Wafanyabiashara walioporwa mabilioni na Mwendazake kurejeshewa fedha hizo na Rais Samia

Wafanyabiashara walioporwa mabilioni na Mwendazake kurejeshewa fedha hizo na Rais Samia

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Naingia kwenye mada moja kwa moja. Leo katika kipindi cha uchambuzi wa magazeti kupitia redio ya Wasafi FM, imeelezwa kwamba wale wafanyabiashara walioporwa mabilioni ya fedha na kikosi kazi kilichoundwa na Mwendazake, sasa watarudishiwa fedha zao rasmi. Hii ni moja ya hatua za kuponya maumivu na uharibifu uliofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake.

Katika taarifa hiyo, imeelezwa yupo mfanyabiashara mmoja aliyeporwa jumla ya Tsh 3.5 bilion na kumpelekea kufilisika kibiashara. Mh mama Samia hataki kuongoza nchi yenye watu waliopondeka mioyo kutokana na kunyanyaswa na serikali iliyopita. Ndio maana anafanya jitihada zote kuhakikisha anatibu majeraha na makovu yote yaliyosababishwa na serikali iliyopita ili nchi isonge mbele bila kinyongo.

MAONI YANGU
Namkubali sana Mh mama Samia kwa ujasiri wake huu ijapokuwa kuna baadhi ya wanaCCM hawapendi kuona watanzania wenzao wakiishi maisha bora katika nchi hii. Sote ni mashahidi jinsi wafanyabishara walivyokuwa wakiporwa fedha na akina Sabaya na Makonda (wateule wa Mwendazake) bila kuchukuliwa hatua zozote, hadi baadhi ya wafanyabiashara wakaamua kuikimbia nchi. Ukweli wa jambo hili umeanza kudhihirika wazi baada ya baadhi ya wafanyabiashara kuwafungulia mashataka wahalifu hawa wawili waliokuwa vipenzi wa Mwnedazake.

Nawasilisha.
 
Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!

Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?

Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
 
Zilienda wapi hizo ela?isije ikawa walikula wengine ,alafu Kodi za wa wananchi wavuja jasho ndio ziwalipe
Wale task force walikuwa wakija wanavunja kwanza camera..

Kisha wanachukua hela zote.. Kisha nusu ya hela wanagawana wao wenyewe..

Nusu inayobaki wanapeleka BOT.. Kisha BOT wanampa taarifa Jiwe kwamba tuna kiasi gani fedha kilichopatikana..

Jiwe akipata taarifa anafurahi sana anaandaa ziara.. Kisha utasikia NCHI HII NI TAJIRI SANA
Kuna watu walitajirika sana kwa mfumo Jiwe..

Kama ni kurudisha sijui watawarudishiaje... Ni mtihani sana
 
Hizo hela anazorudisha anazitoa wapi?.

Na hizo hela zilizoporwa zilikwenda wapi?.
Swali la msingi sana hili, kwasababu mwanzo ilisemekana zile fedha zililiwa na mwendazake na waliokuwa watu wake wa karibu.

Sasa Samia na serikali yake anazitoa wapi hizo fedha za kuwarudishia hawa watu walioporwa, atakwenda kuwachotea hazina pesa za walipakodi? au atafanyaje, haya maswali lazima kwanza yajibiwe kabla hatujaanza kupongeza huruma ya Rais, kwani tunaishi kwenye utawala wa sheria, na sio wa hisia.

Japo kuwarudishia ni haki yao, lakini asijekutoa haki hiyo kwa kuwanyan'ganya wengine, nae atakuwa ni mporaji tu kama mwendazake, hata kama serikali ya CCM imezoea kuchezea kodi zetu.

Vinginevyo tuambiwe ukweli, kama hizo pesa zilikuwepo hazikutafunwa na mwendazake kama ilivyowahi kusemekana, pia ijulikane wazi; au kama zilitumika kununua wapinzani kwa manufaa ya CCM, basi CCM wenyewe wajue namna ya kuzirudisha kwa wenyewe.
 
Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!
Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?
Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
Enzi za kambale kuna mahakama yoyote ingeweza kukubali kupokea mashtaki ya serikali na chawa wake? Umesahau watu walikua wanajisifu kuua hadaharani na wengine waliua na hakuna ahatua yoyote iliyochukuliwa,,ushahaidi hadi wa video lakini bado walikua na nguvu...

Mkuu watu pekee waliokua na nguvu ya kusimama na kupambana na bwana Jiwe alikua Tundu lissu na Ben 8 peke yao na nadhani unakumbuka kilichowapata.
 
Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!
Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?
Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
niongeze na mimi tuwe wawili kwenye kuamini mwishoni kuwa walionewa.
 
Back
Top Bottom