Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Wafanyabiashara wa mikoani mnaochukua vitu Kariakoo, njooni tujuzane machimbo ya bidhaa

Madela jmn bei ya jumla wanakouza chee msaada plz nimepita mbagala reja reja 6000 hadi 10,000 bei ya jumla sijauliza, wap naweza pata msaada?
 
Ngoja nikupe machimbo best. Kizuri kula na mwenzio. Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule Mnazi Mmoja wengi wanaouza Kariakoo wanaenda kufuata huko. Viatu navyo vinapatikana huu Mtaa wa Narung'ombe na Congo pale nenda straight kwenye maduka ya Wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini, nop. Unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile vi-sandles wanauza 2500/pc. Cheni zama Mchikichi katikati kuna Mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki. Magauni nayo ingia ndanindani kule Congo na Aggrey, wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka ku-type ah!

Well done! Vipi kwa wanunuzi wa spare za magari
 
Tafta hela uende china. Kuna masoko yao kule vitu bei cheap kweli. Kuna vijana walianza kdgo kdgo tu this day wanafanya vizuri kweli. Just know ur niche.

Vitu vingine in china the prices are lower kuliko hata hapo Kariakoo.
China shida ni mtaji mkuu
Kiasi gani unaweza kuanza
 
Mi kuna machinga nilikuwa nachukua mzigo kwake,hivyo nampa pesa ye anazunguka kwenda kuchukua mzigo.Ukimuuliza asemi,siku nilienda na vijana wangu watatu ambapo yeye hakuwaona.Hivyo nilivyomkabidhi pesa akaondoka,vijana wangu wakamfuatilia mpaka wakajua maduka yote aliyoingia.Tangia siku hiyo hajaniona na majamaa wa madukani washanizoea hats bila pesa wananipa mzigo au wanatuma mkoani.
Siku zote lazima utumie pesa na akili ili kupata pesa nyingi
 
Kuna shipping agents wanaokutumia vitu vyako huku bongo na kukutolea bandarini (door to door)....Kama Silent Ocean na wengine.

Mzigo Unaulipia charges kwa cbm (cubic meters) inategemea na aina ha bidhaa hyo ina include shipping, agency na taxes. Ila kikubwa ukifika kule inakua na nguvu zaidi unaweza chagua bidhaa unayotaka hata ku negotiate price na wachina masokoni kwao face to face. The more unanunua mzigo kwingi the more discount u get hence the more profit u get ukija uza huku.

Ili umake good money kweli uone unapiga hela kweli uwe na kitu kama 10 M hivi hyo mzgo tu. (Unaweza ukaanza less than that ila mimi naona kuanzia 10 M kuendelea ndio kweli naweza nikasema huyu mtu ana make hela)

mtoto1980

I posted this before.
 
Ngoja nikupe machimbo best. Kizuri kula na mwenzio. Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule Mnazi Mmoja wengi wanaouza Kariakoo wanaenda kufuata huko. Viatu navyo vinapatikana huu Mtaa wa Narung'ombe na Congo pale nenda straight kwenye maduka ya Wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini, nop. Unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile vi-sandles wanauza 2500/pc. Cheni zama Mchikichi katikati kuna Mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki. Magauni nayo ingia ndanindani kule Congo na Aggrey, wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka ku-type ah!
Ubarikiwe kwa roho yako nzuri. Vitambaa vya kushona je?
 
Well done bro! Vipi kwa wanunuzi wa spare za magari
Kama ni Used vifaa vinapatikana karibu na stand ya mwendokasi gerezani..but kwa original ni mtaa wa msimbaz ukitokea fire ila kwa hapa sijui chimbo lake exactly maana vifaa vya magari viko very complicated but kama ulikua ujui kabsa wanapouzia unaweza kucheki hayo maeneo niliyokutajia.
 
Nimepata maswali mengi pm nijibu tu hapa kwa faida ya wengi sababu wengi wao ni wanataka kuanza biashara

Aina ya biashara
Fanya utafiti juu ya biashara unayotaka kufanya like km uko dar tembelea maeneo hata hapo kkoo jifunze vitu vidogo mf unataka kuuza nguo za watoto ziko design nyingi kuna ronya quality kidogo, quality ya Kati na ile quality kabisa pita madukani jifanye kuuliza hata bei soma lebo baada ya muda utajua kutofautisha. hii itakusaidia unaponunua ununue bidhaa inayoenda na pesa na isikupe tabu katika soko lako.

Aina ya wateja
Chagua aina ya wateja wako like maskini, hali ya Kati au matajiri!! Hii itakusaidia kujua watu unaodeal nao na hapo juu umeshapita kuangalia quality na bei sababu kila bei na quality ya nguo ina kundi lake katika Jamii

Location
Location ni muhimu sababu kila kundi katika
Jamii linapatikana sehemu husika so chagua kundi linaloendana na mazingira husika.

Aina za nguo
Kuna aina nyingi za nguo unaweza chagua aina unayotaka Kama vile nguo za watoto kipato cha Kati, nguo za heshima kipato cha Kati, nguo za kimalaya kipato cha Kati... Hii itakusaidia kupata kundi moja kwa wakati mmoja na kwa bei zinazolingana ina maana mteja akija kwako hatoki kirahisi..

Anza biashara
Ukifanya hizo key point kiufasaha anza biashara yako hutapata shida yoyote..

Mtaji.
Wengi wameniuliza kuhusu mtaji sh ngapi
Kwa mie mtaji ni pesa yoyote uliyo nayo as long as unahitaji kuingia kwenye kufanya biashara na si kujaribu biashara.

Mf
Mi nilikosa mtaji kabisa ilikua mwaka 2013 Oct na nilianza na laki na nusu na mzigo wangu wa Kwanza kufunga hapo kkoo ilikua urembo cheni, hereni, bangili na lipsick na huo mzigo niliuza kwa kutembeza na ulizaa 375000 na kupitia huo mzigo nikipata oda nyingi sana za nguo... Kwa pesa hio hio ilinilazimu nitumie usafiri wa kutoka moja kati ya wilaya za mpkani mwa tz mpk dar

Hapo nimetoa mfano tu wa mliouliza kuhusu mtaji.. Anza na ulichonacho kwa mfanyabiashara hakuna hela ndogo.
Muhimu fanya utafiti hata kama umeelekezwa kabla ya kununua fanya utafiti wewe mwenyewe iwe kkoo,, Uganda au nairobi.

Kwa Wale mlioniuliza pm naona nimewajibu
wote kwani kujibu mmoja mmoja siwezi..
 
Jaman mm naomba kujua chimbo la stationeries za jumla na za ukweli, hawa ninao wanasema wanauza jumla inaonekana wanatoa duka la 3 au 4, Stationery nina maana ya vifaa mbalimbali vya maofisini yaan pen, daftari, ream nk.ukinipa no.utakuwa umenisaidia sana. Shukrani
 
Nimepata maswali mengi pm nijibu tu hapa kwa faida ya wengi sababu wengi wao ni wanataka kuanza biashara

Aina ya biashara
Fanya utafiti juu ya biashara unayotaka kufanya like km uko dar tembelea maeneo hata hapo kkoo jifunze vitu vidogo mf unataka kuuza nguo za watoto ziko design nyingi kuna ronya quality kidogo, quality ya Kati na ile quality kabisa pita madukani jifanye kuuliza hata bei soma lebo baada ya muda utajua kutofautisha. hii itakusaidia unaponunua ununue bidhaa inayoenda na pesa na isikupe tabu katika soko lako.

Aina ya wateja
Chagua aina ya wateja wako like maskini, hali ya Kati au matajiri!! Hii itakusaidia kujua watu unaodeal nao na hapo juu umeshapita kuangalia quality na bei sababu kila bei na quality ya nguo ina kundi lake katika Jamii

Location
Location ni muhimu sababu kila kundi katika
Jamii linapatikana sehemu husika so chagua kundi linaloendana na mazingira husika.

Aina za nguo
Kuna aina nyingi za nguo unaweza chagua aina unayotaka Kama vile nguo za watoto kipato cha Kati, nguo za heshima kipato cha Kati, nguo za kimalaya kipato cha Kati... Hii itakusaidia kupata kundi moja kwa wakati mmoja na kwa bei zinazolingana ina maana mteja akija kwako hatoki kirahisi..

Anza biashara
Ukifanya hizo key point kiufasaha anza biashara yako hutapata shida yoyote..

Mtaji.
Wengi wameniuliza kuhusu mtaji sh ngapi
Kwa mie mtaji ni pesa yoyote uliyo nayo as long as unahitaji kuingia kwenye kufanya biashara na si kujaribu biashara.

Mf
Mi nilikosa mtaji kabisa ilikua mwaka 2013 Oct na nilianza na laki na nusu na mzigo wangu wa Kwanza kufunga hapo kkoo ilikua urembo cheni, hereni, bangili na lipsick na huo mzigo niliuza kwa kutembeza na ulizaa 375000 na kupitia huo mzigo nikipata oda nyingi sana za nguo... Kwa pesa hio hio ilinilazimu nitumie usafiri wa kutoka moja kati ya wilaya za mpkani mwa tz mpk dar

Hapo nimetoa mfano tu wa mliouliza kuhusu mtaji.. Anza na ulichonacho kwa mfanyabiashara hakuna hela ndogo.
Muhimu fanya utafiti hata kama umeelekezwa kabla ya kununua fanya utafiti wewe mwenyewe iwe kkoo,, Uganda au nairobi.

Kwa Wale mlioniuliza pm naona nimewajibu
wote kwani kujibu mmoja mmoja siwezi..
gooooooooooooooooooood hapa nimejifunza jambo leo ninna oda kibao kuna nilichojifunza
 
Hivi Karibuni kampuni yetu itaanzisha Huduma za kuwatafutia wafanyabiashara wa mikoani bidhaa wanazohitaji hapa DSM, au nje ya nchi. Tutachukua oda zenu, tutawapa bei, mtatuma pesa, tutanunua na kuwasafirishia mlipo. Tutawatoza ada kidogo tofauti na gharama ungezitumia kuna DSM na kurudi. Stay tuned!
Hapo 'mtatuma pesa' ndo pana ukakasi !
 
Back
Top Bottom