Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 30,567
- 86,748
Ni wapi palipoandikwa kuwa mwanaume anatumia mwanamke anatumiwa tuanzie hapo kwanza unajua haya mambo msilazimishe yawe katika mitazamo yenu binafsi maana kila mtu ana mtazamo wake twende kiuhalisia na ikiwezekana kimaandiko zaidi ukikwepa hapa basi hayo unayoyaongea yanabaki kuwa mtazamo wako wewe binafsi ambao hauna effect yoyote kwenye hii dunia
Hana jina la namna hiyo. Mwanaume ambaye hajawahi kufanya mapenzi haitwi Bikra na hawezi itwa hivyo.
Bikra ni mwanamke asiyewahi kukutana kimwili na Mwanaume. Hiyo ndio maana ya msingi(connotative meaning).
Maana zilizoibuka kutoka kwenye maana ya msingi ni kuwa bikra ni kitu chochote ambacho hakijawahi kutumiwa.
Hii ni kusema mtumiaji hawezi kuwa bikra ila mtumiwaji anaweza kuwa bikra. mfano. Ardhi isiyotukiwa huitwa Virgin land. Yaani ardhi ambayo haijatumiwa. Ardhi haiewezi mtumia mwanadamu. Ila mwanadamu ndiye anaitumia ardhi
Mwanaume kamwe hawezikuwa bikra kwa kuwa yeye ndiye mtumiaji. Mwanamke ni bikra kwa sababu yeye ndiye anatumiwa.
Ndio maana mwanamke akitolewa bikra bila kuolewa tunasema Ameharibiwa. Popote pale duniani. Na adhabu zake zipo na zinafahamika.
Sasa wewe kwa upuuzi wako unaona mwanaume naye anabikra. Huo kama sio wendawazimi ni nini?