji watano wa Simba wasimamishwa kupisha uchunguzi kwa kichapo kikali cha goli 5 kutoka kwa Yanga

Huyo Prisca ni mmbea mbea tuu..
Ndo maana Manara wakati yupo Simba alimtusi
 
Hebu tuache uswahili Tanzania!!
1. Chama anayetuhumiwa si ndo amepiga faulo ambayo ilizaa kona na baadae goli la simba?
2. Inonga amefanyaje?
3. Ukitazama magoli yote matano simba wanapokwa mipira/intercepted passes watu wanaenda kufunga
Kama ni kweli viongozi wa Simba wamewasimamisha wachezaji basi anatafutwa tu mbuzi wa kafara badala ya kufanya utafiti wa kitaalam kuangalia Simba ilizidiwa wapi. Na mpira ni mchezo wa wazi hao viongozi waache uswahili na kuokoteza maneno halafu wanaamua kuwafungia wachezaji badala ya wao kuwajibika kwa uzembe wao mkubwa wa kusajili baadhi ya wachezaji bila kuangalia mahitaji ya timu na kuajiri kocha wa viungo asiyelingana na hadhi ya Simba. Wa kwanza wa kuwajibika ni hao viongozi kabla ya kuwatuhumu hao wachezaji.

Kwa mtu aneyefahamu mpira kwa undani huwa inatokea siku boli linakataa sasa kwa upuuzi huo wa viongozi wa Simba basi kuna wachezaji watakuwa wananonewa. Hapa waliozembea ni benchi la ufundi iwapo mchezaji hakuwa sawa walipaswa wamfanyie sub basi sio kuja kuwapa kimeo wachezaji.
 
Na kama ipo hivyo, kocha yeye kafukuzwa kwa kosa lipi?
Kocha ni kama mbwa asiye na mmliki, hawezi kosa sababu ya kutupiwa jiwe. Sababu inaweza kuwa yoyote ile:

1. Aina ya mpira usio wa falsafa ya Simba
2. Maelewano katika vyumba vya kubadilishia nguo
3. Kutolewa mapema AFL etc etc

Kufungwa si tatizo, tatizo ni kufungwa na Yanga goli nyingi. Hapa lazima apatikane mtu/watu wa kuwajibishwa. Mara nyingi wa kwanza na rahisi kumuondoa huwa ni kocha.
 
Kama ni kweli viongozi wa Simba wamewasimamisha wachezaji basi anatafutwa tu mbuzi wa kafara badala ya kufanya utafiti wa kitaalam kuangalia Simba ilizidiwa wapi...
Hii habari si rasmi, ila tukiweka assumption kuwa ni rasmi basi Kama wameonewa watashtaki. Mambo si marahisi hivyo kuwa utoke tu huko usimamishe wachezaji na kuchafua taswira yao bila ushahidi. Wakisimamishwa halafu wakakubali na kukaa kimya kuna uwezekano ni kweli.
 
Shida kubwa Simba iko kwa Mangungu, hata huyo Robertinho ni bangusilo tu, wale walioshindwa uchaguzi na Mangungu wataihujumu timu hadi aachie nafasi hiyo, Mangungu ananikumbusha enzi za akina marehemu Juma Salum, kabla ya hapo marehemu Jimmy David Ngonya, kulikuwa ni Vita tu ile ya Israel na Hamas ni cha mtoto.Shahidi ni Kassim Dewji vs Juma Salum.

Mangungu sio mtu wa mpira, watu wa friends of Simba hawampendi na hawako tayari kufanya kazi naye, sasa mm najiuliza mbona wenzetu Yanga wamemuachia timu GSM, hamuoni maendeleo hayo.

Haya mambo ya kijinga kijinga ndani ya timu yetu huwa hayaishi na hayataisha, katika mazingira kama haya mjinga gani atakubali kuweka bilioni 20?
Unadhani watasimamishwa bila ushahidi?
Bila hata kupata ushahidi wa ziada,Baleke alionesha wazi hahitaji kuifunga yanga.


Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Bila Simba kurudishwa utamaduni wa kusoma kisomo cha ALALBADIR BAYANA kabla ya mechi itaendelea kuhujumiwa kila siku.

Muwe na utaratibu wa kusoma kisomo kwa wasaliti wa timu.
Muwalishe yamini wachezaji wote na viongozi wote kama wafanyavyo Yanga.

Muone kama Kuna atakayehujumu timu.
 
Unadhani watasimamishwa bila ushahidi?
Bila hata kupata ushahidi wa ziada,Baleke alionesha wazi hahitaji kuifunga yanga.


Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Alionyeshaje mkuu??
Simba walitengeza nafasi ngapiii??
Huyo Baleke ukiacha Ile Nafasi moja aliyopata na kugongesha besera,Kuna nyingine..Me naona wasikurupuke,hata Mchezaji kama Chama ni ngumu kupokea pesa,Nachoona kwake ni kiwango kinekua duni na pia ameshajiona mfalme ndani ya timu.
 
Simba rudisheni utamaduni wa kusoma ALALBADIR BAYANA kabla ya mechi ili kulishana yamini kwa wachezaji na viongozi wote wasaliti.

Zamani Simba na Yanga ilikuwa lazima wazee wasome visomo kwa ajili ya wasa.
Nani aliyefuta utaratibu huu.

Wenzetu Yanga bado visomo vinasomwa kwa wasaliti wa timu kabla ya mechi kubwa na muhimu kwa timu.
 
Mateso huko ni mengi, wakihisi mtu hana bahati 😃😃😃
 

Wachezaji watano wa Simba Sc akiwemo Enock Inonga na Clatous Chota Chama wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi yao baada ya kufungwa na Yanga SC mabao 5-1 siku ya Jumapili.

Wachezaji hao wanatuhumiwa kuihujumu timu kitendo kilichopelekea kupoteza kwa idadi kubwa ya mabao.

Maamuzi hayo yamefanyika katika kikao cha bodi ya Wakurugenzi ya Simba kilichofanyika jana jijini Dar es salaam.

Chanzo cha uhakika kutoka Simba SC kimeiambia Kishamba Media kuwa uongozi umeshapata ushahidi wa awali kuhusu tuhuma dhidi ya wachezaji hao na sasa imeanza uchunguzi wa kina ili kujiridhisha.

Wachezaji hao watakua nje ya kambi ya timu mpaka hapo maamuzi mengine yatakapofanyika.

Chanzo hicho kimesema huwenda leo klabu ya Simba ikatoa taarifa ya wazi kwa Umma juu ya maamuzi waliyofikia kuhusu wachezaji hao au wasitoe ila wahusika wamepewa taarifa.

Maamuzi mengine yaliyofikiwa na bodi ni kufutwa kazi kwa kocha mkuu Robertinho, msaidizi wake pamoja na kocha wa viungo.

Kishamba Updates

Watatu waliobaki ni akina nani katika hao watano?
 
Back
Top Bottom