Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

"Jasho jingi wakati wa mazoezi, damu kidogo wakati wa vita"

Kuna dharura zisizoweza kusubiria uanze mchakato wa kutafuta passport.

Ukiwa nayo tayari tayari, inakurahisishia na kukuepusha na usumbufu.

Fikiria, kwa mfano, mtu anaishi Bukoba, na "Jioni" akapata taarifa kuwa "kesho" atahitajika Kampala, unafikiri ataweza kufanikisha hiyo safari? Kama hana passport, siyo rahisi.
Kwa nchi za jirani, unaweza kupata karatasi kutoka kwa serikali yako ya mtaa inayokuruhusu kusafiri, ila mkuu duniani kote mambo sio rahisi Kama unavyotaka wewe, unataka urahisi kwa upande wako bila kujali ugumu wanaopata upande wa pili/serikali.
 
Kuna mawili, ama "hadhi" yako ilikubeba, au kuna namna ulifanya tofauti na wengine. Uhamiaji hawataiprocess passport usipojibu hicho kipengele cha DHUMUNI LA SAFARI.

Mwaka 2013 niliichukua form Dar Es Salaam, lakini niliishia kwenda kuitunza ndani.

Nilikwama mambo mawili: BARUA YA MWALIKO YA KUTOKA NILIKOTAKA KWENDA pamoja na TIKETI YA NDEGE. Lakini mimi sikuwa nimepanga kusafiri kwa wakati huo, bali niliihitaji kwa ajili ya siku za mbeleni.

Mwanzoni mwa mwaka 2017, rafiki yangu aliyekuwa akifanya kazi nje, alinipa taarifa ya kuwepo kwa nafasi ya kazi huko alikokuwa, ambayo ilihitaji kujazwa haraka sana.

Hakuna lililowezekana. Sikuwa na passport.
Hukuwa na nia tu ya hiyo kazi, kama una Nia na lako jambo ni lazima utalifanikisha, Yani Barua tu ya mualiko ndio inakutisha hivyo, hiyo ni kitu ya kujiandikia wewe mwenyewe kama hujui nenda hata Stationary baada ya hapo tafuta copy yeyote ya passport ya mtu then unaambatanisha na hiyo Barua ya mualiko (ambayo umejiandikia mwenyewe) ambapo ukifika immigration unawapanga kwamba Barua imetoka kwa huyo mwenyeji wako wa mchongo, watakuhoji maswali kadhaa ambayo yanajibika baada ya hapo unasubiria passport yako

Dunia ya sasa sio lazima unyooshe kila kitu, sasa kama kwenye Passport unambwela mbwela hivi, ukitaka ku apply Visa ya Marekani au UK itakuaje? Maana huko ndio kuna vigingi sio mchezo, lakini still watu wana cheat na Visa wanaipata
 
Yaani basi tu alimradi ajione mnyonge na kujidharau.🤣
Kusema ukweli kamwe, hakumfanyi mtu mwenye ufahamu wenye afya ajione mnyonge. Watu wanavyopiga kelele humu kwa sababu ya urasimu uliopo UHAMIAJI, si kwa ajili ya manufaa yao binafsi, la hasha. Wanaongea kwa niaba ya wengi "wanaoumizwa" na huo mfumo lakini hawawezi kusema na wala hawajui pa kusemea.

Kulipigia kelele jambo lenye maslahi kwa wengi kamwe siyo kujiona mnyonge wala kujidharua, bali ni ishara ya mtu aliyejikubali na anayetanguliza mbele maslahi ya wengi.
 
Kusema ukweli kamwe, hakumfanyi mtu mwenye ufahamu wenye afya ajione mnyonge. Watu wanavyopiga kelele humu kwa sababu ya urasimu uliopo UHAMIAJI, si kwa ajili ya manufaa yao binafsi, la hasha. Wanaongea kwa niaba ya wengi "wanaoumizwa" na huo mfumo lakini hawawezi kusema na wala hawajui pa kusemea.

Kulipigia kelele jambo lenye maslahi kwa wengi kamwe siyo kujiona mnyonge wala kujidharua, bali ni ishara ya mtu aliyejikubali na anayetanguliza mbele maslahi ya wengi.
Mkuu, unaposema ni jambo la wengi, unamaanisha wengi kiasi gani?. Mkuu mambo duniani hayapo hivyo, Japan, Canada na Germany hivi Sasa wanahitaji idadi kubwa ya watu kwenda kufanya kazi katika nchi zao kutokana na upungufu wa vijana, pamoja na tatizo kubwa walilonalo, lakini kupata viza za nchi zao ni nguma Sana, kwanini wasifungue mipaka Kila mtu anayependa aende kufanya kazi?
 
Mkuu, hivi utajiri unapatikana kwa kusafiri "aimlessly?". Sera ya nchi yetu ni kutoa passport kwa mtu mwenye sababu za msingi za kutaka kusafiri, ukiwa na sababu za kusafiri ndio unapewa passport.

Mkuu jaribu kufika CapeTown pale "Freedom square" uone jinsi watanzania wanavyoidhalilisha Tanzania, hutaki hata ujulikane Kama wewe ni mtanzania ukifika pale, wale jamaa wengi hawana passport, au walizipata kwa njia haramu.
Kiongozi, kwa mtu mwenye akili zake timamu, hawezi tu kunyanyuka na kupanda usafiri bila lengo, lazima awe na sababu inayomfanya aamue kuingia gharama husika ili afike anakotaka. Kutimiza lengo lake ndiyo muhimu, hata kama hilo lengo halina manufaa kwa wengine. Cha msingi tu, isiwe kinyume cha Sheria.

Sijajua kwa habari ya Watanzania waliopo FREEDOM SQUARE, CAPE TOWN. Bado sijafanikiwa kutia mguu S. A.

Lakini pengine walienda huko kwa kupitia mlango wa nyuma kwa sababu ya kutokuwa na passport. Urasimu wa passport ukipunguzwa, watu wa aina hiyo wataisha au kupungua. Kwa nini mtu asafiri kiwizi wizi kama anaweza kusafiri kihalali?

Na ikitokea mtu amesafiri bila passport, hata kujiamini kwake kunapungua. Atakuwa akiishi kama muhalifu. Kwa hiyo hata akipata tatizo ambalo angeweza kusaidiwa, labda na Serikali, hataweza kujitokeza. Ataanzaje kwenda kutoa taarifa wakati anajua yeye ni mualifu?
 
Kwa mtu binafsi ni ID ila kwa serikali Kuna mambo mengi sana, Kumbuka raia akiwa nje ya nchi serikali inapoteza udhibiti juu yake lakini bado serikali Ina wajibu wa kumlinda Kama ilivyotokea Sudan.

Sudan kulikua na raia wa USA zaidi ya 13,000, pamoja na nguvu za kiuchumi za USA lakini hadi Leo haijaweza kuwasaidia wote, bado wanapambana kuwaondoa.

Raia anapokua nje ya nchi anakua anawakilisha nchi yake, angalia nchi ya Nigeria ilivyoharibu mahusiano yake ya kidiplomasia na nchi zingine duniani kwasababu tu ya tabia ya raia toka Nigeria wanavyojihusisha na vitendo haramu, nchi nyingi hivi Sasa hazitoi visa kwa raia toka Nigeria.
Developed nations wao wanafanya aje?
Tunajifunza from the top level.
 
Kwa nchi za jirani, unaweza kupata karatasi kutoka kwa serikali yako ya mtaa inayokuruhusu kusafiri, ila mkuu duniani kote mambo sio rahisi Kama unavyotaka wewe, unataka urahisi kwa upande wako bila kujali ugumu wanaopata upande wa pili/serikali.
Kiongozi, unaposema "unaweza kupata karatasi kutoka kwa Serikali yako ya mtaa...", unamaanisha nini hasa? Karatasi ya kuvukia mpaka wa nchi au ya kwenda kuombea kibali cha safari UHAMIAJI? Naomba upambanue ulichomaanisha hasa.
 
Kwa Tanzania, sharti uwe na safari ndiyo utapewa pasi ya kusafiria(passport).

Utaratibu ukoje Kenya?
Kenya unachohitaji ukiomba passport ni kitambulisho cha NIDA na cheti chako cha kuzaliwa

Na vitambulisho vya NIDA vya mzazi mmojawapo
 
Kiongozi, kwa mtu mwenye akili zake timamu, hawezi tu kunyanyuka na kupanda usafiri bila lengo, lazima awe na sababu inayomfanya aamue kuingia gharama husika ili afike anakotaka. Kutimiza lengo lake ndiyo muhimu, hata kama hilo lengo halina manufaa kwa wengine. Cha msingi tu, isiwe kinyume cha Sheria.

Sijajua kwa habari ya Watanzania waliopo FREEDOM SQUARE, CAPE TOWN. Bado sijafanikiwa kutia mguu S. A.

Lakini pengine walienda huko kwa kupitia mlango wa nyuma kwa sababu ya kutokuwa na passport. Urasimu wa passport ukipunguzwa, watu wa aina hiyo wataisha au kupungua. Kwa nini mtu asafiri kiwizi wizi kama anaweza kusafiri kihalali?

Na ikitokea mtu amesafiri bila passport, hata kujiamini kwake kunapungua. Atakuwa akiishi kama muhalifu. Kwa hiyo hata akipata tatizo ambalo angeweza kusaidiwa, labda na Serikali, hataweza kujitokeza. Ataanzaje kwenda kutoa taarifa wakati anajua yeye ni mualifu?
Mkuu, unajua wazi kwamba Africa nzina vijana hawana kazi, wengi wanajaribu kukimbia nchi zao vyovyote vile Ili kujaribu maisha nchi za nje, nadhani unajua kuhusu idadi kubwa ya watu wanakufa wakijaribu kuvuka kupitia nchi za Kaskazini me Afrika kuingia Ulaya. Hawa ni raia ambao hawana sababu zinazokubalika ki nchi na kidunia, hivyo wanavunja Sheria za nchi, japo wao wenyewe kwao wanaona ni sababu za msingi.

Nchi haiwezi kubariki raia wake wawe ni tatizo kwa nchi zingine, lazima idhibiti raia wake kwenda katika nchi zingine bila sababu inayokubalika. Pale Cape Town ukifika, watanzania, wamalawi na nchi zingine, ndio wapiga debe, wezi, wavuta bangi na waporaji ombaomba na homeless, ni kero Sana.

Kwahiyo, huyo mtu mwenye akili timamu, hawezi kushindwa kuishawishi uhamiaji sababu za yeye kuhitaji passport, ndio sababu watanzania wengi wenye akili wanapata passpot na wanasafiri kwa wingi Sana.
 
Nlipataga yangu kwa mbinde maana nlifoji hadi admission latter ya chuo cha Stanford University nikawaambia "ili nikubaliwe lazima nijaze PASSPORT NUMBER"
😂😂😂😂😂 ndio nikapata back in 2010
 
Mkuu, hivi utajiri unapatikana kwa kusafiri "aimlessly?". Sera ya nchi yetu ni kutoa passport kwa mtu mwenye sababu za msingi za kutaka kusafiri, ukiwa na sababu za kusafiri ndio unapewa passport.

Mkuu jaribu kufika CapeTown pale "Freedom square" uone jinsi watanzania wanavyoidhalilisha Tanzania, hutaki hata ujulikane Kama wewe ni mtanzania ukifika pale, wale jamaa wengi hawana passport, au walizipata kwa njia haramu.
KWa hivyo ukiwepo tu nchini ndiyo unakuwa na uhakika wa maisha?
 
Kiongozi, unaposema "unaweza kupata karatasi kutoka kwa Serikali yako ya mtaa...", unamaanisha nini hasa? Karatasi ya kuvukia mpaka wa nchi au ya kwenda kuombea kibali cha safari UHAMIAJI? Naomba upambanue ulichomaanisha hasa.
Kwamfano unataka kwenda Kenya, au Uganda na umepata dharura ya siku 3, nenda katika ofisi yako ya kata, peleka picha Moja, watakuandikia barua na kubandika picha yako, watapiga mhuri, hiyo inatosha. Mbona kina mama wengi wenye kufanya biashara za mipakani hawana passport wanatumia hizo barua, wanaita vibali vya muda.
 
Kuna mawili, ama "hadhi" yako ilikubeba, au kuna namna ulifanya tofauti na wengine. Uhamiaji hawataiprocess passport usipojibu hicho kipengele cha DHUMUNI LA SAFARI.

Mwaka 2013 niliichukua form Dar Es Salaam, lakini niliishia kwenda kuitunza ndani.

Nilikwama mambo mawili: BARUA YA MWALIKO YA KUTOKA NILIKOTAKA KWENDA pamoja na TIKETI YA NDEGE. Lakini mimi sikuwa nimepanga kusafiri kwa wakati huo, bali niliihitaji kwa ajili ya siku za mbeleni.

Mwanzoni mwa mwaka 2017, rafiki yangu aliyekuwa akifanya kazi nje, alinipa taarifa ya kuwepo kwa nafasi ya kazi huko alikokuwa, ambayo ilihitaji kujazwa haraka sana.

Hakuna lililowezekana. Sikuwa na passport.
Uhamiaji hata uwaambie hawasikii wameziba masikio.wanasubiri kila kitu Raisi aingilie kati

Basi sababu wao wenyewe uhamiaji hizi kelele humu hawataki kusikia tuombe kila aliye karibu na Raisi Samia amwambie aingilie kati kwenye hili

Na afumue idara ya uhamiaji walioko.sasa sababu kazi ya Afisa wa serikali sio.kufanya maishs ya nwananchi kuwa magumu ni.kumrahisishia

Passport ni eneo mojawapo ambalo ni Kero kwa wananchi linalofanya maisha ya watanzania kuwa magumu bila sababu

Raisi Samia ingilia kati toa maelekezo waondoe hicho kigezo chao cha dhumuni la safari na sijui barua za mwaliko

Fursa huwa haitoi mwaliko unaifuata hukohuko nje ya nchi

Kwa mfumo wa sijui barua za mwaliko maana yake ni kuwa watanzania hawaruhusiwi tu kuinuka na kwenda nje ya nchi kutafuta fursa
 
Kwamfano unataka kwenda Kenya, au Uganda na umepata dharura ya siku 3, nenda katika ofisi yako ya kata, peleka picha Moja, watakuandikia barua na kubandika picha yako, watapiga mhuri, hiyo inatosha. Mbona kina mama wengi wenye kufanya biashara za mipakani hawana passport wanatumia hizo barua, wanaita vibali vya muda.
Joto la jiwe, nimekusoma mkuu. Unachokizungumzia hapo ni kile wanachokiita UJIRANI MWEMA. Kwa wakazi wanaoishi mipakani, ruksa kwenda kupata huduma upande wa pili wa nchi jirani, lakini ni kwa maeneo ya mipakani tu. Hawaruhusiwi kwenda ndani sana. Hilo linafahamika. Japo sipo jirani na Uganda, lakini mwaka huu nilipoenda Bukoba, nilienda hadi Mutukula Uganda, lakini sikwenda ndani sana. Nilitaka niende hadi Kampala lakini ilishindikana, na hata nilipoenda idara ya UHAMIAJI upande wa Tanzania kuomba usaidizi, nilitakiwa niwe na BIRTH CERTIFICATE yangu na ya mzazi wangu, barua ya AFISA MTENDAJI WA KATA(siyo ya MWENYEKITI WA KIJIJI WALA KITONGOJI AU MTAA, HIZO HAZITAMBULIKI UHAMIAJI), NA SH 20,000. Kama ningewapa hizo nyaraka, ndiyo wangeniandalia TRAVEL DOCUMENT, ambayo ni one way traffic. Ikishatumika mara moja, MATUMIZI yake yanakuwa yameisha.

Hata Burundi nilishaingia Lakini nililazimika kuishia pembezoni.

Lakini nilipotaka kwenda Nairobi, ilibidi nikae TRAVEL DOCUMENT. Huwezi kwenda Nairobi na barua ya MWENYEKITI, kama tu UHAMIAJI wenyewe hawaipokei....
 
Mbona hasira Sana?, wewe Kama unasafari nje ya nchi kwa lengo jema na la msingi, nenda uhamiaji ujieleze utapewa, au unataka Kila mtu apewe passport Ili waende wakajiunge na vikundi vya ugaidi huko Somalia, Nigeria, Msumbiji na Afghanistan?
Kuwa na passport hakuwezi kumfanya mtu mwema kuwa mwovu, na kutokuwa na passport hakuwezi kumzuia mwovu kufanya uhalifu.

Na kama mtu anataka passport kwa Nia ovu, kwa jinsi mfumo unavyohamasisha rushwa, ataipata tu, tena bila taabu. Wewe unafikiri urasimu uliopo ni kwa manufaa ya Serikali? Nooo! Ni mradi wa watumishi wasio waaminifu. Urasimu unahamasisha rushwa.

Ndiyo sababu wenye maamuzi hawataki kurekebisha alau ufananie na za nchi zingine "zinazojielewa"
 
Kwa mtu binafsi ni ID ila kwa serikali Kuna mambo mengi sana, Kumbuka raia akiwa nje ya nchi serikali inapoteza udhibiti juu yake lakini bado serikali Ina wajibu wa kumlinda Kama ilivyotokea Sudan.

Sudan kulikua na raia wa USA zaidi ya 13,000, pamoja na nguvu za kiuchumi za USA lakini hadi Leo haijaweza kuwasaidia wote, bado wanapambana kuwaondoa.

Raia anapokua nje ya nchi anakua anawakilisha nchi yake, angalia nchi ya Nigeria ilivyoharibu mahusiano yake ya kidiplomasia na nchi zingine duniani kwasababu tu ya tabia ya raia toka Nigeria wanavyojihusisha na vitendo haramu, nchi nyingi hivi Sasa hazitoi visa kwa raia toka Nigeria.
Siyo jukumu la Serikali kudhibiti raia wake aliye nchi nyingine. Huyo mtu akiwa na shida, yeye ndiye anayepaswa kuripoti ubalozini, siyo Serikali yake.

Serikali yake haina mamlaka juu ya mtu wake aliye kwenye nchi nyingine. Lakini pia ni vyema ifahamike kuwa mafanikio yanaambatana na ujasiri wa kutake risk. Mwoga wa kutake risk siyo rahisi apate mafanikio makubwa. Kama mtu yupo tayari kutake risk, Serikali isimwekee kikwazo. Mbona Huwa haiwazuii wanajeshi kwenda penye vita kunapotokea na uhitaji? Si unafahamu mtu anayeenda vitani Kuna mambo matatu hivi yatakayokuwa yakimkabili? Ama arudi salama, au ajeruhiwe au hata kupoteza maisha. Lakini bado kukitokea uhitaji, Jeshi likiagizwa liende vitanie, litatii. Sasa kwa nini sera za Serikali iwe kikwazo kwa "wapambanaji" wanaotaka kwenda kujaribu maisha sehemu zingine?

Kwamba Wanaigeria wamefanya uhalifu uliopelekea baadhi ya nchi kukataa kuwapa viza si hoja. Mbona Kenya, pamoja na kuwa ndiyo nchi inayoongoza Afrika Mashariki kwa raia wake wengi kuwa nchi za nje, bado passport yao ina nguvu kuizidi ya Tanzania? Hata katika katazo lililotolewa na Dubai mwaka huu, la kukataa kupokea raia wa baadhi ya mataifa, Kenya si miongoni mwao. Dubai kuna raia wengi wa Kenya kuxidi raia kutoka nchi nyingine yo yote ya Afrika Mashariki.

Labda nikutajie na hizo nchi, hasa za Afrika, ambazo raia wa hizo nchi hawatakiwi Dubai kwa sasa(labda kama wameshabadilisha):

Kuna Nigeria, Ghana, Uganda, Sierra Leone, Sudan, Cameroon, Liberia, Burundi, Republic of Guinea, Gambia, Togo, Congo D. R. C., Rwanda, Burkina Faso, Guinea Bissau, Comoros, and the Dominican Republic.

Umeona? Pamoja na Wakenya wengi kuwepo Dubai, hawajahusishwa na zuio la kuingia Dubai.

Kama Wakenya wameweza, hata Watanzania wataweza.
 
Ndio sababu Kenya is ranked poorly on security, Globally Tanzania is ranked position 54, while Kenya 125.
Una uhakika, nenda keny mtz kama utaishi bila kukamatwa, ila tz tunaishi na hadi wachina wana tanzania citize ship
 
Mkuu, unaposema ni jambo la wengi, unamaanisha wengi kiasi gani?. Mkuu mambo duniani hayapo hivyo, Japan, Canada na Germany hivi Sasa wanahitaji idadi kubwa ya watu kwenda kufanya kazi katika nchi zao kutokana na upungufu wa vijana, pamoja na tatizo kubwa walilonalo, lakini kupata viza za nchi zao ni nguma Sana, kwanini wasifungue mipaka Kila mtu anayependa aende kufanya kazi?
Kama unataka kufahamu kuwa ni wengi, ingia Jamii Forum utafute mada zinazohusiana na PASSPORT uone malalamiko yalivyo mengi.

Halafu, si kila anayetaka passport ni kwa sababu anataka kwenda Ulaya. Inawezekana mwingine anataka kwenda Sudan mara tu utulivu utakaporejea.
Na hata kama ataichukua lakini asisafiri, bado hakutakuwepo na hasara kwake au kwa Serikali.

Kule tu kuwa nayo ni faida tosha. Huboresha afya yake ya Kisaikolojia.
 
Una uhakika, nenda keny mtz kama utaishi bila kukamatwa, ila tz tunaishi na hadi wachina wana tanzania citize ship
Kwani mchina kuwa raia wa Tanzania kwa kuukana uchina wake haiwezekani? Haya wahindi ambao hadi leo wengine washawahi kuwa wabunge, sijui madiwani etc ilikuwaje wakawa raia wa Tanzania na wakati haikuwa hivyo hapo mwanzo?
 
Back
Top Bottom