babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 14,478
- 18,341
Siku zote unapoanza safari ya maisha kuanzia chini usitegemee utafanikiwa katika kila jambo. Kumbuka pia tulikuwa na vita, labda kwa kuwa unadhani vita tunaisoma na kuona kwenye tv pekee tunaona ni kitu cha kawaida. Vita iliturudisha nyuma sana kiuchumi. Je, viraka na kukosa mahitaji muhimu yanahalalisha wizi na ufisadi?Wakati tunavaa viraka na kukosa mahitaji muhimu ilikuwa kipindi Cha ubepari?
Enzi zake ukimkosoa kidogo ilikuwa unapotezwa, msome Ludovick Mwijage alifanywa nini akaimbia nchi, kaandika vitabu viwili kuhusu hilo, kuna mtu aliweka hapa JF:Saa nyingine ni ego au kiburi tu, mtu anajua kabisa amekosea ila akijirekebisha hataki maana anaona atakuwa amejishusha mbele ya wakosoaji wake
Nafikiri pengine ni uchanga wa kuendesha nchi ambapo kwa namna moja ama nyengine kiongozi atakuwa tu too idealistic. Kwa mfano uliyotoa kwa nchi tuliyochukua sera zao za kiujamaa wenzetu civilisation yao ni kubwa kwa maana imejengeka kwa miaka mingi. Hivyo kutakuwa na namna kwa wao kuwa rahisi kubadilika.Serikali ni taasisi, Uraisi ni taasisi inayoongoza Serikali hivyo kupatikana kwa majawabu ni rahisi tu. Mambo yote ambayo Raisi Nyerere aliwahi kuyafanya yalianza katika ngazi ya kisera na baadaye kutekelezwa kupitia sheria. Hivyo kwasababu wengi walikuwepo kipindi hicho ni rahisi kufahamu nini kilikuwa kinaendelea hadi kupelekea serikali kutengeneza sera za namna ile na baadaye kuzitungia sheria kandamizi vile.
Mfano, mwaka 1967 wakati tunatanzanga Azimio la Arusha, sababu zilizotolewa ni kwamba jamii ya Tanzania ilikuwa haina usawa kutokana miaka ya ukoloni. Hivyo kujenga usawa na kuondoa matabaka ni lazima nyezo zote za uzalishaji (Major Means of Production) zitaifishwe ili serikali iweze kutoa huduma kwa kila mwananchi. Atleast this is understandable. Ila kwanini serikali ilitumia dola na sheria kandamizi kuhakikisha watanzania tunalala njaa na kukosa hata mavazi mwilini, kwa miaka mitano mfululizo sijapata majawabu yake.
Lengo lake haswa kutuona tukiishi kimasikini vile ilhali ilikuwa inawezekana kutuachia kutafuta mahitaji yetu ilikuwa inawezekana. Somethings defy ordinary human comprehension.
Wavaa kobazi wameungana kupinga Utakatifu wa Nyerere, Sasa wanaanza kumuita Mtakatifu kwa kejeli kabla ya MudaNami nimepata mshangao wa kulitumia neno MTAKATIFU sijui anafanya dhihaka au nini. Kwa namna alivyo humu ndani jf na hiyo lugha anayotumia ndo hayo tunayosema madhaifu ya kibinadamu.
toKiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani, leo atashika hiki atakiacha, kesho atashika kile nacho atakiacha...
Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.
Sasa ndani ya kipindi hicho cha mchakato ndicho kinamfanya kiongozi aendelee kusimamia kile anachokiamini, akiamini atafikia malengo, kama kikija kuwa na matokeo tofauti hayo ni mambo ya kibinadamu, kwamba alikosea, na ndio maana akawapisha wengine.
- Lakini unaposema Nyerere hakuwa na huruma na watu wake unakosea, alikuwa na huruma kupitiliza.
1. Hakujilimbikizia mali yoyote, licha ya madini na kila aina ya rasilimali tulizonazo.
2. Aliwahi kukaririwa akisema; "kiongozi unapita barabarani, unaona hali ya mtanzania ilivyo mbaya, unajua hili ni jukumu langu kumuondoa hapo alipo".
3. Hakuna hata mtoto wake mmoja tunayesikia amewahi kuhusishwa na wizi/ufisadi wa aina yoyote.
Mpaka hapo naamini utapata picha Nyerere alikuwa kiongozi wa aina gani, kwamba licha ya sera yake ya ujamaa kufeli, lakini dhamira ya dhati ya kumkomboa mtanzania toka kwenye lindi la umasikini alikuwa nayo tofauti na ulivyoandika.
Above all, hivi umewahi kujiuliza baada ya Nyerere kuondoka madarakani nini kilifuatia?
Kilichofuatia ndicho kile ambacho Nyerere alikipiga vita na wewe unaonekana kukifurahia, binafsi nchi hii naamini hakuna mabadiliko yoyote ya maana kiuchumi zaidi ya kuwepo pengo kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho, hili Nyerere na Sokoine ndio walikuwa wakilipinga.
- Hii kwangu ni sawa na kusema, licha ya kumuona Nyerere alifeli, lakini hata hao waliofuatia baada yake nao wamefeli pia, hatuna cha maana cha kujivunia, mgao wa umeme, ukosefu wa maji safi na salama, wanafunzi kukosa matundu ya vyoo shuleni na madawati, mambo ni mengi...
Labda uniambie tu kwa sasa unafurahia uwepo wa unga, sabuni, mchele na mahitaji mengineyo mitaani, lakini ukweli wa mambo ni kwamba, licha ya uwepo wa vitu hivyo, bado hali ya mtanzania kiuchumi ni mbaya na ndio maana mpaka leo bado wapo ndugu zetu vijijini wakisubiri kampeni zianze, ili wagaiwe t-shirts na kofia za CCM ziwastiri.
Hivyo kwangu, kumlaumu Nyerere kwa kufeli bila ya kunionesha yule aliyefaulu hapa ndani kwetu sikuelewi, na kutumia mifano ya nje kumhukumu Nyerere bila kunionesha nani aliyefuatia wa hapa ndani akafaulu, umemuonea, that's unfair comparison.
Unless uniambie mahitaji yetu siku zote yangebaki yale yale ya unga, mchele na sabuni kupatikana madukani, jambo ambalo kwangu halina mantiki, naamini mahitaji hubadilika kulingana na wakati, na pale unaposhindwa kuwapa watu wako kile wanachohitaji kwa wakati husika, basi umefeli, there is no way out.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Tunazungumza ya zamani wakati ya Sasa yanatushinda.👩⚖️Mimi kinachonishangaza ni huyu wa sasa ambaye hana uwezo lakini bado tu anangangania.
Funguka uwongo wake ni upiInaonekana kabisa enzi za Mwalimu ulikuwa mtoto mdogo.
Nyerere alikuwa na dira na maono yake.
Na aliyapambania hata Kama mengine yalikwama.
Tena amefariki dira yenu Sasa hivi ni ipi zaidi ya kuuza kila kitu na kuvimba MITUMBO.
Nyerere hakuiba kitu, kaacha nchi Bikra kabisa. Hata Kama alifeli, mmeshindwa nini kupiga hatua miaka 35 Sasa??
Mtoa maoni kaweka rejea yoyote?
Nyerere ambaye alikuwa anasamehe kina Bibi titi, Kambona na Abdul Jumbe??
Mtu asiye na utu ni Kama Kikwete kung'oa meno Ulimboka au Kutandika risasi Kama unaua chatu alikofanya Magu.
Wafuasi wa Nyerere ni Nani Sasa hivi kwenye mfumo?
Maana kina Madaraka, Butiku, WARIOBA hawana usemi kwa Sasa?
Acheni visingizio mavi ya bata.
Hao wavaa kobazi ndio waliompokea na kumlea Nyerere.Wavaa kobazi wameungana kupinga Utakatifu wa Nyerere, Sasa wanaanza kumuita Mtakatifu kwa kejeli kabla ya Muda
Bila Nyerere Hawa wavaa kobazi hata hiyo Elimu wasingekuwa nayo ,
Wanatakiwa wamuheshimu sana
Wapigania uhuru wa Afrika hawakuwa viongozi wazuri wa nchi zao baada ya uhuru kupatikana, na sababu ni nyingi miongoni mwa hizo ni :-Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.
Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.
Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:
1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.
Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.
Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.
Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?
Kawarithisha na wengineo.Ila Nyerere naye kwa maigizo alikuwa hajambo. Anapanga mstari kuwa anachagua kiongozi, lakini tayari alikuwa na matokeo mfukoni! Ogopa kiongozi aliyekuwa anaamini kiongozi wa kweli atatoka ccm, yaani Hawa watoto wa kina Mwigulu ndio Nyerere alimaanisha hao!
Mkuu Eyce, Merry Christmas to you Brother,Nadhani swali kubwa zaidi kujiuliza ni kwa nini pamoja na mateso yote waliyopitia watanzania, bado aliendelea kuwa na ushawishi mkubwa hata baada ya kutoka madarakani na pia kifo chake kilitia simanzi watu wengi haswa maskini waliokuwa wanateseka zaidi.
Kingine cha kujiuliza ni kwa nini baada ya kifo chake, kulitokea mabadiliko makubwa haswa kuleta mfumo wa soko huria lakini bado viongozi waliopo hawajapata imani ya wananchi tofauti na enzi hizo za mateso na wala nchi haijapiga hatua kama nchi ulizozitolea mfano.
Binafsi yangu naamini Nyerere alifanya makosa mengi lakini dhamira yake haikuwa mbaya maana hakunufaika financially kwa yote aliyoyafanya hivyo, alijaribu kujenga misingi ya Tanzania ya ndoto yake tofauti na sasa nchi inavyojiendea bila kuwa na direction.
Naamini pia yeye kuona ugumu na kuuvumilia si kwamba alikuwa haumii ila aliichukulia kama gharama ya kutimiza malengo kama yeye na watu wengine walivyoumia kama gharama ya kuleta uhuru 🙏🏽
Nyerere alikuwa tapeli na kibaraka kama alivyo sema Nkwame NkrumahKwenye hili Nyerere alikuwa ndiye bingwa. Alikuwa kila anayemkosoa anahama nchi. Ni vile tu ukweli hausemwi na bahati mbaya Nyerere katawala ktk kipindi ambacho media outlets zilikuwa hakuna.
Redio ya taifa ilikuwa inaandikiwa nn cha kusema kuhusu rais kwenye taarifa ya habari.
¶ Nyerere ndiye aliyefanya Kambona kuishi ukimbizini maisha yake yote.
¶ Nyerere ndiye aliyechana vyeti vya Tuntemeke Sanga.
¶ Nyerere ndiye aliyemfunga kifungo cha nyumbani (alimuweka kizuini) Kasangatumbo
¶ Nyerere ndiye alimuondoa kwenye urais Abdul Jumbe halafu akamuweka kizuizini hapo Kigamboni mpk umauti.
¶> Nyerere ndiye aliyetunga hili katiba bovu lililomfanya yeye kujipa umungu wa Tanzania.
Nyerere ni dikteta asiyesemwa.
Ila Nyerere naye kwa maigizo alikuwa hajambo.
Sitaki.😎😁Funguka uwongo wake ni upi
Hilo liko wazi kuwa aling'oka kwa aibu.Na hakung'oka mwenyewe kama wengi tunavyodanganywa, maji yalimfika shingoni na aliambiwa ama ung'oke ama wananchi wako waendelee kuangamia, kanisa katoliki likamwabia pumzika urais uendelee kuwa mkuu wa chama staili ya Mao Tse Tung (Mao ze dong).
Mwenyewe akakiri kung'atuka maana alikuwa kang'ata.
Asiyefanya kazi na asile....ndio kanuni insyofanya watu wajitume na kupelekea uvumbuzi mbalimbali duniani wa kurahisisha kazi na kuleta uhuru kwa mtu binafsi.... binadamu hawawezi kuwa sawa kwa sababu sio mifugoUbepari ni ushetani. Wewe una njaa lakini mwenzako anasaza bila huruma ndivyo tunaishi hivyo kwa sasa. Ujamaa unataka wote muende pamoja hata mtu wa mwisho kabisa naye awezeshwe ndio maana tunaita ujamaa ni utu. Hamuoni licha ya matatizo tuliyonayo lakini mtu yupo radhi awe na fedha ambazo hatomaliza milele? Watu wanamiliki magari na majumba ya kifahari na ni viongozi wa serikali na kulipwa fedha nyingi ukiachia mbali kuiba lakini watu wanakosa huduma muhimu?
Vita ya Kagera kisababishi ni Nyerere mwenyewe kwa uchokozi wake, akiingilia siasa za Uganda kwa kufadhili na kuwahifadhi waasi wa Obote ambao walikuwa wanaenda Uganda kujaribu kumuua Idd AminiHii nayo ni mojawapo na setbacks kwenye uongozi wa Nyerere, mleta mada badala ya kutumia muda mwingi kuhukumu tena kwa kutumia mifano nje, nadhani angejielekeza pia kwenye changamoto za kila awamu ili tupime awamu ipi ilikuwa na changamoto nzito zaidi ya nyingine, kisha tuone yupi alikuwa mzembe zaidi.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app