Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

Wakatoliki: Bikra Maria utuombee kwa mwanao Yesu. Je, bado yu hai?

1. Ujue kwamba Mungu alipenda kuukomboa ulimwengu kupitia kwa Maria, mama wa Yesu. Huu haukuwa mchezo wa kuigiza. It's the 'economy of salvation' (mpango wa Mungu wa kuwakomboa wanadamu).
2. Mungu hafungwi na muda. Kila jambo mbele ya Mungu linatenda sasa (Zaburi 90:4 na 2 Petro 3:8). Hakuna wakati uliopita au ujao.
3. Harusi ya Kana (Yohane 2:1-25) na pia Yesu alipobaki Jerusalem (Luka 2:41-52) na kutafuta na wazazi wake, 1) kule Kana waliokuwa harusini walimwendea Maria ili amwambie mwanae kwamba wsmeishiwa divai, na Maria akamwambia, na kisha akawaambia wale watu "atakachowaambia fanyeni". 2) Kule Jerusalem pia Maria na Yosefu walikuwa wakimtafuta Yesu, kisha wakamkuta hekaluni na mama yake akamuuliza "mbona umetufanya hivi...?" Katika masimulizi yote mawili Yesu alifuata au alitimiza aliyoambiwa na mama yake. Kanisa Katoliki linatambua umuhimu wa Maria katika maisha ya Yesu na katika ukombozi wa wanadamu. Haiwezekani Maria akabaki pembeni wakati Mungu mwenyewe alipenda kumshirikisha katika kumzaa Yesu na katika ukombozi wa wanadamu. Hivyo, Maria ana hadhi ya kuwa mama yetu kiroho/mama wa Kanisa na tunaweza kumwomba, kama walivyomwomba kwenye harusi ya Kana, amwambie mwanae kwamba wageni harusini wameishiwa divai na Yesu alitimiza alichoambiwa. Tunapomwomba Maria, tunamwomba atuombee kwa mwanae. Tunataka kuonyesha muunganiko uliopo/uhusiano ulioko kati ya yeye na mwanae na sisi pia. Kumbuka pale msalabani Yesu alimwambia Yohane (mmoja wa wale wanafunzi wake aliyempenda zaidi) "huyu ni mama yako" na kwa Maria "huyu ni mwanao" na kuanzia siku hiyo Maria alikwenda kukaa kwa Yohanne. Pia katika Luka 1:48 baada ya kujazwa na Roho Mtakatifu Maria alisema: "kuanzia sasa vizazi vyote vitaniita mbarikiwa/mwenyeheri."
4. Kwa hiyo, tukimwomba Maria (kama nilivyosema kwamba mbele ya Mungu kila kitu ni sasa) hakuna cha wakati uliopita, yote yanatendeka sasa. Na Yesu alisema "anayemwamini hata kama amekufa, ataishi milele" (Yohanne 11:25). Je, Maria alimwamini Yesu? Je, Maria anaishi? Ndiyo.
Well said!
 
Unaona jinsi mnavyosoma Biblia kama hadithi! Hivi hujawahi kuona msitari ambao Yesu anaagiza chochote tutakachomwomba baba yake kupitia yeye tutakipata? Kazi kweli kweli!
Sawa ila pia wengi hawajui majira ya Muumba kutokana na mapokeo ya dini na dhehebu mbalimbali,maana mistari kweny kitabu imeandikwa ili itimie na majira ya Yesu ilishaisha tupo majira ya Muumba mwenyewe kwa mujibu wa

1Korintho 15:24-28
24
Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.

25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.

28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe (Yesu) naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.

Zekaria 14:9
Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja.

Maana hata Yesu alipotufundisha sala ya Baba yetu,alisema tuombe ufalme wa Baba yake uje.

Mathayo 6:9
Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Mwili tu ndiyo unaokufa roho inashi kati ya sehemu hizi mbili (1) peponi (11) kuzimu kote zinangoja siku ile ya hukumu.Hivyo wanapomwomba Maria,hawamwombi MTU Bali ile roho iliyopeponi kwa kuwa yeye alibarikiwa tayari na Mungu mwenyewe.Je wewe na Mimi tukifa tutaenda idara gani?
 
Mwili tu ndiyo unaokufa roho inashi kati ya sehemu hizi mbili (1) peponi (11) kuzimu kote zinangoja siku ile ya hukumu.Hivyo wanapomwomba Maria,hawamwombi MTU Bali ile roho iliyopeponi kwa kuwa yeye alibarikiwa tayari na Mungu mwenyewe.Je wewe na Mimi tukifa tutaenda idara gani?
1. Kuna kifungu chochote kwenye biblia kinacholazimisha kuongea na Yesu kupitia kwa roho ya bikra Maria badala ya kuongea na Yesu moja kwa moja?

2. Tupe kifungu kwenye biblia kinachoidhinisha roho za wafu kutumika kuwaombea walio hai.
 
Yupo hai kiroho,na katika sala tunahusisha roho kwahiyo kuwasiliana na roho mwanadamu (mwili na roho) anayonafasi yakupitia kwenye roho iliyokaribu katika unyenyekevu.
Wapi pameandikwa kwamba mtu hafiki kwa Yesu pasipo kupitia kwa bikra Maria?
 
Wewe hauwezi kuzungumza na Mama akamueleze Baba kama unahitaji jambo fulani? Bikira Maria ndiye alimzaa Yesu, anamjua mwanaye na aliumia hata wakati anateswa msalabani, Anamfahamu vyema mwanae.Kwenye Harusi ya Kana baada ya Divai kuisha mbona hawakumuendea Yesu moja kwa moja bali walienda kwa mama yake ili akawaombee? Kuna ubaya gani kupitisha maombi yako kwa mama ili yamfikie Baba? Hususan kama una makosa fulani uliyatenda yanayokufanya mpaka unaogopa kwenda kwa Baba.Kuhusu kufa na kufufuka mbona wapo watakatifu wengi tu ambao walikufa miili ila roho zao zi hai, Na wanatuombea kila siku, mfano Yesu alipokuwa mlimani alitokewa na Manabii Musa na Eliya ambao walishakufa zamani, Mifano ni mingi ila kwa leo ngoja tuishie hapa.
 

Attachments

  • 686EF917-88B5-4F56-870E-73B5E0BC1BF4.jpeg
    686EF917-88B5-4F56-870E-73B5E0BC1BF4.jpeg
    53.8 KB · Views: 1
Una swali la msingi na mimi naomba kuuliza kwa kujazia nyama,

Kwani wakristo hawawezi kumuomba Muumba wao (Baba yake Yesu) moja kwa moja bila kupitia kwa Yesu kama alivyosema Yesu wamwabudu baba yake tu?

Yohana 4:23
Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Yohana 17:3
Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma(mtume).

1korintho 15:28
Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe (Yesu) naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
Mbona biblia imeeleza vzr Tu au hamsomi
 
Siku zote nimekuwa nikiwasikia wakatoliki katika sara zao wakimuomba bikra Maria, mama yake Yesu, awaombee. Hata katika nyimbo nyingi wanazotunga, wanamtaja bikra Maria na kumsihi awaombee kwa Yesu. Je, kwani huyu mama bado yu hai? Je, imani ya dini yao haihuruhusu muumini kumuomba Yesu moja kwa moja bila kupitia kwa mama yake?

View: https://www.youtube.com/watch?v=V9C1rqOJfxc
Hili ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu bila majibu lakini nikaona leo nilete hili swali mbele ya wanazuoni wa masuala ya dini mliojaa hapa JF mnisaidie kutegua hiki kitendawili. Mtu yeyote anayefahamu hili suala kinagaubaga naomba anifahamishe nipate kuelewa.

Kwa uelewa wangu mdogo, nafahamu kuwa mtu pekee aliyekufa na kufufuka ni Yesu tu. Sasa huyu bikra Maria ina maana yeye hakufa? Kama bado yu hai yupo wapi? Tunaambiwa Yesu baada ya kufufuka alipaa mbinguni na ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Je, Maria yeye yu wapi? Au yeye ndiye ameketi mkono wa kushoto?

Maswali ni mengi lakini kwa kuwa humu JF kuna watu wenye uelewa mkubwa wa masuala ya dini, wakiwemo mapdre na maaskofu wa kanisa Katoliki mliomo humu, naomba mnifafanulie kuhusu hili jambo nipate kufunguka macho.

Asanteni sana.

Kumbe ni Kwa akili zako fupi hapo sawa....ila haujui kuwa hakufariki alipalizwa mbinguni!?? ....we soma tu madrasa ndugu... Kama sio msabato basi wale wazee wa kobazi na baraghashea ndio mnaujua kuhangaika na Ukatoliki kuliko Imani zenu.
 
Kumbe ni Kwa akili zako fupi hapo sawa....ila haujui kuwa hakufariki alipalizwa mbinguni!?? ....we soma tu madrasa ndugu... Kama sio msabato basi wale wazee wa kobazi na baraghashea ndio mnaujua kuhangaika na Ukatoliki kuliko Imani zenu.
Mkuu sasa kwanini usitupe hiyo elimu tufaidike wote hapa badala ya kutuambia tu kwamba kuna maandiko badala ya kuyaweka hapa hayo maandiko?
 
Lete kifungu tusome mkuu
Yesu Kristo, kulingana na mafundisho ya Biblia, ni njia ya pekee ya kufikia Mungu Baba ,hakuna cha Maria wala mtakatifu yeyote. Katika Yohana 14:6, Yesu anasema:
"Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi."
Hii inaonyesha kwamba Yesu ni mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu, akiunganisha uhusiano uliovunjika na dhambi.

Ni kweli kwamba Yesu mara nyingi aliwafundisha wafuasi wake kumwabudu na kumuomba Mungu Baba moja kwa moja. Kwa mfano:

Katika Mathayo 6:9, Yesu aliwafundisha wanafunzi wake Sala ya Baba Yetu

"Basi, ninyi salini hivi, Baba yetu uliye mbinguni..."
Hii inaonyesha kwamba maombi yanaweza kuelekezwa kwa Baba moja kwa moja.

Katika Yohana 4:23, Yesu anaeleza kwamba waabuduo wa kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli. Hii inaonyesha umuhimu wa uhusiano wa moja kwa moja kati ya muumini na Mungu Baba.

Yesu pia anafahamika kama Kuhani Mkuu wa agano jipya. Katika Waebrania 4:14-16, Yesu anatajwa kama Kuhani Mkuu ambaye anatuwezesha kupata neema mbele za Mungu. Hii inamaanisha kwamba ingawa waumini wanaweza kumuomba Baba moja kwa moja, Yesu ndiye anayefanikisha upatanisho huo.

Katika Yohana 10:30, Yesu anasema:
"Mimi na Baba tu umoja."
Maneno haya yanaonyesha kwamba kumuomba Yesu au Baba ni sawa kwa sababu wana uhusiano wa karibu kabisa. Kwa hivyo, wakati Wakristo wanapomuomba Mungu kupitia Yesu, hawampuuzilii Mungu Baba, bali wanaheshimu jukumu la Yesu kama mpatanishi.

Aya ni nyingi sana zipo
 
Kumbe ni Kwa akili zako fupi hapo sawa....ila haujui kuwa hakufariki alipalizwa mbinguni!?? ....we soma tu madrasa ndugu... Kama sio msabato basi wale wazee wa kobazi na baraghashea ndio mnaujua kuhangaika na Ukatoliki kuliko Imani zenu.
Hakuna hilo andiko si useme ukweli tu mnafata mapokeo ya WANADAMU,

Kuna Aya Huwa mnaitumia ya ufunuo 12:1

Ukweli haihusihani kabisa , fundisho la maria kupalizwa ni fundisho la kipagani na limepokelewa na kanisa katoliki juzi juzi tu hapa ,muwe mnasoma historia

Mnamo tarehe 1 Novemba 1950, Papa Pius XII alitangaza rasmi mafundisho ya kupalizwa kwa Mariamu kuwa fundisho rasmi la imani (dogma) kwa tamko la Munificentissimus Deus. Alisema:
“Baada ya maisha yake duniani, Mama wa Mungu, bila dhambi, alipalizwa mwili na roho kwenda utukufu wa mbinguni.”
 
Maria ni mwanadamu wa kawaida, hana hadhi kuongea mbele za Mungu kwa ajili ya wanadamu wengine kwa sababu hakulipa deni lolote. Yesu Kristo pekee (ambaye ni Mungu) ndiye kafara ambalo Mungu alijifanyia yeye mwenyewe kwa ajili ya wanadamu kupitia kwa maombi, na chochote kama kiunganishi. Yesu Kristo ni Mungu aliyeuvaa mwili hivyo ni Mungu yule yule, na alipofanyika kafara ni kwamba alikuwa anatengeneza kafara yeye mwenyewe ili wanadamu wapitie kwa maombi, kwa wokovu na kwa kila communication. kwa maana hiyo, maraia hana hadhi pia kumwambia Yesu chochote kwa niaba ya wanadamu wengine kwa sababu Yesu ni Mungu. Maria alikuwa anamwambia hivyo Yesu akiwa katika mwili hapa duniani, mwili alioufanya wa kibinadamu, na alikuwa mama kwa kibinadamu na siku Yesu alipokufa na kupaa mbinguni baada ya kufufuka ndio mwisho wa ubinadamu wa Yesu hivyo maria hana hadhi.

kwanini tunasema maria hana hadhi? kwa sababu hakufanyika kafara, hakufa kwa ajili ya wanadamu, hakumwaga damu hata ya kujikwaa kidoleni tu kwa ajili ya wanadamu, hivyo ni ujinga mkubwa sana kumfanya mwombezi wakati hana mandate kumsogeza mwanadamu yeyote mbele za Mungu.

YOHANA 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi

MATENDO 4:12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

YOHANA 14:13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.

hii ni mistari michache tu ambayo Yesu mwenyewe aliagiza kwamba hatuwezi kupata chochote tusipoomba kwa Jina lake, sasa wakatoliki wanamdharau Yesu wanaona bora waombe kwa maria. wanajilisha upepo.

MUNGU ametupatia wanadamu njia ya kuwasiliana naye, namna ya kufika kwake, shetani akaingiza njia anayoijua yeye ili wanadamu wapoteze muda mwingi kuomba bila majibu, na ndio maana hakuna mkatoliki mwenye uwezo kufukuza hata mchawi au pepo, na majority wanategemea waganga, wachawi na washirikika na bado wanaomba kwa maria wao, ninyi wenyewe mashahidi, mnajijua hamna Mungu moyoni, hamjawahi kumwona wala kuhisi, mnamsikia tu. wala Roho wake Mtakatifu hamjawahi kujaa, kanisa la kwanza matendo ya mitume walijaa Roho Mtakatifu na waliweka mikono juu ya watu waliookoka wakajawa na Roho Mtakatifu. ninyi sio tu kwamba mmeukataa wokovu, bali mmemkataa Roho Mtakatifu ambaye Yesu alisema bila huyo hatuwezi kufanya lolote, mnaamua muongozwe kwa mapokeo yaliyokufa na yasiyookoa. Mungu awasaidie.
Unalazimisha ku u-define ukatoliki kwa kutumia ulokole. Hau-ujui undani wa ukatoliki.

Pia sio kazi yetu sisi wakatoliki kukufundusha kitu ambacho hauko tayari kukipokea; ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
 
Hakuna hilo andiko si useme ukweli tu mnafata mapokeo ya WANADAMU,

Kuna Aya Huwa mnaitumia ya ufunuo 12:1

Ukweli haihusihani kabisa , fundisho la maria kupalizwa ni fundisho la kipagani na limepokelewa na kanisa katoliki juzi juzi tu hapa ,muwe mnasoma historia

Mnamo tarehe 1 Novemba 1950, Papa Pius XII alitangaza rasmi mafundisho ya kupalizwa kwa Mariamu kuwa fundisho rasmi la imani (dogma) kwa tamko la Munificentissimus Deus. Alisema:
Sanaaaa..... Inakuhusu nini...... Wewe si una Imani yako Baki nayo ikuponye ...waache wakatoliki na Imani Yao wapotee shida yako nini.... Au unataka Mudi akubusu kama alivyombusu swahaba wake.
 
Sanaaaa..... Inakuhusu nini...... Wewe si una Imani yako Baki nayo ikuponye ...waache wakatoliki na Imani Yao wapotee shida yako nini.... Au unataka Mudi akubusu kama alivyombusu swahaba wake.
Kaka tunajuzana na biblia imeruhusu mijadala ,by the way mm ni mkristo sio muislamu

Ukatoliki ndio ulianzisha uislmau
 
Unalazimisha ku u-define ukatoliki kwa kutumia ulokole. Hau-ujui undani wa ukatoliki.

Pia sio kazi yetu sisi wakatoliki kukufundusha kitu ambacho hauko tayari kukipokea; ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Kama umeona huyo hafundishiki, tufundishe sisi mkuu; achana naye.
 
Back
Top Bottom