Wafanyabiashara walioporwa mabilioni na Mwendazake kurejeshewa fedha hizo na Rais Samia

Wafanyabiashara walioporwa mabilioni na Mwendazake kurejeshewa fedha hizo na Rais Samia

Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!
Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?
Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
Umeshaamka kutoka kwenye usingizi mzito? Au ulikuwa nje ya nchi na hukuwa na muda wa kusoma mambo yaliyokuwa yanatokea humu nchini

Hivi umesahau kwamba Mo alitekwa nyara na jamaa zaake wakatangaza dau la bilioni moja na nusu pale atakapopatikan? Ule mchezo wa kuigiza?

Kama ni kweli walikwepa (na inawezekana sana) kwa nini hakuna ofisa wa TRA aliyepelekwa mahakamani kwa kusaidia au kuruhusu ukwepaji huo wa kodi?
 
Hakuna mtu aliporwa, hao ni wapiga dili haramu na wakwepa kodi kwa mgongo wa vigogo waliokuwa nyuma yao na walipata kile walichostahili kupata, ndomana hutawasikia wakitoka hadharani kuyasema Haya.

Mambo mengine ni mazito yangewekwa hadharani kuna watu husingewaheshimu tena,

Pia kila nchi unayoijua wewe sio kila jambo linapatiwa ufumbuzi mahakamani, zipo njia mbadala ambazo zimetumika kwa watu wengi tu ulimwenguni yakiwemo mauaji, kunyang'anya mali n.k
 
Enzi za kambale kuna mahakama yoyote ingeweza kukubali kupokea mashtaki ya serikali na chawa wake? Umesahau watu walikua wanajisifu kuua hadaharani na wengine waliua na hakuna ahatua yoyote iliyochukuliwa,,ushahaidi hadi wa video lakini bado walikua na nguvu...

Mkuu watu pekee waliokua na nguvu ya kusimama na kupambana na bwana Jiwe alikua Tundu lissu na Ben 8 peke yao na nadhani unakumbuka kilichowapata.
As'habu l'kahfi hao wamelala usingizi wa miaka mia tatu.
 
Zilienda wapi hizo hela? Isije ikawa walikula wengine halafu Kodi za wa wananchi wavuja jasho ndio ziwalipe
Hizo fedha zilijenga uwanja wa ndege Chato, Kivuko cha wasafiri Chato, ndege za serikali Chato, mbuga ya wanyama Chato, hospitali ya rufaa Chato, VETA chato na barabara za Chato. Ijapokuwa hizi fedha zilinufaisha kikundi kidogo cha wananchi, afadhali ilmradi zilitumika hapa nchini.
 
Mh, ni jambo jema lakini hayo asiyafanye kama yeye hakuwemo kwenye ile serikali na yeye alikuwemo na alishiriki
Yes; alikuwemo kwenye serikali lakini mabaya mengi yaliyofanywa na mwendazake yeye hakuhusika. Ndio maana ameamua kuwarejeshea fedha wafanyabiashara, kuwalipa mafao wafanyakazi wa vyeti feki na kumfunga jambazi Sabaya. Hivi ni viashiria tosha kwamba yeye hakuwa mmoja wa watenda maovu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
Hakuna mtu aliporwa, hao ni wapiga dili haramu na wakwepa kodi kwa mgongo wa vigogo waliokuwa nyuma yao na walipata kile walichostahili kupata, ndomana hutawasikia wakitoka hadharani kuyasema Haya.

Mambo mengine ni mazito yangewekwa hadharani kuna watu husingewaheshimu tena,

Pia kila nchi unayoijua wewe sio kila jambo linapatiwa ufumbuzi mahakamani, zipo njia mbadala ambazo zimetumika kwa watu wengi tu ulimwenguni yakiwemo mauaji, kunyang'anya mali n.k
Walikwapuliwa Tsh ngapi? Wanarudishiwa Tsh ngapi? Tutajuaje kuwa kiasi kinachorudishwa ndicho kilichokwapuliwa? Raisi asiyefata taratibu za nchi yake lazima alete maafa mbeleni.

Hata kama ni kweli walikwepa kodi, nani alithibitisha hilo? JPM? Moja ya udhaifu mkubwa wa serikali ya awamu ya 5 ni kupuuza taratibu na sheria tulizojiwekea kama nchi. Na haya ndo matokeo yake, watu wanaweza tumia mwanya pakafanyika ufisadi.

Mtu kakwepa kodi, badala ya kushtakiwa kisha mahakama imuhukumu unakwapua pesa zake.

Mahakama ingetoa hukumu kwa mujibu wa sheria, huo ndo utaratibu tunatakiwa kuufata. Kiongozi wa juu wa nchi alipaswa kuufata, kama walionewa mahakama leo ingethibitisha hilo, pesa zingejulikana ni kiasi gani, na kiasi cha fidia kingekuwa wazi.
 
Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!

Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?

Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja. Leo katika kipindi cha uchambuzi wa magazeti kupitia redio ya Wasafi FM, imeelezwa kwamba wale wafanyabiashara walioporwa mabilioni ya fedha na kikosi kazi kilichoundwa na Mwendazake, sasa watarudishiwa fedha zao rasmi. Hii ni moja ya hatua za kuponya maumivu na uharibifu uliofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake.

Katika taarifa hiyo, imeelezwa yupo mfanyabiashara mmoja aliyeporwa jumla ya Tsh 3.5 bilion na kumpelekea kufilisika kibiashara. Mh mama Samia hataki kuongoza nchi yenye watu waliopondeka mioyo kutokana na kunyanyaswa na serikali iliyopita. Ndio maana anafanya jitihada zote kuhakikisha anatibu majeraha na makovu yote yaliyosababishwa na serikali iliyopita ili nchi isonge mbele bila kinyongo.

MAONI YANGU
Namkubali sana Mh mama Samia kwa ujasiri wake huu ijapokuwa kuna baadhi ya wanaCCM hawapendi kuona watanzania wenzao wakiishi maisha bora katika nchi hii. Sote ni mashahidi jinsi wafanyabishara walivyokuwa wakiporwa fedha na akina Sabaya na Makonda (wateule wa Mwendazake) bila kuchukuliwa hatua zozote, hadi baadhi ya wafanyabiashara wakaamua kuikimbia nchi. Ukweli wa jambo hili umeanza kudhihirika wazi baada ya baadhi ya wafanyabiashara kuwafungulia mashataka wahalifu hawa wawili waliokuwa vipenzi wa Mwnedazake.

Nawasilisha.
Watakwambia Mwendazake alitenda wema akaenda zake 😁😁
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja. Leo katika kipindi cha uchambuzi wa magazeti kupitia redio ya Wasafi FM, imeelezwa kwamba wale wafanyabiashara walioporwa mabilioni ya fedha na kikosi kazi kilichoundwa na Mwendazake, sasa watarudishiwa fedha zao rasmi. Hii ni moja ya hatua za kuponya maumivu na uharibifu uliofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake.

Katika taarifa hiyo, imeelezwa yupo mfanyabiashara mmoja aliyeporwa jumla ya Tsh 3.5 bilion na kumpelekea kufilisika kibiashara. Mh mama Samia hataki kuongoza nchi yenye watu waliopondeka mioyo kutokana na kunyanyaswa na serikali iliyopita. Ndio maana anafanya jitihada zote kuhakikisha anatibu majeraha na makovu yote yaliyosababishwa na serikali iliyopita ili nchi isonge mbele bila kinyongo.

MAONI YANGU
Namkubali sana Mh mama Samia kwa ujasiri wake huu ijapokuwa kuna baadhi ya wanaCCM hawapendi kuona watanzania wenzao wakiishi maisha bora katika nchi hii. Sote ni mashahidi jinsi wafanyabishara walivyokuwa wakiporwa fedha na akina Sabaya na Makonda (wateule wa Mwendazake) bila kuchukuliwa hatua zozote, hadi baadhi ya wafanyabiashara wakaamua kuikimbia nchi. Ukweli wa jambo hili umeanza kudhihirika wazi baada ya baadhi ya wafanyabiashara kuwafungulia mashataka wahalifu hawa wawili waliokuwa vipenzi wa Mwnedazake.

Nawasilisha.
Waliokula hizo Pesa ndio warudishe sio Kodi yetu itumike kuwa refund,sio sawa.
 
Hakuna mtu aliporwa, hao ni wapiga dili haramu na wakwepa kodi kwa mgongo wa vigogo waliokuwa nyuma yao na walipata kile walichostahili kupata, ndomana hutawasikia wakitoka hadharani kuyasema Haya.

Mambo mengine ni mazito yangewekwa hadharani kuna watu husingewaheshimu tena,

Pia kila nchi unayoijua wewe sio kila jambo linapatiwa ufumbuzi mahakamani, zipo njia mbadala ambazo zimetumika kwa watu wengi tu ulimwenguni yakiwemo mauaji, kunyang'anya mali n.k
 
Hivi inamaana waliteuliwa tu baadhi ya wafanyabiashara alafu wakaporwa fedha zao na wengine kama Bakhresa na Mo Dewji wakaachwa ili hali ndiyo mabilionea wakubwa!!

Hii inaingia akilini kweli?mimi naamini wengi wapiobananishwa ni wakwepa Kodi wazuri na vilevile kama kweli walinyang'anywa Mali yao halali mbona hawakuishitaki serikali mahakamani ili warudishiwe Mali zao walizochuma kihalali?

Bado nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa walionewa!!
Ulikuwa unaishi Tanzania au Mars? Unaweza mahitaji Jiwe?
 
Mazito yapi ,Nani asiyemjua Jiwe alikuwa mwongo,katili na ambae alikuwa anasingizia watu?
Hakuna mtu aliporwa, hao ni wapiga dili haramu na wakwepa kodi kwa mgongo wa vigogo waliokuwa nyuma yao na walipata kile walichostahili kupata, ndomana hutawasikia wakitoka hadharani kuyasema Haya.

Mambo mengine ni mazito yangewekwa hadharani kuna watu husingewaheshimu tena,

Pia kila nchi unayoijua wewe sio kila jambo linapatiwa ufumbuzi mahakamani, zipo njia mbadala ambazo zimetumika kwa watu wengi tu ulimwenguni yakiwemo mauaji, kunyang'anya mali n.k
 
Back
Top Bottom