Wakili Mwakubusi: Vyama vya Upinzani kazi yao ni kufukuzia tu ubunge na ruzuku, haviwezi kulikomboa Taifa

Wanaoikubali na kuichangamkia kauli ya Mwabukusi katika mada hii ni watu ambao kiuhalisia wanachukia sana vyama vya upinzani hasa CHADEMA na hususan Mbowe.

Hawa ni mchanganyiko wa wafuasi wa kudumu wa CCM, wapenzi wa Rais awamu ya 6 (SSH) na waumini (diehards) wa Magufuli (MATAGA). Hawa ni watu ambao hawana interest kabisa na uwepo wa upinzani wala demokrasia Tanzania. Hata ukiwashauri wao basi washiriki kuunda upinzani imara kwani kina Mbowe hawana ukiritimba wa kumiliki upinzani nchini, HAWATAKI!

MATAGA hawamtaki kabisa SSH na serikali yake. Lakini hawana mkakati wowote wa kumbadili zaidi ya kulalamika sana! Pia wanachukia sana upinzani hasa CHADEMA na Mbowe kama masihi wao alivyotaka kuiangamiza. Wao ndoto yao kuu ni kumpata Magufuli mwingine awe Rais wa nchi. Kwa CCM, naturally, CHADEMA ni tatizo kubwa kwao. Hivyo, kila mwenye umaarufu wowote anayejitokeza kuiponda anageuka rafiki yao mkubwa.

Hii ni nchi iliyojaa wanafiki na wajinga wengi sana kama alivyodai mjinga mmojawao Dr. Mollel.
 
Tru Ukweli mtupu 100%
 
Sawa.lakini kukiondoa chama madarakani should be a process angalau ya 10 years. Unaanza na kuwa na wabunge wengi ,then ndipo unaipata Kura nyingi za uraisi!!huwezi kusema utachukua Nchi bila ya kuwa na wabunge wengi
Watu wanawaza mambo ya mgom bea binafsi wewe bado unawaza wabunge.Hao wanaopinduaga serikali wanakuaga na wabunge wangapi?.Ukiwa smart wabunge ni kitu kidogo sana.
 
Wakili Msomi na Mtetezi wa Tanganyika huru na Bandari zetu anasema vyama vyote vya Upinzani ni vitalu vya kuwindia Maokoto ya Ruzuku

Sent from my SM-G9500 using JamiiForums mobile app
Kwa bahati nzuri, Wakili Msomi kasema ukweli mtupu.

Kaacha tu kukitaja "Chama Cha Mafisadi"(CCM) kuwa ndiyo chanzo cha hali hiyo inayoonekana huko ndani ya vyama vya upinzani (vyote).
Na hiyo CCM ipo siyo kwa manufaa ya nchi.

Haya yote yanahitaji ufafanuzi makini.
 
Very true, hata ajenda ya bandari ilikua makosa makubwa sana kuwaachia wanasiasa esp chadema kuisimamia.

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Huyo mwabukuzi kashalewa sifa, anaanza kuvamia watu. Watu walipopigwa risasi na kuvunjiwa vitega uchumi vyao alikuwa wapi?.
Hapana.
Kasema ukweli mtupu, ambao ni ukweli mchungu kwetu sote.

Yeye kutosema chochote kuhusu matukio ya huko, hayapunguzi chochote katika anayoyaamini sasa.

Ni wangapi katika nchi hii wametoka mbele kwa jambo lolote, kama alivyofanya yeye.
 
Kwa maneno hayo naona anaweza kupewa Kasi ya kijani wakati wowote.
Kuna vyama wanawindwa kama swala porini halafu yeye amekuja juzi TU anajitia anataka kuikomboa nchi..
Mwamba nilikua napata walakini na wewe kwenye ule uzi wa Ukraine, baada ya kukusoma kwenye nyuzi mbili tatu tofauti nimegundua hamna kitu. Kuna uongo upi katika alichosema wakili?

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Haya aliyoyasema ni sahihi kabisa, hili tunaliona wananchi lakini je, tufanyaje? Mwambukusi hana chama lakini kiukweli namkubali sana. Hivyo sauti ya huyu mwamba itaeleweka pasipokuwa na chama!?
Huyu Jamaa sijui anasubiri nini kuanzisha chama, angejizolea wafuasi lukuki!
 
Huyu Jamaa sijui anasubiri nini kuanzisha chama, angejizolea wafuasi lukuki!
Kinachonishangaza ni watu Kila ukitajwa upinzani wazo linalowajia vichwani mwao ni CHADEMA.

Hivi CHADEMA inazuia vyama vingine kuanzishwa ama kuwa imara dhidi ya CCM??
 
Mwabakusi ni unguided missile
 
Kafika bei
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…