Wakamatwa kwa kujitangaza kutoa huduma ya internet ya Starlink Instagram

Wakamatwa kwa kujitangaza kutoa huduma ya internet ya Starlink Instagram

DAR ES SALAAM: Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao wamewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi wa Kawe, Kinondoni na Hongliang Yang (35) raia wa China , mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria.


Watuhumiwa hao inadaiwa wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya intaneti nchini kupitia mtandao ya kijamii wa instagram kwa akaunti yenye jina la Starlink.

d9c814f23285d0c9f60d20661de7a1fd-1

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Jumanne Muliro amesema baadhi ya vifaa hivyo vimeshauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam, kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Ametaja vifaa vilivyokamatwa ni Starline Dish 12 na Starlink Router 12, hivyo kutoa wito kwa wananchi kuwa makini na matumizi ya vifaa vya mawasiliano, ambavyo havijaidhinishwa na mamlaka husika.

d9c814f23285d0c9f60d20661de7a1fd-2
 
Kamanda Murilo leo ametangaza kukamata watu wawili, mtanzania na mchina kwa kuingiza vifaa na kutangaza kutoa huduma ya internet ya starlink. Polisi wamesema wameuza vifaa hivyo bila kuidhinishwa na TCRA.

Naona kama mitandao yetu wanaipiga pini starlink by fire, by force 😅 Kwanini Serikali wasimalize mchakato kama wananchi ndio wanahitaji.

=========

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao limewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi Kawe na Hongliang Yang (35) Mchina, mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalum SACP Jumanne Muliro anasema Watuhumiwa hao wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya internet nchini kupitia mtandao ya kijamii wa Instagram kwa akaunti yenye jina la STARLINK.

Baadhi ya vifaa vilivyoingizwa nchini imebanika vilishauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

EATV
Mchakato tutaumzliza kwenye uchaguzi wa 2024 na 2025!
 
Ndio maana Tanzania na hata katika nchi nyingine nyingi za ki-Afrika hakuna Ugunduzi wala Uvumbuzi mpya wa kisayansi unaofanyika kutokana na kuwapo kwa tawala mbaya ambazo haziweki mazingira mazuri na wezeshi ya watu kuweza kufanya kazi zao kwa uhuru.
Mkoloni alifanikiwa kututengenezea masheria mabovu ambayo tumeyarithi toka wakati huo mpaka leo vionngozi wetu wameshinda kuyaondoa
 
Kwani ukipata kifaa unaaccess hata kama nchi imezuia?

Kama ipo hivyo, hayo makatazo, mazuio na ukamataji(ambao nao unatangazwa🤨) ni viungo katika tangazo moja kuuuuuuuuuuuuubwa la 'black market' ya starlink.

Ukitumia akili utaiona hiyo 'grand scheme of it'. Akili tu mtu wangu. Bora tu wahalalishe tusipoteze mapato.
Ngoma inakamata popote, huko angani mwamba amemwaga maelfu ya sateline dunia nzima.
 
Kamanda Murilo leo ametangaza kukamata watu wawili, mtanzania na mchina kwa kuingiza vifaa na kutangaza kutoa huduma ya internet ya starlink. Polisi wamesema wameuza vifaa hivyo bila kuidhinishwa na TCRA.

Naona kama mitandao yetu wanaipiga pini starlink by fire, by force 😅 Kwanini Serikali wasimalize mchakato kama wananchi ndio wanahitaji.

=========

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao limewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi Kawe na Hongliang Yang (35) Mchina, mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalum SACP Jumanne Muliro anasema Watuhumiwa hao wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya internet nchini kupitia mtandao ya kijamii wa Instagram kwa akaunti yenye jina la STARLINK.

Baadhi ya vifaa vilivyoingizwa nchini imebanika vilishauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

EATV
Ni kupoteza muda na nguvu tu, hatua hiyo ni kuipa promo tu, huwezi kuzuia kusambaa kwa teknologia, mzigo upo nchini, na unatembea fresh.
Baada ya miezi michache starlink zitakuwa kila mtaa mpaka maporini, utazikuta mpaka nyumbani kwa RPC.
 
Ni kama tunapambana kurudi nyuma, habari kamili hii hapa!

#HABARI Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao limewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi Kawe na Hongliang Yang (35) Mchina, mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalum SACP Jumanne Muliro anasema Watuhumiwa hao wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya internet nchini kupitia mtandao ya kijamii wa Instagram kwa akaunti yenye jina la STARLINK.

Baadhi ya vifaa vilivyoingizwa nchini imebanika vilishauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

#EastAfricaRadio
IMG-20240323-WA0008.jpg
 
Back
Top Bottom