Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Kwasababu hawakujitia mimba

Kwasababu hamuwezi kupangia waowaji na waolewaji nini wanataka, nini wanapenda

Bado ni suala la mtu binafsi.
Hakuna anayepangiwa, wanashauriwa. Na tunashauri kutokana na experience. Na hakuna wa kunipangia nini cha kumshauri mtu, ni suala la mtu binafsi. Acha ushauri utembee, wa kufuata atafuata, wa kuacha aache lakini wameonywa.
 
Hapo nimetolea mfano tu wa watoto wa single mothers wanaofanikiwa lakini sijatolea mfano wa single mothers wenyewe wanaofanikiwa wapo single mothers wanaofanikiwa wanaoteseka na watoto wao hadi wanakuja kufanikiwa sasa labda wewe ndiyo uniambie nini maana ya laana

Halafu naomba zingatia na hiyo aya yangu ya pili tafadhali
Afanikiwe, asifanikiwe, ushauri kuhusu kuoa ndio huo nimeshautoa. Single mother hapana.
 
Huna cha kunifundisha mimi, tunabadilishana mitazamo tu.



Pole wewe, hocho unachokiamini huko ulaya na marekani kimeshondwa na sasa wengi wanafanya marekebisho
Na kwanini haujawahi kuwaambia wanawake wasiolewe na wanaume wenye watoto nje ya ndoa??
 
Na kwanini haujawahi kuwaambia wanawake wasiolewe na wanaume wenye watoto nje ya ndoa??
Kwa sababu mwanamke hachagui mke, bali anachaguliwa. Pia mwanamke haoi bali anaolewa. Kumbuka kwa baadhi ya imani mwqnamume aweza kuoa mke zaidi ya mmoja na ikahesabika sahihi mbele ya jamii, so mwanamke akiwa msaidizi anatolewa kwao kuja kumjenge mwanamume ukoo bila kujali ana mtoto ama la.

Ndoa ni ya mwanamume sio ya mwanamke na mwanamume, get the facts straight first.
 
Nope, ukweli ni kuwa wanawake wanawajibika kwa makosa yao wenyewe. Angalia biolojia ya mwanamume na mwanamke, mmoja anatamani na ndivyo alivyo, mwingine imempasa kumsaidia mwenzake asianguke majaribuni. Lakini ni kipi kinachoendelea? Wanawake wanajipamba kikahaba wakishindana kutafuta kusifiwa na kupendwa na wanaume, na hivyo wanaume wanaingia mtegoni kwa madhaifu yao. Ikitokea mimba hukimbia mbio kwani halikuwa lengo lao, tamaa ndio iliwavuta kuwalala wanawake hawa wasiojitambua.

Kuna msamiati wa ajabu umetungwa hapa mimba zisizotarajiwa! Wewe ulale na mwanamume ufanye naye [Btendo la ndoa[/B] wakati huna ndoa unatarajia nini? Na Mungu anavyo jibu, mkitumia vidonge vya majira mimba zinakimbia, siku ukitaka kuzaa utaishia kwa waganga ama makanisani kuombewa.

Wanaume wataendelea kuwazalisha na kuwakimbia as long as mnawatengenezea mazingira ya kifanya hivyo, nyie endeleeni kunyoosha vidole.
Nakumbuka niilishawahi kukutolea mfano wa kule Eden kwamba Evah ndiye aliyemshawishi Adam kula tunda lakini wote walipewa adhabu!! Sasa kama kweli anayekubali kushawishika hana makosa kwanini naye alipewa adhabu kwanini adhabu asingepewa aliyeshawishi peke yake??

Maana yake ni nini?? Maana yake ni kwamba vishawishi vipo na ni jukumu lako na wajibu wako kuvishinda kwa sababu uwezo wa kuvishinda umepewa ila kwa vile wanaume mnajiona mmeumbwa na tamaa mnavikumbatia hivyo vishawishi halafu mnatafuta sababu za kujitetea na kujiona hamna makosa wakati aliyeshawishi na aliyekubali kushawishika wote wana makosa!!

Mind you hakuna andiko kwenye biblia limesema eti mwanamke anatakiwa amsaidie mwanaume kupunguza tamaa kila jinsia ina maovu yake na kila jinsia inatakiwa ipambane kivyake katika kuacha hayo maovu na siyo kusingizia kuwa eti jinsia fulani ndiyo na ndiyo inatakiwa hakuna kitu kama hiko

Kumbuka hata Mungu alimruhusu Shetani kuja kutujaribu hapa duniani na akatupa uwezo wa kumshinda na watakaoshindwa wakaanguka basi watahukumiwa naye kuenda motoni sasa usitegemee eti siku ya hukumu utaenda kumuambia Mungu kwamba Shetani ndiyo alikufanya ukatenda dhambi hiyo sababu na utahukumiwa wewe pamoja na huyo Shetani wako
 
Kuna binti anakwenda kwa rafiki yake wa kike anakutana na ubakaji, huyu ametengeneza mazingira. Kuna binti anakwenda beach na rafiki zake anaingizwa kuogelea na beach boys anabakwa, huyu katengeneza mazingira.

Kuna binti anakwenda kisimani, anajikuta yuko peke yake anakamatwa kwa nguvu anapiga kelele bila msaada anabakwa, huyu ingawa angeweza kuepuka lakini kabakwa pasipo kutarajia.

Sasa nionyeshe siasa ni nini? Zungumzia uhalisia sio ukitakacho.
Kwahiyo mwanaume kubaka ni sawa hata kama katengenezewa mazingira??
 
Kwenye mimba huo mfano wako hausadifu mazingira. Sheria ya Mungu wote wametenda dhambi na watategemea huruma ya Mungu. Kama ikitokea mimba mwanamume aweza kukataa, kukimbia ama vyovyote vile, mlezi ni mwanamke sababu mazingira pekee yanayokubalika kujenga familia ni ndoa. Nje ndoa ni kujitakia mateso tu kwa mwanamke. Hata sheria haimfungi sana mwanamume kwani hata kama atabainika, imemtaka kumpatia mwanamke peaa za matunzo ya mtoto kulingana na kipato chake.

Hivyo huo mfano hauna uhalisia
Umekwepa ukweli
 
mfano mimi na wewe tunapendana, nikikuomba unizalie unaweza nipa masharti gani?
Mimi binafsi siwezi kuzaa nje ya ndoa ila kumbuka udhaifu wa wanawake wengi ni kupenda kwa dhati na wanaume mkishajua mmependwa huwa kuna vitu mnafanya makusudi sababu mnajua hamuwezi kuachwa

Hivyo kuna wanaume wengine wanautumia huo udhaifu na wanawaambia wanawake wao wawazalie watoto ndiyo watawaoa na wakikataa basi wanaachana sasa kwa mwanamke ambaye kapenda kweli lazima akubali tu hata kama ni kishingo upande na shida ndiyo inaanzia hapo
 
Karma, Biblia inasema aliyedanganywa ni mwanamke na sio mwanamume. Shetani alimdanganya mwanamke, mwanamke akamdangaya mwamume.

Hata leo shetani anamdanganya mwanamke ajiweke uchi, ajipambe kikahaba kisha mwanamke anamdanganya mwanamume.

Ndio maana tunawaonya mrudi kwenye mstari mtuokoe, hata wachungaji wengi wameangushwa na wanawake
 
Kwa binti mwenye maadili, hawezi kuwa kwenye mazingira yatakayo mfanya awe target, hata wazazi wanaojali hawawezi kumweka binti yao kwenye mazingira kama hayo. Kumbuka umeongelea kijijini.
Kwahiyo mkuu wewe unadhani mwanaume kaumbwa na tamaa ila aje aitumie tamaa yake vizuri hapa duniani?? Kwamba hajapewa kabisa uwezo wa kuishinda hivyo hata akiitumia ni sawa tu si ndiyo??
 
Karma, Pia hapa siongelei dhambi ya zinaa, naongelea vijana kutokuoa single mothers. By the way kwa nini ukabadili ID toka Marianah!?
 
Wanawake wanaokubali ombi hili hawafai kuw wake wa ndoa. Ni wasio jitambua kabisa.
Yaani kwanza kabisa haujajibu swali langu halafu pili kwahiyo hao wanaume wanaowaomba wanawake wao wawazalie kabla ya ndoa wakati wanajua siyo vizuri ndiyo wako sahihi na wanafaa kuwa waume wa ndoa si ndiyo??
 
Afanikiwe, asifanikiwe, ushauri kuhusu kuoa ndio huo nimeshautoa. Single mother hapana.
Oohh sasa si ungesema tu tangu mwanzo kwamba huo ni mtazamo wako wewe na siyo uhalisia sasa unapomuingiza hadi Mungu kwenye haya maswala una maana gani?? Kuwa makini!!
 
Mimi binafsi siwezi kuzaa nje ya ndoa ila kumbuka udhaifu wa wanawake wengi ni kupenda kwa dhati na wanaume mkishajua mmependwa huwa kuna vitu mnafanya makusudi sababu mnajua hamuwezi kuachwa

Hivyo kuna wanaume wengine wanautumia huo udhaifu na wanawaambia wanawake wao wawazalie watoto ndiyo watawaoa na wakikataa basi wanaachana sasa kwa mwanamke ambaye kapenda kweli lazima akubali tu hata kama ni kishingo upande na shida ndiyo inaanzia hapo
Jukumu la mwanamke si kupenda bali kutii, mwanamume ndiye mwenye kupenda. Sasa wanawake wa mwendo kasi wanajipa majukumu ya wanaume, matokeo yake ni kupotea.
 
Back
Top Bottom