Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Habari zenu..
Niende moja kwa moja bila kupoteza muda mwenzenu nimepata mke wa kuoa ila huyu mwanamke ni single mother...ninachokifikilia ninaanza vipi kumtambulisha nyumbani kwetu Kwa wazazi?
Kuhusu baba nitampiga kiswahili ataelewa mziki uko kwa mama yangu nitamueleza vipi ili anielewe kuwa naingia mchezoni na mchezo ukiwa ni moja bila ?
Vipi kuhusu ndugu zangu nitawaelezaje kuwa naanza mechi mchezo ukiwa ni moja bila badala ya bila bila!!!
Je hawatapasha kiporo na mzazi mwenzake akija kumuona mwanae au akimpelekea mwanae amuone?

Kwa wanaotarajia kuingia kwenye mdoa kama hii au mliongia kwenye ndoa za moja bila au mbili bila naombeni mnipe ushauri kijana mwenzenu nichukue na mimi jiko niache kula kwa mama ntilie.
 
Tunataka wa mfano!!wewe oa alafu utakuja kutupa mrejesho..
Kuna maswali ya kujiuliza kabla hujaingia kwenye hiyo ndoa.
Kwanini huyo mzazi mwenzie hajamuoa
Kama walioana kwnini wameachana
Mtoto wao ana umri gani
Huyo mzazi mwenzake ameshaoa mke mwingine?
Uwezo wake kiuchumi/huko akiko anafanya shughuli gani
Nani alimuacha mwenzake?
Kwani ni lazima huyo mke kumpeleka mtoto akamuone kwa huyo mzazi mwenzake?kwanini asimpe aishi naye
 
Unaoa mke utakaeishi nae wewe. Badala ya kujiuliza kama anakufaa au atamudu changamoto za ndoa, unaanza kujiuliza kama mama atakubali au ndugu zako watakuonaje!

Inawezekana umri umefika but you still lack that maturity thing!
 


Maswali yote ni relevant.

Ila hilo la mtoto ni crucial. But cruciality yake haina maana.

Kama umependa boga penda na ua. Amlee huyo mtoto, maana mtoto ni hazina si tu kwa Taifa bali hata kwake huyo mwanaume.
 
Unaoa mke utakaeishi nae wewe. Badala ya kujiuliza kama anakufaa au atamudu changamoto za ndoa, unaanza kujiuliza kama mama atakubali au ndugu zako watakuonaje!
Inawezekana umri umefika but you still lack that maturity thing!


Akifata huu ushauri atafanikiwa sana
 
Nawewe tafuta mtoto kwa mama mwingine nje kabla hujaoa ili muwe 1-1....yani both team mmescore first half
Wanawake wa siku hizi bana, hadi kwenye kubeti!

Sasa tutawaongopea nini asee?
 
Nawewe tafuta mtoto kwa mama mwingine nje kabla hujaoa ili muwe 1-1....yani both team mmescore first half
Oohh joanah umenishinda tabia ..yani unazijua mpaka tips za betting ..kweli wewe ni mwanamke wa tofauti
Nb: huwa ninapenda wanawake kama wew wanaojua mambo mengi
 
Mkuu kuhusu mada yako ..yani hapa jf kuna mada nyingi zilisha jadiliwa kama yako na maswali yako yalishajibiwa katika hizo thread zilizopita
Fanya kuzi search utazipata nyingi sana
 
ili ufurahie mahusiano fuata kile moyo wako kinahitaji na kupenda na si kile akili yako inawaza au macho yako huona
 
Wanawake wa siku hizi bana, hadi kwenye kubeti!

Sasa tutawaongopea nini asee?
Nyie watu mmenichekesha!! πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚
Mbona sijahusisha betting hapo
Oohh joanah umenishinda tabia ..yani unazijua mpaka tips za betting ..kweli wewe ni mwanamke wa tofauti
Nb: huwa ninapenda wanawake kama wew wanaojua mambo mengi
 
Ni maamuzi yako ukiyasimamia wazazi wako wataelewa ila swali dogo tu umechunguza sababu ya kuachana kwao, mahusiano yao yapo vipi kwa sasa, mwanamke anafanya shughuli gani kwa sasa? Maana kama waliachana uku sababu ikiwa ni mwanaume ndiyo alimuacha mwanamke ipo nafasi kubwa ya wao kuja kupasha kiporo mana wanawake wakiacha mara nyingi wanaacha kutoka moyoni na kama mwanamke hana shughuli ya kufanya kuna sababu kubwa ya wao kuja kuonana na kupasha kiporo sababu ya ukosefu wa ela kwa mwanamke ata kama ww unayopesa ya kuweza kumuudumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…