Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Bila shaka hawa watakuwa wale wenzetu wavaa vibagharashia. Mimi leo siko huko mkuu. Yesu na Mungu ni roho mbili tofauti; sio kitu kimoja mkuu.
Kama unasema mungu ananguvu nyingi alafu awe na nafsi moja basi huyo mungu hana nguvu, kiumbe chenye nafsi moj6ni mwadamu mungu yeye sio mwadamu kama sisi na tunasema kuwa ananguvu nyingi kwanini jambo la nafsi tatu lishindikane mbele zake.
 
Yesu hana mama yeye alikuwako tangu kabla ya maria,
Maria na Yosefu ni wazazi walezi/walishi wa Yesu, walimlea tangu utoto wake, Hata Yesu mwenyewe anawathamini, wewe ni nani usiwape thamani yao? Mungu ndiye aliwapa heshima ya kutimiza Unabii wake kupitia wao.

Yohane 19:26-27
Basi alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, mwanao.
Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama mama yako. Tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.
 
Tuanze na wewe kwa kunionyesha kwamba hakupaishwa! Tupe kifungu kwamba hakupaishwa.
Kifungu kinachothibitisha kuwa bikra Maria alipaishwa sina mkuu. Kama wewe unacho, unaweza kukiweka hapa kwa faida ya wengi. Kama huna, tusubiri wenyewe waje mkuu.
 
Tuanze na wewe kwa kunionyesha kwamba hakupaishwa! Tupe kifungu kwamba hakupaishwa.

(Marko 9:2-13; Luka 9:28-36)
Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao, uso wake ukang'aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama mwanga. Mose na Elia wakawatokea, wakawa wanazungumza naye.
Hakuna kifungu kinacho onesha kuwa alipaishwa na hakuna kifungu kinacho oneshwa kuwa hakupaishwa, je wewe unaamini alipaishwa kwa kifungu kipi?
 
Kifungu kinachothibitisha kuwa bikra Maria alipaishwa sina mkuu. Kama wewe unacho, unaweza kukiweka hapa kwa faida ya wengi. Kama huna, tusubiri wenyewe waje mkuu.
Kifungu unachopaswa kupewa mkuu ni cha kifungo cha miezi sita na viboko saba vya shingoni.
 
Mnanishangaza sana Waislamu wanamtambua Bikira Maria ila nyinyi protestants hamumtambui?Hizo dini mlinazo zote zilitoka Roma.Baada ya Luther na wengineo kuondoka ndio mkapata haya makanisa yote yaliyopo sasa.Mungu ni mmoja tunaheshimu ila pia msidhihaki vitu ambavyo hamvijui kuna mengi sana ambayo protestants hamyajui.Mimi ni shuhuda wa miujiza ya Bikira Maria na ninasema hapa wakristo tunamheshimu kwa sababu ni mama wa Mungu wetu na msaada wetu katika shida.Utakapokufa Yesu mwenyewe hawezi kumpokea mtu anayemdharau mama yake, kW maneno ya kumdhihaki.Mungu ajakuambia wewe udhihaki dini au imani za watu wengine kitu ambacho hukifahamu sio vyema kukiongelea
 
Tukio la Kusingiziwa

Baada ya Maryam kurudi kwa watu wake akiwa amembeba mtoto mchanga (Isa), watu walistaajabu na kumlaumu kwa kuwa na mtoto bila ya ndoa. Walisema:


(Qur'an 19:27-28)



Hapa, kaumu yake walikuwa wakimshutumu kwa uzinifu kwa sababu hawakuweza kuelewa jinsi alivyopata mtoto bila ya mwanaume.

Utetezi wa Maryam

Maryam hakuweza kujitetea kwa maneno yake. Badala yake, alimfuata amri ya Mungu ya kunyamaza na kuwaonyesha mtoto mchanga, Nabii Isa, ambaye kwa miujiza alianza kuzungumza ili kumtetea mama yake:


(Qur'an 19:30)



Hili lilikuwa ni ushahidi wa wazi kwa watu kwamba Maryam hakufanya dhambi yoyote, na mtoto wake alikuwa muujiza wa Mwenyezi Mungu.
Point na suala ni moja tu; Baada ya hayo yote, Je, Maryamu/Maria anastahili/hastahili HESHIMA kwa kuwa sehemu ya utimilifu wa Unabii wa MUNGU?
 
Luka 1
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?

30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.

33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.

(Maria mnamtoa wapi ?)
 
Biblia imehaririwa sana tu
Luka 1
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?

30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.

31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.

32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.

33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.

34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.

(Maria mnamtoa wapi ?)
 
Kwa nini hamumthamini mama wa Yesu Kristo?Mnadhani katika wananawake wote kwa nini Mungu alimchagua yeye na sio mwanamke mwingine.Mnadhani Yesu hamdhamini mama yake kama ambavyo nyinyi hamumdhamini? Unakuta mtu anasali anasema anamwamini Yesu lakini ni mtu huyohuyo utamkuta anaongea vibaya kuhusu mama yake Yesu.Kama ambavyo na nyinyi mnathamini mama zenu ni hivyo hivyo na Mungu mwana anamheshimu na kumsikiliza mama yake.Kasomeni Ufunuo Bikira Maria ametajwa katika ufunuo,tatizo hamsomi biblia na hata mkisoma hamtaki kuielewa!
1. Nani hamthamini bikra Maria mkuu?
2. Tunaomba utupe vifungu vya huo ufunuo mkuu. Sote hapa tunajifunza. Kama haya masuala unayafahamu vizuri, itapendeza ukitushirikisha.
 
Mtake msitake hata mama yake na mtume halipi hapa kwa bikira mariamu ( maria).
 

Attachments

  • 5887319-0e638715bf809aa1b17ffd05ad57727.mp4
    1.2 MB
Hakuna jina la Maria kwenye Biblia.
Acheni kuwapotosha watu.

Mathayo (Mat) 1:18
Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Piganeni tu 🤣 🤣.
 
Mnanishangaza sana Waislamu wanamtambua Bikira Maria ila nyinyi protestants hamumtambui?Hizo dini mlinazo zote zilitoka Roma.Baada ya Luther na wengineo kuondoka ndio mkapata haya makanisa yote yaliyopo sasa.Mungu ni mmoja tunaheshimu ila pia msidhihaki vitu ambavyo hamvijui kuna mengi sana ambayo protestants hamyajui.Mimi ni shuhuda wa miujiza ya Bikira Maria na ninasema hapa wakristo tunamheshimu kwa sababu ni mama wa Mungu wetu na msaada wetu katika shida.Utakapokufa Yesu mwenyewe hawezi kumpokea mtu anayemdharau mama yake, kW maneno ya kumdhihaki.Mungu ajakuambia wewe udhihaki dini au imani za watu wengine kitu ambacho hukifahamu sio vyema kukiongelea
Huwa wanatafuta mstari mmoja ulio tata kwenye biblia ili waanzishie kanisa la kupata maokoto.Pure conmen!
 
Back
Top Bottom