Wadau wapendekeza Elimu ya Msingi kuishia darasa la 6

Wadau wapendekeza Elimu ya Msingi kuishia darasa la 6


  1. Kutakapotokea wimbi la Wanafunzi kufeli Kwa wingi katika mitihani ya kidato cha nne, msianze kuwalalamikia walimu kwamba ndiyo chanzo.
    Tangu darasa la kwanza mpaka kidato cha nne ndiyo anaukuta mtihani! Mhhh! Ngoja tusubiri tuone itakuaje.
    Kuna wadau hapo Juu wamesema Inawezekana ni sera ya "try and error process"..
Nimeelewa kwamba ni mtihani wa mwisho,yaani ule ambao tulikua tunafaulu lakini hatuchaguliwi,wanaofaulu huo mtihani ni wale ambao hawakuwa wakifanya vizuri miaka yote SITA unusu
 
Naomba Kujua,Sijaelewa,
Mtoto akishafika Darasa La 6 anakwendaje Form-1?
Sababu Nimesoma Kuwa Hakutakiwa na Mitihani Shule ya Msingi,Kutakuwa tuu na Mtihani wa form 4!
Sasa Mtoto akimaliza Darasa la 6 Watajiunga Vipi na Sekondary,Na Sekondary Maalum Pia?
Then Atafanya Mtihani form 4 na Kwenda Form 5!
Wote sekondari,hakuna kubaguana kidini kwenye elimu
 
Sijui kama tutapona....

Haya mambo ya "kufuta" mitihani ndio yamesababisha sasa hivi kuna watoto wanafika form 4 hawajui kusoma wala kuandika.

Enzi zetu, ukiwa hujui kusoma wala kuandika, darasa la 5 huingii hata kwa dawa.
 
Inatakiwa Elimu ya Msingi iende mpaka form four(Compulsory education).
Zile blah blah za form one mpaka four ziingizwe kwenye miaka saba ya primary.Kuanzia form one mpaka four ni technical education tu(Carpentry,Mason, computer science, modern fisheries, modern Agriculture, Bookkeeping, Business Administration, Financial Management, health sciences ,Mining,nk).
Mambo Majimaji war anayetaka atakutana nayo University.
 
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga, amesema kuwa katika sera mpya inayotarajiwa kuzinduliwa hapo baadaye elimu ya msingi itakomea darasa la 6.

Kauli hiyo ameisema hii leo Oktoba 20, 2022, na kuongeza kwamba sera mpya ya elimu itakapozinduliwa hakutakuwa na mtihani wa mwisho wa elimu ya msingi na kwamba mtihani utakuwa ni wa kidato cha nne tu, huku akisema mwanafunzi akianza kidato cha kwanza atakuwa tayari ameshajiweka kwenye mchepuo maalum hadi kidato cha nne.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omary Kipanga amesema kuwa serikali inatazamia kuzindua sera mpya ya elimu kufikia mwezi Desemba, 2022 ili kuleta mabadiliko makubwa kwenye sekta ya elimu na kwamba mabadiliko yataanzia elimu ya msingi.
Mwanafunzi anachagua mchepuo ( kombi) na wakati hajui zipoje. Mtu anachagua PCB , au PCM form one kwa kutumia maarifa ya Science ya msingi anafika form IIC, Logarithms, Trigonometrical ratios, electrolysis, valence, periodic table, classification, Nutrition, zinamwondoa kwenye reli. Anakumbuka HGL, HKL, HGK, ndio chaguo lake( Hapa safari ndefu inaanza ili kusoma kombi za ARTS).
NB
Ni vizuri wanafunzi wakayasoma kwanza masomo hayo wajue changamoto zake na wanapochagua michepuo wawe wamepata uchambuzi wa kina kutokana na kuyapitia hayo masomo kwa undani zaidi.
 
Haya ndio maendeleo, ila tulipaswa tuwe kama US, 8-4-4

Primary miaka 4
Mtoto anaanza la kwanza akiwa na miaka 4 na kumaliza elementary akiwa 12 anakwenda sekondari at 13 years for 4 years na kumaliza at 16 anaingia college at 17 years for 4 years na degree zao ni masters!.

US mtu haruhusiwi kusomea sheria kama hana degree nyingine, hivyo kule kwenye sheria, sciences na udakitari wa binadamu, hakuna kilaza atapenya! Sio hapa vilaza wanakimbilia LL.B na kupewa degree za michongo!, kufika LST wana stopishwa basi ni kelele mwanzo mwisho!.

Kule hawana A level!.

P.
Sisi tunafata system ya uingereza ambao wanishia A level na unngia university ukifaulu na kusomea degree unayotaka kutokana na ufaulu wako ikiwa Sheria au sayansi huo mfano uliotoa ww ni was marekani hatujaamua sisi kuufuata.
 
Wawe makin, maana wakizingua hapo wameharibu maisha ya vizaz vijavyo.

Wakishamaliza kuandaa huo utaratibu mpya wa elimu, wahakikishe unapitiwa vzr na wadau mbalimbal wakiwemo wananchi wenye uelewa mpana, na sio hawa vilaza wa kulalamika kila jambo.

Baada ya kuupitia huo utaratibu vzr basi watenge week kadhaa ama mwez mzima wa kuwapeleka semina Walimu wote nchi nzima, na kila mkoa wakipewa mafunzo maalum na wakufunzi walioupitia huo utaratibu mpya.

Zichapishwe nakala za kutosha kwaajili ya kila mwalimu kupata uzoefu wa mfumo mpya.

Kiingereza sio muhimu kwa taifa, hapa ndipo pagumu, kiswahil ni lugha ya mataifa, hivyo kifundishwe kiusahihi na icho kiingereza mnacholalamikia kiwe kama additional language ambayo mtu anaisoma for other benefits.

Masomo yote ya sayansi yatafsiliwe kwa lugha ya kiswahili, ikiwepo kuibua misamiati mipya ya maneno ambayo hayakuwepo ktk lugha ya kiswahil, mfano yale ya kifizikia, na masomo ya kitabibu misamiati ipewe maana na matamshi kwa lugha ya kiswahili.

Hakuna ulazma wa kupoteza muda na kingereza, hii nchi watu wangekuwa wakujua hiyo lugha basi wangeijua vzr kwa juhud za walimu mashulen, lkn bado hiyo lugha ni mtihani kwa waTz wengi kwann? Kwasababu tunaforce mambo ambayo si ya msingi, hakuna ulazima wa watu wote kuijua hiyo lugha, wenye uhitaji waisome na wasiohitaj waipotezee.

Huo utumwa wa kukalilishana kuwa msomi lazma ajue kingereza upitwe na wakati, usomi haupimwi kwa kujua lugha.

Elimu ya vyuo vya ufundi na tiba ipewe kipaumbele zaid ya hizo takataka walizokuwa wakiwapotezea muda wanafunzi
 
Waliahidi kugawa vishikwambi kwa walimu wote nchini sijui imekuwaje mpaka sasa
 
Kiswahili kifutwe lugha ya kufundishia iwe kiingereza, kiswahili libaki kama somo tu.

Ilikufanikisha azma hii walimu wa lugha ya kigeni ya Kiingereza waletwe kutoka Malawi, Zambia, Zimbabwe ili wafundishe kwa muda wa mpito wa mabadiliko.

Hivyo baada ya miaka 10 tutapata waalimu wa primary na sekondari waTanzania wanaokimanya lugha hii muhimu ya kimataifa kuweza kuwapa wanafunzi uwezo endelevu kuelewa masomo mengine yaliyopo ktk lugha ya kiingereza kama masomo ya sayansi pia mengine kama historia na kiingereza kama somo lugha.


Shule za binafsi za English medium zimefanikiwa kutumia waalimu toka nchi jirani, umefika wakati shule zote za serikali za kata kupewa waalimu kutoka nchi hizo za jumuiya ya SADC ili kuondoa pengo lililopo baina ya wanafunzi waendao shule binafsi na wale wa shule za kata.
 
kuwa na lugha sahihi ya kufundishia kuanzia msingi mpaka chuo kikuu ndio mwanzo wa uelewa kwa wanafunzi pia.

Tutumie kiswahili mpaka chuo kikuu au tutuumie English msingi mpaka chuo kikuu.

Kumfundisha mtu shuleni kwa kiingereza ambacho hakijui ndio chanzo chakuwa na wahitimu waliokariri shuleni, naamini malalamiko ya wengis yapo kwenye mafunzo kutolewa kwa kiingereza huku hicho kiingereza mfundishaji na mfundishwaji wote hawakijui.
Kwahiyo ni bora tungeamua kuwafundisha watu kwa lugha moja wanayoielewa ili waweze kuelewa wanachofundishwa.

Binafsi naamini, Ni bora tutumie kiingereza na kuhakikisha watu wetu wanajua kiingereza maana ndio Lugha inayotumika sehemu nyingi kimataifa na hata technolojia nyingi zinakuja kwa lugha hiyo, huko mbele tukishakuwa na maarifa ya kutosha basi tunaweza kubadili mtaala na kurudi kwenye kiswahili hasa pale tutakapokuwa na maguvu ya kiuchumi na kujitegemea
 
Em ngoja tuone. Maana CCM haijawahi kuwa serious kabisa na Elimu !! Let's get the full package of this first.
 
Kila siku huwa unalalama mawakili wetu wa sasa hawana uwezo kama wale wa zamani, sijui hao mawakili wetu hutokea wapi kama sio LST.

Kumbe basi hata LST hutoa vilaza.

Na unavyotaka tuwaige Marekani, hizo facilities ikiwemo standard ya education itafanana nao? ikiwa huku kwetu walimu wachache, hakuna vitabu vya kutosha, nk..
Huyo shoga Pascal Mayalla huwa ananifurahisha sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Mwaka huu alipewa uwakili wa zawadi kutoka kwa waziri, basi kutwa kuchwa kuwatusi vijana wa LST kwamba ni vilaza.

Kuna kipindi cha nyuma hapo huyu Pasco alifumaniwa akiwa kwenye skendo ya ushoga na boss mstaafu wa ATCL.

Anzia hapo, utajua kwanini huyu shoga ana gubu dhidi ya mawakili wasomi waliopitia LST.
 
MTU anafika form four hajielewii kabisaa as if Shule ndo imempolute. Ngoja tuone. Mpaka Leo hii mtu anasoma majimaji war!?!??
 
Back
Top Bottom