Wajibu wa wanawake walioolewa katika kutunza familia na waume zao

Wajibu wa wanawake walioolewa katika kutunza familia na waume zao

Jaman, baadhi ya wanawake walioolewa wanajisahau sana. Unakuta mchafu, ananuka jasho, haogi kwa wakati, hata kufua kwake ni mtihani. Kuna hawa wake za watu walioajiriwa, jamani, hata kama mmeajiriwa, jitahidini kuwajali waume zenu. Wanatoka home rafu sana. Kuna mkaka namjua ameoa, na ndoa yake ya miaka mingi sana, mkewe ameajiriwa. Jamani, huyo baba anaenda kazini, nguo zimejikunja. Nguo zake ni nzuri, lakini hayupo smart. Unakuta shati zimejikunja, kavaa tu, hata hajali. Viatu vimejaa vumbi.

Jamani, mlioolewa, jitahidini kuwajali waume zenu hata kama mmeajiriwa. Wawekeni smart waume zenu, jamani. Inasikitisha sana. Huyo baba akipata michepuko msafi, akamfulia, akampa mapenzi moto, akampikia chakula kizuri, atahamia huko huko. Maana kila siku yeye ni kula chakula cha house girl, nguo anavaa hazilowekwi, kama zimetafunwa. Jamani, sijui kwanini watu wakiolewa wanajisahau. Wajali waume zenu, jamani.

Sasa huyo baba kwa jinsi anavyoishi, utasema hana mke. Ni huruma, kwa kweli. Embu wajali waume zenu waonekane smart. Mtu kaoa lakini mke hata kumuandalia nguo hapana, kumsafishia viatu mke hatimizi majukumu yake kama mke. Inasikitisha. Kuna mwingine yeye ni kulala tu, hana kazi ni mama wa nyumbani, lakini hata kufua nguo za wanae ni mtihani. Nyumba nzima inanuka mikojo na mavi ya watoto. Nepi za mavi anarundika siku mbili, nyumba inanuka uozo, na ni mke wa mtu. Ni mchafu sana. Wanaume wanavumilia mengi, jamani, yaani wanaume wanavumilia jamani hawasemi tu. Jamani, jamani, wake za watu ni wachafu sana, asilimia kubwa wanajisahau, wanabweteka. Hata kujiweka smart hawawezi. Yaani ni huzuni. Poleni sana wale wote mliooa wanawake wavivu.
Interesting
 
Kwa nyakati hizi sishauri mtu kuoa.
Na ukioa,bila msaada wa Mungu mchepuko haukwepeki.
Na ukiwa freemason,kumtoa mke kafara ni jambo jepesi.
Wanawake wa siku hizi ni pasua kichwa.
 
Yeah hata na heshima inakuwepo....
Japo Kuna muda yanamtoka maneno anasema...nsingekuoa ingekuwaje.. na nshakutumia😅😅
All in all nashukuru mungu tu
Na mimi Nimewaza hivyo ila umewapa heshima kubwa sana wazazi wako, 😌😌 kama unamdogo wako wa kike nifanyie mpango basi najua na yeye atakua kama wewe
 
Back
Top Bottom