Wadau wapendekeza Elimu ya Msingi kuishia darasa la 6

Wadau wapendekeza Elimu ya Msingi kuishia darasa la 6

Hizi sera ambazo kila waziri akija anakuja kivuake ni "supply driven" ndiyo hizi ambazo hata wadau muhimu huwezi kusikia wakishirikishwa katika kuziandaa. Sera nzuri ni lazima ziwe "demand driven" kwa kuwa wadau muhimu hutambua "missing gaps" zilizopo katika mfumo wa elimu uliopo hivi sasa.

Ili tupate sera nzuri ya elimu hapa nchini, ni vyema kushirikisha wadau muhimu kama vile wataalamu, watafiti na wanataaluma kutoka fani mbalimbali ili kuweka vigezo vizuri vya kuzingatia wakati wa ufundishaji, wakufunzi, walimu, wazazi, walezi, n.k. ili kupitia katika majukwaa yao maoni muhimu yaweze kukusanywa na kufanyiwa kazi kabla ya kuiandaa sera husika ya elimu.

Serikali isiishi kwa "trial & error" bali ifanye tafiti nyingi na za uhakika ili iweze kuthibitisha uamuzi wake. Mzee Mwinyi aliwahi kugusia kuhusu sifa ya mtu kuwa "kichwa cha mwendawazimu"
Kama vipi tuchukue waingereza warudi tu watutawale na elimu nzuri watupe mbona hivi
 
Hatua nzuri sana kwa sababu ,hataachwa mwanafunzi yeyote yule kwani mtoto mwenye uelewa mdogo ataenda ufundi na mwenye uelewa mkubwa atachugua mwenyewe aende ufundi au aendelee na masomo ya juu.

Tatizo naliona hapo kutoka darasa la sita kwenda ufundi au sekondari bila kufanya mtihani.tunampimaje huyo mtoto Kama ataweza kumudu masomo ya sekondari au ufundi?.

Mtihani ungekuepo tu ili kujiridhisha kwa usahihi uelewa wa mtoto kabla ya kumpeleka mbele
Mimi ninachokiona ni kuwa wanaamua Sasa kuitanua elimu ya msingi, Yaani baads ya kuishia drs la 6, Sasa mtoto atasoma hadi kidato Cha nne.. Hii ina maana kuwa elimu ya msingi itaanzia drs la 1- kidato Cha nne, na ndiyo maana wameondoa drs moja hapo ili kupunguza mzigo. Kuhusu mtihani watafanya kidato Cha nne Kama tathmini ya kumpima mwanafunzi.. Kosa ninaloliona hapo ni ktk lugha ya kujigunzia,kuchagua tahasusi mtoto akimaliza tu elimu ya msingi, pia ni Kosa.
 
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga, amesema kuwa katika sera mpya inayotarajiwa kuzinduliwa hapo baadaye elimu ya msingi itakomea darasa la 6.

Kauli hiyo ameisema hii leo Oktoba 20, 2022, na kuongeza kwamba sera mpya ya elimu itakapozinduliwa hakutakuwa na mtihani wa mwisho wa elimu ya msingi na kwamba mtihani utakuwa ni wa kidato cha nne tu, huku akisema mwanafunzi akianza kidato cha kwanza atakuwa tayari ameshajiweka kwenye mchepuo maalum hadi kidato cha nne.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omary Kipanga amesema kuwa serikali inatazamia kuzindua sera mpya ya elimu kufikia mwezi Desemba, 2022 ili kuleta mabadiliko makubwa kwenye sekta ya elimu na kwamba mabadiliko yataanzia elimu ya msingi.
Huu mpango umewashirikisha wenye nchi lakini?
Au bafo tunaendelea kuamini kaba Viongozi ndo wana akili mbadala zaidi ya wenye nchi?
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukos maarifa,mtoto wa darasa la sita atachagua nini,mnataka kuiua nchi ili wenye nacho waendelee kutamba.
Mtoto wa miaka 13 hajui masomo gani anataka kuchukuwa? elimu gani wanayotoa darasa la saba? wakati watoto wa Kenya tu hapo miaka 12 wako chuo kikuu miaka 8 na 4 kwisha wako mitaani wanatafuta maisha sisi tunapiga miaka 13 7-4-2 na quality zero halafu unataka kushindana? mtoto yuko primary mpaka anabeba mimba maana miaka 14 yuko primary hata haogopi tena lazima tubadilike miaka michache lakini quality. Jirani zetu wa Kenya kwa sababu wanatutangulia mwaka watoto zao wako sokoni wakati wa kwetu bado wako shuleni wakitoka nafasi zimejaa.
 
la msingi kama Mwandishi nguli na mbobezi ni vyema sasa ukaanzisha harakati za kuhakikisha elimu ya Tanzania inakuwa ni kiingereza msingi mpaka chuo kikuu au kiswahili mpaka chuo kikuu, tusimamie kimoja katika hivyo na kuwekeza huko.
Mkuu nyau wangu, Nangu Nyau , hii inahitaji specialization, mimi nimejikita kwenye developmental news, watu wa educatinal news wapo watalifanyia harakati.
P
 
Huu mpango umewashirikisha wenye nchi lakini?
Au bafo tunaendelea kuamini kaba Viongozi ndo wana akili mbadala zaidi ya wenye nchi?
Wenye nchi wako busy ku comment kwenye picha za Zari huko sheria ikipita ndio utaona ehhh kuna nini tena kimetokea ni kama yale ya tozo yanapitishwa watu wako busy Fiesta...na betting
 
Mkuu nyau wangu, Nangu Nyau , hii inahitaji specialization, mimi nimejikita kwenye developmental news, watu wa educatinal news wapo watalifanyia harakati.
P
Kuna haja ya kujiuliza kwani shida hapa ni lugha au kufahamu unachojifunza? Germany, Russia, Korea, China, Turkeym Finland sijui Japan hawa wanajifunza kwa English? hizi nchi wanatoa elimu kwa lugha zao na English ni somo tu tuache kudhani mtoto akiongea kizungu ndio ana akili watoto wapimwe kwa kuweza kujieleza na ufahamu wa mambo lugha ni chachu maana kama kuongea tu English ndio kipimo chetu basi safari ndefu tunayo. Hapo India tu wanatumia lugha yao na herufu zao hata Israel lakini English ni somo tu kama masomo mengine.
 
Mtoto wa miaka 13 hajui masomo gani anataka kuchukuwa? elimu gani wanayotoa darasa la saba? wakati watoto wa Kenya tu hapo miaka 12 wako chuo kikuu miaka 8 na 4 kwisha wako mitaani wanatafuta maisha sisi tunapiga miaka 13 7-4-2 na quality zero halafu unataka kushindana? mtoto yuko primary mpaka anabeba mimba maana miaka 14 yuko primary hata haogopi tena lazima tubadilike miaka michache lakini quality. Jirani zetu wa Kenya kwa sababu wanatutangulia mwaka watoto zao wako sokoni wakati wa kwetu bado wako shuleni wakitoka nafasi zimejaa.
Nikuulize Kenya hawapati mimba????Na hiyo elimu ya Kenya inatuzidi nini???Ukienda Kenya asilimia kubwa ya Wanawake wa Kenya wanakuja kuolewa lakini wanakuwa walishazaa kitambo.
 
Kuna haja ya kujiuliza kwani shida hapa ni lugha au kufahamu unachojifunza? Germany, Russia, Korea, China, Turkeym Finland sijui Japan hawa wanajifunza kwa English? hizi nchi wanatoa elimu kwa lugha zao na English ni somo tu tuache kudhani mtoto akiongea kizungu ndio ana akili watoto wapimwe kwa kuweza kujieleza na ufahamu wa mambo lugha ni chachu maana kama kuongea tu English ndio kipimo chetu basi safari ndefu tunayo. Hapo India tu wanatumia lugha yao na herufu zao hata Israel lakini English ni somo tu kama masomo mengine.
Lakini wanaongea Kiingereza fasaha tofauti na sisi hao wote uliowataja.
 
Nikuulize Kenya hawapati mimba????Na hiyo elimu ya Kenya inatuzidi nini???Ukienda Kenya asilimia kubwa ya Wanawake wa Kenya wanakuja kuolewa lakini wanakuwa walishazaa kitambo.
Elimu ya Kenya inatuzidi nini? kweli unataka nikujibu hapa au unafanya utani. Nadhani jiulize wakati tunataka kuruhusu ajira free EA Tanzania walisema nini? bado hatuko tayari kushindana na wa Kenya sasa waulize wanasiasa walikuwa wanamaanisha nini.
 
Lakini wanaongea Kiingereza fasaha tofauti na sisi hao wote uliowataja.
Wafaransa hawaongei, Wa Japan lugha yao tu Spain lugha yao na hata wa Italy yao na wakiongea English wengi wao bora wewe ila Germany wanaongea sababu ni somo muhimu kwao. Lakini hata hapa yuko Wema sepetu ana English maridadi sana lakini kichwani zero.
 
Wenye nchi wako busy ku comment kwenye picha za Zari huko sheria ikipita ndio utaona ehhh kuna nini tena kimetokea ni kama yale ya tozo yanapitishwa watu wako busy Fiesta...na betting
Unaweza kunieleza lini Bunge letu liliwahi kutunga sheria?

Natumaini umelielewa swali langu
 
Back
Top Bottom