Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Wajamaa mnisaidie, hivi Nyerere aliwezaje kuvumilia haya?

Unaonekana una tatizo binafsi na Nyerere, unataka kutudanganya hapa viwanda vyote alivyoacha Nyerere havikuwa vikifanya kazi?!

Ile General Tyre kule Arusha haikuwa ikifanya kazi? Mwanza Textiles haikuwa ikifanya kazi? Musoma... Tanga....

Wewe ni muongo, mmejaa ushabiki maandazi tu na wenzako hamna hoja yoyote zaidi ya mihemko.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Wewe ndio unasikiliza propaganda za TBC kuwa kipindi cha Nyerere nchi ilikuwa ya maziwa na asali lakini sivyo

Hivyo viwanda alivyoacha Nyerere vilikuwa na output ndogo kuliko gharama, bidhaa za bei juu na quality ya chini huku serikali ikitakiwa kuvipa tena hela
Yaani ni vilikuwa vimejifia tu
Ndio maana nikatolea case study kiwanda cha bia cha TBL, ambacho kilikuwa kiwanda bora kabisa kabla Serikali ya Nyerere haijakitaifisha..... Baada ya kutaifisha kiwanda kikawa hakina ufanisi tena, hadi mwnyi alipochukua uamuzi mgumu wa kubinafsisha ndio tuna TBL ya leo, mlipakodi mkuu wa serikali na ajira za moja kwa moja nyingi
 
Wacha usanii, wewe ulikuwa unamsifu Mkapa kwa vigezo gani?!

Umenifanya nimecheka, kumbe hukuwa na vigezo vyovyote vya kumsifu Mkapa!

Mimi sikuja na mada hapa ya kumsifu au kumponda anyone, wewe mleta mada ndie mwenye jukumu la kutuonesha ubaya wa yule unayemponda, kisha utuoneshe uzuri wa yule unayemkubali kwa vigezo, wala sio kuishia kumtaja kwa jina tu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Waswahili husema maneno matupu hayavunji mfupa. Dunia nzima inafahamu kwamba kwa mara ya kwanza uchumi wa Tanzania unakua kwa asilimia 7% na zaidi kwa mwaka ni kazi ya Mzee Mkapa. Hata kipato cha mwananchi mmoja-mmoja kupanda ilikuwa ni kipindi cha Mzee Mkapa. Ni mtu asiyefahamu tu, ndiyo atapingana na huu ukweli.​
 
Wewe ndio unasikiliza propaganda za TBC kuwa kipindi cha Nyerere nchi ilikuwa ya maziwa na asali lakini sivyo

Hivyo viwanda alivyoacha Nyerere vilikuwa na output ndogo kuliko gharama, bidhaa za bei juu na quality ya chini huku serikali ikitakiwa kuvipa tena hela
Yaani ni vilikuwa vimejifia tu
Ndio maana nikatolea case study kiwanda cha bia cha TBL, ambacho kilikuwa kiwanda bora kabisa kabla Serikali ya Nyerere haijakitaifisha..... Baada ya kutaifisha kiwanda kikawa hakina ufanisi tena, hadi mwnyi alipochukua uamuzi mgumu wa kubinafsisha ndio tuna TBL ya leo, mlipakodi mkuu wa serikali na ajira za moja kwa moja nyingi
Hiki ulichoandika hapa ni muendelezo wa ujinga ule ule wa kumlaumu Nyerere kwa kila jambo, amejenga viwanda, akaviacha hapo, badala ya kuviendeleza mkaviua kabisa, kama tatizo lilikuwa management au vinginevyo nini kiliwashinda kutafuta management nzuri ya kuviendeleza?

Usiniletee ngonjera za TBC hapa, hamna jipya.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Waswahili husema maneno matupu hayavunji mfupa. Dunia nzima inafahamu kwamba kwa mara ya kwanza uchumi wa Tanzania unakua kwa asilimia 7% na zaidi kwa mwaka ni kazi ya Mzee Mkapa. Hata kipato cha mwananchi mmoja-mmoja kupanda ilikuwa ni kipindi cha Mzee Mkapa. Ni mtu asiyefahamu tu, ndiyo atapingana na huu ukweli.​
Huo uchumi ulivyopanda ndio ndugu zetu kule vijijini wakaacha kuvaa viraka vile alivyowaachia Nyerere?!

Tusidanganyane hapa kwa 7% ya kwenye makaratasi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Hiki ulichoandika hapa ni muendelezo wa ujinga ule ule wa kumlaumu Nyerere kwa kila jambo, amejenga viwanda, akaviacha hapo, badala ya kuviendeleza mkaviua kabisa, kama tatizo lilikuwa management au vinginevyo nini kiliwashinda kutafuta management nzuri ya kuviendeleza?

Usiniletee ngonjera za TBC hapa, hamna jipya.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Sio kumlaumu tunataja facts, facts ambazo unaweza kuzi verify kama ni uongo ama kweli
Huwezi kuzuia kujadiliwa kwa Nyerere kwa mabaya au mazuri sababu tayari alishakuwa kiongozi wa kitaifa hivyo lazima ajadiliwe tu

Naona utakuwa na tatizo la uelewa pia au kukaririshwa mambo na kushindwa kuyafanyia utafiti, maana hilo la viwanda nishakujibu mara 3 ila umebaki na ulichokaririshwa, umeshindwa hata kwenda kusoma hivyo viwanda vilikuwa katika hali gani

Ujinga wa nyerere umerekebishwa kwa kiasi japo bado kazi ipo
 
Huwa najiuliza sana lakini sipati majawabu, lakini naomba wasomi wa humu ndani mnisaidie.

Hivi Mzee Nyerere alikuwa ana roho ya namna gani kuona mambo kama haya yakitokea kwa wananchi lakini bado hataki kubadilika na akaendelea kutumia mkono wa chuma kuhakikisha anasigina kabisa uwezo binafsi wa mtanzania kuweza kujikwamua kiuchumi. Ujamaa wa Tanzania hakuleta matokeo yoyote makubwa na ya kuchangaza ukilinganisha na kule Asia na Ulaya ambako walau walifanya mapinduzi ya sayansi na teknolojia.

Uchina walifanikiwa sana baada ya Raisi Deng Xiaping kuanza kuwaonea huruma raia wake akifahamu kabisa kwamba njia waliyokuwa wanaenda ilikuwa siyo sahihi. Aliruhusu watu waanze kumiliki mali zao binafsi na kufanya biashara. Najiuliza sana, miaka yote 18 ya Ujamaa, yalifanyika na kutokea mambo mengi mno kwa watanzania, kiasi kwamba kiongozi yoyote mwenye huruma na wananchi ni lazima angekaa chini na kujifanyia tathmini, lakini Raisi Nyerere hakufanya hivyo, aliendelea kuwa na moyo mgumu kama Farao. Hebu tuzingatie haya:

1. Sera ya utaifishaji wa mali, ilileta umasikini mkubwa sana kwa watu.
2. Kufuta vikundi ya ushirika (Cooperatives) na kuweka vile vya TANU kulididimiza mno sekta ya kilimo.
3. Kupiga marufuku watu binafsi kuagiza bidhaa nje ya Tanzania kulipelekea uhaba wa bidhaa na huduma muhimu.
4. Kuweka ugumu katika kusafiri (Travelling Restrictions) kulisababisha ukosefu wa ujuzi kwa watanzania.
5. Kuminya uhuru wa mawazo na kutumia nguvu ya dola kunyamazisha watu kulidumaza ukomavi wa demokrasia.

Mpaka kufika miaka ya 80's Ujamaa ulikuwa umefeli vibaya mno. Tanzania tulikuwa hatuna hata unga wa kupikia, mafuta, wala sukari. Mtaa mzima mlikuwa mnaenda kwa mwenyekiti kuomba sukari au sabuni kutoka maduka ya ushirika. Ukikamatwa na mafuta, sabuni au dawa za binadamu zilizolanguliwa kutoka Kenya lazima ushughulikiwe na dola. Kama ulisoma miaka ya 80's unaweza kukumbuka kwamba hata sare za shule zilikosa rangi, watu tukawa tunavaa vitu vya ajabu vilivyochakaa kama vile vichaa. Ukibahatika kukutana na wamishionari au taasisi za kidini ndiyo ulikuwa unaweza kupewa hata nguo, mahitaji na wazungu.

Yote haya yanafanyika, Mzee Nyerere na Sokoine wakaingia mtaani kuanza kushughulikia maelfu ya watanzania ambao wanahujumu uchumi. Ila ukifuatilia zile kesi nyingi, utafahamu kwamba hao wahujumu uchumi ni wale watanzania wenye akili za haraka ambao walijiongeza na kuweza kupata mahitaji muhimu ili kuhudumia familia zao. Wahujumu uchumi kwelikweli, ambao wengi walikuwa ni vigogo wa serikalini hawakuguswa. Kiukweli, kama nchi ina kiongozi mwenye huruma haya yote yasingetokea bila yeye kujirudi.

Hivi kwanini MTAKATIFU na MWENYEHERI, Raisi Nyerere hakuwa na chembe ya huruma moyoni ?
Kuna mambo nikikumbuka huwa naumia sana na nakosa majawabu. Hivi alikuwa anapenda kutuona sisi vile ?​

Successors wake wamebadili nini ama wameleta fundamental changing zipi? Hata Yule wa Kizimkazi ndo kazidi kuididimiza ft 12 Tanganyika bado humlaumu unabaki kubweka kama koko badala uangalie Ndio tuliwahi jikwaa so what? Leta solution sio kufungua pages zilizopita akati zilizopo huzisomi? Tunaongela 40years back yet todate nchi haina umeme bado raia wanashindia uji we unaleta mambo kikoloni wakati huu kha[emoji1544][emoji1544], we zuzu tu kama Kizimkazi na Msoga!
 
Successors wake wamebadili nini ama wameleta fundamental changing zipi? Hata Yule wa Kizimkazi ndo kazidi kuididimiza ft 12 Tanganyika bado humlaumu unabaki kubweka kama koko badala uangalie nini tufanye sasa baada ya miaka 40. Ndio tuliwahi jikwaa so what? Leta solution sio kufungua pages zilizopita akati zilizopo huzisomi? Tunaongela 40years back yet todate nchi haina umeme bado raia wanashindia uji we unaleta mambo kikoloni wakati huu kha[emoji1544][emoji1544], we zuzu tu kama Kizimkazi na Msoga!
 
Nakubali kwamba Tanzania kuna changamoto nyingi tu, niseme haya yafuatayo:

Mosi, Tanzania inaweza kutengeneza Healthiest Dependency Ratio kwasababu, watu wenye uwezo wa kufanya kazi (Working Age Population) ni wengi kuliko wale wasioweza kufanya kazi (Dependents). Hili ni tatizo la kisera ambalo serikali ikiwa makini inaweza kulimaliza kama Uchina walivyofanya. Injecting the youths into the Market, either through employment and self-employment. Tanzania imejaa vijana waliomaliza chuo kikuu wenye utaalamu mwingi ambao wanaweza kufanya kazi endapo watawezeshwa na kusaidiwa.

Pili, FDI ni muhimu na Tanzania ni nchi ambayo ni kivutio kikubwa. Hili mbona halina ubishi. Tatizo ni lilelile la kisera, kwamba tunafanyaje kuhakikisha kwamba watanzania wa kawaida wananufaika na uwekezaji kutoka nje, aidha kwa kupitia kodi, ajira, ujuzi na ushirikishwaji katika uwekezaji. Mpaka sasa faida haionekani kwasababu kuna sehemu panavuja na hatujasimama kidete kuhakikisha tunarekebisha. Mashirika mengi yanapewa Tax Holidays na mikataba ya uwekezaji ina changamoto kama ule wa bandari. Ila binafsi naamini leo hii tukiamua kukusanya kodi kwa mashirika yanayowekeza hapa nchini, hela ipo nyingi mno.

Tatu, kwenye biashara ya kimataifa sisi ni Commodity Based Economy bado hatujawa Industrial Based Economy au Financial Based Economy nadhani tuendelee kujikita huko ambako tuna Comparative Advantage. Soko la dunia ya leo linahitaji sana rasilimali za uzalishaji ambazo Tanzania inazo kwa wingi na zinaiuzwa kwa Benchmark Price. Tunaweza kufanya mambo mengi mno kupitia Bilateral Trade na tukafanikiwa vizuri sana, tatizo ni kwamba watu wanafanya maksudi kwasababu wanataka kupata mafungu ya kumi (Ten Percent).

Nne, viwanda vidogo-vidogo vya kutengeneza Toothpick vinaweza kuanzishwa nchini Tanzania hata kesho endapo tutaamua. Kipindi hiki inawezekana kwasababu watu wengi wana mitaji na ujuzi, na uwepo wa soko la ajira la bei nzuri (Cheap Labour). Tatizo tunarudi palepale, kwamba watu wananufaika wenyewe na hii hali.

Niseme tu, hakuna pesa ambayo inatengenezwa Tanzania isionekane. Pesa zipo lakini zinaingia mifukoni kwa watu ndiyo maana uchumi kweli unakua lakini wewe mtu wa kawaida huuoni kwasababu, watu wachache wanazitafuna na kujimilikisha nchi. Hili ndiyo changamoto yetu Tanzania.​
NCHI NGUMU

Ukiona watu wanakimbilia madaraka na kutafuta vyeo vikubwa vya nchi, ipo namna jambo hili ni la kushangaza sana !
Muingereza aliyesema 'Only Fools rush In' alikuwa mwerevu...

Matatizo ya kitaifa, tuseme ya kinchi-dola ni adha mchangamano za ufahamu, utayari, upeo na uwezo -- si tu miongoni mwa watawala/viongozi/watu wa madaraka -- ni suala la umma wote; iivyo ni wananchi wote.

Sisi kama wananchi hatuna budi kuhimizana, kukumbushana, kuoneshana na kuimarisha mapito yetu katika safari ya kuhama kutoka katika ustawi duni kuelekea katika ustawi bora.

Jitihada zetu sisi kama watu, ikiwa tunafanya vizuri katika kuwa 'chumvi ya dunia na nuru ya ulimwengu'; basi ndiyo mengi mabovu katika ulimwengu wa leo yataanza kuyeyuka na hatimaye kutoweka.

Mwalimu Kambarage Nyerere, siyo mtu wa kufananisha na aina yeyote ya viongozi-viti/viongozi madaraka... Kwa kuwa huyu alikuwa ni mtu wa maono, nidhamu, uthubutu na kukomaa; chochote unachoweza kukitafsiri labda 'alifanya makosa' hiyo inaweza kuwa ni 'busara ya mtu kwa wakati'. Ukijua ilivyobora, utabadili fikra hasi/mashaka/dharau dhidi yake--kama unayo kwa muktadha huu ama mwingine.

Mwalimu Kambarage Nyerere alikuwa ni mtu wa Imani, Tumaini na Pendo-Utumishi... Tafakari kuhusu dhamiri ya 'Kuuwasha Mwenge wa Uhuru', utavibaini hivi vitatu; na hivi si 'vitu vyepesi vyepesi' kama matamanio ya madaraka ya mchongo...

Tazama media hii:

View: https://www.youtube.com/watch?v=Ur8EbQ2F2x4

Kwenye hii media, 1988, Mwalimu Nyerere zungumza mengi -- mengi kuhusiana na 'Uhuru wa Bendera', 'changamoto za Ubeberu wa Kaskazini/Magharibi dhidi ya Kusini isiyo na mshikamano.

Kubwa la kuchukua katika hiyo khotuba ya Mwalimu ni ukweli, uhalisia na vizingiti vya 'Mifumo'; mifumo ya dunia kiuchumi, tawala na siasa.

SASA, wito aliutoa Mwalimu kwetu sisi, hiyo jana na hata sasa, ni kuzitazama kwa karibu na umakini changamoto hizi za mifumo; kuzitazama kwa jicho la tatu ili sisi watu wa mataifa machanga tuweze kuotea muktadha wa mshikamamo kwa ajili ya kujikwamua na 'undava wa mataifa yaliyoendelea'.

Humo kwenye hiyo media anatoa kabisa mifano halisi ya kimaisha na harakati kupambana na 'hali ilivyo'; Visa vya kwa mfano, Rais Ronald Regan wa Merekani kuona jitihada za kujenga umoja wa sauti na makubaliano ya mataifa ya kusini kama 'mchezo mchezo' , jitihada za awali kupitia mkutano mmoja kule Amerika ya Kusini'--yeye Reagan kusisitiza hijimoni za 'Uliberali Kiuchumi'; kwa maana ya yeye kuyapendekezea mataifa kama yetu eti tuwe na juhudi za kutanua wigo wa 'soko huria'...

Sasa uliberali Masoko, bado hata leo unanufaisha mataifa yaliendelea, tena kwa sababu zile zile ambazo Mwalimu Nyerere anazitaja katika hotuba hiyo: Biashara Globali zinazodhibitiwa ama kulinda maslahi ya nchi zenye viwanda vikubwa... Haya yote ni adha za kukosekana kwa makubaliano ya kimataifa ama makubaliano yanayokosa mkazo kwa upande wa nchi zetu changa, ama pia kudharauliwa mbele ya mataifa yaliyoendelea; na kumbe, kwa upande wa vinara wa mifumo, wao 'wamejipanga kweli' na figisu za namna moja hata ingine.

Kwa hivyo na sisi tunajipangaje?

Kitaifa, bado tunajisuka kitaasisi...

Katika hili la kujisuka kitaasisi, ni vema sote tufahamu fika... Jukumu la kuyaleta mageuzi ya kijamii ni la kwetu sote. Hili daima ni msalaba wetu, na basi tuubebe pasi manung'uniko.

Haitufadii kitu, tukiendekeza kasumba za kuwatazama viongozi wa nchi kama 'wakombozi' ama 'vinara' wa mabadiliko jamii; kwa maana hata wao kasumba zao ama/na mapungufu yanayoweza kukwamisha 'harakati' -- vyovyote vile, viongozi hawa ni ndugu zetu, ikiwa tuna nidhamu bora ya utu kiroho, maadili na miiko tunaweza kuwasahihisha ama basi kujisahihisha pamoja kama wananchi.

Tunalo jukwaa la kitaaluma ambalo linaweza kuimarisha 'dhamira zetu' juu ya 'harakati'; kilicho ni Chuo cha Ulinzi cha Taifa. Tukiwa kama wadau wa maendeleo jamii, ulinzi wa Taifa ni pamoja na jitihada zetu zenye kuzingatia sera bora -- kuhakikisha tunakuwa na sera bora zinazoongoza utendaji wa serikali kwa manufaa yetu sote.

Utendaji wote, wa serikali ya watu, ni vema kuwa unaongozwa na sera zinazozingatia utawala na ustawi bora wa taifa la watu/wananchi wanaojielewa, kuwajibika na kutekeleza malengo na mikakati ya kitaifa ili kuwepo na uhuru na umoja wa kweli miongoni mwao/mwetu.

Uhuru na Umoja, si kauli tupu ambayo mwananchi wa Kitanzania, anaiona na kuisoma katika nembo ya taifa; ni zao la 'ufahamu' na 'dhamiri' ya uzalendo kwa nchi-taifa. Mazungumzo yetu, nidhamu yetu katika matendo na 'tafsiri za mambo' havina budi kuwa na koherensia na pia sinejia katika muktadha wowote wa watu, maendeleo, ustawi na usalama wa jamii.

Tunapoona 'kiongozi' anaulalamikia mfumo, basi ndiyo tuelewe--kitaifa ama nchi-dola; kuna namna 'mtihani wetu katika kuusanifu muktadha wa watu, maendeleo na utamaduni ni mmoja' na basi vyeo na madaraka visitufanye kujichanganya ama/na kudaganyana--hili Mwalimu Nyerere analizungumza kinaga ubaga kwenye hiyo media...

Ikiwa wananchi hawana 'upeo' wa mawazo ama wanalemazwa na watawala wadanganyifu--jambo ambalo Mwalimu Nyerere kwenye hiyo media anawasimulia kama aina ya viongozi wanaowaambia wananchi tumekuja kuwakomboa na kumbe wameingia kukomboa matumbo yao, basi ndiyo litukumbushe tofauti ya 'mtihani' wa awali kpindi cha Mwalimu Nyererer na Nyakati hizi. Hivyo kwenye hiyo media anagusia suala la hali ilivyokuwa kwa wastani wa upeo wa wanachi, kipindi cha wakati wa uhuru mpya ki-nchi-dola ya Tanzania, kulikuwa naidadi ndogo sana ya wanaojua kusoma(17%)' na tulipambana na hilo hadi kufikia idadi kubwa ya wanaojua kusoma(1988, 92?%).

Sisi wananchi tupo kwenye nyakati zenye changamoto nyingine pana kwa mustabali wa maendeleo yetu -- haijatutoshea tu kuwa na taifa la watu wanaojua kusoma na kuandika; tunalohitaji la taifa la watu wanaoweza kufikiria nje na ndani ya sanduku. Kwa hivyo, hata aina ya viongozi wenye kutamba kwa 'madesa' bado siyo suluhu ya kutungia mikakati ya kukabiliana na walimwengu walio ni mafundi wa kuchezea visomo, ili kughiribu akili za wasomi -- wasomi na hata wanazuoni wa visomo mashudu.

Kujitegemea kifedha na maendeleo lau kutatupunguzia adha ya visomo vya mchongo, na uhuni wa 'mtama kwa watoto'. Hili nalo Mwalimu Nyerere analizungumzia katika hiyo media--KUJITEGEMEA.

Ikiwa sisi wananchi hatufanyi bidii kujiongeza -- kuwa na namna ya Elimu Madhubuti ya Utu na Maendeleo, daima tutajihujumu kwa ghiriba za mafikara, upepo wa maoni na 'kufuata mkumbo'

Mzee Benjamini Mkapa alikuwa akiyaelewa masuala, ila alikosa wadau wa kuunganisha nao nguvu na wakati ulimtupa mkono; aliyoyazungumza March 18, 2020 NDC yaliakisi 'viporo'.

THE CRISIS OF MULTILATERALISM AND ITS IMPLICATION TO AFRICA kama alivyodadavua Mzee Mkapa ni 'marejeo ngamani'.

Hatutakuwa salama ikiwa 'uhuni wa duniani', umeingia hadi ndani yetu; hili linatutaka uwezo, ujuzi na upeo wa kuisafisha nyumba. Ikiwa wananchi hazungumzi lugha moja ya 'watu na maendeleo ya ukweli' basi ndiyo hivyo--majanga!;

Kila mtu mwenye kujua ilivyo bora ni vema arejee ngamani.

Kwa hivyo kama alivyosisitiza Mwalimu Nyerere, tunahitaji jukwa na sauti moja ili kusimama kidete dhidi ya 'Himaya'.
Ikiwa tumejisahau sana, basi bado kwa kweli tunafuga adha ya masuala yetu ya 'Viukoo Ukoo'...

Mitego ya Kibepari na soko huria itapalia makaa ya 'mbio za panya'... Michezo ya sisi kwa sisi kutoboa mtumbwi, kushindana kuokoa chombo kisizame na huku baadhi yetu tunafuga kambi za waharibifu ni upotofu wa dira ya kiroho, maadili na miiko...

Tunahitaji namna ya 'lugha mpya', maarifa na mapinduzi kwa mifumo mibovu ya stawi na maendeleo ya watu.

Elimu, Elimu, Elimu
 
Hivyo vitu vyote hatukuwanavyo.

Unapaswa ufahamu kabisa Nyerere mkatoliki alialikwa na Waislam katika kudai uhuru hiyo ni sababu ya kwanza kuonesha huo udini haukuwepo kabisa kwetu.

Makabila ya kusini yaliungana kwenye vita vya maji maji dhidi ya mkoloni.

Kanda zote ziliungana na zilipokea wapigania uhuru na vyama vya ushirika katika kanda mbalimbali vilianzishwa ili kudai uhuru kwa pamoja.

Huo ukanda,udini na ukabila haukuwepo hivyo Nyerere alipigana na upepo.
Mataifa karibia yote yaliyokuwa na mchanganyiko mkubwa kama sisi yalianza kuliwa na ukanda, udini na ukabila baada ya wakoloni kuondoka. Penda usipinde Nyerere aliweza kudhibiti hilo na kuunda taifa, wengi waliochanganyikana kama sisi waliishia kuwa na nchi na kuhasimiana tu.
 
UJAMAA HAUKUANGUKA ILA ULIANGUSHWA. Ukweli usiopingika nchi nyingi baada ya kupata uhuru ziliangukia katika vipindi vingi vya mapinduzi ya kijeshi na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Vita hivi vilichochewa na wakoloni wenyewe ili kutengeneza mfumo ambao utaendelea kunufaisha mataifa yao.
 
Sisi wengine tulikuwepo kipindi chote cha Nyerere mbona hatukuona huo ugumu wa maisha anaoueleza huyu ndugu. ??!
Maajabu haya !! 😅😅
Ebu acheni unafiki na jaribuni kuwa wakweli walau kidogo.

Dr. Salim akiwa waziri mkuu alipofanya ziara mkoa wa Lindi ilikuwa mwaka 1984 alikuta hali gani huko na ndipo aliporejea Dar akakaa na Nyerere ikulu kwenye mazungumuzo ya kina na kupelekea mitumba kuruhusiwa kuingizwa rasmi nchini.

Je unafahamu kwamba utekelezwaji wa sera ya azimio la Arusha kulipelekea watu wengine kudhulumiwa mali zao walizohenyeka kuzipata.

Je unafahamu kwamba kwenye kutekeleza sera ya watu kuhamishiwa kwenye vijiji vya ujamaa ulisababisha baadhi kupoteza maisha na wengine kupoteza mali zao na hakuna fidia yoyote iliyotolewa.?

Je unafahamu kwamba lengo la Tanzania kumng'oa Idi Amin ilikuwa ni mbinu ya Nyerere kumrejesha rafiki yake Obote madarakani na madhara yake tutaishi nazo milele.

Je unafahamu kwamba hii katiba mbovu ya mwaka 1977 pamoja na kwamba Nyerere alikiri kwa kinywa chake mwenyewe kwamba ilikuwa haifai lakini aliiacha itumike tu na leo ndio maana wananchi wa Tanzania wanapiga kura isiyo na maana kama misukule huku ccm iking'ang'ania na kubaki kuwa sehemu ya dola.

Je unafahamu kwamba Nyerere baada ya kuona serikali nyingi za nchi mbalimbali za kiafrika zikipinduliwa mara tu baada ya uhuru aliamua kuifanya jeshi la wananchi Tanzania kuwa kitengo fulani ndani ya chama hali ambayo imepelekea hadi leo jeshi hilo kukosa kabisa uzalendo na kuacha kulinda maslahi ya nchi na badala yake kulinda maslahi ya watawala wa ccm kwa kuhakikisha kwamba wanang'ang'ania madarakani..
😛😛😛😛😛😛😛😛😛😛😛😛😛
 
Katiba ya Nyerere ndio ilifanya rais awe Mungu mtu, na hakuna namna yoyote ya kweli ya kumuwajibisha.
Mbona Kenya waliweza kuiondoa KANU na katiba yake?? Kuna mambo mengi yanayochangia Tanzania kuwa tulivyo ikiwemo namna tulivyotawaliwa na tulivyopata uhuru wetu. Tanganyika kutokuwa koloni la ki-settler na pia kupata uhuru kwa mazungumzo ni mambo yaliyohusika kutengeneza historia yetu ya sasa pia, Nyerere asitwishe mzigo wa kila kitu.
 
Serikali ni taasisi, Uraisi ni taasisi inayoongoza Serikali hivyo kupatikana kwa majawabu ni rahisi tu. Mambo yote ambayo Raisi Nyerere aliwahi kuyafanya yalianza katika ngazi ya kisera na baadaye kutekelezwa kupitia sheria. Hivyo kwasababu wengi walikuwepo kipindi hicho ni rahisi kufahamu nini kilikuwa kinaendelea hadi kupelekea serikali kutengeneza sera za namna ile na baadaye kuzitungia sheria kandamizi vile.

Mfano, mwaka 1967 wakati tunatanzanga Azimio la Arusha, sababu zilizotolewa ni kwamba jamii ya Tanzania ilikuwa haina usawa kutokana miaka ya ukoloni. Hivyo kujenga usawa na kuondoa matabaka ni lazima nyezo zote za uzalishaji (Major Means of Production) zitaifishwe ili serikali iweze kutoa huduma kwa kila mwananchi. Atleast this is understandable. Ila kwanini serikali ilitumia dola na sheria kandamizi kuhakikisha watanzania tunalala njaa na kukosa hata mavazi mwilini, kwa miaka mitano mfululizo sijapata majawabu yake.

Lengo lake haswa kutuona tukiishi kimasikini vile ilhali ilikuwa inawezekana kutuachia kutafuta mahitaji yetu ilikuwa inawezekana. Somethings defy ordinary human comprehension.
Tukumbuke pia wakati wa Nyerere kulikuwa na vita kali baridi ya Magharibi na Mashariki, Nyerere hakuwa anapenda ubepari wa Magharibi lakini pia hakuwa tayari kufuata ule ujamaa halisi na ukatili wake kama wa USSR na China hapo ni kama alipatwa na dilemma ya kujua muelekeo ni upi na akalitatanisha taifa pia, japo kwa nia njema kwamba Tanzania inatakiwa kuwa sovereign na sio kibaraka wa yoyote.
 
Mbona Kenya waliweza kuiondoa KANU na katiba yake?? Kuna mambo mengi yanayochangia Tanzania kuwa tulivyo ikiwemo namna tulivyotawaliwa na tulivyopata uhuru wetu. Tanganyika kutokuwa koloni la ki-settler na pia kupata uhuru kwa mazungumzo ni mambo yaliyohusika kutengeneza historia yetu ya sasa pia, Nyerere asitwishe mzigo wa kila kitu.
Miongoni mwa makosa Nyerere aliyokiri kwa kinywa chake akiwa hai ni pamoja na udikteta na kufanya Watanzania waoga kupitiliza sioni lawama zikimkwepa katika hili
 
Back
Top Bottom