Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja
Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao
Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo
Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini
Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho
Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS
Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo
Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini
Comasava
Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao
Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo
Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini
Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho
Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS
Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo
Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini
Comasava