Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Kiongozi lazima awe na principles zake, kusimamia kile anachokiamini mpaka mwisho, kiongozi asiye na msimamo ndie chanzo cha kuyumba kwa taifa lolote hapa duniani, leo atashika hiki atakiacha, kesho atashika kile nacho atakiacha...

Kulalamika miaka yote ya Nyerere kuwepo madarakani halafu bado hali ya maisha ya mtanzania ikaendelea kuwa mbaya, kwangu sioni kama kuna mantiki yoyote, kwasababu siku zote mabadiliko hayaji kwa usiku mmoja, ni mchakato.
Bwana Denoo,

Kumsoma MTAKATIFU RAISI NYERERE kwenye vitabu na kuishi kipindi cha utawala wake ni vitu viwili tofauti kabisa. Inawezekana kweli alikuwa ni mtu mwema kama unavyosema hapa, lakini nachotaka kuuliza ni kwanini mtu mwema alikosa kuwa na huruma na watanzania kipindi ambacho tulikuwa tunapitia kwenye umasikini hata wa kukosa nguo?

Tena mbaya zaidi, kwanini aliamua kutumia mkono wa dola kushughulikia watanzania waliokuwa wanahangaika kulisha familia zao. Mahakama walioitengeneza ilikuwa mwaka 1983 ilikuwa haina tofauti na THE STAR COURT CHAMBER iliyowashitaki wakina Lord Francis Bacon. Ulifanyika uvunjifu mkubwa mno wa haki za binadamu kuwahi tokea hapa nchini. Wengi tutatea kwasababu aidha tulikuwa wadogo, tulikuwa hatujazaliwa au tunafanya ushabiki.

Lakini nikwambie tu machache, ile mahakama ya SOKOINE ilikuwa ina 3 Personnel. Moja alikuwa mwanasheria na wawili ni watu kutoka vyombo vya usalama. Kanuni za mahakama (Special Tribunal) zilikuwa zinavunja miiko yote ya sheria za utu ambazo hata CCM na TANU waliziamini. Ile mahakama ilionea maelfu ya watanzania ambao walinyang'anywa mali zao na kutiwa kwenye lindi kubwa la umasikini. Kanuni za mahakama zilikuwa hivi endapo ukikamatwa:

1. Huna haki ya kupata wakili (No Right to Legal Representation)
2. Huna haki ya kukata rufaa (No Right to Appeal)
3. Huna haki ya kijitetea (No Right to be heard)

Ulikuwa ukikamatwa tu na mali yoyote, wewe ni muhujumu uchumi na unaswekwa ndani. Mwishowe mambo yalivyokuwa magumu wakaamua kuhamishia kesi zote Mahakama Kuu. Unafahamu ni kwanini walifanya hivyo ? Ndiyo maana huwa napata shida kuelewa lengo haswa la MTAKATIFU RAISI NYERERE lilikuwa ni lipi kwenye kufanya haya. Labda wewe unisaidie​
 
Nyerere alishaondoka duniani na madarakani, Leo tuna rais mwingine ambaye tatizo la umeme ameshindwa kutatua, wakati wa Nyerere hakukuwa na mgao wa umeme Tena tulikuwa na viwanda vikubwa.
Badala ya kupambana na Nyerere pambana na Ras wako anayekuletea mgao Hadi kipindi Cha mvua.
Matatizo makubwa ya nchi hii msingi wake ni utawala wa Nyerere. Kumbuka Hadi Leo tunatawaliwa kwa shuruti na katiba ya Nyerere. Chama kinachotutawala bila ridhaa yetu ni Cha Nyerere, na zaidi ya nusu ya falsafa zake Hadi Leo ni za Nyerere.
 
Sasa mzee wangu, majibu utayapataje wakati muhusika ameshafariki? Ilipaswa awe hai kisha umuulize mwenyewe uso kwa macho
Serikali ni taasisi, Uraisi ni taasisi inayoongoza Serikali hivyo kupatikana kwa majawabu ni rahisi tu. Mambo yote ambayo Raisi Nyerere aliwahi kuyafanya yalianza katika ngazi ya kisera na baadaye kutekelezwa kupitia sheria. Hivyo kwasababu wengi walikuwepo kipindi hicho ni rahisi kufahamu nini kilikuwa kinaendelea hadi kupelekea serikali kutengeneza sera za namna ile na baadaye kuzitungia sheria kandamizi vile.

Mfano, mwaka 1967 wakati tunatanzanga Azimio la Arusha, sababu zilizotolewa ni kwamba jamii ya Tanzania ilikuwa haina usawa kutokana miaka ya ukoloni. Hivyo kujenga usawa na kuondoa matabaka ni lazima nyezo zote za uzalishaji (Major Means of Production) zitaifishwe ili serikali iweze kutoa huduma kwa kila mwananchi. Atleast this is understandable. Ila kwanini serikali ilitumia dola na sheria kandamizi kuhakikisha watanzania tunalala njaa na kukosa hata mavazi mwilini, kwa miaka mitano mfululizo sijapata majawabu yake.

Lengo lake haswa kutuona tukiishi kimasikini vile ilhali ilikuwa inawezekana kutuachia kutafuta mahitaji yetu ilikuwa inawezekana. Somethings defy ordinary human comprehension.
 
Bwana Denoo,

Kumsoma MTAKATIFU RAISI NYERERE kwenye vitabu na kuishi kipindi cha utawala wake ni vitu viwili tofauti kabisa. Inawezekana kweli alikuwa ni mtu mwema kama unavyosema hapa, lakini nachotaka kuuliza ni kwanini mtu mwema alikosa kuwa na huruma na watanzania kipindi ambacho tulikuwa tunapitia kwenye umasikini hata wa kukosa nguo?

Tena mbaya zaidi, kwanini aliamua kutumia mkono wa dola kushughulikia watanzania waliokuwa wanahangaika kulisha familia zao. Mahakama walioitengeneza ilikuwa mwaka 1983 ilikuwa haina tofauti na THE STAR COURT CHAMBER iliyowashitaki wakina Lord Francis Bacon. Ulifanyika uvunjifu mkubwa mno wa haki za binadamu kuwahi tokea hapa nchini. Wengi tutatea kwasababu aidha tulikuwa wadogo, tulikuwa hatujazaliwa au tunafanya ushabiki.

Lakini nikwambie tu machache, ile mahakama ya SOKOINE ilikuwa ina 3 Personnel. Moja alikuwa mwanasheria na wawili ni watu kutoka vyombo vya usalama. Kanuni za mahakama (Special Tribunal) zilikuwa zinavunja miiko yote ya sheria za utu ambazo hata CCM na TANU waliziamini. Ile mahakama ilionea maelfu ya watanzania ambao walinyang'anywa mali zao na kutiwa kwenye lindi kubwa la umasikini. Kanuni za mahakama zilikuwa hivi endapo ukikamatwa:

1. Huna haki ya kupata wakili (No Right to Legal Representation)
2. Huna haki ya kukata rufaa (No Right to Appeal)
3. Huna haki ya kijitetea (No Right to be heard)

Ulikuwa ukikamatwa tu na mali yoyote, wewe ni muhujumu uchumi na unaswekwa ndani. Mwishowe mambo yalivyokuwa magumu wakaamua kuhamishia kesi zote Mahakama Kuu. Unafahamu ni kwanini walifanya hivyo ? Ndiyo maana huwa napata shida kuelewa lengo haswa la MTAKATIFU RAISI NYERERE lilikuwa ni lipi kwenye kufanya haya. Labda wewe unisaidie​
Ukijaribu kitazama vizuri, hayo mambo ya utawala wa enzi za Nyerere yana tofauti ndogo sana na sasa. Hata Sasa hakuna uhakika wa kupata haki huko mahakamani iwapo viongozi watatoa maelekezo toka juu. Unaweza kuporwa mali yako na viongozi na usifanye Lolote. Rejea alichofanya Magufuli na fedha za Plea bargaining, na fedha za bureau De change. Mabadiliko yaliyoko sasa ni maigizo tu, lakini tabia zile zipo Hadi Leo.
 
Msingi gani mbovu unazungumzia ikiwa Nyerere baada ya kuondoka madarakani, kila kitu walikipindua upside down?!

Ulichokiandika hapa hakina maana, kujenga taifa sio sawa na kujenga nyumba, taifa halijengwi kwa matofali kwamba ukikosea msingi uwe umeharibu, taifa linajengwa kwa akili zilizochangamka, hivyo kama tumeshindwa kujisogeza mbele hilo haliwezi kuwa kosa la Nyerere, kwasababu hakuondoka na akili zetu, labda aliondoka na zako!.

- Leo tuna wasomi wengi.

- Tuna kila aina ya maarifa.

- Vyuo vikuu vingi.

Kuendelea kumlaumu Nyerere, miaka 38 baada ya kuondoka madarakani ni udumavu wa kifikra, binafsi sioni kingine zaidi ya hicho. Ndio maana hata Nyerere mwenyewe kwa kutambua watu wake ni wajinga, aliwahi kunukuliwa akisema; "ajabu wanaacha yale mazuri yangu, wanachukua mabaya"!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Hapa hakuna anayelaumu. Anayezungumziwa ni Nyerere na madhaifu yake.

Nafikiri ukiambiwa msingi unaenda moja kwa moja kwenye matofali.

Hao waliobadilisha walibadilisha Nyerere akiwa hai.

Miaka zaidi ya 20 ingemtosha Nyerere kujenga Msingi imara wa kiutawala ili watawala waweze kusimamia Watu na raslimali zingine.

Mtoa mada ametoa maelezo ya mambo ambayo anayaona hayakuwa na msingi wowote wakati wa Nyerere.

Kwa mfano, kulikuwa na sababu gani ya maana ya Watu kuzuiwa kumiliki Mali ikiwa nchi ni huru na Watu wake wapo huru?

Msingi wa kifikra na kifalsafa ndio unaojenga taifa.
Mfano, Nyerere alikuwa na falsafa na fikra za Watu kujitegemea kupitia elimu ya kujitegemea lakini muda huohuo anashutumiwa kwa kukataa mawazo pinzani. Yeye ni wale wa zidumu fikra za mwenyekiti. Alafu muda huohuo Watu wakitegemea. Hivi ni akili hiyo
 
Bwana Denoo,

Kumsoma MTAKATIFU RAISI NYERERE kwenye vitabu na kuishi kipindi cha utawala wake ni vitu viwili tofauti kabisa. Inawezekana kweli alikuwa ni mtu mwema kama unavyosema hapa, lakini nachotaka kuuliza ni kwanini mtu mwema alikosa kuwa na huruma na watanzania kipindi ambacho tulikuwa tunapitia kwenye umasikini hata wa kukosa nguo?

Tena mbaya zaidi, kwanini aliamua kutumia mkono wa dola kushughulikia watanzania waliokuwa wanahangaika kulisha familia zao. Mahakama walioitengeneza ilikuwa mwaka 1983 ilikuwa haina tofauti na THE STAR COURT CHAMBER iliyowashitaki wakina Lord Francis Bacon. Ulifanyika uvunjifu mkubwa mno wa haki za binadamu kuwahi tokea hapa nchini. Wengi tutatea kwasababu aidha tulikuwa wadogo, tulikuwa hatujazaliwa au tunafanya ushabiki.

Lakini nikwambie tu machache, ile mahakama ya SOKOINE ilikuwa ina 3 Personnel. Moja alikuwa mwanasheria na wawili ni watu kutoka vyombo vya usalama. Kanuni za mahakama (Special Tribunal) zilikuwa zinavunja miiko yote ya sheria za utu ambazo hata CCM na TANU waliziamini. Ile mahakama ilionea maelfu ya watanzania ambao walinyang'anywa mali zao na kutiwa kwenye lindi kubwa la umasikini. Kanuni za mahakama zilikuwa hivi endapo ukikamatwa:

1. Huna haki ya kupata wakili (No Right to Legal Representation)
2. Huna haki ya kukata rufaa (No Right to Appeal)
3. Huna haki ya kijitetea (No Right to be heard)

Ulikuwa ukikamatwa tu na mali yoyote, wewe ni muhujumu uchumi na unaswekwa ndani. Mwishowe mambo yalivyokuwa magumu wakaamua kuhamishia kesi zote Mahakama Kuu. Unafahamu ni kwanini walifanya hivyo ? Ndiyo maana huwa napata shida kuelewa lengo haswa la MTAKATIFU RAISI NYERERE lilikuwa ni lipi kwenye kufanya haya. Labda wewe unisaidie​
Kwanza sijui kwanini unatumia jina MTAKATIFU ikiwa bado Kanisa Katoliki halijamuidhisha kuitwa hivyo, sijui una malengo gani, muhimu ukumbuke tu, chakula huliwa kikiwa na chumvi ya wastani, ikizidi au kupungua huondoa ladha kwa walaji.

- Hilo suala la huruma unalozungumzia sijui hata unataka huruma ya aina gani? kwani ni kiongozi gani wa hili taifa amewahi kuwa na huruma na watanzania? tena kwangu afadhali ya Nyerere kuliko hawa waliomfuatia, ni walafi na mafisadi wa kutisha, tuliza mihemko utafakari kwa makini.

- Unaposema kuwashtaki waliokuwa wakilisha familia zao una maana gani? hao waliolisha familia zao walifuata sheria za wakati huo au walikiuka? kama walikiuka kwanini sheria isichukue mkondo wake? nakuona upo upande wa kutetea wahalifu bila sababu ya msingi.

Sitaki kuamini kama Nyerere na Sokoine walikuwa wakikamata watu hovyo barabarani na kuwabambikia kesi kama unavyotaka kuonesha hapa, hao waliokamatwa palikuwepo na vyombo vya usalama wakati huo vikajiridhisha, kama hawakuwa na maelezo ya kutosha kuelezea walipopata hizo mali sioni tatizo kwao kukamatwa.

- Ajabu kwako wahujumu uchumi unawaona wajanja kwa kuwaita walikuwa na akili za haraka, mindset yako na Nyerere ziko tofauti kabisa, hivyo sishangai ukimuona mkosefu. Jiulize; hao wenye akili za haraka leo wako wapi na wengine kule vijijini/mijini nao wako wapi kiuchumi? Jibu unalo.

Suala la mahakama kuwa ya aina gani hilo kwangu siwezi kuingilia, wao ndio walioona pawepo na mahakama ya aina gani kwa wakati husika ili kupeleka mambo kwa haraka, kama mambo yaliharibika mbeleni nimeshakwambia Nyerere nae hakuwa malaika, alikosea kama hawa wanaokosea wakati huu, sijui kwanini unalazimisha makosa ya Nyerere yaonekane ndio makubwa kupita ya wote waliomfuatia.

NB.
Matumizi ya neno MTAKATIFU kwenye majibu yako kwangu naona unavuka mipaka, ni either uache kutumia hilo neno, niendelee kuwepo hapa, au uendelee kulitumia hilo neno niondoke hapa. Hayo mambo kwa sasa yapo chini ya Kanisa Katoliki kimchakato, hivyo naamini huna sababu yoyote ya maana ya kutumia jina hilo zaidi ya ujuaji ulionao.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Ndiye Rais pekee aliyejitambua na kuthamini kila binadamu na kumpa thamani yake

FB_IMG_1654103401853.jpg
 
Ubepari ni ushetani. Wewe una njaa lakini mwenzako anasaza bila huruma ndivyo tunaishi hivyo kwa sasa. Ujamaa unataka wote muende pamoja hata mtu wa mwisho kabisa naye awezeshwe ndio maana tunaita ujamaa ni utu. Hamuoni licha ya matatizo tuliyonayo lakini mtu yupo radhi awe na fedha ambazo hatomaliza milele? Watu wanamiliki magari na majumba ya kifahari na ni viongozi wa serikali na kulipwa fedha nyingi ukiachia mbali kuiba lakini watu wanakosa huduma muhimu?
Wakati tunavaa viraka na kukosa mahitaji muhimu ilikuwa kipindi Cha ubepari?
 
Sera ya ujamaa na kujitegemea haikuwa mbaya kwa kiwango hicho.

Leo una sehemu ya kuishi, umesoma unatukana Nyerere.

Of course, wenye mali kwa wakati huo, wenginwakiwa wahindi ambao kiuhalisia walipewa upendeleo.wakati wa ukoloni ndio walikuwa na mali ndio waliumia
Leo nchi hii bado Ina ardhi, una kisehemu cha kuishi unabweka bweka tu.

Nenda Kenya kwa Mabepari ukajionee.

Wakati wa uhuru,umoja ulihitajika kuliko chochote.

Cooperative zilikuwa chini ya Nani kabla ya kuwekwa chini ya TANU?

Watu binafsi kina ani waliokuwa na uwezo huo?

Huu ni uwongo.

Uhuru wa mawazo, kivipi wakati hakukuwa na magazeti Wala social network.

Sana sana waliokuwa na vita na Nyerere zilikuwa za madaraka hasa kutokana na kutofautiana itikadi.

Kuna watu walitaka , wakitoka wakoloni wao ndio wawe wakoloni.

Wengine walitaka nchi iwe na dini.

Wengine walitaka makabila yao yawe TOP Kwasababu wamesoma kuliko wengine. Ulitakaje?

Ujamaa umefeli miaka ya 1980's haya tangu wakati huo mmeshafanya nini nje ya mawazo ya Nyerere.

  • Kaacha mashirika ya umma zaidi ya 400
  • Kaacha viwanda vya kutosha Kama General Tyre, Musoma Textile, Mwamza Textile etc leo mmefika wapi?

Nyerere ameachiwa Madaraka mwenyewe kwa hiari miaka 1985 huku nchi ikiwa mbichi.
  • Hakuchimba madini
  • Hakuuza bandari, Ngorongoro Wala Loliondo

Aliemdesha nchi hivyo kigumu kwa kutumia mazao ya wakulima.

Haya nyie Sasa hivi baada ya miaka karibu 40 mko wapi, zaidi ya kunywa makonyagi na kufirwa tu ndio mmegundua.
Unasema kina nani walikuwa na uwezo wa kuagiza vitu nje ? Kwan Mwinyi aliporuhusu ni nani walikuwa wanaagiza ?

Aliminya maoni, gazeti la serikali tu, Redio moja nch nzima hakuna nyingine, Huruhusiwi kumiliki TV au Radio, ukikutwa na computer 💻 ni kosa kubwa wanaweza kukutoa pumbu bila ganzi kisha wakupe ule na pilipili

Hivyo viwanda Nyerere kaviacha vina hali mbaya balaa, mitambo ilikuwa ipo very outdated, productions cost zikiwa juu unrealistically, mauzo yakiwa chini sanaaa, (mana aliua uchumi wa mtu mmoja mmoja yeye mwenyewe) ,
Sema tu aliacha magofu ya viwanda,

Kifupi tu Nyerere ni raisi wa ovyo sana hii nchi kupata
 
Ndiye Rais pekee aliyejitambua na kuthamini kila binadamu na kumpa thamani yake

View attachment 2852299
Ila Nyerere naye kwa maigizo alikuwa hajambo. Anapanga mstari kuwa anachagua kiongozi, lakini tayari alikuwa na matokeo mfukoni! Ogopa kiongozi aliyekuwa anaamini kiongozi wa kweli atatoka ccm, yaani Hawa watoto wa kina Mwigulu ndio Nyerere alimaanisha hao!
 
Mtoa mada nadhani unakosea kwa kusema Nyerere hakuwa na huruma hata kidogo. Umechambua upande wa udhaifu wake ndio maana unaona hakua na huruma hata kidogo.
Chambua na upande wa mazuri yake ndipo utaiona huruma ya Nyerere kwa wananchi wake.
1. Nyerere kwa kipindi alichoongoza alikua na nafasi ya kuiba mali za umma na kujilimbikizia kadri atakavyo na asingekuwepo wa kumpigia kelele lakini hakufanya hivyo.
2. Mwl. J.K. Nyerere angetaka kutoa madaraka makubwa kwa watoto wake angefanya hivyo lakini mpaka sasa nadhani Makongoro Nyerere ndio kakumbukwa juzi hapa kuwa Mkuu wa Mkoa angalia hao wengine wanavyowapaisha watoto wao.
Inakua rahisi kumchambua udhaifu wake kwa kuwa kimepita kipindi kirefu inakua rahisi kuona makosa yake.
Kumbuka:
3. Mwl. Nyerere alitoka madarakani Nchi ikiwa na viwanda vingi sana lakini kutokana na ubinafsi na Ubepari leo hii viwanda karibu vyote vimeuzwa na kutelekezwa matokeo yake ajira nyingi sana zimepotea.
4.Harakati za kuunganisha Nchi unaweza kuzichukulia rahisi kwa kuwa unaona matokeo tu lakini mchakato wake sio wa kubeza. Pale ilifanyika kazi kubwa sana kuwaungansha watanzania na kuondoa ukabila na udini.
5. Nadhani nia ya Mwl.ilikua nzuri sana ila matokeo ndio hayakua mazuri.
Kitu kingine matokeo ya vita ya Kagera kwa uchumi wetu ilileta athari kubwa sana.
Vile vile Mwl.alijihusisha sana na ukombozi wa Nchi nyingine za Afrika. Hivyo alikua na mambo mengi sana ya kupigania katika lindi la ufukara wa Taifa.
Tujiulize
Miaka 38 tangu Mwl. Nyerere atoke madarakani ni eneo gani kama Taifa tunalifanya kwa ufanisi ndani ya Ubepari.
Nadhani sekta ya uchawa tu ndio tuko njema zaidi.
Mwl.apewe heshima yake
Masuala ya msingi ambayo nataka mnieleweshe ndugu watanzania ili niwaelewe vizuri.

Mosi, hivi kweli mna uhakika kwamba bila Ujamaa nchi ya Tanzania isingeendelea na kuwa na umoja wa kitaifa ? Kwamba nchi zote ambazo wanatumia mfumo wa Ubepari hawana umoja wa kitaifu, utulivu na maendeleo. Au mnataka kuniambia nchi ambazo zinafanya vizuri sana kiuchumi leo hii ni kwasababu ya mfumo wa Ujamaa?

Pili, kukosea kila kiongozi anakosea. MTAKATIFU RAISI NYERERE hakuwa malaika. Ila unafanya nini baada ya kuona umekosea, hilo ni suala jingine kabisa. Tokea mwaka 1970 baada ya matatizo ya uchumi yaliyoikumba dunia, wachumi wetu nguli kama Edwin Mtei na Justinian Rweyemamu walimshauri MTAKATIFU RAISI NYERERE kufanya mabadiliko fulani fulani, lakini akagoma. Baada ya uchumi kuanguka mwaka 1980 na Tanzania kuishiwa kabisa FOREX Reserves, Mzee Nyerere bado aliendelea kugoma kubadilika. Hata pale alipoona watanzania ni masikini wa kutupwa. Tena akatumia mkono wa chuma kutuumiza. Hivi mtu mwenye UTU na UUNGWANA anaweza kufanya vile kweli kwa watu ambao wanahangaika na umasikini ? Lengo lake haswa lilikuwa nini ?

Tatu, MTAKATIFU RAISI NYERERE alikuja kuzikubali sera zote ambazo alizikataa mwanzoni. Ambacho wengi hamkifahamu ni kwamba STRUCTURAL ADJUSTMENT PROGRAM (SAP) zilisainiwa na Raisi Nyerere wakati anaondoka Ikulu na kuanza kutekelezwa na Raisi Ali Hassan Mwinyi wakati Raisi Nyerere bado ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi. Hapa huwa napata shida sana kumuelewa Nyerere, kama sera hizi alizikataa miaka ya 70's kwanini alikuja kuzikubali tena miaka ya 80's ilhali akifahamu kwamba ni mbaya ?

Hebu tusaidiane hapa....​
 
Sikuwepo duniani kipindi cha Nyerere,lakini kupitia maandiko mbalimbali unaweza kuona utawala ule ulikua na ahueni kwa wananchi licha ya changamoto mbalimbali zilizojitokeza.waliokuwepo enzi hizo wanasema hakukua na mgao wa umeme,elimu ilikua bora zaidi,huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kwamba zilikua chache lakini zilitolewa kwa wakati na bila upendeleo wowote na tena kwa kiwango cha juu, utu wa Mtanzania ulikua ni kipaumbele cha serikali, serikali iliwajibika kisawasawa.je tujiulize miaka 38 sasa tangu Nyerere atoke madarakani zaidi ya kuongezeka majengo marefu kwenye miji mikubwa kama Dar nini cha maana serikali zilizopita zimefanya ambacho hakikufanywa na serikali ile ya Nyerere?
Hebu tusaidiane ndugu yangu, huo umeme unaouzungumzia ulikuwepo mikoa mingapi hapa Tanzania ?
 
Sera ya ujamaa na kujitegemea haikuwa mbaya kwa kiwango hicho.

Leo una sehemu ya kuishi, umesoma unatukana Nyerere.

Of course, wenye mali kwa wakati huo, wenginwakiwa wahindi ambao kiuhalisia walipewa upendeleo.wakati wa ukoloni ndio walikuwa na mali ndio waliumia
Leo nchi hii bado Ina ardhi, una kisehemu cha kuishi unabweka bweka tu.

Nenda Kenya kwa Mabepari ukajionee.

Wakati wa uhuru,umoja ulihitajika kuliko chochote.

Cooperative zilikuwa chini ya Nani kabla ya kuwekwa chini ya TANU?

Watu binafsi kina ani waliokuwa na uwezo huo?

Huu ni uwongo.

Uhuru wa mawazo, kivipi wakati hakukuwa na magazeti Wala social network.

Sana sana waliokuwa na vita na Nyerere zilikuwa za madaraka hasa kutokana na kutofautiana itikadi.

Kuna watu walitaka , wakitoka wakoloni wao ndio wawe wakoloni.

Wengine walitaka nchi iwe na dini.

Wengine walitaka makabila yao yawe TOP Kwasababu wamesoma kuliko wengine. Ulitakaje?

Ujamaa umefeli miaka ya 1980's haya tangu wakati huo mmeshafanya nini nje ya mawazo ya Nyerere.

  • Kaacha mashirika ya umma zaidi ya 400
  • Kaacha viwanda vya kutosha Kama General Tyre, Musoma Textile, Mwamza Textile etc leo mmefika wapi?

Nyerere ameachiwa Madaraka mwenyewe kwa hiari miaka 1985 huku nchi ikiwa mbichi.
  • Hakuchimba madini
  • Hakuuza bandari, Ngorongoro Wala Loliondo

Aliemdesha nchi hivyo kigumu kwa kutumia mazao ya wakulima.

Haya nyie Sasa hivi baada ya miaka karibu 40 mko wapi, zaidi ya kunywa makonyagi na kufirwa tu ndio mmegundua.
Ujamaa haukuwa mbaya kwa hivyo ni kweli, ila ujamaa ulikuwa sio kabisa. Nyerere aliacha viwanda 400+, lakini ukweli ni kuwa vingi vilikuwa vimekufa au vinaelekea kufa. Misingi mibovu ya kiutawala ya Nyerere ndio tatizo Hadi sasa, na tatizo kubwa ni hii katiba iliyomfanya yeye kuwa Mungu mtu.
 
Hapa hakuna anayelaumu. Anayezungumziwa ni Nyerere na madhaifu yake.

Nafikiri ukiambiwa msingi unaenda moja kwa moja kwenye matofali.

Hao waliobadilisha walibadilisha Nyerere akiwa hai.

Miaka zaidi ya 20 ingemtosha Nyerere kujenga Msingi imara wa kiutawala ili watawala waweze kusimamia Watu na raslimali zingine.

Mtoa mada ametoa maelezo ya mambo ambayo anayaona hayakuwa na msingi wowote wakati wa Nyerere.

Kwa mfano, kulikuwa na sababu gani ya maana ya Watu kuzuiwa kumiliki Mali ikiwa nchi ni huru na Watu wake wapo huru?

Msingi wa kifikra na kifalsafa ndio unaojenga taifa.
Mfano, Nyerere alikuwa na falsafa na fikra za Watu kujitegemea kupitia elimu ya kujitegemea lakini muda huohuo anashutumiwa kwa kukataa mawazo pinzani. Yeye ni wale wa zidumu fikra za mwenyekiti. Alafu muda huohuo Watu wakitegemea. Hivi ni akili hiyo
Nimeshakwambia Nyerere aliondoka madarakani miaka 38 iliyopita, kwani aliondoka na akili zetu mpaka tuendelee kumlaumu mpaka leo? hapa sio suala la msingi wala paa!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Ujamaa haukuwa mbaya kwa hivyo ni kweli, ila ujamaa ulikuwa sio kabisa. Nyerere aliacha viwanda 400+, lakini ukweli ni kuwa vingi vilikuwa vimekufa au vinaelekea kufa. Misingi mibovu ya kiutawala ya Nyerere ndio tatizo Hadi sasa, na tatizo kubwa ni hii katiba iliyomfanya yeye kuwa Mungu mtu.
Miaka 38 tangu ametoka madarakani, hiyo misingi imara mnasubiri mpaka afufuke aje kutengeneza?
 
Back
Top Bottom