Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Uje tena shangazi, shangazi shangazi enhe! Mchana utasikia wimbo ule hivi sasa ni lunch time... Na mwisho wa mwezi kulikuwa na wimbo wake wa kasim kama hana pesa nyumbani hatoki......!
Umenikumbusha mbali sana. Nilipenda sana kusikiliza huo wimbo wa Lunch Time uliotungwa na kuimbwa na mwanamuziki wa Kenya aitwae Gabriel Omolo Aginga (Mr. Lunch Time). Ni bahati mbaya sana kwamba huyu mzee alifariki mwanzoni mwa mwaka huu. Huo wa Kassim ni wa Orchestra Mlimani Park. Ni kupitia vipindi kama hivyo vya RTD tuliweza kupata nafasi ya kusikiliza kwa wingi nyimbo za wanamuziki wa Tanzania na majirani zetu hususani Kenya na wale wa Zaire (kwa sasa DRC).
 
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app
Pwagu na Pwaguzi.
 
Hiki niwe mkweli sikuwahi kukisikia ila majina nilikuwa nayasikia
Hivi kipindi cha Mahoka na Pwagu na Pwaguzi vilikuwa ni vipindi viwili tofauti au Mahoka ndiyo lilikuwa jina la kipindi huku Pwagu na Pwaguzi wakiwa ndiyo waigizaji wake?
 
Jamani kweli siku hazigandi. Nakumbuka enzi hizo hakuna utitiri wa redio stations ukitaka kusikiliza huna option kama kipindi kilichopo hukipendi uzime tu radio.
Hata mfumo wa vipindi ulikuwa tofauti sana na huu wa sasa...enzi hizo vipindi vililenga kutoa elimu zaidi kuliko burudani. Kama kipindi ni cha kutoa elimu kuhusu masuala ya umeme let's say, hakuna porojo ni elimu tu mwanzo mwisho.
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwishoni hivi, kuna vipindi nilikuwa sipitwi kabisa hata kama nilikuwa kucheza muda huo ntafanya juu chini niwepo

Kulikuwa na vipindi vya watoto kimoja nilikuwa kinaitwa Mama na mwana kilikuwa kinarushwa jumamosi saa nane na nusu. Nilikuwa sipitwi kabisa....kulikuwa na hadithi zilikuwa zinasimuliwa naikumbuka moja tu ya Binti Chura.

Kuna kipindi kingine kilikuwa kinaitwa Twende na wakati ulikuwa mchezo wa kuigiza unarushwa kila jumamosi saa mbili na nusu usiku. Nilikuwa nafuatilia hatua kwa hatua maana ulikuwa haurudiwi ukipitwa ndo tuonane next episode.
Karibu mdau tukumbushane wewe ulikuwa unapenda vipindi gani?


Sent using Jamii Forums mobile app

Mimi hunitoi hapo kipindi cha BP chini yake marehemu Uncle J.Nyaisanga.Huyuhuyu aliendesha Bwana chai kama sikosei.Kumbuka, vipindi vingi vilikuwa na break, mnakula ngoma moja hivi mnaendelea.

Usisahau Malenga wetu.Unakula mistari na vina toka kwa wazee wa Kilwa na Rufiji.Nimemsahau yule aliyekuwa akighani mashairi. Usisahau vipindi kama NASACO! SUKITA, T.E.S

Hiyo T.E.S(shirika la ugavi wa vifaa vya elimu) basi tangazo lao lilikuwa kitu kama hivi:

A:Aaah!una kalamu nzuri, umeipata wapi?

B: T.E.S

A: Na wino?

B: T.E.S

Yani ilikuwa burdaaaaaaaaaani.

Usisahau tulikuwa na idhaa mbili, taifa na biashara

Asante
 
Kuna wahenga wengi, ngoja nilinde huu ubongo
FB_IMG_1542084466400.jpeg
 
Hivi kipindi cha Mahoka na Pwagu na Pwaguzi vilikuwa ni vipindi viwili tofauti au Mahoka ndiyo lilikuwa jina la kipindi huku Pwagu na Pwaguzi wakiwa ndiyo waigizaji wake?
Sijui boss sijawahi kuwasikia hao pwagu na pwaguzi wakiigiza pengine wakati huo mzee alikuwa hajanunua redio
 
Hivi kipindi cha Mahoka na Pwagu na Pwaguzi vilikuwa ni vipindi viwili tofauti au Mahoka ndiyo lilikuwa jina la kipindi huku Pwagu na Pwaguzi wakiwa ndiyo waigizaji wake?


Vipindi viwili tofauti.Ila baadhi ya waigizaji ni walewale.
 
ATC hewani kale kawimbo kalikua kananivutia sana...Kipindi kingine ni Majira hasa Ben Kiko Tabora aki report...Richard Leo....Ukweli mambo ya RTD ilikua imeivaa kila Idara
 
Ooh kumbe...kuna kingine kile kilikuwa kinaitwa pole kwa kazi nadhani kilikuwa kinaanza saa sita
Kulikua na kipindi kinaitwa wakati wa kazi. Kilikua kinaanza saa tano kamili hadi saa sita kamili mchana, na walikua wanatembelea wafanyakazi mbalimbali katika maeneo yao ya kazi na kuzungumza nao kuhusu shughuli wanazofanya na kisha wanapewa fursa ya kutuma salamu kwa ndugu na jamaa halafu wanachugua muziki wautakao wanachezewa

Saa sita kamili hadi saa saba mchana kulikua na hicho kipindi cha mchana mwema ambacho nacho kilikua ni cha salamu na muziki

Pole kwa kazi ilikua ni jioni na pia kulikua na jioni njema
 
Kulikua na kipindi kinaitwa wakati wa kazi. Kilikua kinaanza saa tano kamili hadi saa sita kamili mchana, na walikua wanatembelea wafanyakazi mbalimbali katika maeneo yao ya kazi na kuzungumza nao kuhusu shughuli wanazofanya na kisha wanapewa fursa ya kutuma salamu kwa ndugu na jamaa halafu wanachugua muziki wautakao wanachezewa

Saa sita kamili hadi saa saba mchana kulikua na hicho kipindi cha mchana mwema ambacho nacho kilikua ni cha salamu na muziki

Pole kwa kazi ilikua ni jioni na pia kulikua na jioni njema
Shikamoo Muhenga Ses. 🙈🙈🙈🙈

Japo sivijui hivyo vipindi huku na mie ni Muhenga pia Ses kwa hili naomba nikazie tu maana sina jinsi.💃💃💃💃💃
 
Kipindi cha Sitasahau-RFA kila jumapili

Kipindi cha Wosia wa Baba wa Taifa-Radio Tz(TBC FM) kila baada ya taarifa ya habari saa 2 usiku

Kipindi cha Matagazo ya Vifo-Radio Tz(TBC FM) saa kumi jioni

Kipindi cha Darubini ya leo-RFA siku kuanzia saa 4(sina uhakika, nishasahau)
 
Kulikua na kipindi kinaitwa wakati wa kazi. Kilikua kinaanza saa tano kamili hadi saa sita kamili mchana, na walikua wanatembelea wafanyakazi mbalimbali katika maeneo yao ya kazi na kuzungumza nao kuhusu shughuli wanazofanya na kisha wanapewa fursa ya kutuma salamu kwa ndugu na jamaa halafu wanachugua muziki wautakao wanachezewa

Saa sita kamili hadi saa saba mchana kulikua na hicho kipindi cha mchana mwema ambacho nacho kilikua ni cha salamu na muziki

Pole kwa kazi ilikua ni jioni na pia kulikua na jioni njema
Haha uko sawa kabisa boss kwa kweli umekwiva
 
Kipindi cha Sitasahau-RFA kila jumapili

Kipindi cha Wosia wa Baba wa Taifa-Radio Tz(TBC FM) kila baada ya taarifa ya habari saa 2 usiku

Kipindi cha Matagazo ya Vifo-Radio Tz(TBC FM) saa kumi jioni

Kipindi cha Darubini ya leo-RFA siku kuanzia saa 4(sina uhakika, nishasahau)
Nakumbuka baada ya kuacha kusikiliza TBC na kuhamia RFA nilikuwa napenda kusikiliza hiki kipindi cha Sitasahau kilikuwa kinarushwa saa mbili asubuhi siku ya jumapili kikifuatiwa na kile cha vitu vilivyovunja record sijui kiliitwaje baada ya hapo kilifuatiwa na Je huu ni uungwana???? Nlikuwa shabiki sana wa hilki kipindi wakati huo mtangazaji alikuwa Fredua ( sijui ndio inaandikwa hivi? ) baadae akaja mwingine anaitwa nani sijui mtani.
 
Back
Top Bottom