Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Bikra Maria alipalizwa mbinguni akiwa mzima bila kufa.
Lete ushahidi wa andiko.
Imeandikwa Mathayo ngapi aya ya ngapi?
Hata kama imeandikwa kwenye misale ya waumini tuambie ni ukurasa wa ngapi?
 
Wewe hauwezi kuzungumza na Mama akamueleze Baba kama unahitaji jambo fulani? Bikira Maria ndiye alimzaa Yesu, anamjua mwanaye na aliumia hata wakati anateswa msalabani, Anamfahamu vyema mwanae.Kwenye Harusi ya Kana baada ya Divai kuisha mbona hawakumuendea Yesu moja kwa moja bali walienda kwa mama yake ili akawaombee? Kuna ubaya gani kupitisha maombi yako kwa mama ili yamfikie Baba? Hususan kama una makosa fulani uliyatenda yanayokufanya mpaka unaogopa kwenda kwa Baba.Kuhusu kufa na kufufuka mbona wapo watakatifu wengi tu ambao walikufa miili ila roho zao zi hai, Na wanatuombea kila siku, mfano Yesu alipokuwa mlimani alitokewa na Manabii Musa na Eliya ambao walishakufa zamani, Mifano ni mingi ila kwa leo ngoja tuishie hapa.

Hapa mkuu naona umeongea mawazo yako maandiko hayaonyeshi kama watu walimfuata mama wa Yesu kuomba divai ila mama wa Yesu yaani Mariamu mwenyewe alimwambia Yesu kua divai imeisha.
 
Dokta hi symbol ya Mkono mmoja na vidole vi2 juu umeona Miungu mingapi Hadi Sasa katika alama hiyo. ?
Hiyo Symbol Ni Mudra Inaitwa Prana Mudra ni Mudra ambayo inabalance karibu vital elements zote earth, water, na fire..
Na mara Nyingi hutumika Kutaka Kuwatakia au Kueneza Amani kwa Wote..
Hata Yesu Ana picha Nyingi akionyesha Prana Mudra kw sababu ni Kama Ukiwa Unasema Amani iwe Juu yenu...
Krishna Amewahi kutoa Salamu au Mudra hiyo na Karibu Miungu yote imewahu kutoa Salamu hiyo au Mudra hiyo..
Ni peace Mudra..
Kuonyesha Kujaza amani kwa Watu au Ni sawa na Kusema Amani iwe nawe
 
Hapa mkuu naona umeongea mawazo yako maandiko hayaonyeshi kama watu walimfuata mama wa Yesu kuomba divai ila mama wa Yesu yaani Mariamu mwenyewe alimwambia Yesu kua divai imeisha.
Mama wa Yesu alikuwa anakunywa Divai peke yake? Na kwanini awape maelekezo ya nini cha kufanya ili kupokea muujiza huo wa maji kuwa divai kutoka kwa Yesu?
Yohane 2;
Siku ya tatu kulikuwa na harusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo, naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!” 4Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.” 5Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha. 7Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu. 8Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.” 9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi, 10akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
 
"Salam Maria umejaa neema bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa,
Maria mtakatifu mama wa MUNGU utuombee sisi ni wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu .Amina"🙏
 
Wakatoliki tuna amini kuwa kuna makundi yetu matatu.
Kundi la kwanza ni la walio hai kimwili. Hawa ndio sisi tuonatype humu. Hili kundi linahubiri na kuhubiriwa. Wanaomba na kuombea kwa Mungu.
Kundi la pili na la tatu ni la wafu wa kimwili. Hawa waliishi ila wameshakufa. Hawa wapo makurdi mawili, watakatifu na walio tohorani. Tohorani maana yake ni kwamba wapo katika hali flani ya Dhambi ambayo yapaswa msamaha wa Mungu. Bahati mbaya hawa hawawezi kuomba au kuombea. Hawa wanaombewa na kundi/kanisa la duniani. Ndio maana ya kuombea wafu. Katika wafu wa kimwili, kuna watakatifu. Hawa waliishi maisha ambayo yalifanya wafe kifo chema. Bikira Maria tunaamini ni mtakatifu. Kwa hiyo whether alikufa au kutwaliwa haijalishi cha msingi ni Mtakatifu. Watakatifu wanaombea makundi yote ila wao hawajiombei maana tayari wapo "cleared".
Katika harusi ya Kana, waalikwa walivyoishiwa na mvinyo, hawakwenda kwa Yesu moja kwa moja bali walipitia kwa bikira Maria, mama mtu. Kwa hiyo, wakatoliki wameiga kilichofanyika siku ile maana walifanikiwa kwa Yesu kubadili maji kuwa divai bora zaidi.
 
KATI YA MARIA NA YESU NANI NI MKUBWA?
TUANZIE HAPA THEN MAJIBU MTAYAPATA WENYEWE.
 
Hiyo Symbol Ni Mudra Inaitwa Prana Mudra ni Mudra ambayo inabalance karibu vital elements zote earth, water, na fire..
Na mara Nyingi hutumika Kutaka Kuwatakia au Kueneza Amani kwa Wote..
Hata Yesu Ana picha Nyingi akionyesha Prana Mudra kw sababu ni Kama Ukiwa Unasema Amani iwe Juu yenu...
Krishna Amewahi kutoa Salamu au Mudra hiyo na Karibu Miungu yote imewahu kutoa Salamu hiyo au Mudra hiyo..
Ni peace Mudra..
Kuonyesha Kujaza amani kwa Watu au Ni sawa na Kusema Amani iwe nawe
Vipi kuhusu Baphomet ?
 
Vipi kuhusu Baphomet ?
Baphomet ina maaelezo mengi sana But yeah Baphomet pia Ina Prana mudra..
KAma nilivyosema Prana Mudra inaconnect Energy za Upande wa 4 Elements Zote na Kuzibalance..

Baphomet ina pande Mbili.kama Utakuwa umeiangalia Vizuri ina Upande wa Jua/Mwezi wenye Mwanga ambao ni wa Juu na Inaupande wa Giza au Mwezi wenye Giza wa Chini..

So hiyo inaashiria Kinachofanyika kwa Upamde wa Giza ma wa Nuri pia Hifanyika.hivyo ila kwa Pande ya Opposite yake..

Nakunaliana ma weww Kuhusus Baphomet Sema Wengi sana hawaielewi Baphomet haga kidogo
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Unajua mambo ya dini hayafai kuyachambua tuwaache kila mtu aamini atakavyo
 
Wewe hauwezi kuzungumza na Mama akamueleze Baba kama unahitaji jambo fulani? Bikira Maria ndiye alimzaa Yesu, anamjua mwanaye na aliumia hata wakati anateswa msalabani, Anamfahamu vyema mwanae.Kwenye Harusi ya Kana baada ya Divai kuisha mbona hawakumuendea Yesu moja kwa moja bali walienda kwa mama yake ili akawaombee? Kuna ubaya gani kupitisha maombi yako kwa mama ili yamfikie Baba? Hususan kama una makosa fulani uliyatenda yanayokufanya mpaka unaogopa kwenda kwa Baba.Kuhusu kufa na kufufuka mbona wapo watakatifu wengi tu ambao walikufa miili ila roho zao zi hai, Na wanatuombea kila siku, mfano Yesu alipokuwa mlimani alitokewa na Manabii Musa na Eliya ambao walishakufa zamani, Mifano ni mingi ila kwa leo ngoja tuishie hapa.
Kama mariam n mama yetu, basi yesu ni kaka yetu. Naogopaje kumwambia kaka yangu kua nimemega kamke kajirani yangu naomba unisamehe!?!?

Hapa ni rahisi kuliko kwenda kumwambia mama habar hiz
 
Wakatoriki ndio Wana vitabu vyote vya maarifa kuhusu mambo yanayoonekana na yasiyoonekana ,biblia na zaidi ya biblia, biblia Yao tu Ina vitabu 72, Tena vina uvuvio, ila mlivoshindwa kuvielewa kwa msaada wa Mungu mkasema havina uvuvio,. , hakuna jambo wanafanya kwa bahati mbaya, ila SEMA nyie kwenye kuhangaika kutafuta maana mmekuwa mkiibuka na maana potoshi alafu mnamsingizia roho MTAKATIFU
Uvuvio are you serious??
 
Hakuna jina la Maria kwenye Biblia.
Acheni kuwapotosha watu.

Mathayo (Mat) 1:18
Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
alionekana na mimba ya miezi mingapi wakati ndio kwanza kaposwa?

Yusuph nae angedai fidia unaoaje single mother
 
Back
Top Bottom