Victoire
JF-Expert Member
- Jul 4, 2008
- 24,386
- 57,588
Ua jekundu bwana.Adili na nduguze unaikumbuka?Hivi ilikuwa ua jekundu au Koti jekundu... Life was good those days.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ua jekundu bwana.Adili na nduguze unaikumbuka?Hivi ilikuwa ua jekundu au Koti jekundu... Life was good those days.
Ok. Uzee huu memory zinakata [emoji2] [emoji2] [emoji2]Ua jekundu bwana.Adili na nduguze unaikumbuka?
Mchana masikio kwenye radio mama na mwana. Ila hadithi ilibamba sana hiyo. Ikisimuliwa unasisimka na kuogopa kama unaangalia movie live [emoji23] [emoji23]Ok. Uzee huu memory zinakata [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Mahoka ilikuwepo na wahusika wake wakuu walikuwa pwagu & pwagusi muombe radhi
Nikurekebishe kidogo kwa KBC, kipindi cha je huu ni UUNGWANA kilitangazwa na mzee Leonard Mambombotela.Mama na mwana.. cha edda sijui naniii pamoja na pwagu na pwaguzi.
Kuna pia mazungumzo baada ya habari. Ukija miaka ya 2000 kuna ule mdundo wa majira aseeh nilikuwa naupenda pamoja na utangazaji wa Ezekiel malongo kwenye mpira.
Kuna kipindi nilikuwa nachukua kanda na tape RTD. Moja ya vipindi nilivyowahi ku-tape ni cha ule mdundo majira na ule wimbo wa tunaye Rais Ben will wa Tanzania.
Ila pia kwa wale wa KBC je huu ni uungwana cha mzee mbotela kiliiteka Kenya kipindi hicho.
Hahahahaha,acha tu ,ila tunatakiwa tuzipige stater.Ok. Uzee huu memory zinakata [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Hili lilikuja kumalizwa na ujio wa radio one stereo!Kumbe na we ni Ancestor.
Kuna anayeyekumbuka radio zilikua zikifika saa 6 usiku zinazimwa?
Muhimu [emoji23] [emoji23] [emoji23]Hahahahaha,acha tu ,ila tunatakiwa tuzipige stater.
Taarifa ya habari ya saa moja jioni kutoka radio Tanzania Zanzibar, sijui kama wanajiunga tena siku hizi, nna miaka zaidi ya 15 bila kusikiliza rtdNakumbuka kipindi hicho kulikuwa na Idhaa ya Taifa, halafu kulikuwa na External Service na kulikuwa na Idhaa ya Biashara iliyokuwa ikifunguliwa saa kumi jioni.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hiki ni kipindi cha neno, KBC Nairobi na Mchungaji peter kimani, kila siku saa nne asubuhi hadi tano! Hadi wakati mwingine, na nenoooo...litaendelea!Nikurekebishe kidogo kwa KBC, kipindi cha je huu ni UUNGWANA kilitangazwa na mzee Leonard Mambombotela.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mama na mwana mtangazaji alikuwa Eda Sanga ukiacha hadithi ya binti chura ilikuwepo hadithi ya Adili na nduguze,nakumbuka kulikuwa na idhaa ya biashara ilikuwa inafunguliwa saa kumi baada ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku inafuata mazungumzo baada ya habari yalikuwa yanasomwa na Abdul Ngalawa saa mbili na robo kipindi cha vijana Leo mtangazaji alikuwa Julias Nyaisanga ukipenda anko J,nakumbuka mbali sana ilikuwa mida ya jioni unajiunga na radio RSA Hapo utamsikia Moses Mkandawile,UJERUMANI, Hapo utamsikia Umani Heri,mabingwa wa salamu namkumbuka Kondo Ali Kondo,Zakaria Ndefoo mwinda tembo,chivalavala wa chivalavala wa mahuta newala nisimalize utamuJamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo
Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.
Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Umenimumbusha Yusuf Omary Chunda nilisha msahau [emoji106] [emoji106] [emoji106]Tumbuizo Asilia - Michael Katembo , Khalid Ponera baadae Malima Ndelema
Starehe na BP - Julius Nyaisangah
Misakato - Julius Nyaisangah
Ugua pole - Walikuwa wanazunguka hospitali mbalimbali nchini kupitia wawakilishi wa mikoani na wale wa Dar
Nipe Habari - Siwatu Luanda
Mama na Mwana - Deborah Mwenda
Club Raha Leo Show - Julius Nyaisangah, Enock Ngombale na Geofrey Erneo
Kijaruba - Abdallah Mlawa
Mchana Mwema/Pokea Salamu - Christine Chokunegela na wenzake wengi
Chaguo la msikilizaji - Malima Ndelema
Mkoa kwa Mkoa - Michael Katembo, Nadhir Mayoka, Malima Ndelema
Disco Show - Julius Nyaisangah
General tyre na gari lako - Samadu Hassan
Ngano za Muziki - Salama Mfamao, Siwatu Luanda na wengine
Majira ya asubuhi na saa 3 usiku...
Watoto wetu - Watangazaji wa kike..
Mikingano - Salum Seif Nkamba 'SS Nkamba'
Mkulima wa Kisasa - Malima Ndelema
Michezo/Matangazo ya Mpira - Mshindo Mkenyenge, Omary Jongo, Ahmed Jongo 'Father', Dominick Chilambo, Mikidah Mahmoud, Charles Hillary, Juma Nkamia, Salim Mbonde, Abdallah Idrissa Majura na wengine..
Taarifa ya Habari - Julisu Nyaisangah, Charles Hillary, Betty Mkwasa, Sarh Dumba, Halima Kihemba, Jacob Tesha, Sekione Kitojo, Tido Mhando, Mikidad Mahmoud, Christine Chokunegela, Abdallah Mlawa, Abdul Ngalawa, Eddah Sanga, Aboubakary Liongo, Iddi Rashid Mchatta na wengine...
Mazungumzo baada ya Habari - Abdul Ngalawa, Mikidad Mahmoud
Pia walikuwepo wawakilishi wa Kanda/mikoa
Nyanda za Juu Kusini - Idrissa Sadallah, Martha Ngwila
Kanda ya Mashariki - Halima Kihemba , Penzi Nyamungumi, Monica Lyampawe..
Kanda ya Magharibi - Titus Philipo
Kigoma - Chisunga Stephen
Songea - Abisai Stephen
Lindi - Angalieni Mpendu
Ziwa Victoria - Dominick Chilambo, Nathan Rwehabura
Kanda ya Kati - Ben Kiko, Ahmed Kipozi, Sangi Kipozi, Hendrick Michael Libuda, Daniel Msangya, Wilson Malosha, Hellen Masele na wengine
Mtwara - Cassim Mikongoro
Kanda ya Kaskazini - Ahmed Jongo
Zanzibar - Yusuph Omary Chunda na Makame Abdallah
Hawa ni kwa uchache tu....
Walikuwa wanatuma post card wanawake tu akituma mwanaume inachanwaJe wakumbuka kipindi kilichoitwa KIJALUBA CHANGU kilikuwa kikitangazwa na Abdallah Mlawa enzi hizo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mikingamo ni sauti ya uma,tuandike yuko wapi na anafanya nini kulihujumu taifa,nasi tutamtafuta kokote aliko