Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Hiyo Symbol Ni Mudra Inaitwa Prana Mudra ni Mudra ambayo inabalance karibu vital elements zote earth, water, na fire..
Na mara Nyingi hutumika Kutaka Kuwatakia au Kueneza Amani kwa Wote..
Hata Yesu Ana picha Nyingi akionyesha Prana Mudra kw sababu ni Kama Ukiwa Unasema Amani iwe Juu yenu...
Krishna Amewahi kutoa Salamu au Mudra hiyo na Karibu Miungu yote imewahu kutoa Salamu hiyo au Mudra hiyo..
Ni peace Mudra..
Kuonyesha Kujaza amani kwa Watu au Ni sawa na Kusema Amani iwe nawe
Yesu hajawai piga picha
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Yupo karibu na Mungu,anasaidia kumshawishi Mungu wetu
 
Mama wa Yesu alikuwa anakunywa Divai peke yake? Na kwanini awape maelekezo ya nini cha kufanya ili kupokea muujiza huo wa maji kuwa divai kutoka kwa Yesu?
Yohane 2;
Siku ya tatu kulikuwa na harusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo, naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!” 4Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.” 5Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha. 7Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu. 8Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.” 9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi, 10akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”

Bado hakuna sehemu inaonyesha watu walimtuma Mariamu.
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Wakati unajibiwa ongeza na hili. Wale ma bikra 72 watatosha wanaume wote huko kwenye pepo ya mashariki ya kati? Au ni mwendo wa ku share hao 72 kwamba ni free ?
 
Hapa unawaambia nini ambao huamini kua Yesu ni Mungu? kwa mujibu wa andiko lako hapa ni kua Yesu na Mungu ni vitu viwili tofauti,

Ufafanuzi tafadhali.
YESU na Mungu ni tofauti ndio, ila Yesu ni Mungu

Soma hapa kwenye zaburi

Zaburi 45:6-7 (Agano la Kale)

Kiebrania cha Asili:

"Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, ni cha milele na milele; Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Umeupenda haki, ukachukia ubaya; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta kwa mafuta ya furaha kuliko wenzako."



Aya hii inamtaja mfalme (katika muktadha wa zaburi hii) kama Mungu (kwa lugha ya heshima), lakini pia inasema Mungu ndiye aliyemtia mafuta, akionyesha mamlaka ya juu zaidi.

Waebrania 1:8-9 (Agano Jipya)

Aya hii inamnukuu Yesu kama mfano wa utimilifu wa unabii huo wa Zaburi 45:6-7:

"Lakini kuhusu Mwana asema:
‘Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, ni cha milele na milele,
Na fimbo ya haki ni fimbo ya ufalme wako.
Umependa haki na kuchukia maasi;
Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta ya furaha zaidi ya wenzako.’"
 
Yesu alipokuwa anazungumza na MUSA na ELIYA alikuwa anazungumza na marehemu?
Wazee mbona hamsomi maandiko , mtatapeliwa sana na kina mwamposa kwa mtindo huu ,

Musa na Eliya hawakuwa wafu, Eliya alipaa mbinguni anawakilisha ambao hawataonja mauti, Musa ALIKUFA ,baadae akaja kufufuliwa na malaika ,anawakilisha watakaokufa na kufufuliwa

Ushahidi wa maandiko

Biblia inaonyesha kwamba Eliya hakufa bali alichukuliwa mbinguni akiwa hai. Hili liko wazi katika:

2 Wafalme 2:11

"Ikawa walipokuwa wakienda, wakizungumza, tazama, gari la moto na farasi wa moto likawatenganisha; Eliya akapanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli."

Hii inaonyesha kwamba Eliya hakuonja mauti, bali alichukuliwa moja kwa moja na Mungu.

Musa Alikufa na Akafufuka - Maandiko Husika

Biblia inasema wazi kwamba Musa alikufa, lakini kuna ushahidi wa kihisia kwamba alifufuliwa, na hili linatokana na tafsiri ya baadhi ya maandiko:

Kifo cha Musa:

Kumbukumbu la Torati 34:5-6

"Basi Musa, mtumishi wa Bwana, akafa huko katika nchi ya Moabu, kama Bwana alivyosema. Akamzika katika bonde, katika nchi ya Moabu, juu ya Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo."


Musa Akifufuka (Hili linafahamika kupitia Yuda 1:9):

Yuda 1:9

"Lakini Mikaeli, malaika mkuu, alipokuwa akishindana na Ibilisi, akibishana juu ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumleta shitaka la kumhukumu, bali alisema, ‘Bwana na akukemee.’"
 
Kwa nini hamumthamini mama wa Yesu Kristo?Mnadhani katika wananawake wote kwa nini Mungu alimchagua yeye na sio mwanamke mwingine.Mnadhani Yesu hamdhamini mama yake kama ambavyo nyinyi hamumdhamini? Unakuta mtu anasali anasema anamwamini Yesu lakini ni mtu huyohuyo utamkuta anaongea vibaya kuhusu mama yake Yesu.Kama ambavyo na nyinyi mnathamini mama zenu ni hivyo hivyo na Mungu mwana anamheshimu na kumsikiliza mama yake.Kasomeni Ufunuo Bikira Maria ametajwa katika ufunuo,tatizo hamsomi biblia na hata mkisoma hamtaki kuielewa!
Mbona mnajichanganya sana? Mnasema yesu ni mungu, alaf hapohapo unasema mungu wenu alimchagua Maria awe mama wa yesu sasa yesu ni mungu au siyo mungu? au ndo alijichagulia mama?
 
Wakati unajibiwa ongeza na hili. Wale ma bikra 72 watatosha wanaume wote huko kwenye pepo ya mashariki ya kati? Au ni mwendo wa ku share hao 72 kwamba ni free ?
Tusubiri wenyewe waje mkuu
 
Yesu hana mama biblia inasema yesu alikuwako tangu mwanzo wa misingi ya ulimwengu kilicho fanyika pale ni yesu kuuvaa ubinadamu ili adhihirishe upendo wake kwa wanadamu, leo hii watu wengi wanasema mungu anatupenda ukiuliza alitufanyia nini tulianguka dhambini lakini bado yupo pamoja nasi hakutuacha hata akaja kutoka mbinguni kukaa nasi hivyo yeye hana mama alikuwako.

Je wewe mungu wako anaupendo? Je kama anaupendo tuambie alikufanyia nini? Au unasema tu unaupendo alafu hakuna kitu alicho kufanyia, lakini yesu anatupenda alituumba kwa mfano wake na hata baada ya sisi kuingia dhambini hakutuacha alikuja kukaa nasi na ame ahidi anaebda kuandaa makao ili alipo sisi tuwako.


Nina ndugu zangu wengi na marafiki zangu wengi ni wakatoliki lakini katika uhalisia ukatoliki umetengeneza vitu vingi vya uzushi ambavyo hata katika historia ya yesu na mitume wake kwenye biblia hawakuvifanya.


Yesu haku muabudu maria wala mitume, yesu hakutengeneza sanamu ya maria wala mitume, pia kanisa hili limetafuta sanamu bandia za muigizaji wa uhusika wa yesu na kuzifanya kama huyo ndio yesu yule halisi, vile vile kanisa hilo limefanya na kwa maria pia limechukua sanamu za muigizaji na kuanza kuliabudu haya yote ni uzushi na upotoshaji mkubwa wa wawtu wa mungu.
Pole sana kwa kukosa maarifa. Hakuna unachokijua. Umchanga sana katika imani. Jibidishe ili uujue ukweli wa kiimani. Hakuna kitu hata kimoja kinachofanywa na Kanisa Katoliki kisicho na msingi wa kiimani.
 
Wewe ndio unajichanganya soma vizuri biblia soma vizuri nilichoandika
Mbona mnajichanganya sana? Mnasema yesu ni mungu, alaf hapohapo unasema mungu wenu alimchagua Maria awe mama wa yesu sasa yesu ni mungu au siyo mungu? au ndo alijichagulia mama?
 
Bikra Maria alipalizwa mbinguni akiwa mzima bila kufa.
Bado anaendelea na safari ya mbinguni au ameshafika ametulia sehemu ? Na atakua anafanya shuhuli gani hapo mahali kwa miaka yote hiyo
 
Hakuna jina la Maria kwenye Biblia.
Acheni kuwapotosha watu.

Mathayo (Mat) 1:18
Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Nadhani original ni marry sasa kuipeleka kwenye lugha yako ni maamuzi
 
Back
Top Bottom