Wakili Sweetbert Nkuba kupinga ushinda wa Wakili Boniface Mwabukusi kuwa Rais wa TLS

Sijasoma sheria ila naelewa kuhusu neno "Tetesi" Tatizo la ndugu yangu hakuonesha kipaumbele kwa wanasheria vijana kuwa atawasaidiaje bila kujuwa wao ndiyo wengi kuliko wazee.
 
Kwel kabisa ume eleza kila kitu nkuba atulie
 
Huyu na yeye aache tu hili lipite, asijitie aibu zaidi
 

"Mojawapo ni kuona karatasi za kupigia kura kuisha na kwenda kuchapishwa zingine, kufanyiwa vurugu na kusambaa taarifa mitandaoni ushindi wa mpinzani wangu kabla ya kutangazwa na msimamizi wa uchaguzi," amesema Nkuba.​
Tatizo alikuja na mbinu zote za ki-ccm zikafeli.
Karatasi chache - kwanini!? Hapa ilikuwa "zipigwe kura za maruwani kwa jina la Nkuba kufikia idadi ya wapiga kura halali - hapa ccm mara nyingi wanaiba kupitiliza idadi. 2020 waliiba hadi waliona aibu kupost matokeo ya Urais kituo kwa kituo!

Kusambaa taarifa mitandaoni - katika kitu ccm hawataki kusikia ni matokeo raw kupatikana kabla ya uchakachuaji na maelekezo maalum kutoka juu! Yaani kifupi hawataki alternative tallying center! Rejea 2015 walivamia tallying center ya Lowasa na kuiba computers!

Team Mwabukusi kwenye hili wanastahiki pongezi za dhati kudhibiti mianya ya goli la mkono!

Natamani hii kesi ifike mahakamani ili mbivu na mbichi zijulikane mapema kabla chaguzi ya zijazo!
Ila naona machawa na makada wazoefu washaanza kumtuliza Nkuba!
 
Kama wanasheria nao wanalalamika hivi kwenye chaguzi zao, je kwenye chaguzi za viongozi wa mitaa na vitongoji hapa Kizuramimba na Kakonko itakuwaje?
Tatizo la mawakili wengi wanapenda sana debate hata pasipokuwepo na hoja ya msingi!!
 
Yaani unaenda mahakamani kwa kigezo cha taarifa za mitandaoni. Huyu Wakili wa wapi?
Labda anaamini anaweza ishawishi Mahakama na taarifa za mitandaoni,mwisho wa siku Mahakama itaziweka hizo taarifa kwenye mizani, na majibu ya Mahakama yatatoka kwa wahusika!!
 
Atakuwa kapewa "maelekezo' na "wale watu" kwani walimwaminisha atashinda!
Anapoteza muda wake bure huyu mtu angetumia muda huo kuweka familia vyema!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…