Wakati mzee kilomoni anapinga janja ya Mo dewji alionekana mbaya

Wakati mzee kilomoni anapinga janja ya Mo dewji alionekana mbaya

Ila upande wa Yanga nako mchakato umeganda kilichopo sasa sivyo ndivyo ilivyopaswa iwe. Kuna michakato bado kama vile Yanga kuwa kampuni, idadi ya wawekezaji kama ilivyotakiwa, n k. Sijui labda mchakato utaendelea mbele au watu wanaona kinachoendelea ni ishara nzuri ya mafanikio bora kuishia hapo.

Kilomoni hakukataa uwekezaji Bali alipinga namna zoezi Zina la uwekezaji lilivyoendeshwa. Mtu akihoji uwekezaji was no wengi wanafikiri wanapinga uwekezaji sio kweli.
Sheria ulisema timu za wanachama Kama Simba na yanga ziruhusiwe kuuza hisa zisizopungua asilimia 49 kwa wawekezaji wasiopungua watatu. Kwanini mo amepewa hisa zote peke take? Hapo ndio tatizo linaanza.
Mo kazuia udhamini wa Azam wa miaka 10 kwa bilioni 41 akidai brand ya Simba ipo juu zaidi ya yanga hivyo hawawezi kupata udhamini sawa na Simba Kama watapungukiwa pesa wamwombe. Hapo unaona kabisa no hataki Simba ijitegemee. Yeye mwenyewe kajaza matangazo yake kwenye jezi ya Simba kwa matangazo ya milioni 250. Kampuni yake ya Moro polyester inauza kanga za Simba bila club kupata hata Senti tano. Yeye mwenyewe analalamika anapata hasara lakini anasema wakati timu inaingia makundi walipata mdhamini wa kulipa bilioni 1.6 lakini akakataa kwa sababu alitaka kutangaza visit Tanzania.
Mo ndio tatizo namba moja Simba anaitumia Simba kwa manufaa binafsi ndio maana uwanja inaitwa mo Arena, alianzisha madoli akawa anayaita no friend na Kilomoni alimjua ndio maana akakataa kumpa hati za jengo.
Mwanzoni alisusa akaenda Singida utd lakini pia singida ikamshinda kwa kuwa haina base ya kutosha ya mashabiki,,

Akarudi Simba,,
Tuende mbele turudi nyuma mo anapata faida ndio mana hatak wenzie waingie,,
 
Hivi kweli mkuu vitu vingine tutumie akili tu ya kawaida kufikiria. Mnataka mwenye asilimia 51 awe tu na sauti kubwa za mdomoni tu pasipo utendaji? Yaani mwenye asilimia 49 atoe pesa zake kusajili na kulipa mishahara halafu nyie msiotoa ela mue na sauti kwasababu mna asilimia 51. Hilo jambo gumu sana, kama mnataka hivyo na nyie wenye 51 inabidi mtoe mpunga kuendesha timu
Mkuu embu rudi shule.
 
Kuchekana ndio utani wenyewe, ni upepo tu,, unafikiri Hersi apigi 10%? Kutesa kwa zamu,, mda wenu huu mfuraie kwani kukaa namba 1 haishindikani ila kukaa milele haiwezekani,

Miaka ile enzi za sarpong [emoji16] mliona kila rangi,,
Acha mzee, enzi za Yikpe, Nchimbi n.k
 
Kwamba Simba masikini ilikuwa inasajili vizuri kuliko hii? Sawa twende kwa mifano iliyo hai, je Simba masikini iliwahi kujihakikishia kucheza makundi ya michuano ya CAF kuwa ni swala la kawaida? Kipi ilichofanikiwa hiyo Simba masikini katika kipindi chote hiko kabla ya Mo? Msidamganye na kujiona wa maana na kumdharau huyo Mo wakati kabla ya Mo mlikuwa hata mtambuliki Africa ila leo hii Simba imekuwa maarufu kwenye soka la Africa. Hata kama Mo akaondoka akaja muwekezaji mwingine lakini haiwezi futa ukweli kuwa Mo ndiye aliyeipa Simba mafanikio na ndiye aliyewaonesha mwanga.
Mkuu suala la kuonesha mwanga ni suala la muda, lingeweza kudondokea kwa mwekezaji yoyote yule, mbona simba imewahi kufika mpaka fainal? MO alikuwepo miaka hiyo ya huko nyuma?
 
Hivi kweli mkuu vitu vingine tutumie akili tu ya kawaida kufikiria. Mnataka mwenye asilimia 51 awe tu na sauti kubwa za mdomoni tu pasipo utendaji? Yaani mwenye asilimia 49 atoe pesa zake kusajili na kulipa mishahara halafu nyie msiotoa ela mue na sauti kwasababu mna asilimia 51. Hilo jambo gumu sana, kama mnataka hivyo na nyie wenye 51 inabidi mtoe mpunga kuendesha timu
Kifupi ni kwamba huu mfumo wa 51/49 hauwekaniki
 
Hivi hiyo timu angepewa mzee Kilomoni angeweza kulipa hata jezi ya mchezaji mmoja?

Timu ina gharama zake,safari za ndege na mafuta ya gari kila mechi misimu yote,hoteli za kulala,malazi na vyakula .

Halafu unaanza kuleta mada za futuhi kabla ya kufikiri
Hapa umetaja matumizi tu mkuu, sasa taja na mapato ya timu

Una akili kama za MO wewe, kila saa ni kutaja matumizi tu hivi mbona hamtaji hela inayopatikana nyie watu?
 
Hivi hiyo timu angepewa mzee Kilomoni angeweza kulipa hata jezi ya mchezaji mmoja?

Timu ina gharama zake,safari za ndege na mafuta ya gari kila mechi misimu yote,hoteli za kulala,malazi na vyakula .

Halafu unaanza kuleta mada za futuhi kabla ya kufikiri
Swala sio timu kupewa kilomoni hoja zake baada ya miaka mitano ndo zimeonekana zina-mashiko

We unaona ni sahii una mwenyeketi ambaye hana mamlaka yeyote yale
 
Mgawanyo wa hisa
Simba Sports Club - 51%
Mo Dewji - 49%

Mwekezaji hadi leo hawajeka 20b za hisa 49%, ila ndio anaendesha kila kitu na kutengeneza faida bila jasho.

Mwenye hisa 51%, hana sauti kwa lolote, wakati timu ni ya kwake , na akaunti yake iko zero.
Ndo tatizo linapoanzia hapa hata dewji ukimuuliza hili swali anakua mbogo
 
Kilomoni hakukataa uwekezaji Bali alipinga namna zoezi Zina la uwekezaji lilivyoendeshwa. Mtu akihoji uwekezaji was no wengi wanafikiri wanapinga uwekezaji sio kweli.
Sheria ulisema timu za wanachama Kama Simba na yanga ziruhusiwe kuuza hisa zisizopungua asilimia 49 kwa wawekezaji wasiopungua watatu. Kwanini mo amepewa hisa zote peke take? Hapo ndio tatizo linaanza.
Mo kazuia udhamini wa Azam wa miaka 10 kwa bilioni 41 akidai brand ya Simba ipo juu zaidi ya yanga hivyo hawawezi kupata udhamini sawa na Simba Kama watapungukiwa pesa wamwombe. Hapo unaona kabisa no hataki Simba ijitegemee. Yeye mwenyewe kajaza matangazo yake kwenye jezi ya Simba kwa matangazo ya milioni 250. Kampuni yake ya Moro polyester inauza kanga za Simba bila club kupata hata Senti tano. Yeye mwenyewe analalamika anapata hasara lakini anasema wakati timu inaingia makundi walipata mdhamini wa kulipa bilioni 1.6 lakini akakataa kwa sababu alitaka kutangaza visit Tanzania.
Mo ndio tatizo namba moja Simba anaitumia Simba kwa manufaa binafsi ndio maana uwanja inaitwa mo Arena, alianzisha madoli akawa anayaita no friend na Kilomoni alimjua ndio maana akakataa kumpa hati za jengo.
Ahsante kwa kunielewa kilimon haya mambo aliyaona na moja ya vitu alivyopinga ukitoa mfumo wa uongozi ni uwanja wa simba wa bunju kuitwa mo arena
 
Historian ya Simba Afrika inaanzia mwaka 74, mwaka 79 iliweka rekodi ya Aina take ya come back na mwaka 93 ulifika fainali ya Afrika, mwaka 2013 ilimtoa bingwa mtetezi na kuingia makundi. Mo aliichukua African Lyon ikamshinda, aliichukua Singida ikamshinda na wakati mchakato unaanza wapo wawekezaji waliojitokeza Kama mtoto wa Bakhresa ambao walikuwa na ofa nzuri Ila alitumia rushwa na ushawishi awe peke take kusema bila mo Simba isngejulikana Afrika ni kuikosea heshima.tatizo kubwa ilikuwa namna timu inavyoendeshwa. Dalali na elimu take ya darasa la nne alibuni Simba day na mapato akanunua uwanja wa Bunju ambao mpaka Sasa hakijafanyika kitu kikubwa.
Mo dewji akiondoka sahivi simba hawawezi kosa mwemezaji matajiri wengi sana wanaitamani ile timu
 
Mwekezaji ananufaika na timu kupitia kutangaza bidhaa zake, fikiria mo Energy inavyo uzika bado bidhaa nyingine, kumbuka pia mwekezaji huyo huku kwenye hesabu zake za kampuni anaweka hesabu zake, ametumia mamilioni kutangaza bidhaa hizo, ndiyo maana mwekezaji italazimika aingie gharama kuihudumia timu, anayonufaika nayo kibiashara.

Hawa wenye asilimia 51 hawa mchango wao mkubwa ni fansbase,
 
Mambo ya mangungu kutokua na mamlaka hilo ni lake,na kama ni hivyo ajiuzulu sasa ili tuone tatizo la Moo.Wanachama wana haki yakumpigia kelele mangungu kwasababu yeye ndiye anayehusika kuwaunganisha wanachama na Moo.Mapungufu ya Moo yeye ndiye aliyetakiwa ayaelezee kwa wanachama ili ufumbuzi upatikane.Kama hawajibiki awapishe wanaoweza.Ni rahisi kumuwajibisha mangungu kuliko kumtoa Moo simba.Hizo kauli za kusema kuna wafanyabiashara wengi wanaitamani simba uko ni kutaka kubet.Waulize yanga baada ya Manji kuondoka waliishije na imewachukua miaka mingapi kumpata Gsm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom