Wakazi wa Madale wapatwa na taharuki baada ya kuvamiwa na Nyati wa Porini

Chui nae alionekana salasala.
Hawamjui Mbogo , Jf imeboa aisee kila kitu siasa
 
Nyati naona wanarudi makazi yao ya zamani miaka ya nyuma madale kulikua na nyati na yupo Mzee mmoja aliwafuga hapo karibu na dawasco boko hata wanyama wakali pia inasemekana madale walikuepo sidhani kama wataishia kuja hawa ng'ombe mwitu tuu...
 

Hivi madale hakuna wale wamasai wenye sime kiunoni?
 
Kumuua yule nyati kumeniuma sana.....ni jike......automatically alipotea kutoka kwenye kundi.....alikuwa bado binti......
Kwa nini wasimswage akarudi porini.....?.....
Angekuwa wale mabazazi wanaofukuzwa kundini sawa......huyo alichanganyikiwa.......ki ukweli kaniuma.....
 
Unaijua madale?.
Kuna pori kubwa tu
Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 

Walifikiria ni TL kaja kivingine lakini safari hii wakasema hatufanyi makosa bali nikumpelekea kichwani tu
 
Sasa na wewe nyati mmoja anakufanya uwafokee watu.?.
Kuna nyati zaidi ya milioni hapa Tanzania acha watu wale
Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Hili doa la uchaguzi kabisa. Mnyama pori anauawa kikatili si angepiga hata mguu kama mbinu ziliisha.
Tena jike ambaye angezaa nyati kadhaa.
Maliasili na wizara ashughulike na mpiga risasi
 
wewe mtaalam wa mtandaoni, nyati katinga kwenye makazi ya watu na ameshasababisha hasara na madhara kadhaa kwa mifugo, askari wa wanayamapori wana kambi gani dsm hapa!!!! si wanaishi porini kwenye wanyama huko??

igetokea ameua mtu, ungekuwa wakwanza kuuliza polisi wanaowahi mikutano ya tundu lissu walikuwa wapi mpaka anaua watu!!!!
 
Nyati utamkamata vipi?

Unavyodhani polisi wana risasi za usingizi?
 
Nilivyoona tu kuna Mnyama Pori kaonekana nikajua ufumbuzi pekee walionao Watu wetu ni kumuua.

Hivi hawa Maofisa wa Wanyama Pori huwa hawana kabisa mafunzo ya kukamata Wanyama walioingia kwenye makazi ya Watu?. yaani kuua iwe ni hatua ya mwisho?.
Umeambiwa maofisa wa wanyama pori au anti robbery ndio waliofanya hivyo

Soma habari kwa umakini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…