Wakili Mwambukusi huenda akashidwa kwenye kura uchaguzi wa TLS

Wakili Mwambukusi huenda akashidwa kwenye kura uchaguzi wa TLS

Boi Manda

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2023
Posts
388
Reaction score
506
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja

Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao

Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo

Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini

Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho

Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS

Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo

Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini

Comasava
 
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja

Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao

Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo

Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini

Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho

Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS

Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo

Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini

Comasava
Acheni utoto hakuna uchaguzi unafanyika ili mtu flani asishinde
 
Bwashee ni mwaka mmoja tu. Akishinda kama ilivyo kwa tulia akson raisi wa CPU

Hii miamba miwili itakutana pale Jimbo la Mbeya mjini kwenye ubunge

Mmoja ni raisi wa CPU mwingine ni raisi wa TLS
Ilikuwa ni mwaka moja... Ila kuanzia uchaguzi huu itakuwa ni miaka 3. Ndiyo maana serikali inaogopa mtu kama Mwambukusi kuwa hapo kwa muda mrefu hivyo.
 
Kina Kibatala na ule msimamo wao wa kutaka Adv. Mwabukusi arudishwe kugombea, lakini kusema wazi hawatampigia kura ulikuwa ni mpango mbovu.

Kama kura ni siri sikuona sababu kwanini watangaze machaguo yao hadharani, ile ilikuwa ni sawa na kuwafanyia kampeni wagombea wao kwa kivuli cha kutetea haki ya Adv. Mwabukusi, kwangu naona walikosea pakubwa.

Nasema walikosea pakubwa kwasababu kwa hiyo misimamo yao walijigeuza kuwa vibaraka wa watawala bila wao wenyewe kujua.

Hii pia inaweza kuwa ndio sababu ya Adv. Mwabukusi kushinda kesi yake ijumaa, kwasababu watawala walijua kumbe Adv. Mwabukusi hakubaliki miongoni mwa wapiga kura kama walivyokuwa wakihofia.
 
alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini
Na hivi ndivyo wananchi pia wanavyochukulia hiko chama maana hakina msaada wowote kwao ni kweli hajakosea kama alisema hivyo..
 
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja

Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao

Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo

Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini

Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho

Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS

Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo

Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini

Comasava
Ubaya ubwela.
 
Back
Top Bottom