Wakati Watanzania wakibishana juu ya Bandari ya Bagamoyo, Kenya wafungua Bandari ya Lamu

Bandari ya bagamoyo mwaka huu kwenye bajeti haipo na ikitokea pakahitajika kuongezwa bandari nyingine mahali itakapojengwa pataamuliwa huko mbeleni.
Au ijengwe
Bandari ya bagamoyo mwaka huu kwenye bajeti haipo na ikitokea pakahitajika kuongezwa bandari nyingine mahali itakapojengwa pataamuliwa huko mbeleni.
Saiv tunaboresha hifadhi ya burigi kwanza, au nasema uongo ndugu yang Philipo
 
 
Wewe jipe moyo tu,Sudan ya kusini ,Uganda ,Ethiopia na wengineo Sijui kama wafanyabiashara wao watapenda invalid mrefu kwenye kusafirisha mzigo yao
 
Kwa hiyo kwa sababu Kenya wamezindua bandari mpya basi ni kigezo cha sisi kujenga bandari ya Bagamoyo? Je bandari za Dar es salaam, Tanga na Mtwara tumeziwezeshaje ili ziweze kutoa huduma nzuri na kubeba mizigo mingi?
Bandari tulizo nazo tu bado hazijaweza tumika ipasavyo, nina uhakika zinatumika chini ya 70%


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania inahitaji kuwaindoa kwenye nafasi nyeti au hata kwenye ajira wale wote walioluwa wanamdanganya mjuzi wa wajuvi mpaka kushindwa kusonga mbele kama Taifa,tena ikibidi watiwe viboko 42
 
Halaf hii kitu naitafuta sana mkuu, unaweza weka evidence ya hao jaman walivyokua wanapinga hayo uliyo mention? Ili angalau nione hoja yao ilikua ni nn.
Hoja yao kuu ni kwamba hayo ni maendeleo ya vitu na si watu
 
Kuna mda Hadi nawazaga nchi hii mapandikizi ya nchi jirani yamejaa sana kuzuia nchi hii isiwe na miradi ya maendeleo mizuri ya kuleta maendeleo ya kweli.
Hakuna mapandikizi, ni ujinga wa watu uliosababishwa na siasa za kipuuzi za ujamaa na kukosa elimu ya kutufanya kuwa competitive kwenye biashara...

We think the world will stop and wait for us kwa vile sisi ni important sana duniani wakati kiukweli we are negligible...
 
Umeandika kwa Uchungu mwingi sana, nimekuelewa....uko 100% correct
 
Bandari tulizo nazo tu bado hazijaweza tumika ipasavyo, nina uhakika zinatumika chini ya 70%


Sent using Jamii Forums mobile app
Zimeshapitwa na wakati kwa vile dunia inaenda kasi sana kwenye technology...

ni sawa na leo useme serikali iweke mkazo kwenye simu za mezani kwa kuwa hata asilimia 10 ya watu hawana hizo, utaonekana kichekesho...dunia ishatoka huko...bado zipo relevant lakini ni kwa kiwango kidogo sana
 
Tanzania tayari tuna bandari sijui mapepe ya bandari nyingine ni ya nini wakati mizigo inatosha pale Dar pakipanuliwa vizuri.
Hoja hii nimeisikia mara kadhaa!!

Hebu tafakari hili! Bandari ya Dar es salaam inatumika na Tanzania, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Uganda, DRC!! Jambo la kukera kabisa, miongoni mwa nchi zote hizo, Tanzania ndo inaonekana eti ndo yenye uchumi mzuri!

Ninachotaka kusema ni kwamba, Bandari ya Dar es salaam inatumiwa na nchi maskini!! Na pamoja na kutumika na nchi maskini zenye exports ndogo sana, lakini bado Bandari ya Dar es salaam inafikia wakati inaelemewa!

Hivi ulishawahi kujiuliza endapo by average uchumi wa nchi hizi unafikia kama ule wa Kenya tu, je Bandari ya Dar es salaam itaweza ku-handle shehena ya nchi 7 ambazo kila moja, by average inafikia angalau kama uchumi wa Kenya tu ambayo na yenyewe ni maskini?!

Je, kama miongoni mwa nchi hizo 7, mbili tu miongoni mwao zinafikia angalau uchumi wa South Africa (ambayo na yenyewe ni maskini) tu, bado unaamini Bandari ya Dar es salaam itakuwa na uwezo wa ku-handle uchumi wa hizo nchi?

Itoshe tu kusema kwamba, hoja yako inaweza kuwa sahihi endapo tu unaamini nchi zote zinazotumia Bandari ya Dar es salaam uchumi wake utabaki hivyo hivyo kwa angalau miaka 25 ijayo!!

Lakini ni ujinga kujenga bandari nyingine kwa mikopo na kuwapa wageni waendeshe kwa faida zao.
Hapo unaonesha wazi huna uelewa kuhusu mambo ay projects financing and operations! How come ujenge bandari kwa mkopo halafu tena umpe Mchina aiendeshe?
China anafikiria kufanya sehemu ile iwe kambi ya jeshi na dampo la vitu vya China.
Propaganda zilikuingia barabara!!!

1. Propaganda za Kambi ya Jeshi zilianzishwa na Marekani... ziwe ni kweli au si kweli ni kwa sababu Marekani wanaamini ni wao tu na washirika wake ndio wenye haki ya kuwa na Military Bases kwenye nchi za wenzao!!!

Pale Djbouti kwa mfano... the so-called Mabeberu ndio walitangulia kujenga military base! China alipofanya uwekezaji kwenye bandari, reli, na industrial complex, nae akaweka military base!!

Kuona hivyo, US wakaanza sasa kusambaza kwa nguvu dhana ya China na Military Bases huku Marekani wakilenga kudhohofisha Belt and Road Initiative iliyokuwa imeletwa na Chin!!

Ajabu, wakati Marekani wanatahadhalisha nchi za Africa kuhusu China kwamba moja ya malengo ya Belt and Road Initiative ni kwa Wachina kujenga military bases, wao wakajisahaulisha kwamba ndio wanaongoza kwa kuwa na military base!

Na usisahau, Propaganda za Military Bases Tanzania hazijaanza leo!!! Kila mwenye masikio alisikia propaganda za eti JK ameiuza Kigamboni kwa George Bush ili Wamarekani wajenge military base!!!

Anyway, sijafika Kigamboni muda mrefu sana... unaweza kuniambia hiyo military base tuliyokuwa tunaambiwa imejengewa upande upi?! Au Shujaa Magu alipoingia madarakani alipiga marufuku ujenzi wa hiyo military base?
Yaani hapa ndo umedanganywa kwa 100% kwa sababu HAKUNA kitu kama hicho!!!

Hicho unachosema miaka 100 ni miaka 99! Na sio miaka 99 ya uendeshaji wa bandari bali Mchina ali-propose amilikishwe ardhi kwa miaka 99!! And remember, Sheria zetu za ardhi zinasema mwekezaji anaweza kumilikishwa ardhi ama kwa miaka 33 (renewable), miaka 66 (renewable) au miaka 99.

Of course, hata mimi sikubaliani na suala la kuwamilikisha ardhi kwa miaka 99 kwa sababu, based on research ambayo tuliifanya, proposal ilikuwa ni kwa Mchina kuendesha bandari kwa miaka 40! Sasa kama aendeshe bandari kwa miaka 40, kwanini tena atake amilikishwe ardhi kwa miaka 99!

Unahoji "je, Kenya wametoa miaka 100?" Hapo ndipo unatakiwa kutafakari kauli yangu ya hapo juu kwamba "How come ujenge bandari kwa mkopo halafu tena umpe Mchina aiendeshe?"

Kifupi HUWEZI kujenga project yako kwa pesa za mkopo halafu project hiyo iendeshwe na mwingine kwa staili hiyo unayosema wewe! Inaweza kuendeshwa ONLY under the so-called Management Contract!! Wakati NMB inaanzishwa, serikali ilitumia hii syetem ya management contract, na CEO alikuwa Mmarekani (jina nimelisahau)!

Mmarekani huyu alikuja kubwaga manyanga baada ya Mkapa kulazimisha kuiuza NMB kwa hoja kwamba benki inajiendesha kwa ruzuku ya serikali wakati by the time, benki ilikuwa inajiendesha yenyewe!

Ukiona project inakuwa financed na kuendeshwa na mwingine (mbali na management contract) basi fahamu financing yake sio mkopo bali imekuwa financed under the so-called Build Operate Transfer... Yaani BOT Financing Scheme!!

Sitaki kusema mengi, lakini Investopedia wanaelezea BOT Scheme kwamba:-
At individual level, BOT ni kama pale mtu unaifanyia ukarabati mkubwa nyumba ya baba mwenye nyumba kwa gharama zako mwenyewe halafu unaishi "bure" kwa muda fulani ili kufidia zile gharama zako!

Kule Kariakoo, BOT imefanyika sana baada ya baadhi ya watu kushtuka kuuza "nyumba" zao moja kwa moja! Ukaanza utaratibu, Bosi unaenda na pesa yako, lakini badala ya kununua nyumba, mwenye nyumba anakuruhusu ujenge kwa gharama zako halafu ama mnagawana floor au unafanya biashara kwa muda fulani na ule muda ukiisha, unarudisha nyumba kwa mwenye eneo, na kama utataka kuendelea na biashara, utakuwa mpangaji!!
 
Wewe jipe moyo tu,Sudan ya kusini ,Uganda ,Ethiopia na wengineo Sijui kama wafanyabiashara wao watapenda invalid mrefu kwenye kusafirisha mzigo yao
Mbona hueleweki unaeleza nini mkuu!

"...Sudan ya Kusini, Uganda, Ethiopia na wengine sijui kama wafanya biashara wao watapenda 'invalid'(?) mrefu kwenye kusafirisha mzigo yao."

Unataka kueleza nini na maneno hayo?

Kama una maana ya umbali, kwamba wafanyabiashara wa Ethiopia wataiona bandari ya Lamu kuwa karibu zaidi ya zile mbili wanazozitumia sasa hivi; yaani bandari za Djibouti na Eritrea? Yaani Lamu ichukue mizigo ya Ethiopia badala ya hizo bandari mbili?

Uganda wataacha kutumia Mombasa ili wahamie Lamu kwa sababu zipi hasa?

Sudan ya Kusini, bandari ya Port Sudan iliyoko Sudan, sio karibu zaidi kuliko kupitishia Lamu?

Hata kama bandari yetu ya Bagamoyo haitashindana kupeleka kwenye hizo nchi zilizotajwa hapo, wewe bado huoni kwamba bado ina nchi nyingi sana inazoweza kuzihudumia bila ya kuwa na ushindani wowote toka kwenye bandari ya Lamu?

Hata kama hukusoma lolote kuhusu somo la jiografia, huwezi kushindwa kuangalia ramani na ikakupa uelewa wa kujua nchi hizo zilipo na uwezekano wa kuhudumiwa na bandari zilizopo karibu na nchi hizo.

Hii si kujipa moyo, ndio ukweli wenyewe ulivyo. Lamu na Bagamoyo haziwezi kushindana. Zipo mbalimbali kabisa.
 
Ile barabara inayojengwa sasa hivi toka JKIA hadi mjini inajengwa kwa mpango huo wa BOT.

Nimependa mfano uliotoa wa nyumba za Kariakaoo; hili nilikuwa silijui.

Sasa kama nchi sijui 'merits' na 'demerits' za mbango huo wa BOT, na kwa miradi ipi, na kwa sababu zipi.

Sidhani kwamba kila mradi utakuwa na manufaa kwa nchi kwa kutegemea mpango huo.

Kw hiyo uamzi hutolewa kwa kila aina ya mradi baada ya kupima mambo kadhaa katika mipango ya nchi husika.

Hatuwezi kuwa tunaamua tu kutumia BOT kwa kila kitu tunachotaka kufanya.

Kama hatutaki bandari ya Bagamoyo iwe kwenye mbango huo, kwa sababu zetu maalum, basi na itakuwa hivyo.
 
Serikali ya Kenya imesema bandari ya Lamu iliyojengwa na China itapokea meli yake ya kwanza tarehe 20 mwezi huu.

Taarifa iliyotolewa na Hazina ya nchi hiyo jana imesema, kampuni ya Ujenzi na Mawasiliano (CCCC) ya China imekamilisha ujenzi wa gati la kwanza katika bandari hiyo ya pili ya kibiashara nchini Kenya, huku gati la pili na la tatu yakitarajiwa kukamilika mwezi Oktoba.
Taarifa hiyo imesema, ujenzi wa awamu ya kwanza wa bandari hiyo, unaohusisha magati matatu, ulianza mwaka 2015, huku awamu zinazofuata zikitarajiwa kufanywa na sekta binafsi chini ya mfumo wa uhusiano wa sekta binafsi na ya umma, ambapo magati 23 yatajengwa katika eneo hilo lenye urefu wa kilomita 10.
 

Wabongo kelele nyingi na kaubinafsi ndani yake, mnataka ninyi muendeshe bandari wakati uwezo huo hamuna.. ..williamson diamonds iliyoko mkoa wa Shinyanga selikali waliwanyang'anya wazungu huo mgodi, sasa ikawashinda kuimeneji.. ..end of the day wakaamua kuwarudishia.



πŸ‡¦πŸ‡·πŸ‡¦πŸ‡·πŸ‡¦πŸ‡·πŸ”₯πŸ”₯
 
Sina ufahamu kuhusu hiyo barabara inayojengwa under BOT!!

Aidha, hapa hakuna suala la kuamua kila mradi kuwa under BOT!

Kama ulivyoona hiyo quote ya Investopidia, duniani kote BOT inatumika sana kwenye LARGER Infrastructure Projects!

Na suala hilo la duniani kote linakuwa more relevant kwa nchi maskini...

Tuchukulie Mradi wa Bagamoyo kwa mfano... kama tunataka kwa ukubwa ule ule wa wanaotaka China, Bandari peke yake ni USD 10 Billion.

Ukitaka kui-utilize hiyo bandari, ni lazima na supporting infrastructure projects, kama vile reli. Sasa kwa haraka haraka tu hizo ni takribani TZS 25 TRILLIONS!!!

Katika ulimwengu wa PPP, it's IRRATIONAL kwa serikali kutumia TZS 25 TRILLIONS kuwekeza kwenye infrastructure project huku vital sectors kama elimu na afya zinadumaa eti ili mradi tu tujimwambafai tunajenga kwa "pesa zenu wenyewe"!!!

Na hata ukijenga kwa loan, kuna hatari kabla mradi huja-take off ukawa unalimbikiza riba na hatimae kuongeza mzigo wa madeni kwa serikali! Hili ndilo lilitokea Hambantota Port, Sri Lanka!!

Serikali ya Sri Lankailichukua mkopo na kujenga bandari!! Kwa u-selfish tu usiozingatia miiko ya biashara kama tunachojaribu kufanya sisi, Serikali ya Sri Lanka ikagoma kabisa kushirikiana na sekta binafsi huku ikitaka kila kitu waendeshe wenyewe!!!

Kwa mfano, wapo waliotaka kuwekeza kwenye oild storage facility lakini serikali ikagoma wakitaka kila kitu wafanye wenyewe! Kama mnaweza, well and good but the question is: Do you have what it takes to run everything on your own!!

Private Sector ikanawa mikono!!

Sitaki kurudia kueleza ambacho kilitokea pale Hambantota Port coz' wewe ni miongoni mwa wale waliowepo kwenye mjadala wa thread niliyokuwa nimeanzisha kuhusu hili suala, lakini kwa kifupi tu, Deni la ujenzi wa Bandari ya Hambantota likawa linakua siku baada ya siku huku bandari ikishindwa kufanya biashara iliyotarajia!
 
Sijui kama wanaweza kukuelewa hapo kwenye RED!
 
Ni wazi umewekeza sana kwenye huu mradi wa Bagamoyo, ndiyo maana huoni kingine chochote bali Mchina na bandari hiyo.
Aidha, hapa hakuna suala la kuamua kila mradi kuwa under BOT!
Basi kubali, kwenye mradi huu wa Bagamoyo, tunaweza kufanya tofauti na hivyo unavyopigania, kwani tatizo ni nini, hivyo vitisho vya TRILLION 25?
Ni lazima kila sehemu ya mradi huo ijengwe kwa muda huo mfupi, yaani miundo mbinu zote kwa pamoja? Mbona hiyo Lamu wameanza na sehemu ndogo ya ghati tatu pekee?
Kama ulivyoona hiyo quote ya Investopidia, duniani kote BOT inatumika sana kwenye LARGER Infrastructure Projects!

Na suala hilo la duniani kote linakuwa more relevant kwa nchi maskini...
Hata kama masharti ya ujenzi nchi inaona hayana faida nchi ikubali tu hiyo BOT kwa vile "Duniani kote BOT inatumika"?

Halafu sasa unatishia hata mikopo nchi isiitumie kujenga miradi yake, kwa vile Sri Lanka na Bandari yao walishindwa! Mradi huu wa Bandari ya Bagamoyo ni kama inakutoa akili kabisa, usione kingine chochote zaidi ya uchuuzi huo unaotafutwa hapo.

Tuliza akili, hatuwezi kukurupuka tu kwa vile kuna PPP na kusahau maslahi mapana ya nchi. Kama mkataba una manufaa kwetu, Bandari ijengwe kwa njia yoyote, iwe mkopo, sisi wenyewe na vidafu vyetu hata kwa miaka ishirini, au hata kwa hiyo BOT.

Naona kinachokusumbua sana wewe na wengine ni uhusika wa serikali kwenye miradi kama hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…