Wahuni wa Kinshasa Julai 17 1997- Desemba 25 2024

Wahuni wa Kinshasa Julai 17 1997- Desemba 25 2024

TUNAENDELEA....!!!!!
YAKAPITA MAAMUZI NA UTARATIBU.
1 : Hakuna kujihushisha na siasa.......kinachopewa kipaumbele ni pesa.
2 : Hakuna kupeleka malalamiko ubalozi wa Tanzania hata litokee tatizo gani....tutalimaliza chini kwa chini.
3 : Hakuna kushirikiana na waarabu wa Lebanon na WASHIRIKA wa RPF sababu hawaaminiki.
4 : Mzee Kabila.....aeshimiwe kama kiongozi mbadala wa Anko Seseseko...Dili zake tusizitolee tamaa.....sababu tukubali ukweli SESESEKO hayupo tena nyakati zimebadilika.
5 : Hakuna kujionyesha mbele za watu kama tuna Hela........pale michongo ya mawe inapokubali.
6 : TUSISAHAU KUSAIDIANA KAMA WATANZANIA NA WOTE NI KITU KIMOJA..HAIJALISHI TUMETOKEA MIKOA TOFAUTI.
***********************************
Kazi ikawa kusikilizia hali ya upepo Kinshasa inaendaje.......... kipindi hilo mitaa yote ya Kinshasa kuanzia kule Boulevard na Masina na kule Pakadjuma......na mitaa mingine mingi usalama ulikua mdogo.
Na serikali mpya ilikua inapambana kurudisha usalama sababu Kinshasa ndio makao makuu ya nchi.....iliyopewa jina jipya CONGO DRC.
Wadau wote wamekimbia nchi...... kwahiyo inatubidi tuanzie upya kuchora ramani.
Na WANYARWANDA ni wabinafsi...hasa watu wa jamii za watusi.
Kama unavyojua mtafutaji hachoki...mikakati ikapangwa ikapangika.
Mungu ni mwema pakapatikana pa kuanzia mpango kazi.
MPANGO KAZI NO : 01
************************************************
COL RUTAREMWA/ RWANDESE BUSINESSMAN.
Kiuhasilia huyu jamaa hakua mwanajeshi Bali mtoto wa mjini ndani ya jeshi la RDF... chini ya
Amiri jeshi Abby Juve.
Rutaremwa alihudumu ndani ya jeshi la RDF kwa zaidi ya miaka 13...akianzia cheo cha chini mpaka kupanda juu na kua Col.
Biashara zote za mawe kati ya Kigali na Kinshasa alikua mtu wa kati ni yeye.
Na ndie mmojawapo wa wenyeji wetu..ukimtoa PAPAA MUNDENDE.
Ikabidi atafutwe tujue tunaanzia wapi.
Akatupa jibu kua.....kama kweli tunapenda mawe na tunataka Hela tuache kukaa Cabinda au Kinshasa bali tuingie uwanja wa fujo kama tulivyokua tunapita KIVU KASKAZINI NA KIVU KUSINI.
Kila kitu atasimamia yeye kuhusu usalama wetu....ila atakupa anachukua asilimia 40%.....ya faida ya kila mmoja kwenye team kazi.
UWANJA WA FUJO.
Sababu ya kuyaita maeneo yote ya Kivu kusini na Kivu kaskazini kua uwanja wa fujo....ni sababu kipindi hicho majimbo haya yalikua kama shamba la bibi... mwenye nguvu anajizolea mali.
Waganda wanajizolea.
Wanyarwanda wanajizolea.
Wakenya wanajizolea.
Wazimbabwe wanajizolea.
Waangola wanajizolea.
Warundi wanajizolea.
Walebanoni wanajizolea.
Wazambia wanajizolea.
Watanzania walikua wachache mno.

KATIKA NYUZI AMBAZO NINGWEZA KUSIMULIA HAYA MAMBO ILA NILIZISITISHA KWA SABABU ZA KIUSALAMA NI KWAMBA SIKU MOJA NIKIWA MPAKANI MWA DRC NA BURUNDI...NILIWAHI KUKUTANA NA DOGO ANA KILO KAMA TISA HIVI ZA DHAHABU CHAFU ILIYOSAGWA SAGWA KIENYEJI.
AFU DOGO AKATAKA KUNIPA NIZIVUSHE...NIKAOGOPA MSALA.
SASA HUYO NI DOGO TU...USHAWAHI KUFIKIRIA AKINA PAULO NA AKINA NAMBA SABA NA AKINA MUHOOZI NA WADAU WOTE WENYE NGUVU NA MAMLAKA UKANDA HUU WA MAZIWA MAKUU WANAPIGA HELA KIASI GANI KUANZIA MWAKA 1997 MPAKA 2024.....KATIKA UKANDA HUU WA FUJO....?????
Turudi kwenye simulizi..!!!!
Col Rutaremwa akatushauri tuondoke haraka mjini KINSHASA tuingie uwanja wa fujo.
Pesa inatafutwa kwa jasho na damu.
Pesa inafitinisha WASHIRIKA.
Pesa ndio siasa na siasa ni pesa.
Basi uamuzi ukapita wote tukutane kisangani....pale ndio patakua starting point ya kuingia mzigoni.
Na kiini cha simulizi yangu INAANZIA hapa.
Safari ya kuingia uwanja wa fujo.
Itaendelea...........!!!
Hii stori kwangu ni ngumu ila nitajitahidi hivo hivo kuelewa 😜😜😊
 
Maisha yanaenda kwa kasi mno.
Ni miaka mingi imepita ila nawakumbuka ndugu zangu vijana wa kitanzania....kutoka Mbagala, Temeke, Kinondoni na Kariakoo walioenda ukanda wa maziwa makuu kujitafutia mawe.
Kinshasa ya zamani sio hii ya leo.
Kigali ya zamani sio hii ya leo
Bujumbura ya zamani sio hii ya leo
Dar ya zamani sio hii ya leo.

Kabla ya yote niombe Mungu awalaze mahali pema peponi ndugu zangu hawa.
1 : Rais wa Rwanda.....Anko Juve.
2 : Rais wa Zaire.......Anko Seseseko.
3 : Kanali Fred wa RPF.
4 : My brother Hamed.
5 : Col Rutaremwa.
6 : My homie James Zugazuga.
Wengine wengi siwezi kuwataja hapa Bali nitawataja mbeleni Uzi uliendelea.

MAISHA YANATUFUNZA...KUFA HATUFI ILA CHA MOTO TUNAKIONA.
WATOTO WA KIUME TUNAKAZA

HATUKUZALIWA FAMILIA ZA KISHUA....ILIBIDI TUHANGAIKE KUWATUNZA WANAOTUTEGEMEA.

I HOPE HUU UZI SITOZUIWA NA WAHUSIKA KUENDELEA KUUANDIKA.
MAANA UZI ZANGU ZOTE..... WAHUSIKA WAGA WANANIKATAZA.
NA MIMI NATII SHERIA BILA SHURUTI.

Baada ya ukimya mrefu nimerudi Ili niwape story wadogo zangu kuhusu harakati za kutafuta tulizopitia kaka zenu.

STORY HII INAANZIA KINSHASA JULY 17 1997

Karibuni sana.

View attachment 3193900
.
 
Back
Top Bottom