Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Ok. Uzee huu memory zinakata [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Mchana masikio kwenye radio mama na mwana. Ila hadithi ilibamba sana hiyo. Ikisimuliwa unasisimka na kuogopa kama unaangalia movie live [emoji23] [emoji23]
 
Jamani kulikuwa na kipindi kinaitwa OMBI LANGU mwakikumbuka? ilikuwa mtu anatuma ombi la muziki aupendao halafu mtangazaji anaurusha hewani!
Dah! Kumbuka kipindi cha ZILIPENDWA!
Ama hakika siku siku zimekwenda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mama na mwana.. cha edda sijui naniii pamoja na pwagu na pwaguzi.

Kuna pia mazungumzo baada ya habari. Ukija miaka ya 2000 kuna ule mdundo wa majira aseeh nilikuwa naupenda pamoja na utangazaji wa Ezekiel malongo kwenye mpira.

Kuna kipindi nilikuwa nachukua kanda na tape RTD. Moja ya vipindi nilivyowahi ku-tape ni cha ule mdundo majira na ule wimbo wa tunaye Rais Ben will wa Tanzania.

Ila pia kwa wale wa KBC je huu ni uungwana cha mzee mbotela kiliiteka Kenya kipindi hicho.
Nikurekebishe kidogo kwa KBC, kipindi cha je huu ni UUNGWANA kilitangazwa na mzee Leonard Mambombotela.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka kipindi hicho kulikuwa na Idhaa ya Taifa, halafu kulikuwa na External Service na kulikuwa na Idhaa ya Biashara iliyokuwa ikifunguliwa saa kumi jioni.

Sent using Jamii Forums mobile app
Taarifa ya habari ya saa moja jioni kutoka radio Tanzania Zanzibar, sijui kama wanajiunga tena siku hizi, nna miaka zaidi ya 15 bila kusikiliza rtd

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app
Mama na mwana mtangazaji alikuwa Eda Sanga ukiacha hadithi ya binti chura ilikuwepo hadithi ya Adili na nduguze,nakumbuka kulikuwa na idhaa ya biashara ilikuwa inafunguliwa saa kumi baada ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku inafuata mazungumzo baada ya habari yalikuwa yanasomwa na Abdul Ngalawa saa mbili na robo kipindi cha vijana Leo mtangazaji alikuwa Julias Nyaisanga ukipenda anko J,nakumbuka mbali sana ilikuwa mida ya jioni unajiunga na radio RSA Hapo utamsikia Moses Mkandawile,UJERUMANI, Hapo utamsikia Umani Heri,mabingwa wa salamu namkumbuka Kondo Ali Kondo,Zakaria Ndefoo mwinda tembo,chivalavala wa chivalavala wa mahuta newala nisimalize utamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumbuizo Asilia - Michael Katembo , Khalid Ponera baadae Malima Ndelema

Starehe na BP - Julius Nyaisangah

Misakato - Julius Nyaisangah

Ugua pole - Walikuwa wanazunguka hospitali mbalimbali nchini kupitia wawakilishi wa mikoani na wale wa Dar

Nipe Habari - Siwatu Luanda

Mama na Mwana - Deborah Mwenda

Club Raha Leo Show - Julius Nyaisangah, Enock Ngombale na Geofrey Erneo

Kijaruba - Abdallah Mlawa

Mchana Mwema/Pokea Salamu - Christine Chokunegela na wenzake wengi

Chaguo la msikilizaji - Malima Ndelema

Mkoa kwa Mkoa - Michael Katembo, Nadhir Mayoka, Malima Ndelema

Disco Show - Julius Nyaisangah

General tyre na gari lako - Samadu Hassan

Ngano za Muziki - Salama Mfamao, Siwatu Luanda na wengine

Majira ya asubuhi na saa 3 usiku...

Watoto wetu - Watangazaji wa kike..

Mikingano - Salum Seif Nkamba 'SS Nkamba'

Mkulima wa Kisasa - Malima Ndelema

Michezo/Matangazo ya Mpira - Mshindo Mkenyenge, Omary Jongo, Ahmed Jongo 'Father', Dominick Chilambo, Mikidah Mahmoud, Charles Hillary, Juma Nkamia, Salim Mbonde, Abdallah Idrissa Majura na wengine..

Taarifa ya Habari - Julisu Nyaisangah, Charles Hillary, Betty Mkwasa, Sarh Dumba, Halima Kihemba, Jacob Tesha, Sekione Kitojo, Tido Mhando, Mikidad Mahmoud, Christine Chokunegela, Abdallah Mlawa, Abdul Ngalawa, Eddah Sanga, Aboubakary Liongo, Iddi Rashid Mchatta na wengine...

Mazungumzo baada ya Habari - Abdul Ngalawa, Mikidad Mahmoud

Pia walikuwepo wawakilishi wa Kanda/mikoa

Nyanda za Juu Kusini - Idrissa Sadallah, Martha Ngwila

Kanda ya Mashariki - Halima Kihemba , Penzi Nyamungumi, Monica Lyampawe..

Kanda ya Magharibi - Titus Philipo

Kigoma - Chisunga Stephen

Songea - Abisai Stephen

Lindi - Angalieni Mpendu

Ziwa Victoria - Dominick Chilambo, Nathan Rwehabura

Kanda ya Kati - Ben Kiko, Ahmed Kipozi, Sangi Kipozi, Hendrick Michael Libuda, Daniel Msangya, Wilson Malosha, Hellen Masele na wengine

Mtwara - Cassim Mikongoro

Kanda ya Kaskazini - Ahmed Jongo

Zanzibar - Yusuph Omary Chunda na Makame Abdallah

Hawa ni kwa uchache tu....
Umenimumbusha Yusuf Omary Chunda nilisha msahau [emoji106] [emoji106] [emoji106]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom