Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Mnanishangaza sana Waislamu wanamtambua Bikira Maria ila nyinyi protestants hamumtambui?Hizo dini mlinazo zote zilitoka Roma.Baada ya Luther na wengineo kuondoka ndio mkapata haya makanisa yote yaliyopo sasa.Mungu ni mmoja tunaheshimu ila pia msidhihaki vitu ambavyo hamvijui kuna mengi sana ambayo protestants hamyajui.Mimi ni shuhuda wa miujiza ya Bikira Maria na ninasema hapa wakristo tunamheshimu kwa sababu ni mama wa Mungu wetu na msaada wetu katika shida.Utakapokufa Yesu mwenyewe hawezi kumpokea mtu anayemdharau mama yake, kW maneno ya kumdhihaki.Mungu ajakuambia wewe udhihaki dini au imani za watu wengine kitu ambacho hukifahamu sio vyema kukiongelea
Shida ni tunamtambua kwa namna gani, yesu alikuwako tangu kabla yake na ndie alie muumba maria je wewe unakubali haya yote kama ni ndio inakuwaje yesu aliye muumba maria ndio haje kuwa mtoto wa maria?
 
Watu wa dini mnapaswa kutambua kitu kimoja usidhihaki imani ya mtu mwingine Mungu hapendi na hajakutuma kufanya hivyo.Mimi siwezi kumdhihaki maombi ya walokole najua kuna watu wameombewa na wachungaji wa kilokole na wakapona,hivyo hivyo kwa Lutheran,Sabato na mengineyo. Maria ni mtumishi wa Mungu na Mungu alimchagua kwa kusudi hilo ,Mungu hajakuita wewe kudharau watumishi wake,au kuwahukumu kwa namna yeyote ile,hata kwa wenzetu waislamu Mungu hajakutuma wewe kuwadhika au kuwasema .Sababu Mungu ni Mungu wa watu wote
 
Watu wa dini mnapaswa kutambua kitu kimoja usidhihaki imani ya mtu mwingine Mungu hapendi na hajakutuma kufanya hivyo.Mimi siwezi kumdhihaki maombi ya walokole najua kuna watu wameombewa na wachungaji wa kilokole na wakapona,hivyo hivyo kwa Lutheran,Sabato na mengineyo. Maria ni mtumishi wa Mungu na Mungu alimchagua kwa kusudi hilo ,Mungu hajakuita wewe kudharau watumishi wake,au kuwahukumu kwa namna yeyote ile,hata kwa wenzetu waislamu Mungu hajakutuma wewe kuwadhika au kuwasema .Sababu Mungu ni Mungu wa watu wote
Samahani lakini, wewe akili huna
 
Wewe hauwezi kuzungumza na Mama akamueleze Baba kama unahitaji jambo fulani? Bikira Maria ndiye alimzaa Yesu, anamjua mwanaye na aliumia hata wakati anateswa msalabani, Anamfahamu vyema mwanae.Kwenye Harusi ya Kana baada ya Divai kuisha mbona hawakumuendea Yesu moja kwa moja bali walienda kwa mama yake ili akawaombee? Kuna ubaya gani kupitisha maombi yako kwa mama ili yamfikie Baba? Hususan kama una makosa fulani uliyatenda yanayokufanya mpaka unaogopa kwenda kwa Baba.Kuhusu kufa na kufufuka mbona wapo watakatifu wengi tu ambao walikufa miili ila roho zao zi hai, Na wanatuombea kila siku, mfano Yesu alipokuwa mlimani alitokewa na Manabii Musa na Eliya ambao walishakufa zamani, Mifano ni mingi ila kwa leo ngoja tuishie hapa.
Kwahiyo mnazungumza na marehemu??
 
Jamani Maria alikuwa binadamu kama binadamu mwingine na aliendelea kuzaa watoto wengine maana alikuwa ameolewa ana mume sasa suala la Kristo alikuwa mtu tu aliyembeba sasa biashara ya kuomba Maria akuombee hicho kitu hamnaga maana hakunaga aliyemwomba Maria amuombee kwa Yesu huu ni upotofu Maria ni mtu tu hapaswi kuabudiwa jamani wakatoliki geukeni maana naona mnaongeza bidii kutengeneza masanamu ya huyu mama wa watu ABUDUNI MUNGU ALIYEJIDHIHIRISHA KWA NJIA YA KRISTO PEKEE muende mbinguni achen iman potofu
 
Tukio la Kusingiziwa

Baada ya Maryam kurudi kwa watu wake akiwa amembeba mtoto mchanga (Isa), watu walistaajabu na kumlaumu kwa kuwa na mtoto bila ya ndoa. Walisema:


(Qur'an 19:27-28)



Hapa, kaumu yake walikuwa wakimshutumu kwa uzinifu kwa sababu hawakuweza kuelewa jinsi alivyopata mtoto bila ya mwanaume.

Utetezi wa Maryam

Maryam hakuweza kujitetea kwa maneno yake. Badala yake, alimfuata amri ya Mungu ya kunyamaza na kuwaonyesha mtoto mchanga, Nabii Isa, ambaye kwa miujiza alianza kuzungumza ili kumtetea mama yake:


(Qur'an 19:30)



Hili lilikuwa ni ushahidi wa wazi kwa watu kwamba Maryam hakufanya dhambi yoyote, na mtoto wake alikuwa muujiza wa Mwenyezi Mungu.
Hapa tumsubiri bibi yetu FaizaFoxy aka FaizaFixy aje kutufafanulia mkuu.
 
Biblia imehaririwa sana tu
Imeharibiwa vipi tena.
Kuna mali imetaja jina la Maria ?
Mama wa Yesu anaitwa Mariamu na Biblia imeandikwa hivyo kabla ya Qurani kuliiga Hilo jina.

Wanao mwita Maria ndio wanakosea.
 
Hicho ndicho kinafanya awe hajazaliwa na Maria ili umdharau?
Mtu huyu huyu ana mstari wa Biblia ambapo unasema Yesu alizaliwa kwenye hori la ng'ombe na huyuhuyu anakuja kuandika hivi.Alizaliwa kwenye hori la ngombe alizaliwa na nani ?na je huyo aliyemzaa Yesu hivyo hakuwa mama yake?Yesu kipindi cha uhai wake akiwa anakaa na Mama Maria alikuwa anamwita nani?
 
Imani ni ufunuo kwa ajili ya watu fulani

Kama wakatoliki ndo wamefunuliwa hivyo na wewe hujafunuliwa bado hayo , basi yaache

Hata Neema ya ukristo tumefunuliwa wachache na ambao hawajafunuliwa hutuona sisi machizi kwahiyo usikonde

Mariam ni mama wa KRISTO YESU hivyo anaweza kweli kukuombea kwa mwanae amini Amin amin
Kwanini msiombe kupitia kwa mama zenu waliowazaa?
 
Kumkataa na kumuandika kihuni ni dharau tosha.Hebu jifikirie,nimeikuta picha tu ya mama yako mzazi halafu nikaichana,utajisikiaje?
Ninanaribu kukupa maarifa lakini unayakataa kumuheshimu mtu sio kuabudu ni vitu viwili tofauti Kwahiyo mimi nina muheshimu maria lakini namuabudu mungu na sio maria, Kwasababu kuabudu na kuheshimu ni vitu viwili tofauti
 
Mnanishangaza sana Waislamu wanamtambua Bikira Maria ila nyinyi protestants hamumtambui?Hizo dini mlinazo zote zilitoka Roma.Baada ya Luther na wengineo kuondoka ndio mkapata haya makanisa yote yaliyopo sasa.Mungu ni mmoja tunaheshimu ila pia msidhihaki vitu ambavyo hamvijui kuna mengi sana ambayo protestants hamyajui.Mimi ni shuhuda wa miujiza ya Bikira Maria na ninasema hapa wakristo tunamheshimu kwa sababu ni mama wa Mungu wetu na msaada wetu katika shida.Utakapokufa Yesu mwenyewe hawezi kumpokea mtu anayemdharau mama yake, kW maneno ya kumdhihaki.Mungu ajakuambia wewe udhihaki dini au imani za watu wengine kitu ambacho hukifahamu sio vyema kukiongelea
Nani kafanya haya yote unayotamka hapa mkuu? Umesoma uzi au umesoma heading tu? Hebu soma uzi kwamza halafu urudi hapa kuchangia.
 
Back
Top Bottom