Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala(PhD) aitwa Polisi kutokana na maoni yake kuhusu bandari

Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala(PhD) aitwa Polisi kutokana na maoni yake kuhusu bandari

Wamefanya vizuri tena sana, watu wachache hawawezi kusambaza chuki, kuleta mgawanyiko wa nchi kwa sababu zao binafsi. Zile siyo lugha ya mtu mwenye akili timamu kwanza apimwe akili. Utafikiri hajalelewa na wazazi, huwezi kumtukana mwanamke mtu mzima kiasi kile achilia mbali ndiyo eais wa nchi yetu. Vyombo vya ulinzi na usalama visicheke na watu km hao hata kidogo. Bado yule mnyakyusa Mwabukusi. Km wana stress zao watafute namna ya kuzimaliza huko huko wasitumie mipango mizuri ya serikali.
Wewe ni hewa kabisa 🤣 unasikitisha.
 
Dr, Nashala anatakiwa aende saa tisa alfajiri (asubuhi) kama alivyo ambiwa ktk barua ya wito. Atakuta ofisi ya DCI imefungwa anarudi zake nyumbani kulala.
Hakuna kesi tena alishatii wito.
Hahahah saa 9 asubuhi🤣
 
Ebu iweke hiyo mipaka na utuambie sheria inayoweka hiyo mipaka.

Kama wanaona ana jinai,wampeleke mahakamani ili ujinga wao umaonekane wazi, siyo kumtishia.
Hahahah sahizi uhuru wa maoni ni wa kusifu na kumtukuza kiongozi. Ukionekana unatoa maoni yanayokuwa kinyume na kusifu maana yake unapewa kesi ya jinai. 🤣
 
Haya mambo haya ila jamaa alikuwa anapoint nzuri kuhusu huo mkataba ila kauli hasi na zakebehi zinaaribu lengo la maoni yake Mungu amjalie awe na mwisho mwema.
 
Hawa watu wanabadilisha watu neutral kwenda nao against...

Why kutumia nguvu Kiasi hiki

Mimi kama mtanzania naona ifike wakati sasa sio tuangalie tu huu Mkataba bali kuhakikisha kwamba mikataba yote kuanzia huu wa sasa na ijayo yote inakuwa wazi (Transparency)
Tusingefika huku kama Bunge lingefanya wajibu wake inavyopaswa.
 
Waandishi wa habari huru, wenye youtube channels zao.

Waitwe mmoja mmoja na kujieleza ni nani anawalipa.

Simu na mawasiliano yao yachunguzwe kwa kina. Naamini serikali inaweza kufanya uchunguzi mzuri na wa haraka na unaofata sheria.
Wewe nani anakulipa waanze na wewe
 
Hii safi sana, maana kuna watu wanasambaza uongo, inatakiwa upelelezi chunguze namba zote wanazowasiliana nazo kwa simu na kwa messgaes. Vyanzo vitajulikana tu.

Hii ni vita ya kiuchumi kwa nchi yetu. Aidha watangazie waende wenyewe kwenye vyombo vya uchunguzi au waitwe namna hii.

Nashauri watazamwe ma group yao yote ya wharsapp, telegram, twitter, facebook na jadhalika. Ili vyanzo vijulikane.

Mimi nakisia. vyanzo vya haraka haraka:

1) Anna Tibaijuka.
2) karamagi
3) Adani
4) AD Ports
5) DP World
6) Wakurugenzi waliovunjiwa bodi yao bandarini.
9) Wakurugenzi wa shirika la meli lilitojajwa namba moja.
10) Taasisi za kidini.
11) Sukuma gang
12) Vyama vya siasa ikiwemo CCM yenyewe.

Naamini wengi humu JF ni makondoo tu yaliyokosa mchungaji. Vyanzo vitajulikana tu.

nawapa pongezi sana serikali kwa kuanza kuchukuwa hatua. Maana uongo ukizidi utaonekana ni ukweli.
Nguvu yote hii ni kwa ajili ya kunyamazisha watu wasiukatae mkataba ambao hauko sawa tu ama kuna jingine.
 
Haya sasa mliokuwa mkimshangilia wakati anamtukana Rais, kama mna upendo nae huu ndio wakati wa kuongozana nae mpaka kwa DCI ili mkamtetee.
 
Waliozoea kula nyama ya mbwa wameanza,punde tutaanza kusikia fulani katekwa na watu wasiyojulikana na viroba vilivyosheheni raia wema vitafufuka tena.
 
Barua hiyo ya wito kutoka ofisi ya DCI inamtaka Dkt. Nshala kufika kwa ajili ya mahojiano


Ofisi hii inafanya uchunguzi kuhusiana na kauli ulizotoa tarehe 03 Julai 2023 na kisha kusambazwa katika vyombo vya habari na mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusiana na mkataba wa uwekezaji katika bandari ya Dar es Salaam

Ili tuwe kukamilisha uchunguzi wetu, ofisi hii inakutaka ufike ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya Jinai Kanda Maalum Dar es Salaam tarehe 11 Julai, 2023 saa 09:00 asubuhi bila kukosa kwa ajili ya mahojiano.




Pia soma:
Rugemeleza Nshala: Tutafungua Kesi kupinga Mkataba wa DP World na Tanzania
Dkt. Rugemeleza Nshala: Nimetishiwa maisha baada ya kutoa maoni kuhusu mkataba wa Bandari na DP World
Ofisi gani inaanza kuandika na namba 2 badala ya 1? Na ofisi gani hiyo ambayo ina saa 09:00 asubuhi? Saa 09:00 (saa 9), ni alasiri siyo asubuhi!

Wahusika wa ofisi wakajifunze kuhesabu, kuandika na kusoma saa za Kiswahili na Kiingereza.
 
Kwa sasa bado ni malalamiko tu siku mkijitambua hamtotawaliwa.
Mbona mumetuletea majeshi , kambi kila mtaa , usalama wa taifa mpaka wengine wanavaa kimasai, hujaingiza askari kutoka Burundi mliowakodi wakati wa uchaguzi kuja kupiga watu

Yaani watu milioni 2 tupigane na watu milioni 60 , ??

Yaani mtu mmoja apigane na watu 30

Dawa ni kuwala chini kwa chini kama mchwa , endeleeni kulia na bandari kwanza
 
Mbona mumetuletea majeshi , kambi kila mtaa , usalama wa taifa mpaka wengine wanavaa kimasai, hujaingiza askari kutoka Burundi mliowakodi wakati wa uchaguzi kuja kupiga watu

Yaani watu milioni 2 tupigane na watu milioni 60 , ??

Dawa ni kuwala chini kwa chini kama mchwa , endeleeni kulia na bandari kwanza
Kwani kuna ubaya gani wakati ndio serikali yako unayoipenda.
 
Huo muda wa saa 9:00 asubuhi haijawahi kuwepo kwenye sayari hii. Na kwa msingi huo barua inakosa mashiko. Namshauri asiende kwani mudq aliopangiwa hautakaa ufike Hadi tunaingia kuzimu!
Mwandishi ni Kama amelazimishwa kuiandika na ama hakubaliani na hatua zinazochukuliwa na polisi.
Ni FUTUHU
 
Back
Top Bottom