Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

Ndio sababu Kenya is ranked poorly on security, Globally Tanzania is ranked position 54, while Kenya 125.
Sidhani kama kuna uhusiano wo wote kati ya hali ya usalama wa Kenya na uhuru wa raia wake kwenda ng'ambo.

Tishio la kiusalama linaweza likachangiwa na kupakana na nchi zenye vita kama Sudan na Somalia. Passport hazihusiki kabisa.

Nionavyo mimi, kwa kuwarahisishia raia wake mchakato wa passport, siyo kwamba kumeisaidia tu kiuchumi, bali pia kiusalama.

Unajua maamuzi ya mtu mwenye njaa yalivyo? Kama ajira za ndani hazitoshelezi, na hujawatengenezea watu wako mazingira ya kwenda kutafuta kwingineko, itakuwa unajitengenezea bomu litakalokuja kukulipukia.

Kwa kuwatengenezea watu wake mazingira ya kuweza kwenda nchi zingine kirahisi, Kenya wameua ndege wawili kwa jiwe:

1. Inanufaika kiuchumi
2. Imedumisha usalama wa ndani
 
Kuwa na passport hakuwezi kumfanya mtu mwema kuwa mwovu, na kutokuwa na passport hakuwezi kumzuia mwovu kufanya uhalifu.

Na kama mtu anataka passport kwa Nia ovu, kwa jinsi mfumo unavyohamasisha rushwa, ataipata tu, tena bila taabu. Wewe unafikiri urasimu uliopo ni kwa manufaa ya Serikali? Nooo! Ni mradi wa watumishi wasio waaminifu. Urasimu unahamasisha rushwa.

Ndiyo sababu wenye maamuzi hawataki kurekebisha alau ufananie na za nchi zingine "zinazojielewa"
Mkuu, serikali lazima iwe na uwezo wa kudhibiti watu wake kutoka nje ya nchi, Kama ambavyo ni lazima kudhibiti raia wa nchi nyingine kuingia nchini kwake, hakuna serikali yoyote yenye kuacha watu wake hasa kwa hizi nchi changa ambazo watu wake wengi hawana ajira, ni rahisi Sana hawa vijana kwenda na kufanya uhalifu katika nchi za watu, sio sifa kwa nchi kuonekana raia wake ndio wanafanya uhalifu kwa wingi katika nchi za watu wengine.

Nitakubaliana na wewe Kama utailaumu serikali kwa kushindwa kuwasaidia vijana wake kuweza kujiajiri lakini sio kufikiria kuwapa passport kirahisi Ili wakajazane South Afrika kuuza madawa na kuvunja Nyumba za watu.

Mkuu, hao wanaohitaji na kukosa passport hawazidi laki 5, ni chini ya 0.5% ya watanzania wote. Hapa JF sidhani Kama tunazidi watu laki Moja, na wanaolalamika kuhusu passport hawazidi hata elfu 1.

Mkuu, nchi lazima ifanye kazi kwa kutumia taarifa zilizofanyiwa kazi. Bei ya Passport Moja ni zaidi ya Tsh 50,000 ni "source nzuri sana ya kupata pesa kwa uhamiaji, hawana sababu yoyote ya kuzikataa pesa nyingi kiasi hicho, wangekuwa wabinafsi wangeamua kuzitoa hovyo passport Ili wakusanye mapato, lakini ni hatari Sana kwa usalama na heshima ya nchi, zingeangukia mikononi mwa raia wa nchi nyingi na mwisho passport yetu ingepoteza thamani.

Mkuu, Passport ya Tanzania enzi za Nyerere ilikua na nguvu sana, lakini kadri miaka inavyozidi kwenda inapoteza nguvu kutokana na vitendo vyetu vya kujihusisha na hasa madawa ya kulevya na vijana wetu kushiriki ktk mambo maovu ukiwemo ugaidi, lazima passport idhibitiwe kwa nguvu zote
 
Mkuu, unajua wazi kwamba Africa nzina vijana hawana kazi, wengi wanajaribu kukimbia nchi zao vyovyote vile Ili kujaribu maisha nchi za nje, nadhani unajua kuhusu idadi kubwa ya watu wanakufa wakijaribu kuvuka kupitia nchi za Kaskazini me Afrika kuingia Ulaya. Hawa ni raia ambao hawana sababu zinazokubalika ki nchi na kidunia, hivyo wanavunja Sheria za nchi, japo wao wenyewe kwao wanaona ni sababu za msingi.

Nchi haiwezi kubariki raia wake wawe ni tatizo kwa nchi zingine, lazima idhibiti raia wake kwenda katika nchi zingine bila sababu inayokubalika. Pale Cape Town ukifika, watanzania, wamalawi na nchi zingine, ndio wapiga debe, wezi, wavuta bangi na waporaji ombaomba na homeless, ni kero Sana.

Kwahiyo, huyo mtu mwenye akili timamu, hawezi kushindwa kuishawishi uhamiaji sababu za yeye kuhitaji passport, ndio sababu watanzania wengi wenye akili wanapata passpot na wanasafiri kwa wingi Sana.
Kama hawana kazi, itakuwa ni hekima kuendelea kuwafungia ndani? Lengo litakuwa ni lipi, wafe njaa?

Watu wengine, tena wachache, wasifikiri wana akili kuzidi wengine wote.

Ni ukatili kuwafungia watu ndani, hiyo tabia iachiwe Serikali katili ya North Korea.

Passport ni haki ya Mtanzania. Hauhitaji kushawishi ndipo upewe. Cha msingi ni kukidhi tu vigezo, na vigezo pekee ni kuthibitishwa kuwa wewe ni Mtanzania.

Zaidi ya hapo, kitakachokuwa kikitafutwa ni wewe ukubali kutumia mbinu ya ziada, yaani, kushawishi kwa kutumia hela.

Passport ni sh 150,000/=. Lakini ukienda na sh 300,000/=, wala hutahangaika, utasaidwa na mambo mengine yatakayohitajika.

Ushawishi kama huo unafanyika sana. Ndiyo maana inasemekana kuna watu wengi wasio raia wa Tanzania wanaotumia passport ya Tanzania. Unafikiri wamepataje? Wameshawishi, si kwa maneno matupu, kwa hela.

Nafahamu sana kuwa huo ushawishi unatumika sana. Na ndiyo maana Uhamiaji wamekomaa kutokuondoa hicho kipengele. Kikiondolewa, hakutakuwepo tena na watu wa kuwashawishi. Kukiondoa hicho kipengele ni kuwakosesha "chakula" watumishi wasio waaminifu.
 
Sidhani kama kuna uhusiano wo wote kati ya hali ya usalama wa Kenya na uhuru wa raia wake kwenda ng'ambo.

Tishio la kiusalama linaweza likachangiwa na kupakana na nchi zenye vita kama Sudan na Somalia. Passport hazihusiki kabisa.

Nionavyo mimi, kwa kuwarahisishia raia wake mchakato wa passport, siyo kwamba kumeisaidia tu kiuchumi, bali pia kiusalama.

Unajua maamuzi ya mtu mwenye njaa yalivyo? Kama ajira za ndani hazitoshelezi, na hujawatengenezea watu wako mazingira ya kwenda kutafuta kwingineko, itakuwa unajitengenezea bomu litakalokuja kukulipukia.

Kwa kuwatengenezea watu wake mazingira ya kuweza kwenda nchi zingine kirahisi, Kenya wameua ndege wawili kwa jiwe:

1. Inanufaika kiuchumi
2. Imedumisha usalama wa ndani
Kenya imeathirika pakubwa Sana kwa kuruhusu watu wake kutoka kwa wingi bila udhibiti;
1)Wasomi wengi na wataalamu wazuri wameikimbia Kenya wako nje ya nchi Yao, matokeo ni haya ya uchumi wao kuporomoka kwa Kasi kwasababu waliobaki Kenya ni wale wa daraja la chini, majumba yanaporomoka Kila siku na miradi Yao yote ipo "poorly done".

2)Wasichana wa kikenya wengi wanatumikishwa Kama watumwa, wengi wanauliwa huko Uarabuni, thamani ya raia wa Kenya huko Uarabuni ipo chini Sana.

3)Kiusalama huko ndio usiseme kabisa, wasomali wote wako na Passport ya Kenya, wakitaka kuingia na kufanya unyama ni kitu Cha kawaida Sana. Hoja ya kukosekana usalama Kenya kuhusisha na kupakana na Somalia au South Sudan, mbona Ethiopia yenye kupakana na nchi hizohizo haina tatizo la Kiusalama?, Mbona Uganda imepakana na DRC na South Sudan lakini haina hilo tatizo?
 
Nlipataga yangu kwa mbinde maana nlifoji hadi admission latter ya chuo cha Stanford University nikawaambia "ili nikubaliwe lazima nijaze PASSPORT NUMBER"
😂😂😂😂😂 ndio nikapata back in 2010
Uhamiaji inawatesa Raia wema.
 
Kenya imeathirika pakubwa Sana kwa kuruhusu watu wake kutoka kwa wingi bila udhibiti;
1)Wasomi wengi na wataalamu wazuri wameikimbia Kenya wako nje ya nchi Yao, matokeo ni haya ya uchumi wao kuporomoka kwa Kasi kwasababu waliobaki Kenya ni wale wa daraja la chini, majumba yanaporomoka Kila siku na miradi Yao yote ipo "poorly done".

2)Wasichana wa kikenya wengi wanatumikishwa Kama watumwa, wengi wanauliwa huko Uarabuni, thamani ya raia wa Kenya huko Uarabuni ipo chini Sana.

3)Kiusalama huko ndio usiseme kabisa, wasomali wote wako na Passport ya Kenya, wakitaka kuingia na kufanya unyama ni kitu Cha kawaida Sana. Hoja ya kukosekana usalama Kenya kuhusisha na kupakana na Somalia au South Sudan, mbona Ethiopia yenye kupakana na nchi hizohizo haina tatizo la Kiusalama?, Mbona Uganda imepakana na DRC na South Sudan lakini haina hilo tatizo?
Acha ujinga. Badala yake wakenya in diaspora ni wachangiaji wakubwa wa uchumi wa Kenya. Pili inawasaidia kupunguza ukosefu wa ajira. Mind you rais juzi amesema wanaanzisha training maalumu kwa wakenya iwasaidie kwenda nadhani Japan kufanya kazi. Hivyo swala la kufanya kazi nje sio issue kwao. Nyie hapa mnashidndwa kuajiri Hata wachache waliopo.

Swala la Somalia na Kenya ni la kijiografia na sio mambo ya passport.
 
Kama hawana kazi, itakuwa ni hekima kuendelea kuwafungia ndani? Lengo litakuwa ni lipi, wafe njaa?

Watu wengine, tena wachache, wasifikiri wana akili kuzidi wengine wote.

Ni ukatili kuwafungia watu ndani, hiyo tabia iachiwe Serikali katili ya North Korea.

Passport ni haki ya Mtanzania. Hauhitaji kushawishi ndipo upewe. Cha msingi ni kukidhi tu vigezo, na vigezo pekee ni kuthibitishwa kuwa wewe ni Mtanzania.

Zaidi ya hapo, kitakachokuwa kikitafutwa ni wewe ukubali kutumia mbinu ya ziada, yaani, kushawishi kwa kutumia hela.

Passport ni sh 150,000/=. Lakini ukienda na sh 300,000/=, wala hutahangaika, utasaidwa na mambo mengine yatakayohitajika.

Ushawishi kama huo unafanyika sana. Ndiyo maana inasemekana kuna watu wengi wasio raia wa Tanzania wanaotumia passport ya Tanzania. Unafikiri wamepataje? Wameshawishi, si kwa maneno matupu, kwa hela.

Nafahamu sana kuwa huo ushawishi unatumika sana. Na ndiyo maana Uhamiaji wamekomaa kutokuondoa hicho kipengele. Kikiondolewa, hakutakuwepo tena na watu wa kuwashawishi. Kukiondoa hicho kipengele ni kuwakosesha "chakula" watumishi wasio waaminifu.
Mkuu, ni jukumu la serikali yoyote kuwapatia maisha bora watu wake, sio kuwaacha na kusababisha uhalifu kwa majirani. Baba yeyote mwenye hekima hawezi kushindwa na watoto wake na akawaruhusu kwenda kuiba na kufanya fujo kwa Nyumba ya jirani.

Nchi yenye kujielewa, kamwe haiwezi kuwasaidia raia wake kwenda kuishi katika nchi za watu bila shughuli maalumu, huko ni kupeleka uhalifu kwa majirani zako.

Mkuu, nchi hii Kuna watu wengi wazuri wenye hekima, elimu na busara nyingi ukiwemo wewe, lakini Kumbuka hauko peke yako, wengi wameona si busara kutoa passport bila kudhibiti, ila wapo wenye maoni Kama wewe, lakini kwa bahati mbaya wenye mawazo Kama wewe mpo wachache, au hamjashika madaraka, kwahiyo utalazimika kukubaliana na walio wengi au waliopo madarakani, ila unaruhusiwa kutoa maoni yako.
 
Acha ujinga. Badala yake wakenya in diaspora ni wachangiaji wakubwa wa uchumi wa Kenya. Pili inawasaidia kupunguza ukosefu wa ajira. Mind you rais juzi amesema wanaanzisha training maalumu kwa wakenya iwasaidie kwenda nadhani Japan kufanya kazi. Hivyo swala la kufanya kazi nje sio issue kwao. Nyie hapa mnashidndwa kuajiri Hata wachache waliopo.

Swala la Somalia na Kenya ni la kijiografia na sio mambo ya passport.
Idadi ya vyuo vikuu Japan ni zaidi ya mara 100 ya idadi ya vyuo vya Kenya, iweje Kenya iwe na Wasomi wengi wa kuwapeleka Japan?, tulitegemea iwe kinyume chake. Kenya Kuna shida, hiyo nchi viongozi wao wanafikiria kinyumenyume Sana

Kenya pamoja na kuwa na Diaspora kubwa, lakini bado hawana "Foreign currencies", uchumi wao unazidi kuzorota, unemployment ndio kubwa kuliko nchi zote na inazidi kuongezeka.

Conclusion: Jibu la matatizo ya Kenya lazima wajenge uchumi wa ndani kwa kutumia Wasomi na raia wao Ili watengeneze ajira, sio kuwapeleka nje ya nchi huku nyumbani wanabaki "less Qualified people "
 
Idadi ya vyuo vikuu Japan ni zaidi ya mara 100 ya idadi ya vyuo vya Kenya, iweje Kenya iwe na Wasomi wengi wa kuwapeleka Japan?, tulitegemea iwe kinyume chake. Kenya Kuna shida, hiyo nchi viongozi wao wanafikiria kinyumenyume Sana

Kenya pamoja na kuwa na Diaspora kubwa, lakini bado hawana "Foreign currencies", uchumi wao inazidi kuzorota, unemployment ndio kubwa kuliko nchi zote na inazidi kuongezeka.

Conclusion: Jibu la matatizo ya Kenya lazima wajenge uchumi wa ndani kwa kutumia Wasomi na raia wao Ili watengeneze ajira, sio kuwapeleka nji ya nchi huku nyumbani wanabaki "less Qualified people "
Sijasema kupeleka wasomi. Nimesema nafasi za ajira in general. Leo kuna mtz rafiki yangu kapata kazi ya ass lecturer US penye wasomi wote.
Ninyi kama mnalimiti wasomi mmedhibiti brain drain why bado Kenya inawazidi uchumi pamoja na numerical na resource advantage?
 
Ila hii nchi ina watu wajinga na wadhaifu kuliko watu wote chini ya Jua na nchi mbalimbali.
Watu wanaburutwa na mifumuko ya bei, ufisadi, hali duni, elimu mbovu, hakuna ajira, on top of that mambo ya passport tena?
watu wapo tu yani wapo tu

Nakuhakikishia kuwa Danganyika inaongoza kuwa na watu wajinga wengi


kama unabisha ntajie nchi 1 yenye ujinga kuzid Bongo
Lipa bill zako,kula Bata na Bia laini,fanya road trip,vuta denu mkali,kuwa na mchepuko mkali,safari kidogo ulaya,punguza kelele,fanya yako
 
Sijasema kupeleka wasomi. Nimesema nafasi za ajira in general. Leo kuna mtz rafiki yangu kapata kazi ya ass lecturer US penye wasomi wote.
Ninyi kama mnalimiti wasomi mmedhibiti brain drain why bado Kenya inawazidi uchumi pamoja na numerical na resource advantage?
Mkuu, ni mtu mjinga pekee atakayewekeza pesa nyingi katika elimu nchini kwake, Kisha akasherehekea Wasomi wake kwenda kufanya kazi nchi zingine.
 
Uhamiaji hata uwaambie hawasikii wameziba masikio.wanasubiri kila kitu Raisi aingilie kati

Basi sababu wao wenyewe uhamiaji hizi kelele humu hawataki kusikia tuombe kila aliye karibu na Raisi Samia amwambie aingilie kati kwenye hili

Na afumue idara ya uhamiaji walioko.sasa sababu kazi ya Afisa wa serikali sio.kufanya maishs ya nwananchi kuwa magumu ni.kumrahisishia

Passport ni eneo mojawapo ambalo ni Kero kwa wananchi linalofanya maisha ya watanzania kuwa magumu bila sababu

Raisi Samia ingilia kati toa maelekezo waondoe hicho kigezo chao cha dhumuni la safari na sijui barua za mwaliko

Fursa huwa haitoi mwaliko unaifuata hukohuko nje ya nchi

Kwa mfumo wa sijui barua za mwaliko maana yake ni kuwa watanzania hawaruhusiwi tu kuinuka na kwenda nje ya nchi kutafuta fursa
Hivi C.A.G. mstaafu, Prof. Assad alisemaje? Asilimia 60 ya watumishi wa Serikali uwezo wao ni duni?

Kwa yanayofanywa na UHAMIAJI, nani atambishia Prof. Assad?
 
Mkuu, ni mtu mjinga pekee atakayewekeza pesa nyingi katika elimu nchini kwake, Kisha akasherehekea Wasomi wake kwenda kufanya kazi nchi zingine.
Emu elezea hizo kazi unatoa hutoi km hutoi so Bora ugawe passport bure km ulivyogawa vitambulisho vya taifa kisha watu wakatafute kazi kwengine uko Duniani, kuliko kurundikana sehemu moja majobless kibao
 
Una uhakika, nenda keny mtz kama utaishi bila kukamatwa, ila tz tunaishi na hadi wachina wana tanzania citize ship
Joto la jiwe anaamini ukiwa na kikaratasi kilichogongwa muhuri wa Mwenyekitie wa kijiji utakuwa salama. Hajui kuwa Kenya si pa mchezo mchezo!
 
Back
Top Bottom