Wakala wa Voda amedukua laini yangu na kuiba mamilioni

Wakala wa Voda amedukua laini yangu na kuiba mamilioni

nipo online

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2022
Posts
1,039
Reaction score
2,657
Picha imeanza hivi alipita wakala hapa maskani akidai anaweza kuiwezesha laini na kua five G yani hata niwe kijijini mimi nitatamba tu.

Nikampa simu yangu ili aapdate mafaili kama alivyoniambia, alivyomaliza hakutaka nimpe hela akasema yeye anapewa kwa kamisheni.

Akaondoka mara tu nikapiga simu kwa rafiki yangu nashangaa anasema nimebadilisha namba nikamuliza kivipi wakati ni laini yangu ya siku zote?

Nikacheki salio nashangaa naambiwa namba ya siri ni wrong. Nikapiga simu makao makuu kuwambia wanasema laini yangu IMEHAKIWA et nini? Nikawatajia namba za laini yangu halisi wakasema imehamishwa laki 3.

Kupiga simu NBC kitengo cha sim banking wakasema kuna namba imehamishwa milion 5 na hiyo namba haipo hewani. Nilizimia hadi hospital. Kufanya hadith iwe fupi kesi ipo police nao wanadai nimetapeliwa kizembe so wanataka laki 5 ili nifungue kesi.

Sina hata shilingi Nimebaki kupagawa hii dunia sio sawa.
 
Back
Top Bottom