Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

Wakenya Tupeni Uzoefu Wenu Kuhusu Passport

90% ya Wasomi Afrika husomeshwa kwa pesa ya serikali au hutumia miundombinu ya serikali. Lengo la kuwasomesha watu sio kwa ajili ya kuajiriwa tu, ni kutengeneza watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ubora na ufanisi popote pale, hasa katika private sector.
Uongo sasa hivi watu wanajisomesha wenyewe hawasomeshwi na serikali

Wanakopa mikopo bodi ya mikopo,kwenye mabenki nk kujisomesha vyuoni ambayo watailipa wenyewe sio kuwa watalipiwa na serikali

Hiyo 90.% yako uongo mkubwa
Mfano mzuri ni Tanzania hakuna hiyo kitu ya uongo.wako watu wanajisomesha
 
So wasomi wote wameajiriwa hapa? Pili notion ya kwamba watu wanasomeshwa na serikali mnaioata wapi?
Serikali ya Tanzania kwa sasa haisomeshi.watu vyuoni wanajidomesha kwa mikopo ambayo watailipa

Huyo atakuwa ni wale vikongwe waliodoma enzi za Nyerere bure na ndio kikwazo kikubwa cha kuzuia watanzania kupata passport kirahisi

Wana mawazo mgando sana na wagumu kubadilika .Kola kitu ukisema utasikia kijana kaa mbali sisi tuna uzoefu toka enzi za Nyerere passport tunatoa tu mtu akiwa na safari .Untaniambia nini wewe.? Miaka yote tunafanya hivi hivi. waliosoma bure enzi Nyerere hata hawajui hata nchi tu inaendaje kuwa kwa sasa elimu vyuoni serikali haisomeshi bure tena ni wajibu wa mwanafunzi mwenyewe na mzazi au.mlezi watafute pesa za kusomea iwe kukopa au kokote
 
Mkuu, serikali lazima iwe na uwezo wa kudhibiti watu wake kutoka nje ya nchi, Kama ambavyo ni lazima kudhibiti raia wa nchi nyingine kuingia nchini kwake, hakuna serikali yoyote yenye kuacha watu wake hasa kwa hizi nchi changa ambazo watu wake wengi hawana ajira, ni rahisi Sana hawa vijana kwenda na kufanya uhalifu katika nchi za watu, sio sifa kwa nchi kuonekana raia wake ndio wanafanya uhalifu kwa wingi katika nchi za watu wengine.

Nitakubaliana na wewe Kama utailaumu serikali kwa kushindwa kuwasaidia vijana wake kuweza kujiajiri lakini sio kufikiria kuwapa passport kirahisi Ili wakajazane South Afrika kuuza madawa na kuvunja Nyumba za watu.

Mkuu, hao wanaohitaji na kukosa passport hawazidi laki 5, ni chini ya 0.5% ya watanzania wote. Hapa JF sidhani Kama tunazidi watu laki Moja, na wanaolalamika kuhusu passport hawazidi hata elfu 1.

Mkuu, nchi lazima ifanye kazi kwa kutumia taarifa zilizofanyiwa kazi. Bei ya Passport Moja ni zaidi ya Tsh 50,000 ni "source nzuri sana ya kupata pesa kwa uhamiaji, hawana sababu yoyote ya kuzikataa pesa nyingi kiasi hicho, wangekuwa wabinafsi wangeamua kuzitoa hovyo passport Ili wakusanye mapato, lakini ni hatari Sana kwa usalama na heshima ya nchi, zingeangukia mikononi mwa raia wa nchi nyingi na mwisho passport yetu ingepoteza thamani.

Mkuu, Passport ya Tanzania enzi za Nyerere ilikua na nguvu sana, lakini kadri miaka inavyozidi kwenda inapoteza nguvu kutokana na vitendo vyetu vya kujihusisha na hasa madawa ya kulevya na vijana wetu kushiriki ktk mambo maovu ukiwemo ugaidi, lazima passport idhibitiwe kwa nguvu zote
Nchi changa ni ipi? Labda South Sudan. Lakini zingine kama Tanzania, haziwezi kuwa changa. Nchi yenye umri wa miaka 62 haiwezi kuwa changa. Ni Rika moja na South Korea.

Vijana wataenda kufanya uhalifu nje? Kwani hizo nchi hazina vyombo vya usalama kiasi kwamba Tanzania inapaswa kuzilinda dhidi ya uhalifu? Kwa kuwa Tanzania ina vyombo makini vya dola, iwabaini wale wote wenye tabia za uhalifu ili isiwape passport. Wengine wote watakaosalia, wapewe, maadam tu wanahitaji.

Kama Serikali haikuwa makini wakati wa kutoa vitambulisho vya NIDA, basi ni rahisi hilo la raia wa nje KUPEWA passport ya Tanzania. Lakini kama zoezi lilienda vizuri, basi hilo haliwezi kutokea kwa sababu vitambulisho vya NIDA vilibainisha na uraia.

Kuhusu idadi ya wanaohitaji passport, ni kubwa sana kuliko unavyofikiri.
 
Mkuu, ni jukumu la serikali yoyote kuwapatia maisha bora watu wake, sio kuwaacha na kusababisha uhalifu kwa majirani. Baba yeyote mwenye hekima hawezi kushindwa na watoto wake na akawaruhusu kwenda kuiba na kufanya fujo kwa Nyumba ya jirani.

Nchi yenye kujielewa, kamwe haiwezi kuwasaidia raia wake kwenda kuishi katika nchi za watu bila shughuli maalumu, huko ni kupeleka uhalifu kwa majirani zako.

Mkuu, nchi hii Kuna watu wengi wazuri wenye hekima, elimu na busara nyingi ukiwemo wewe, lakini Kumbuka hauko peke yako, wengi wameona si busara kutoa passport bila kudhibiti, ila wapo wenye maoni Kama wewe, lakini kwa bahati mbaya wenye mawazo Kama wewe mpo wachache, au hamjashika madaraka, kwahiyo utalazimika kukubaliana na walio wengi au waliopo madarakani, ila unaruhusiwa kutoa maoni yako.
Mkuu, unaishangaza dunia kwa huo mtazamo. Ni North Korea pekee ndiyo inaweza ikakubaliana na mtazamo wako, kwa kuwa haipendi raia wake wajue jinsi Dunia inavyoenda. Kule watu "wanafugwa" na "kutumikishwa" kwa maslahi ya watawala.
 
Kenya imeathirika pakubwa Sana kwa kuruhusu watu wake kutoka kwa wingi bila udhibiti;
1)Wasomi wengi na wataalamu wazuri wameikimbia Kenya wako nje ya nchi Yao, matokeo ni haya ya uchumi wao kuporomoka kwa Kasi kwasababu waliobaki Kenya ni wale wa daraja la chini, majumba yanaporomoka Kila siku na miradi Yao yote ipo "poorly done".

2)Wasichana wa kikenya wengi wanatumikishwa Kama watumwa, wengi wanauliwa huko Uarabuni, thamani ya raia wa Kenya huko Uarabuni ipo chini Sana.

3)Kiusalama huko ndio usiseme kabisa, wasomali wote wako na Passport ya Kenya, wakitaka kuingia na kufanya unyama ni kitu Cha kawaida Sana. Hoja ya kukosekana usalama Kenya kuhusisha na kupakana na Somalia au South Sudan, mbona Ethiopia yenye kupakana na nchi hizohizo haina tatizo la Kiusalama?, Mbona Uganda imepakana na DRC na South Sudan lakini haina hilo tatizo?
Mkuu, inaelekea hata Kenya bado hujafika. Hakuko hivyo kama unavyofikiri. Ina wasomi wa kutosha na ziada, ndiyo maana Serikali yake inafanya jitihada kuwatafutia raia wake kazi katika mataifa mengine.
 
Idadi ya vyuo vikuu Japan ni zaidi ya mara 100 ya idadi ya vyuo vya Kenya, iweje Kenya iwe na Wasomi wengi wa kuwapeleka Japan?, tulitegemea iwe kinyume chake. Kenya Kuna shida, hiyo nchi viongozi wao wanafikiria kinyumenyume Sana

Kenya pamoja na kuwa na Diaspora kubwa, lakini bado hawana "Foreign currencies", uchumi wao unazidi kuzorota, unemployment ndio kubwa kuliko nchi zote na inazidi kuongezeka.

Conclusion: Jibu la matatizo ya Kenya lazima wajenge uchumi wa ndani kwa kutumia Wasomi na raia wao Ili watengeneze ajira, sio kuwapeleka nje ya nchi huku nyumbani wanabaki "less Qualified people "
Nimekubali sera ya ujamaa na ukomunisti hupofusha fikra.
 
Nashangaa these guys wanasema tz unapaswa ku apply ukiwa unataka kusafiri
Sio kutaka kusafiri tu uonyeshe vithibitisho kama kweli unataka kusafiri among them barua ya mwaliko. Kinyume na hapo utumie madalali uhonge.
 
Ndio sababu Kenya is ranked poorly on security, Globally Tanzania is ranked position 54, while Kenya 125.
Kenya imekuwa ranked poorly kwa sababu inapakana na Somalia,
Somalia kila siku ni vita na mashambulizi ya al shabaab
 
90% ya Wasomi Afrika husomeshwa kwa pesa ya serikali au hutumia miundombinu ya serikali. Lengo la kuwasomesha watu sio kwa ajili ya kuajiriwa tu, ni kutengeneza watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ubora na ufanisi popote pale, hasa katika private sector.

Muwekezaji yeyote anapotaka kuwekeza nchini lazima achunguze kuwepo kwa skilled people, Sasa Kama skilled people wako nje ya nchi na waliobaki ni "semi skilled", unategemea kupata uwekezaji wa maana kweli?
Serikali haisomeshi, bali inatoa mikopo tena kwa baadhi tu.

Kuna wengine, wengi tu, walisoma kwa kujilipia au kulipiwa na wazazi au walezi wao.
 
Mkuu, inaelekea hata Kenya bado hujafika. Hakuko hivyo kama unavyofikiri. Ina wasomi wa kutosha na ziada, ndiyo maana Serikali yake inafanya jitihada kuwatafutia raia wake kazi katika mataifa mengine.
Sahihi serikali ya Kenya karibuni imeingia makubaliono na serikali ya ujerumani kupeleka wafanyakazi wakenya 250,000 kwenda ujerumani kujaza nafasi mbalimbali zilizo wazi ujerumani na wamekubakiana mafunzo ya lugha ya kijerumani yaanze Kenya ili kuwaanda watakaoenda kufanya kazi

According to President William Ruto of Kenya, an agreement between Kenya and Germany is in the works and may see Berlin welcome Kenyans to fill some of the 250,000 unfilled positions to help the European country's enormous labor need.
Chancellor Olaf Scholz of Germany and President Ruto of Kenya relayed the information during a joint news conference from the State House in Nairobi.
According to the deal, the European nation would take in more professionals, skilled workers, and semi-skilled Kenyans. Nairobi wants Berlin to reconsider and relax immigration restrictions so that Kenyans can work in Germany in order to make this possible.

Source: Media za Kenya
 
Sahihi serikali ya Kenya karibuni imeingia makubaliono na serikali ya ujerumani kupeleka wafanyakazi wakenya 250,000 kwenda ujerumani kujaza nafasi mbalimbali zilizo wazi ujerumani na wamekubakiana mafunzo ya lugha ya kijerumani yaanze Kenya ili kuwaanda watakaoenda kufanya kazi

According to President William Ruto of Kenya, an agreement between Kenya and Germany is in the works and may see Berlin welcome Kenyans to fill some of the 250,000 unfilled positions to help the European country's enormous labor need.
Chancellor Olaf Scholz of Germany and President Ruto of Kenya relayed the information during a joint news conference from the State House in Nairobi.
According to the deal, the European nation would take in more professionals, skilled workers, and semi-skilled Kenyans. Nairobi wants Berlin to reconsider and relax immigration restrictions so that Kenyans can work in Germany in order to make this possible.

Source: Media za Kenya
Serikali ya watu wanaojitambua.
 
Tatizo ni pale wanapotumia pesa ya serikali Kisha wanatoroka, Sasa vipi unataka serikali ijitathimini?.

Hivi wewe ukimsomesha msichana kwa lengo la kuja kumuoa aje kuwa mkeo na mlikubalian hivyo,lakini mara tu baada ya kumaliza chuo, akamuona jamaa anaishi maisha mazuri kukuzidi wewe akaamua kuachana na wewe na kwenda kuolewa na huyo jamaa mwengine, tatizo liko kwako au kwa huyo msichana?
Kama umesoma, katika harakati zako zote za kusoma kwako hadi level uliyofika, KUNA PAHALA ULIKUBALIANA NA SERIKALI KWAMBA UTAKUJA KUFANYA KAZI SERIKALINI BAADA YA KUSOMA KWA KODI ZINAZOKUSANYWA NA SERIKALI? Haya, serikali imekaa miaka mingapi haijaajiri mtu, wale wahitimu wafanyeje? Kuna wakati tuwe waharisia tuachane na nadharia..!!

BTW, siku hizi elimu kwa mkopo ambao unakuja kuulipa baadaye...!!!

Kuna makampuni, wakikupeleka baadhi ya training, hasa zenye gharama kubwa, unasaini mkataba kuwa ukitoka huko utafanya kazi kwao kwa kipindi fulani, say mika mitatu..!! Ukimwacha mtu huru ujuzi uliompa anaweza akaenda kuutumia kwingine...!!

Turudi huko kwenye serikali. Kama serikali ingekuwa inaajiri kila aliyesoma kwa kodi za serikali, kungekuwa na wasomi mitaani wasio na ajira?

Kukujibu swali lako na huyo msichan kuolewa na mtu mwingine, TATIZO LIPO KWAKO WEWE ULIYEMSOMESHA. UMEWEKEZA BILA KUJIHADHARI. HIVI UNADHANI KWANINI HATA MAKAZINI TUNA MIKATABA? KWANINI HATA KUTOA HELA YAKO ULIYOIWEKA BENKI LAZIMA UWEKE SAHIHI? HUKO KUTOCHUKUA TAHADHARI MAPEMA NDO HUPELEKEA WATU KUUWA..!!
 
Swali lako halijakaa sawa. Ninalotaka kusema ni kwamba, nchi ikiwa na Wasomi wengi ni miongoni mwa vivutio vya uwekezaji nchini, Kama Wasomi wako unawaacha waende nchi zingine, wawekezaji wengi hawatopenda kuja kuwekeza kwasababu atakosa watu wa kufanya kazi zake, haiwezikani muwekezaji kuja na wafanyakazi 200 toka nchini kwake
Unazungumzia wasomi majobless? Yaani mtu amalize chuo leo, halafu amsubiri mwekezaji miaka minne bila ajira..!!!
YOU NEED TO CHANGE YOUR THINKING KWENYE JAMBO HILI..!!
 
Mkuu, nchi hii Kuna watu wengi wazuri wenye hekima, elimu na busara nyingi ukiwemo wewe...
Kumbe unafahamu hilo. Inawezekana na wewe uko kwenye system. Kama kuna mahali mmekwama, mseme msaidiwe. Kuna Watanzania wengi wenye mawazo mbadala na wako tayari kuyatoa bure, bila kudai malipo yo yote.
 
90% ya Wasomi Afrika husomeshwa kwa pesa ya serikali au hutumia miundombinu ya serikali. Lengo la kuwasomesha watu sio kwa ajili ya kuajiriwa tu, ni kutengeneza watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ubora na ufanisi popote pale, hasa katika private sector.

Muwekezaji yeyote anapotaka kuwekeza nchini lazima achunguze kuwepo kwa skilled people, Sasa Kama skilled people wako nje ya nchi na waliobaki ni "semi skilled", unategemea kupata uwekezaji wa maana kweli?
Unafahamu kuwa Tanzania kuna maelfu ya watu ambao tokea wahitimu Vyuo zaidi ya miaka kumi iliyopita, hawajapata ajira mpaka sasa?

Unafurahia unapowaona wakitembea na bashasha za khaki huku viatu vimeisha soli kwa kusaka ajira?
 
90% ya Wasomi Afrika husomeshwa kwa pesa ya serikali au hutumia miundombinu ya serikali. Lengo la kuwasomesha watu sio kwa ajili ya kuajiriwa tu, ni kutengeneza watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ubora na ufanisi popote pale, hasa katika private sector.

Muwekezaji yeyote anapotaka kuwekeza nchini lazima achunguze kuwepo kwa skilled people, Sasa Kama skilled people wako nje ya nchi na waliobaki ni "semi skilled", unategemea kupata uwekezaji wa maana kweli?
Unafahamu kuwa Tanzania kuna maelfu ya watu ambao tokea wahitimu Vyuo zaidi ya miaka kumi iliyopita, hawajapata ajira mpaka sasa?

Unafurahia unapowaona wakitembea na bashasha za khaki huku viatu vimeisha soli kwa kusaka ajira?
 
Back
Top Bottom