Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Mfate tu, Paroko atakujibu vizuri tu, maana hili jambo limeulizwa humu na kutolewa majibu, nyuzi zingine zilifutwa
Hizo nyuzi sikubahatika kuziona mkuu. Majibu gani yalitolewa?
 
Katika harusi ya Kana, waalikwa walivyoishiwa na mvinyo, hawakwenda kwa Yesu moja kwa moja bali walipitia kwa bikira Maria, mama mtu. Kwa hiyo, wakatoliki wameiga kilichofanyika siku ile maana walifanikiwa kwa Yesu kubadili maji kuwa divai bora zaidi.
Kule kana walimtumia akiwa hai. Sasa hivi wanamtumiaje wakati tayari ameishakufa mkuu?
 
Wazee mbona hamsomi maandiko , mtatapeliwa sana na kina mwamposa kwa mtindo huu ,

Musa na Eliya hawakuwa wafu, Eliya alipaa mbinguni anawakilisha ambao hawataonja mauti, Musa ALIKUFA ,baadae akaja kufufuliwa na malaika ,anawakilisha watakaokufa na kufufuliwa

Ushahidi wa maandiko

Biblia inaonyesha kwamba Eliya hakufa bali alichukuliwa mbinguni akiwa hai. Hili liko wazi katika:

2 Wafalme 2:11



Hii inaonyesha kwamba Eliya hakuonja mauti, bali alichukuliwa moja kwa moja na Mungu.

Musa Alikufa na Akafufuka - Maandiko Husika

Biblia inasema wazi kwamba Musa alikufa, lakini kuna ushahidi wa kihisia kwamba alifufuliwa, na hili linatokana na tafsiri ya baadhi ya maandiko:

Kifo cha Musa:

Kumbukumbu la Torati 34:5-6




Musa Akifufuka (Hili linafahamika kupitia Yuda 1:9):

Yuda 1:9
Kwa hiyo kupaishwa mbinguni kwa Eliya na Musa na bikra Maria (kama inavyodhabiwa), moja kwa moja waumini wanaweza kupitishia maombi yao kwa watu hawa badala ya kumuomba Yesu moja kwa moja mkuu?
 
Kwa hiyo kupaishwa mbinguni kwa Eliya na Musa na bikra Maria (kama inavyodhabiwa), moja kwa moja waumini wanaweza kupitishia maombi yao kwa watu hawa badala ya kumuomba Yesu moja kwa moja mkuu?
Hakuna maandiko yanayosema mariamu alipaishwa

Pia maandiko yanasisitiza hakuna jina WALILOPEWA WANADAMU ISIPOKUWA JINA LA YESU Tu
 
Kwa hiyo mkuu hapa inabidi tuamini tu bila kuhoji kama vile wapagani wanavyoamini tunguli za sangoma?
Hapo ndio kunashida ya dini hii,ukianza kuhoji unaonekana we ni mpotevu.
 
Hakuna maandiko yanayosema mariamu alipaishwa

Pia maandiko yanasisitiza hakuna jina WALILOPEWA WANADAMU ISIPOKUWA JINA LA YESU Tu
Sawa mkuu. Sasa naanza kupata mwanga kwamba maombi ya wakatoliki kupitia kwa bikra Maria ni ya kudhania tu.
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Una swali la msingi na mimi naomba kuuliza kwa kujazia nyama,

Kwani wakristo hawawezi kumuomba Muumba wao (Baba yake Yesu) moja kwa moja bila kupitia kwa Yesu kama alivyosema Yesu wamwabudu baba yake tu?

Yohana 4:23
Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Yohana 17:3
Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma(mtume).

1korintho 15:28
Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe (Yesu) naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
 
Una swali la msingi na mimi naomba kuuliza kwa kujazia nyama,

Kwani wakristo hawawezi kumuomba Muumba wao (Baba yake Yesu) moja kwa moja bila kupitia kwa Yesu kama alivyosema Yesu wamwabudu baba yake tu?

Yohana 4:23
Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Yohana 17:3
Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma(mtume).

1korintho 15:28
Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe (Yesu) naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
Unaona jinsi mnavyosoma Biblia kama hadithi! Hivi hujawahi kuona msitari ambao Yesu anaagiza chochote tutakachomwomba baba yake kupitia yeye tutakipata? Kazi kweli kweli!
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

1. Ujue kwamba Mungu alipenda kuukomboa ulimwengu kupitia kwa Maria, mama wa Yesu. Huu haukuwa mchezo wa kuigiza. It's the 'economy of salvation' (mpango wa Mungu wa kuwakomboa wanadamu).
2. Mungu hafungwi na muda. Kila jambo mbele ya Mungu linatenda sasa (Zaburi 90:4 na 2 Petro 3:8). Hakuna wakati uliopita au ujao.
3. Harusi ya Kana (Yohane 2:1-25) na pia Yesu alipobaki Jerusalem (Luka 2:41-52) na kutafuta na wazazi wake, 1) kule Kana waliokuwa harusini walimwendea Maria ili amwambie mwanae kwamba wsmeishiwa divai, na Maria akamwambia, na kisha akawaambia wale watu "atakachowaambia fanyeni". 2) Kule Jerusalem pia Maria na Yosefu walikuwa wakimtafuta Yesu, kisha wakamkuta hekaluni na mama yake akamuuliza "mbona umetufanya hivi...?" Katika masimulizi yote mawili Yesu alifuata au alitimiza aliyoambiwa na mama yake. Kanisa Katoliki linatambua umuhimu wa Maria katika maisha ya Yesu na katika ukombozi wa wanadamu. Haiwezekani Maria akabaki pembeni wakati Mungu mwenyewe alipenda kumshirikisha katika kumzaa Yesu na katika ukombozi wa wanadamu. Hivyo, Maria ana hadhi ya kuwa mama yetu kiroho/mama wa Kanisa na tunaweza kumwomba, kama walivyomwomba kwenye harusi ya Kana, amwambie mwanae kwamba wageni harusini wameishiwa divai na Yesu alitimiza alichoambiwa. Tunapomwomba Maria, tunamwomba atuombee kwa mwanae. Tunataka kuonyesha muunganiko uliopo/uhusiano ulioko kati ya yeye na mwanae na sisi pia. Kumbuka pale msalabani Yesu alimwambia Yohane (mmoja wa wale wanafunzi wake aliyempenda zaidi) "huyu ni mama yako" na kwa Maria "huyu ni mwanao" na kuanzia siku hiyo Maria alikwenda kukaa kwa Yohanne. Pia katika Luka 1:48 baada ya kujazwa na Roho Mtakatifu Maria alisema: "kuanzia sasa vizazi vyote vitaniita mbarikiwa/mwenyeheri."
4. Kwa hiyo, tukimwomba Maria (kama nilivyosema kwamba mbele ya Mungu kila kitu ni sasa) hakuna cha wakati uliopita, yote yanatendeka sasa. Na Yesu alisema "anayemwamini hata kama amekufa, ataishi milele" (Yohanne 11:25). Je, Maria alimwamini Yesu? Je, Maria anaishi? Ndiyo.
 
Mtuache jamani na imani zetu..yani huku kwetu hakuna umaskini wa kutupwa wala majini wala mapepo..wakatoliki tuna kula raha hapa duniani..tunaishi kwa raha bila masharti kama waganga..nyumba zetu zina furaha na amani...tunakunywa ka mvinyo ketu na kula kitimoto kg moja...
Yanii kiufupi tuu tuna raha..
Na ukitaka kumjua mama Bikira Maria sali rozali yake...utaona maajabu mengi atakayokutendea kupitia mwanae Yesu Kristo...
Malizia kwa kusema haya
"Bikira Maria Malkia wa amani,mama wa msaada,kimbilio la wakosefu,mama wa tumaini jema,malkia wa familia...msaada wa wagonjwa....n.k
Utuombeee
 
Yupo hai kiroho,na katika sala tunahusisha roho kwahiyo kuwasiliana na roho mwanadamu (mwili na roho) anayonafasi yakupitia kwenye roho iliyokaribu katika unyenyekevu.
 
Back
Top Bottom