KERO Wafanyabiashara ya chakula acheni kurudisha mabaki

KERO Wafanyabiashara ya chakula acheni kurudisha mabaki

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kuna wauza chips zaidi ya mmoja nimewashuhudia wakiulizwa chips ni za moto basi wao wanazipima joto kwa mkono nyuma ya kiganja ...tatizo wengi ya wauza chips ni watu washamba wa vijijini wana tabia za uchafu wa asili wanashindwa kujua jema na baya.
Nimewahi kuona muuza juice anachokonoa sikio halafu akaenda kukata matunda ya kuweka kwenye blender kutengeneza juice bila hata kunawa mikono.
 
Hizi adha tunakutana nazo sana sisi bachelor sana sana.

Mfano kuna kihoteli kimoja ni hapa mtaani niliweka oda ya chakula mchana na usiku nikawapatia na hotpot langu special kwaajir ya kuweka chakula changu pekee.

Picha linaanza siku ya kwanza mchana naletewa chakula mfuniko wa hotpot una alama alama ya vidole vya maji machafu, nikajifariji ni mfuniko pekee, ile nimemaliza kula tu tumbo likaanza kuunguruma nikajifariji labda maji ya kunywa.

Kesho tumbo likanisumbua nikafahamu ni madonda tumbo yameamka maana huwa nina tatizo hilo nikapotezea ila nikatoa ahadi jioni nitaenda kufuata chakula mwenyewe nijionee uandaaji hadi uhifadhi wa chakula.

Jioni nimefika eneo la tukio, kwanza hotpot langu limetupwa chini hapo kuanzia mchana halikuoshwa linasubilia mida ya chakula ndipo lioshwe.

Basi nikawaambia waniandalie chakula changu niondoke ile hotpot limechukuliwa likasuuzwa kwenye maji flani yalikuwa yameisha badili rangi na kuanza kuwa ya brown kisha kukung'utwa na kuwekewa chakula mfuniko wake, kwa vile yule mdada alikuwa busy kuweka chakula akamuomba boda boda mmoja amsaidie kuuosha aiseee 🤧🤧🤧

Yaani nilishikwa na hasira haswa isingekuwa na utu rohoni siku hiyo tungetukanana nikasogea pembeni kidogo na kuwaacha waendelee ya uchafu wao....

Nilivyotoka hapo aiseee ......
Pole mkuuni uchafu uliopitiliza halafu wenyewe hawajali,hawajistukii
 
Juzi kati nilikuwa mgahawa Fulani nikabakiza chapati na ilikuwa ya mwisho. Mteja akapiga simu akaambiwa imebaki moja, nikaashangaa ila nikauchuna tu.
Usikute hata ulizokula zilibakishwa na mwingine na wewe ukabakisha moja ikanunuliwa na mteja wa tatu.
 
Kuna hii tabia ya kurudisha mabaki ya mteja kwenye chakula Kwa wafanyabiashara hasa wa maeneo ya kawaida japo huwa hatuoni ila utakutana nayo tu.

Juzi Kuna mtu kasema aliwahi shuhudia mama ntilie anarudisha mchuzi uliobakishwa na mteja kwenye sufuria ya mboga nikakumbuka visa vyangu, silagi Kwa mama ntilie ila chips haziepukiki.

Pia soma: Huwa unakagua usafi sehemu unayoenda kupata chakula?

Eneo la kwanza ni Mikocheni karibu na hospital kubwa sana, wakati nakula chips mayai kufungua katikati nakuta nzi wamenasa ilibidi njikaze tu kuwaondoa nsije tupa chakula na nna njaa.

Eneo la pili Ubungo mitaa ya hosteli ndanindani kwenye hotel kama nyota tatu, nikiwa na rafiki ikaagizwa chips mayai na nyama, wakati nakula katikati nakuta mifupa midogomidogo ya kuku ilikwishaliwa liwa imenasia, na pieces za kabichi, means mteja akibakisha wao wanatoa kile kilichobaki wanarudisha kwenye kisafi wanachanganya.

Juzijuzi Tena Niko Magomeni, kwenye chips tu pembeni ya main Rosa, chips mayai nakula katikati nashangaa naona ugumu kufosi naibuka na toothpick kama tatu zimelala katikati ya mayai. nkitafuta nakuata vipande vya nyama.

Sijawahi kutana na haya mambo mtaani kwetu ila maeneo yenye biashara ndo nakutana nayo.

Mbona mnatufanyia hivi, imagine mtu unahangaika tangu asubuhi hata kunywa maji hukumbuki, unaamua kupoza tumbo unaletewa vyakula vilivyorudishiwa mabaki?

What if huyo aliekula hapo akabakisha ana maradhi yanayoambukizwa Kwa mate kama hepatitis?
What if akiwa anakula kapiga chafya vikarukia humo?
What if wamewekeana sumu au madawa?

Mteja anatoa pesa kamili Kwa kile anachostahili hata mkimwaga hayo mabaki shida yenu Iko wapi, si unauza kama ulivyoplan? Kwanini mnarisk Maisha ya wengine kutafuta extra profit toka kwenye kilekile mlichozalisha. Mnapata hasara mkimwaga ilhali kishalipiwa?
Mnaua biashara za wengine pia.

Badilikeni!!
Nimeshtushwa sana khaaa
 
Naongezea hapo vyombo pia vinaoshwa na maji machafu sana.
Maji ya kuoshea vyombo hua hayamwagwi, ni hayo hayo kuanzia asubuhi mpaka usiku. Sahani inaoshwa kuondoa ule uchafu kisha inafutwa na kitaulo/kitambaa kichafu mchezo umeisha.
 
Kuna hii tabia ya kurudisha mabaki ya mteja kwenye chakula Kwa wafanyabiashara hasa wa maeneo ya kawaida japo huwa hatuoni ila utakutana nayo tu.

Juzi Kuna mtu kasema aliwahi shuhudia mama ntilie anarudisha mchuzi uliobakishwa na mteja kwenye sufuria ya mboga nikakumbuka visa vyangu, silagi Kwa mama ntilie ila chips haziepukiki.

Pia soma: Huwa unakagua usafi sehemu unayoenda kupata chakula?

Eneo la kwanza ni Mikocheni karibu na hospital kubwa sana, wakati nakula chips mayai kufungua katikati nakuta nzi wamenasa ilibidi njikaze tu kuwaondoa nsije tupa chakula na nna njaa.

Eneo la pili Ubungo mitaa ya hosteli ndanindani kwenye hotel kama nyota tatu, nikiwa na rafiki ikaagizwa chips mayai na nyama, wakati nakula katikati nakuta mifupa midogomidogo ya kuku ilikwishaliwa liwa imenasia, na pieces za kabichi, means mteja akibakisha wao wanatoa kile kilichobaki wanarudisha kwenye kisafi wanachanganya.

Juzijuzi Tena Niko Magomeni, kwenye chips tu pembeni ya main Rosa, chips mayai nakula katikati nashangaa naona ugumu kufosi naibuka na toothpick kama tatu zimelala katikati ya mayai. nkitafuta nakuata vipande vya nyama.

Sijawahi kutana na haya mambo mtaani kwetu ila maeneo yenye biashara ndo nakutana nayo.

Mbona mnatufanyia hivi, imagine mtu unahangaika tangu asubuhi hata kunywa maji hukumbuki, unaamua kupoza tumbo unaletewa vyakula vilivyorudishiwa mabaki?

What if huyo aliekula hapo akabakisha ana maradhi yanayoambukizwa Kwa mate kama hepatitis?
What if akiwa anakula kapiga chafya vikarukia humo?
What if wamewekeana sumu au madawa?

Mteja anatoa pesa kamili Kwa kile anachostahili hata mkimwaga hayo mabaki shida yenu Iko wapi, si unauza kama ulivyoplan? Kwanini mnarisk Maisha ya wengine kutafuta extra profit toka kwenye kilekile mlichozalisha. Mnapata hasara mkimwaga ilhali kishalipiwa?
Mnaua biashara za wengine pia.

Badilikeni!!
Kuna Siku moja nilikuwa natoka Mazinde Juu.. pale Mombo kwenye Nyama Choma (pale magari yanayoenda Arusha na Sehem mbali mbali za Mkoa Wa Kilimanjaro ) yana posi mama nikiwa naagiza Nyama niliona kuna dogo anakusanya mabaki toka kwenyr sahani zilizokuwa na Nyama makombo. Nilifikiri labda wanakusanya for Dogs- niliagiza Mbavu za Mbuzi... walipoleta nyama yote aina ata mfupa mmoja😁 Ugomvi ule uliisha kesho yake baada ya Bwana afya wa Wilaya na Wahusikanwengine kuingilia kati , nilirudishiwa pesa yangu na ilikubalika kuwekwa mbali dust bin ya makombo ... ambalo lilikuwepo pale mpaka upanuzi wa barabara ulipovunja pale ila kwa sasa sijui wanafanyaje. So kuwa makini unapoagiza Nyama choma pale Mombo kabla ya kufika Liverpool Hotel. Pale Same Dogo alinipa Nyama ingine na aliomba msamaha.
 
Back
Top Bottom