Wageni wanapewa vibali vya kununua ardhi Zanzibar na Tanganyika. Mtanganyika hawezi nunua ardhi Zanzibar. Mbona sielewi?

Wageni wanapewa vibali vya kununua ardhi Zanzibar na Tanganyika. Mtanganyika hawezi nunua ardhi Zanzibar. Mbona sielewi?

Hao wageni wananunua ardhi na kufanya uwekezaji kama kujenga hotels, n.k, wewe uje ujenge kijumba chako cha vyumba vitatu huoni kama ni matumizi mabaya ya ardhi, na huko bara mapori bado yapo acha wazenji wapajaze jaze.
Mimi namfahamu demu mmoja wa ufaransa (miaka 32) ni mchepuko wangu na hata sasa bado huwa namnyandua from time to time…Kwa sasa anajenga zenz 3 bedroom house Kwa ajili ya kutunza Mbwa na Paka. Na Ardhi kapewa na huyu unamzungumziaje?
 
Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) imewakabidhi Raia wanne wa kigeni vibali na kadi za utambulisho wa kuishi Zanzibar na Tanzania kwa ujumla baada ya baadhi ya kanuni za uhamiaji kuruhusu Wageni walionunua nyumba Zanzibar zenye thamani ya dola laki moja za Kimarekani ( zaidi ya milioni 250 ) wapewe vitambulisho hivyo vya Makaazi.

Serikali ya Zanzibar ilipendekeza sharti hilo kama kivutio kwa Wageni kununua nyumba Zanzibar ambapo yeyote atayenunua nyumba kwa dola laki moja za Kimarekani ataruhusiwa kukata kibali cha kupata kitambulisho kitakachomtambua kuwa ni Mkaazi wa Zanzibar.

@AyoTV_ imefahamishwa kuwa kitambulisho hicho ambacho kitakua cha matumizi ya muda wa miaka miwili kitatolewa kwa dola 550 (Tsh. milioni 1.4) kwa Wageni kutoka Nchi nyingine huku Wageni kutoka Nchi za Afrika Mashariki wakilipia dola 300 za Kimarekani ( Tsh. 776,851).

Masharti mengine yaliowekwa na Mamlaka ya ZIPA na Uhamiaji ili Mgeni kuupata kitambulisho huo ni uthibitisho wa nyumba iliyonunuliwa kwa dola laki moja, TIN namba ya Mnunuaji wa nyumba hiyo, uthibitisho wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar ZIPA pamoja na uthibitisho kutoka Polisi.

Wageni hawa wanne waliopewa vibali hivyo leo wote ni Raia wa Uholanzi ambapo hii inakua ni mara ya kwanza kutolewa kwa vibali hivyo vya ukaazi Visiwani Zanzibar na vitaendelea kutolewa kwa Wageni wataokidhi vigezo vilivyowekwa. #MillardAyoUPDATES

View attachment 2987134
Hiyo kawaida
 
you will eventually own nothing, so mzungu is more important than tanganyika people. na why zanzibar apewe acceptness hadi bala.



mali asili zetu tunashindwa kuzilinda. for our future generations.


hii corruption ipo wazi
Nyie ndio mnafanya hii nchi iendelee kuwa masikini kwa kuwa ni fikra finyu
 
Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) imewakabidhi Raia wanne wa kigeni vibali na kadi za utambulisho wa kuishi Zanzibar na Tanzania kwa ujumla baada ya baadhi ya kanuni za uhamiaji kuruhusu Wageni walionunua nyumba Zanzibar zenye thamani ya dola laki moja za Kimarekani ( zaidi ya milioni 250 ) wapewe vitambulisho hivyo vya Makaazi.

Serikali ya Zanzibar ilipendekeza sharti hilo kama kivutio kwa Wageni kununua nyumba Zanzibar ambapo yeyote atayenunua nyumba kwa dola laki moja za Kimarekani ataruhusiwa kukata kibali cha kupata kitambulisho kitakachomtambua kuwa ni Mkaazi wa Zanzibar.

@AyoTV_ imefahamishwa kuwa kitambulisho hicho ambacho kitakua cha matumizi ya muda wa miaka miwili kitatolewa kwa dola 550 (Tsh. milioni 1.4) kwa Wageni kutoka Nchi nyingine huku Wageni kutoka Nchi za Afrika Mashariki wakilipia dola 300 za Kimarekani ( Tsh. 776,851).

Masharti mengine yaliowekwa na Mamlaka ya ZIPA na Uhamiaji ili Mgeni kuupata kitambulisho huo ni uthibitisho wa nyumba iliyonunuliwa kwa dola laki moja, TIN namba ya Mnunuaji wa nyumba hiyo, uthibitisho wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar ZIPA pamoja na uthibitisho kutoka Polisi.

Wageni hawa wanne waliopewa vibali hivyo leo wote ni Raia wa Uholanzi ambapo hii inakua ni mara ya kwanza kutolewa kwa vibali hivyo vya ukaazi Visiwani Zanzibar na vitaendelea kutolewa kwa Wageni wataokidhi vigezo vilivyowekwa. #MillardAyoUPDATES

View attachment 2987134
Umewahi fuata hizo taratibu za kununua Ardhi kama wageni ukakataliwa? Ardhi ya Zenj hainunuliwi hovyo kama matembele au kama inavyofanyika Bara.
 
Miradi hii iliyoisha inahihaji wanunuzi kama hao Zanzibar
Location sahihi, mpangilio na sera sahihi zavutia wageni na diaspora kununua nyumba Zanzibar .

1715413519023.png
 
Tanganyika kule Kigamboni walichagua eneo lisilo sahihi mradi huu wa NSSF ungevutia

1715413634911.png

201720 Sept
Mradi mkubwa wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni Dar es Salaam uitwao Dege Eco Village ulioanzishwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii 'NSSF' na kusimama ujenzi wake mwaka 2016 unapigwa mnada.


Kuliripotiwa kuwepo kwa ufisadi wa zaidi ya TSH bilioni 179 katika mradi huo na sasa anatafutwa Mwekezaji atakaeuchukua.
1715415509152.png


View: https://m.youtube.com/watch?v=gmf8Y4ZAY8g
 
Changamoto ya sekta ya Maghorofa ni Kigamboni Dar es Salaam Tanganyika ni miundombinu na mazingira yasiyo na mpangilio ujenzi holela usioona mbali n.k


View: https://m.youtube.com/watch?v=dRrCul3aMlY

9Jan2024
Wakazi wa mbutu mkwanjuni Kigamboni wamelazimika kufunga barabara huku wakishinikiza malori yanayopita katika barabara hiyo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa barabara pamoja na makazi yao kuathiriwa na mashimo yaliyopo katika maeneo hayo sambamba na hilo wameitaka serikali kuingilia kati kutatua changamoto hizo za muda mrefu ambazo wanadai zimekuwa kero na kupelekea kuathiri shughuri zao za kibinadamu....


View: https://m.youtube.com/watch?v=355M5rRSJf0

Magogoni Mikadi Beach Kigamboni wananchi walalamika hakuna mitaro, mitaa watu wanajenga bila mipango ni kama uyoga unajichipukia mwituni maji hayana njia kwenda baharini ...


View: https://m.youtube.com/watch?v=6m22WEKwQWc
 
Watu wabwaga manyanga na kutekeleza majumba ya kifahari Ununio Dar es Salaam yabaki kama mithili ya maghofu ya maruhani (ghost town)


View: https://m.youtube.com/watch?v=7uoirQ2gCtI

16 Dec 2023
In this video I present to you my tour in the Multi-Million Luxurious Abandoned residential house project found in Ununio Kinondoni District Dar es salaam, Tanzania
 
9 December 2023

Breaking Boundaries: Hamidu City Park Kigamboni (Documentary)

Explore the future of urban living in Dar es Salaam, Tanzania, with Hamidu City Park. Join us on a captivating journey through this self-sustaining micro-satellite city.


View: https://m.youtube.com/watch?v=2-isH2fFjUo

1715416897975.png
 
If we want to completely colonize Zanzibar tutumie njia ya Wakatoliki Amerika kusini, tuchukue wanawake wa Kizanzibar

Ukimchukua binti wao automatically unakuwa mmiliki wa Ardhi yake, this is what Spain did to Latin America, vijana wa Kispain walijitwalia wake wa jamii za asili huko Amerika, wakawatawala hadi leo.

Tusilalamike
 
Hawa kina NSSF, Hamidu Park, Bakhresa n.k wangepewa maeneo sahihi ya uwekezaji tungepata miji mipya inayovutia wanunuzi wa ndani na nje, lakini tunawapa kaeneo kadogo mwishowe wanazungukwa na makazi holela.

Miji yote mfano makao makuu Dodoma wangepewa eneo ukubwa wa wilaya nzima ndiyo wilaya hawa waliothubutu kina NSSF, Hamidu City , Bakhresa n.k maeneo hayo makubwa ya miji yetu ingepangika na kuwa ya kisasa badala ya ilivyo sasa.
 
UJENZI WA KUKURUPUKA
CCM waanche kuingilia mambo wasiyoweza, mfano michuano ya Afcon kule Arusha porini Olmothi maeneo yanayozunguka uwanja huo au stendi mpya Bondeni City ungelenga kuwa na mji mpya wa mfano uliopangika badala ya kugawa viwanja kimoja kimoja uwekezaji wa mfano wa aina ya kina Hamidu City Park ndio ungetiwa mkazo watu wanunue majengo na nyumba zilizojengwa kwa mpango na mipangilio siyo vurugu za ujenzi holela

View: https://m.youtube.com/watch?v=aiJCrekUkW0

BILIONI 2.5 KULIPA FIDIA WATAKAOPISHA UJENZI WA UWANJA WA MPIRA ARUSHA...​

thumb_1451_800x420_0_0_auto.jpg
Posted On: December 18th, 2023
Na Elinipa Lupembe.

Kufuatia mkakati wa Serikali ya awamu ya sita, wa kujenga uwanja wa mpira wa miguu, ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), yanayotarajiwa kufanyika mapema mwaka 2027, Halmasahuri ya Jiji la Arusha, imetenga Shilingi Bilioni 2.5 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi watakayotoa maeneo yao.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo, kwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Damian Ndumbaro ( MB), Mkurugenzi Mtendaji, Jiji la Arusha, Mhandisi Jumaa Hamsini, amesema kuwa Serikali ilitoa maagizo ya kupatikana Eka 83 na mpaka sasa tayari zimepatikana Eka 39, zikiwa zimeandaliwa Hati Miliki, huku Jiji la hilo likitenga shilingi Bilioni 2.5, kwa ajili ya kulipa fidia wananchi watakaopisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo wa mpira.

Amesema kuwa, tayari hatua zote zimeshafanyika, na Jiji limetenga kiasi hicho cha fedha, ambacho kitatumika kulipa fidia kwa wananchi ili kupata eneo la Eka 44 zitakazokwenda kukamilisha Eka 83 zinazotakiwa na Serikali ili kutekeleza ujenzi huo.

"Sisi kama Jiji la Arusha, tumeshajipanga vema, kuhakikisha adhma ya Serikali ya awamu ya sita, inafikiwa kwa kiwa na uwanja wa mashindano, viwanja vya mazoezi pamoja na miundombinu yote inayohitajika inajengwa hapa Mtaa wa Murongoine kata ya Olmoth na tutahakikisha mashindano hayo yatafanyika kama yalivyopangwa".Ameweka wazi Mhandisi Hamsini.

Awali, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, ametembelea na kukagua eneo linaloandaliwa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa mpira na viwanja vya mazoezi, na hatimaye Jiji la Arusha kumkabidhi mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella Hati Miliki ya Eka 39 na Kumkabidhi Waziri huyo mwenye dhamana.

Ikumbukwe kuwa ujenzi wa uwanja wa mpira wa kimataifa mkoani Arusha, licha ya kuwa ni kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ya AFCON lakini zaidi ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi unaokwenda kuwekeza kwenye utalii wa michezo katika mkoa wa Arusha na Tanzania kwa ujumla wake.

#arushafursalukuki

IMG_20231219_053442_702.jpg

FB_IMG_1702966983532.jpg

FB_IMG_1702966979907.jpg

Source : arusha.go.tz​


Waziri Mkuu akagua ujenzi Mji wa Serikali Mtumba​

thumb_4367_800x420_0_0_auto.jpg
Imewekwa Tarehe: July 3rd, 2023
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa leo Julai 03, 2023 amekagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kukagua ujenzi huo, Mheshimiwa Majaliwa ameagiza kuwa ifikapo Oktoba mwaka huu, majengo hayo yawe yamekamilika na kuwekwa samani, ili azma ya Serikali ya watumishi kuhamia kwenye majengo hayo ifikapo Januari Mosi, 2024 itimie.

“Dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kutaka kuona watumishi wote waliohamia Dodoma wanafanya kazi kwenye majengo rasmi fedha imetengwa, imetolewa na itaendelea kutolewa”
1715418343994.png

“Tafuteni mbinu za kiufundi za kukamilisha majengo haya kwa wakati bila kuathiri viwango”Moja ya mbinu ni kusimamia ujenzi huu usiku na mchana, tunataka tumalize majengo haya, Watanzania wanataka kuona majengo yanakamilika na kutumika.”

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amewataka wasimamizi wa ujenzi wa majengo kwenye mji wa Serikali watumie bidhaa zinazozalishwa na viwanda vilivyopo nchini“. Rais Dkt. Samia amesisitiza kuhusu uwekezaji na amekuwa akialika wawekezaji wa nje na wa ndani kujenga viwanda vya bidhaa mbalimbali hapa nchini ikiwemo marumaru (tiles). Tutumie bidhaa zao badala ya kuagiza bidhaa hizo kutoka nje.”
Source : dodoma.go.tz
 
Binafsi yangu siwezi kununua ardhi Zanzibar hata kama katiba na sheria ingeruhusu. Wale watu ni wabaguzi wa kupindukia
 
Ukakasi unakuja hapo ambapo hao wageni wanapata uhalali hata wa kuja kuvinjari bara kama raia. Kuna shida kubwa kwenye huu muungano
Na wakija bara tiyari wanakuwa na sifa za kununua na kumiliki Ardhi kama raia wa kawaida, hawa viongozi wetu ni kama vile tiyari wameshatuuza
 
Hao wanaokalamika ni uhasidi wa mbwa kufukuza mbuzi kula majani wakati wao wenyewe hawawezi kuyala hayo majani.
Ardhi ipo kubwa Bara unalalamikia ardhi ndogo ya Zanzibar. Nunua ardhi Bara kama una uwezo.Na pia kama una uwezo timiza masharti yaliyowekwa huko Zanzibar halafu nunua hiyo ardhi.
Huna uwezo huo waachie wenye uwezo wafanye hivyo..
Kuendelea kubweka bweka kwako hakutakuongezea kipato.Fanya kazi kwa bidii ubadilishe maisha yako sio kulalama kama kigoli chenye mimba changa.Kila jambo kwake ni kero.
 
Back
Top Bottom