Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Haha, sasa sijui lengo la kuzima lilikuwa wafanyakazi wa kalale?

Mimi hadi leo ninayo kanda ya Jangalason nimetape baadhi ya vipindi.

Na tulishapigana na kaka yangu sababu ya kutape kanda zake hadi nikamchoma Kisu cha mguu.
Japo nilikuwa Mdogo lakin nakumbuka yote nimecheka sanaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app
Jamani
Pale [HASHTAG]#Mambo[/HASHTAG] yote tisa 10 zinduka
Nilikuwa sipitwi
 
"Tuache kazi ya miradi tutakula kwako" ene ujangili magendo na rushwa dini" MZEE Mwinamila akiburudisha katikati ya kipindi cha Mikingamo

Kuna mwaka Mei Mosi ilifanyika Shinyanga basi Kulikuwa na kibwagizo kinaimbwa kuelekea siku hiyo. Wasukuma sahihisheni nilipokosea....

"Utakwilima....Bana ba Shinyanga mwaka ugu ba shile kabisa. Ukulima gwa kisasa gwaleni gwangazile gwange kuyupa ni mbolela mala ku ga beche,
 
"Tuache kazi ya miradi tutakula kwako" ene ujangili magendo na rushwa dini" MZEE Mwinamila akiburudisha katikati ya kipindi cha Mikingamo

Kuna mwaka Mei Mosi ilifanyika Shinyanga basi Kulikuwa na kibwagizo kinaimbwa kuelekea siku hiyo. Wasukuma sahihisheni nilipokosea....

"Utakwilima....Bana ba Shinyanga mwaka ugu ba shile kabisa. Ukulima gwa kisasa gwaleni gwangazile gwange kuyupa ni mbolela mala ku ga beche,
Huyu mzee namkumbuka sana,nakumbuka mzee julius alimjengea nyumba pale dodoma, kuna nyimbo alikuwa anaimba zilitumika redioni wakati huo kama huu
"msukosuko wa wimbi maji yanapoingia.......huko mbele nimesahau
Mwingine ni huu
"kuleni kuku mayai na kuujenga mwili pakulala pawe bora....mbele nimesahau malizia mkongwe,kuna mwengine anasema "dereva kalewa gongo aah hiyo si sawa dereva acha vituko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama na mwana mtangazaji alikuwa Eda Sanga ukiacha hadithi ya binti chura ilikuwepo hadithi ya Adili na nduguze,nakumbuka kulikuwa na idhaa ya biashara ilikuwa inafunguliwa saa kumi baada ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku inafuata mazungumzo baada ya habari yalikuwa yanasomwa na Abdul Ngalawa saa mbili na robo kipindi cha vijana Leo mtangazaji alikuwa Julias Nyaisanga ukipenda anko J,nakumbuka mbali sana ilikuwa mida ya jioni unajiunga na radio RSA Hapo utamsikia Moses Mkandawile,UJERUMANI, Hapo utamsikia Umani Heri,mabingwa wa salamu namkumbuka Kondo Ali Kondo,Zakaria Ndefoo mwinda tembo,chivalavala wa chivalavala wa mahuta newala nisimalize utamu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo kwa RSA siyo Moses Mkandawile bali ni Duncan Kandawile na wenzake Francis Chandiona, William Joranji na Boston Caleja Kaunda.
 
Kuna mtangazaji Lenard Mtawa nasikia alifariki. Bujaga Izengo Kadago nikasikia ni afisa uhusiano na masoko pale SUA. Wengine kama Mohammed Kisengo na Nyambona Masamba sijui wako wapi hao siku hizi?
 
Back
Top Bottom