Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wakati tunavaa viraka na kukosa mahitaji muhimu ilikuwa kipindi Cha ubepari?
Siku zote unapoanza safari ya maisha kuanzia chini usitegemee utafanikiwa katika kila jambo. Kumbuka pia tulikuwa na vita, labda kwa kuwa unadhani vita tunaisoma na kuona kwenye tv pekee tunaona ni kitu cha kawaida. Vita iliturudisha nyuma sana kiuchumi. Je, viraka na kukosa mahitaji muhimu yanahalalisha wizi na ufisadi?
 
Saa nyingine ni ego au kiburi tu, mtu anajua kabisa amekosea ila akijirekebisha hataki maana anaona atakuwa amejishusha mbele ya wakosoaji wake
Enzi zake ukimkosoa kidogo ilikuwa unapotezwa, msome Ludovick Mwijage alifanywa nini akaimbia nchi, kaandika vitabu viwili kuhusu hilo, kuna mtu aliweka hapa JF:

 
Nafikiri pengine ni uchanga wa kuendesha nchi ambapo kwa namna moja ama nyengine kiongozi atakuwa tu too idealistic. Kwa mfano uliyotoa kwa nchi tuliyochukua sera zao za kiujamaa wenzetu civilisation yao ni kubwa kwa maana imejengeka kwa miaka mingi. Hivyo kutakuwa na namna kwa wao kuwa rahisi kubadilika.

Nimejaribu tu kuwaza.
 
Nami nimepata mshangao wa kulitumia neno MTAKATIFU sijui anafanya dhihaka au nini. Kwa namna alivyo humu ndani jf na hiyo lugha anayotumia ndo hayo tunayosema madhaifu ya kibinadamu.
Wavaa kobazi wameungana kupinga Utakatifu wa Nyerere, Sasa wanaanza kumuita Mtakatifu kwa kejeli kabla ya Muda

Bila Nyerere Hawa wavaa kobazi hata hiyo Elimu wasingekuwa nayo ,

Wanatakiwa wamuheshimu sana
 
to
Mimi kinachonishangaza ni huyu wa sasa ambaye hana uwezo lakini bado tu anangangania.
Tunazungumza ya zamani wakati ya Sasa yanatushinda.👩‍⚖️
 

Biashara yangu ya bata inahusiana nini na uzi juu
 
Wavaa kobazi wameungana kupinga Utakatifu wa Nyerere, Sasa wanaanza kumuita Mtakatifu kwa kejeli kabla ya Muda

Bila Nyerere Hawa wavaa kobazi hata hiyo Elimu wasingekuwa nayo ,

Wanatakiwa wamuheshimu sana
Hao wavaa kobazi ndio waliompokea na kumlea Nyerere.

Nyerere hazungumzwi kwa sababu ya ukatoliki wake. Kichwa unacho kazi yake ni kufikiri sio kujaza kinyesi
 
Wapigania uhuru wa Afrika hawakuwa viongozi wazuri wa nchi zao baada ya uhuru kupatikana, na sababu ni nyingi miongoni mwa hizo ni :-
1-Azma yao kubwa ni kujitawala, lakini utaalamu wa kujitawala walikuwa hawana.
2-Uendelezaji wa uchumi kutoka katika nidhamu ya kikoloni kwenda katika mfumo wa kitaifa uliaathirika.
3-Ukosefu wa wataalamu wazalendo katika fani mbalimbali.
4-Kutofautiana wenyewe kwa wenyewe katika njia gani ya kendesha nchi (ujamaa au ubepari).
5-Tofauti za kikabila, kiimani na hata kichama ziliweza kuwagawa baadhi ya viongozi.
6-Vita vya wenyewe kwa wenyewe.
7-Wakoloni kuwacha vibaraka wao kwa maslahi yao.
8-Elimu duni kwa wananchi.
9-Kuwasaidia wengine ambao waliyokuwa wakiishi chini ya ukandamizwaji ilhali uwezo wa kusaidia ni mdogo.
 
Mkuu Eyce, Merry Christmas to you Brother,

Mzee Nyerere is a controversial, enigmatic, mysterious and polarizing figures. Wengi wanamkubali na wengine hawamkubali, hasahasa kizazi ambacho kiliyaishi makosa ambayo aliyafanya Mzee Nyerere. Huu ndiyo ukweli mchungu. Kukosea kila mtu anakosea hapa duniani, jambo ambalo linanitatiza ni kwamba hata baada ya kuiingiza Tanzania vitani dhidi ya Uganda na kuifilisi Tanzania, Raisi Nyerere hakukubali makosa na akaendelea kutumia mkono wa chuma kudhibiti watanzania ambao walionekana kutoridhika na ile hali. Kwanini hakutaka kubadilika hata baada ya kuona watanzania wako kwenye lindi kubwa la umasikini ambao ulisababishwa na sera zake?

Miaka mitano ya mwisho ya Mzee Nyerere ilijaa taharuki mambo ya kuogopesha kuwahi kutokea Tanzania. Wengi hawafundishwi lakini Tanzania ilipitia changamoto nyingi za kiusalama, na ziliondoka punde tu baada Mzee Nyerere kung'atuka madarakani. Hebu tupitishane kwa harakaharaka.

1. Utekaji wa ndege uliofanya na vijana waliotaka Raisi Nyerere ajiuzulu.
2. Mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa na maafisa wa jeshi waliotaka Raisi Nyerere auawawe.
3. Uasi kanda ya ziwa, maafisa wa kijeshi huko mkoa wa Mara walianzisha nchi yao iitwayo Jamhuri ya Chui.
4.Mzee Nyerere anamrudisha Waziri Mkuu Sokoine madarakani huku akilalamika kwa Samora kwamba wanapishana.
5. Kuna minong'ono kwamba kuna chama cha kisiasa kinataka kuanzishwa na kina mahusiano na taifa la Ujerumani Mashariki.
6. Harakati za kusaka wahujumu uchumi zinaanza ambapo chama kiligawanyika na Sokoine katishia hadi maaskofu.
7. Waziri Mkuu anauwawa kwa ajali, jambo ambalo siyo kawaida kwenye msafara wake. Postmertem haikufanywa.
8. Nyerere anazungukwa na wajanja kina Thabiti Kombo ambao wanamwambia Mwinyi akubali kuwa Raisi.
9. Aboud Jumbe ameshinikizwa kwamba Zanzibar ijitoe kwenye muungano na anawekwa kizuizini.

Watanzania ni watu wenye utulivu mno, ukiona hadi wamefikia hatua ya kutumia jeshi, vurugu na kukuzunguka kisiasa, suala zima la kukubalika kwa Mzee Nyerere linatutia wengi ukakasi. Mwishoni Mzee alishindwa kuidhibiti dola na chama, watu wakawa wanamfanyia hujuma waziwazi. Nini kilipelekea hili kutokea ?​
 
Nyerere alikuwa tapeli na kibaraka kama alivyo sema Nkwame Nkrumah
Ndie aliye sababisha hatuna umoja wa Africa kama state badala yake akaleta regional blocks,
Ndie aliye asisi hili joka kuu Muungano na first born CCM,
Ndie aliye asisi mfumo wa chama kimoja kwa Tamaa zake mbaya(zidumu fikra za mwenyekiti),
Ali asisi ujamaa wa kitapeli wa kuua baadhi ya mahasimu wake kiuchumi.
Alikuwa sehemu ya mauaji ya Lumumba na Yule mawanaharakati wa msumbiji pale morogoro.
Japo hakuna ushaidi wa kuwa na Tamaa za pesa nyingi kama Mobutu, alikuwa na Tamaa
Za sifa entitlement kuwa ana akili.
Kwangu mimi huyu ndio anabeba lawama zote za mema na mbaya yaliyopo bongo
 
Hilo liko wazi kuwa aling'oka kwa aibu.
 
Asiyefanya kazi na asile....ndio kanuni insyofanya watu wajitume na kupelekea uvumbuzi mbalimbali duniani wa kurahisisha kazi na kuleta uhuru kwa mtu binafsi.... binadamu hawawezi kuwa sawa kwa sababu sio mifugo
 
Vita ya Kagera kisababishi ni Nyerere mwenyewe kwa uchokozi wake, akiingilia siasa za Uganda kwa kufadhili na kuwahifadhi waasi wa Obote ambao walikuwa wanaenda Uganda kujaribu kumuua Idd Amini
Ila History ya ki propaganda inasema Idd Amin aliibuka tu bila sababu yoyote kuja kuvamia Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…