Wadau wapinga Rais Samia na Makamu wake kuingia na Viti binafsi Kanisani, yadaiwa ni kujikweza

Wadau wapinga Rais Samia na Makamu wake kuingia na Viti binafsi Kanisani, yadaiwa ni kujikweza

Dr. Philip Mpango ni mkatoliki na amesali hapo bukoba cathedral mara kadhaa na makanisa mengine anapokua ziarani hatujawahi kuona akiletewa kiti chake. Hapo aliyefanya viletwe viti "vya wageni" ni Mama. Hoja za kiusalama, usafi, ukubwa nk...sizikatai Ila pia sizikubali, sana sana ni hoja ya Mila na desturi za wahaya, mgeni uhayani anapewa heshima iliyopitiliza tena hasa kama ni kiongozi au mtu mwenye mafanikio kimaisha (wahaya wanaelewa ninachozungumza) na hivyo hawatamruhusi kamwe kukaa kama wanavyokaa wao Wala kula wanachokula wao, watamwandalia kila kitu chake Cha tofauti, kizuri na kwa heshima na hofu kubwa. Kuna simulizi za zamani kuwa "abakama" yaani machifu wa kihaya walipokwenda mahala kutembea hawakuruhusiwa hata kukanyaga ardhi, walichukiliwa vijana wa kiume na kulala barabarani ambapo wakubwa wale walikanyaga migongo yao kwenda mahala palipoandaliwa kutoa hotuba. Kama Hilo halitoshi, wakati wa hotuba simulizi zinasema Omkama alisimika mkuki wake kwa kuuchoma kwenye mguu wa kijana ambaye badae alipewa ng'ombe na mke mzuri. Hata hivyo, hoja yangu inapata maana kama vile viti viliandaliwa na kanisa kwani viongozi na waamini wengi wa bukoba karibu wote ni wahaya. Kama ni viongozi wa mkoa wakiongozwa na mkuu wa mkoa kwamba ndo waliomba walete viti maalum kwa ajiri ya viongozi wakuu wa kitaifa, kanisa lisingeweza kukataa maana ibada haiwezi kuathirika kwa namna yoyote Ile, sasa labda kama ni hoja ya uchawa, itakua kwa hao waliovileta. Mimi hata hivyo bado nampongeza mama kwa kushiriki ibada ile na kukubali kuingia kanisani na kufuata matendo yote ya ibada ya kikristo, zamani ilikua kama raisi sio mkristo, ibada ziliandaliwa nje ya kanisa...huu ni unyenyekevu wa aina yake unapaswa kupongezwa sio tuangalie mambo madogo madogo yasiyokua na maana. Mkisema mbona kiongozi fulani alikua anaenda msikitini wakati ni mkristo, mkumbuke wakristo hawana katazo la moja kwa moja kwenda nyumba za ibada za wengine kama ndugu zao wale, kwa hiyo mama mpaka anakaa pale mbele na kusikiliza mahubiri ya askofu kilaini ujue amevuka vihunzi vingi sana., mama mitano tena.
 
Wewe hupaswi kuwalaumu hao viongozi moja kwa moja.

Erythrocyte!
Umeandika as if walikuja wamebeba viti vyao,wakati ukweli ni kwamba kama ni kasoro imetokea.na kama ni kulaumiwa ni hao waliokuwa na jukumu la maandalizi na sidhani kama ni maagizo ya Mheshimiwa Rais wala Makamu wake.
Wao wameingia na kuelekezwa mahali walipoandaliwa kukaa.

Baadhi ya vitu sio lazima uvipinge kwa sababu havina tija kwa maendeleo chanya wala havitowi fundisho lolote kwa jamii.
Pia kuwa pingapinga sio alama ya elimu bali ni dalili za ubishi usio na tija pia.

Rais akipanda basi mnasema kadharauliwa,je kipi afanye ili awafurahishe?

Mtaendeleza bifu la kukaa benchi mpaka 2025?

Si mtafika mmechoka Sana?

Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe.
Ndugu voicer kwani kuna ubaya gani kwa Erythrocyte kutoa maoni yake kwa namna anavyoona yeye juu ya tendo hilo...?

Hayo ni maoni yake. Ni vyema sana kuheshimu maoni ya wengine ili mradi hayajavunja sheria yoyote...

Unaweza kukubaliana naye au ukatofautiana naye. Kwa sababu hata wewe kwa maoni yako haya kuna wanaoamini kinyume chake...

Back to the topic;


Nami nasema Samia na Philipo Mpango wamechemka big time bila kujali wameagiza wao ifanyike hivyo ama wamekuta wasaidizi wao wamefanya vile..

Ni mbaya sana kwa kilichofanyika ndani ya nyumba ya ibada. Ni kujikweza na kujiona kuwa wao ni maalumu zaidi mbele ya macho ya waumini ambao ni wananchi wao. Ni mfano mbaya waliouonyesha mbele ya watu..

Najua utaendelea kubisha. Haijalishi, lakini ukweli ndiyo huo..

Au nikuulize swali hili;

Kwamba, hivi ingewezekana kweli mama Samia kwenda msikitini akiwa na zulia lake kutandika chini siku ya Ijumaa ili asali akidharau zulia ndani ya msikiti kwa ajili ya kila mtu...??

Kwa ufupi sana, ni kuwa, ukiwa na viongozi wa aina hii na wenye tabia za kujikweza hata katika mambo ya imani, inaweza kutokea siku za usoni wakatoa amri ya wao kutaka waabudiwe kama mungu kama alivyofanya Mfalme Nebukdneza...!

Nakuhakikishia jambo moja, kuwa, kwa tendo lao hilo hata Mungu Yehova waliyekuwa mbele yake hakufurahishwa nalo..!
 
Acha kuchukulia vitu kwa wepesi, kila sehemu kun misingi yake, na unapofika lazima ufuate Sheria..

katika Hilo Hilo kwnn aendapo msikitini abebi jamvi lake, watu wanaweza uliza hvo by the way.

Pale ni sehemu ya Ibada ni vema kufuata taratibu za mule Kama hawezi kwa kuona yey no Bora San Basi asiingie.
Yapo ya msingi ya kuyachukulia kwa umakini kuliko hili suala la kiti cha SSH kanisani.
 
Well, hajalazimishwa aingie kanisani, lakini ukiamua kwenda kwenya nyumba ya kuabudu ya wenzio inapendeza kufuata taratibu zao

Mtangulizi wake alivua viatu mlangoni kwa sababu wenzake Waislam huvua viatu


m1.jpg



Na hakuona aibu Rais kukaa sakafuni mbele ya Mwenyezi Mungu Subhana wa Taala

RAIS%2BMAGUFULI%2BAKAGUA%2BMSIKITI%2BWA%2BKIMATAIFA.jpg


Samia Suluhu anavunja misingi ya kuheshimiana kidini iliyojengwa na watangulizi wake. Rais anapaswa kuwa chachu ya kuwa inspire watu kuwa wamoja japo wanatofautiana kidini. Kuleta kiti cha Ikulu kanisani imesikitisha Watanzania wengi.

Samia Suluhu amekuwa Rais wa kwanza kufanya jambo lililosababisha watu kuchambana dini zao mitandaoni na mitaani.
Pole sana kama wewe ni Team Magufuli unayetafuta sababu hata ya kitoto ya kumzodoa SSH.
 
Queen+Duke+Edinburgh+Visit+St+Columba+Church+ip-afaxjhe-x.jpg

Waumini wote kanisani tunakalia mabenchi ya mbao

Hata wafalme na malkia wa himaya zilizotawala dunia wanajinyenyekeza mbele za Mungu

Japo wanaweza kutandaza makochi ya ngozi na sufi kanisa zima lakini wanajishusha mbele ya madhabahu ya Mungu kwa sababu wanajua Yesu Kristo alizaliwa kwenye josho la kulishia ng'ombe akiwa ni mtoto wa muweza wa yote.
 
Dr. Philip Mpango ni mkatoliki na amesali hapo bukoba cathedral mara kadhaa na makanisa mengine anapokua ziarani hatujawahi kuona akiletewa kiti chake. Hapo aliyefanya viletwe viti "vya wageni" ni Mama. Hoja za kiusalama, usafi, ukubwa nk...
Sasa kama hawaamini kuwa walikwenda kumwabudu Mungu Yehova aliye chanzo cha uhai na usalama wao, basi hakukuwa hata na maana wao kwenda kanisani..

Imeandaliwa, "...Bwana (Mungu Yehova) asipoilinda nyumba, ailindaye afanya kazi bure..." Aidha imeandikwa pia "...Amelaaniwa yeye amtegemea mwanadamu (kwa maana na vitu vyote vilivyotengenezwa na mwanadamu) kuwa vitamlinda..."
sizikatai Ila pia sizikubali, sana sana ni hoja ya Mila na desturi za wahaya, mgeni uhayani anapewa heshima iliyopitiliza tena hasa kama ni kiongozi au mtu mwenye mafanikio kimaisha (wahaya wanaelewa ninachozungumza) na hivyo hawatamruhusi kamwe kukaa kama wanavyokaa wao Wala kula wanachokula wao, watamwandalia kila kitu chake Cha tofauti, kizuri na kwa heshima na hofu kubwa. Kuna simulizi za zamani kuwa "abakama" yaani machifu wa kihaya walipokwenda mahala kutembea hawakuruhusiwa hata kukanyaga ardhi, walichukiliwa vijana wa kiume na kulala barabarani ambapo wakubwa wale walikanyaga migongo yao kwenda mahala palipoandaliwa kutoa hotuba. Kama Hilo halitoshi, wakati wa hotuba simulizi zinasema Omkama alisimika mkuki wake kwa kuuchoma kwenye mguu wa kijana ambaye badae alipewa ng'ombe na mke mzuri.
Unachanganya mambo...

Hapo walikuwa kanisani. Hawakwenda kwenye tukio la kiutamaduni wa asili ya kihaya. Kama walikwenda kwenye tukio la namna hiyo, basi maoni yako yana apply, kinyume chake... HAPANA...!

Kanisa la Yesu Kristo halishikamani na mila na desturi za kienyeji ambazo mara zote huhusisha kuabudu miungu mingine...

Ndani ya kanisa tuna mila moja tu. Kumwabudu Mungu wa kweli katika Kristo YESU...
Hata hivyo, hoja yangu inapata maana kama vile viti viliandaliwa na kanisa kwani viongozi na waamini wengi wa bukoba karibu wote ni wahaya. Kama ni viongozi wa mkoa wakiongozwa na mkuu wa mkoa kwamba ndo waliomba walete viti maalum kwa ajiri ya viongozi wakuu wa kitaifa, kanisa lisingeweza kukataa maana ibada haiwezi kuathirika kwa namna yoyote Ile, sasa labda kama ni hoja ya uchawa, itakua kwa hao waliovileta.
Kwa muumini wa kweli anayemjua Mungu aliyekwenda kumwabudu, hawezi kukubali kukwezwa kiasi cha yeye kujiona ni maalumu sana mbele za Mungu kwamba atadhani yeye atapata special treatment kuliko waumini wengine. Ni UONGO na wamejidanganya nafsi zao...!

Biblia (Neno la Mungu) linasema; "...ajikwezaye atadhiliwa na ajidhiriye atakwezwa...!!"
Nakuhakikishia jambo moja, kuwa, hao bila kukujali situation ya tendo lao, basi ndugu zetu hao kwa kujikweza kwao huko, basi wameshadhiliwa tayari unless watambue kosa lao na kutengeneza...!

By the way, kwa tendo lao hilo, wameonesha mfano mbaya kwa waumini ambao ndiyo wananchi wao wanawaongoza..!
Mimi hata hivyo bado nampongeza mama kwa kushiriki ibada ile na kukubali kuingia kanisani na kufuata matendo yote ya ibada ya kikristo, zamani ilikua kama raisi sio mkristo, ibada ziliandaliwa nje ya kanisa...huu ni unyenyekevu wa aina yake unapaswa kupongezwa sio tuangalie mambo madogo madogo yasiyokua na maana.
Kwa pongezi, it's okay..hakuna shida..

Lakini tendo lake hilo limeingia kasoro kubwa kwa namna alivyoshiriki kwa kuonyesha kuwa she is more special than all other people ndani ya nyumba ya ibada...!

That's bad example for a president...

Yesu KRISTO mfano wa viongozi wote hakuwa na tabia hii ya kupenda kukwezwa kwezwa kama walivyokuwa mafarisayo...!
Mkisema mbona kiongozi fulani alikua anaenda msikitini wakati ni mkristo, mkumbuke wakristo hawana katazo la moja kwa moja kwenda nyumba za ibada za wengine kama ndugu zao wale, kwa hiyo mama mpaka anakaa pale mbele na kusikiliza mahubiri ya askofu kilaini ujue amevuka vihunzi vingi sana., mama mitano tena.
Hili wala siyo ishu hapa..

Lakini uzuri ni huu, kwamba, kwa Mungu LANGO LA KUINGILIA ILI KUMUONA NI MOJA TU - Yesu Kristo iwe kwa masikini na matajiri, wenye vyeo na wasio na vyeo, wazungu kwa waafrika, wasomi kwa wasio soma nk nk...

Laiti viongozi wetu hawa wangetambua hili, wangejishusha na kujinyenyekeza mbele za Mungu badala ya kujikweza walivyofanya...!

Asante..
 
Queen+Duke+Edinburgh+Visit+St+Columba+Church+ip-afaxjhe-x.jpg

Waumini wote kanisani tunakalia mabenchi ya mbao

Hata wafalme na malkia wa himaya zilizotawala dunia wanajinyenyekeza mbele za Mungu
Vipi mapadre na maaskofu wao wanakalia mabenchi? Kujinyeyekeza kwa Mungu?
 
Samia ni Askofu ?
Hivi kwa nini kipindi cha sadaka mnataka kila mtu atoe sadaka hata kama sio mkatoliki lakini ikifika saa ya mlo wa sakramenti mnataka wakatoliki tu ndio wale baada ya kuchukua pesa na wakatoliki wenyewe hamuwapi mlo kamili wa mkate na divai anakula wenyewe maaskofu na mapadre mkate na divai na waumini wengine kuwapa mkate tu wameze na mate?
 
Hivi kwa nini kipindi cha sadaka mnataka kila mtu atoe sadaka hata kama sio mkatoliki lakini ikifika saa ya mlo wa sakramenti mnataka wakatoliki tu ndio wale baada ya kuchukua pesa na wakatoliki wenyewe hamuwapi mlo kamili wa mkate na divai anakula wenyewe maaskofu na mapadre mkate na divai na waumini wengine kuwapa mkate tu wameze na mate?
Umeenda kwenye mikate na divai na sadaka za wakatoliki...
Total waste of time... enjoy the rest of your day
 
Wewe hupaswi kuwalaumu hao viongozi moja kwa moja.

Erythrocyte!
Umeandika as if walikuja wamebeba viti vyao,wakati ukweli ni kwamba kama ni kasoro imetokea.na kama ni kulaumiwa ni hao waliokuwa na jukumu la maandalizi na sidhani kama ni maagizo ya Mheshimiwa Rais wala Makamu wake.
Wao wameingia na kuelekezwa mahali walipoandaliwa kukaa.

Baadhi ya vitu sio lazima uvipinge kwa sababu havina tija kwa maendeleo chanya wala havitowi fundisho lolote kwa jamii.
Pia kuwa pingapinga sio alama ya elimu bali ni dalili za ubishi usio na tija pia.

Rais akipanda basi mnasema kadharauliwa,je kipi afanye ili awafurahishe?

Mtaendeleza bifu la kukaa benchi mpaka 2025?

Si mtafika mmechoka Sana?

Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe.
Sitaongelea kingine zaidi hapo uliposema wameletewa na kuandaliwa. Kwenye macho ya wengi au kikawaida inaleta picha kwamba wao ndio walioamua iwe hivyo. Vinginevyo wao walipaswa kujiweka sawa na waumini waumini wengine kwa kuagiza visogezwe pembeni na waa kutumia kama vya waumini wengine. Wangejipatia credit sana kuliko haya maswali
 
Queen+Duke+Edinburgh+Visit+St+Columba+Church+ip-afaxjhe-x.jpg

Waumini wote kanisani tunakalia mabenchi ya mbao

Hata wafalme na malkia wa himaya zilizotawala dunia wanajinyenyekeza mbele za Mungu

Japo wanaweza kutandika makochi ya ngozi na sufi kanisa zima lakini wanajishusha mbele ya madhabahu ya Mungu kwa sababu wanajua hata Yesu Kristo alizaliwa kwenye josho la kulishia ng'ombe akiwa ni mtoto wa muweza wa yote.
Mnaweza kukufuru huko mnapoelekea na hizi hoja zenu za kulazimisha. Kwamba Samia kwenda na kiti cha rais mle kazini tayari amejikweza kwa Mungu!!.

Mungu anaangalia moyo wako hatazami muonekano wako wa nje upo vipi. Unaweza kupotea mazima kama unajihesabia haki ukijiona upo njia iliyonyooka kumbe umeshatumbukia shimoni.
 
Hivi kwa nini kipindi cha sadaka mnataka kila mtu atoe sadaka hata kama sio mkatoliki lakini ikifika saa ya mlo wa sakramenti mnataka wakatoliki tu ndio wale baada ya kuchukua pesa na wakatoliki wenyewe hamuwapi mlo kamili wa mkate na divai anakula wenyewe maaskofu na mapadre mkate na divai na waumini wengine kuwapa mkate tu wameze na mate?
Kuweza kuyaelewa haya ondoka huko ulipo karibu katika ukatoliki kwa mikono miwili. Utapewa shule ya kina.
 
Mm nimeona ni vema sehemu ya ibada ikaheshimiwa na lakin vilevile ulinzi Wa Rais ni muhimu.Binadamu wote ni sawa Kwa MUNGU,ila kimahitaji sisawa,ndio maana Kuna anayewaza atakula nn,na mwingine anawaza atakufa lini🤪🤪🤪🤪🤪🤪
 
Back
Top Bottom