Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,828
- 3,579
Hakuna anayepangiwa, wanashauriwa. Na tunashauri kutokana na experience. Na hakuna wa kunipangia nini cha kumshauri mtu, ni suala la mtu binafsi. Acha ushauri utembee, wa kufuata atafuata, wa kuacha aache lakini wameonywa.Kwasababu hawakujitia mimba
Kwasababu hamuwezi kupangia waowaji na waolewaji nini wanataka, nini wanapenda
Bado ni suala la mtu binafsi.
Wanawake wanaokubali ombi hili hawafai kuw wake wa ndoa. Ni wasio jitambua kabisa.Kwani hakuna wanaume wanaowaomba wanawake wawazalie?? Na kwanini wawaombe??
Afanikiwe, asifanikiwe, ushauri kuhusu kuoa ndio huo nimeshautoa. Single mother hapana.Hapo nimetolea mfano tu wa watoto wa single mothers wanaofanikiwa lakini sijatolea mfano wa single mothers wenyewe wanaofanikiwa wapo single mothers wanaofanikiwa wanaoteseka na watoto wao hadi wanakuja kufanikiwa sasa labda wewe ndiyo uniambie nini maana ya laana
Halafu naomba zingatia na hiyo aya yangu ya pili tafadhali
Na kwanini haujawahi kuwaambia wanawake wasiolewe na wanaume wenye watoto nje ya ndoa??Huna cha kunifundisha mimi, tunabadilishana mitazamo tu.
Pole wewe, hocho unachokiamini huko ulaya na marekani kimeshondwa na sasa wengi wanafanya marekebisho
Defend yourself at all times! Yaani niache wanangu na niwapendao wanaangamia hivihivi? Big NO!Hii huwa ndiyo defense mechanism yenu siku zote
Wa kusingizia atajulikana tu, njia ya mwongo ni fupi.Naona sasa mnataka single mothers wengi waanze kusingizia kwamba watoto wao ni matokeo ya kubakwa
Kwa sababu mwanamke hachagui mke, bali anachaguliwa. Pia mwanamke haoi bali anaolewa. Kumbuka kwa baadhi ya imani mwqnamume aweza kuoa mke zaidi ya mmoja na ikahesabika sahihi mbele ya jamii, so mwanamke akiwa msaidizi anatolewa kwao kuja kumjenge mwanamume ukoo bila kujali ana mtoto ama la.Na kwanini haujawahi kuwaambia wanawake wasiolewe na wanaume wenye watoto nje ya ndoa??
Nakumbuka niilishawahi kukutolea mfano wa kule Eden kwamba Evah ndiye aliyemshawishi Adam kula tunda lakini wote walipewa adhabu!! Sasa kama kweli anayekubali kushawishika hana makosa kwanini naye alipewa adhabu kwanini adhabu asingepewa aliyeshawishi peke yake??Nope, ukweli ni kuwa wanawake wanawajibika kwa makosa yao wenyewe. Angalia biolojia ya mwanamume na mwanamke, mmoja anatamani na ndivyo alivyo, mwingine imempasa kumsaidia mwenzake asianguke majaribuni. Lakini ni kipi kinachoendelea? Wanawake wanajipamba kikahaba wakishindana kutafuta kusifiwa na kupendwa na wanaume, na hivyo wanaume wanaingia mtegoni kwa madhaifu yao. Ikitokea mimba hukimbia mbio kwani halikuwa lengo lao, tamaa ndio iliwavuta kuwalala wanawake hawa wasiojitambua.
Kuna msamiati wa ajabu umetungwa hapa mimba zisizotarajiwa! Wewe ulale na mwanamume ufanye naye [Btendo la ndoa[/B] wakati huna ndoa unatarajia nini? Na Mungu anavyo jibu, mkitumia vidonge vya majira mimba zinakimbia, siku ukitaka kuzaa utaishia kwa waganga ama makanisani kuombewa.
Wanaume wataendelea kuwazalisha na kuwakimbia as long as mnawatengenezea mazingira ya kifanya hivyo, nyie endeleeni kunyoosha vidole.
Kwahiyo huyo aliyemshawishi hana makosa??Hata kama alimshawishi abebe mimba bado ni uamuzi wa mwenye tumbo lake
Kwahiyo mwanaume kubaka ni sawa hata kama katengenezewa mazingira??Kuna binti anakwenda kwa rafiki yake wa kike anakutana na ubakaji, huyu ametengeneza mazingira. Kuna binti anakwenda beach na rafiki zake anaingizwa kuogelea na beach boys anabakwa, huyu katengeneza mazingira.
Kuna binti anakwenda kisimani, anajikuta yuko peke yake anakamatwa kwa nguvu anapiga kelele bila msaada anabakwa, huyu ingawa angeweza kuepuka lakini kabakwa pasipo kutarajia.
Sasa nionyeshe siasa ni nini? Zungumzia uhalisia sio ukitakacho.
Umekwepa ukweliKwenye mimba huo mfano wako hausadifu mazingira. Sheria ya Mungu wote wametenda dhambi na watategemea huruma ya Mungu. Kama ikitokea mimba mwanamume aweza kukataa, kukimbia ama vyovyote vile, mlezi ni mwanamke sababu mazingira pekee yanayokubalika kujenga familia ni ndoa. Nje ndoa ni kujitakia mateso tu kwa mwanamke. Hata sheria haimfungi sana mwanamume kwani hata kama atabainika, imemtaka kumpatia mwanamke peaa za matunzo ya mtoto kulingana na kipato chake.
Hivyo huo mfano hauna uhalisia
Mimi binafsi siwezi kuzaa nje ya ndoa ila kumbuka udhaifu wa wanawake wengi ni kupenda kwa dhati na wanaume mkishajua mmependwa huwa kuna vitu mnafanya makusudi sababu mnajua hamuwezi kuachwamfano mimi na wewe tunapendana, nikikuomba unizalie unaweza nipa masharti gani?
Kwahiyo mkuu wewe unadhani mwanaume kaumbwa na tamaa ila aje aitumie tamaa yake vizuri hapa duniani?? Kwamba hajapewa kabisa uwezo wa kuishinda hivyo hata akiitumia ni sawa tu si ndiyo??Kwa binti mwenye maadili, hawezi kuwa kwenye mazingira yatakayo mfanya awe target, hata wazazi wanaojali hawawezi kumweka binti yao kwenye mazingira kama hayo. Kumbuka umeongelea kijijini.
Yaani kwanza kabisa haujajibu swali langu halafu pili kwahiyo hao wanaume wanaowaomba wanawake wao wawazalie kabla ya ndoa wakati wanajua siyo vizuri ndiyo wako sahihi na wanafaa kuwa waume wa ndoa si ndiyo??Wanawake wanaokubali ombi hili hawafai kuw wake wa ndoa. Ni wasio jitambua kabisa.
Oohh sasa si ungesema tu tangu mwanzo kwamba huo ni mtazamo wako wewe na siyo uhalisia sasa unapomuingiza hadi Mungu kwenye haya maswala una maana gani?? Kuwa makini!!Afanikiwe, asifanikiwe, ushauri kuhusu kuoa ndio huo nimeshautoa. Single mother hapana.
Jukumu la mwanamke si kupenda bali kutii, mwanamume ndiye mwenye kupenda. Sasa wanawake wa mwendo kasi wanajipa majukumu ya wanaume, matokeo yake ni kupotea.Mimi binafsi siwezi kuzaa nje ya ndoa ila kumbuka udhaifu wa wanawake wengi ni kupenda kwa dhati na wanaume mkishajua mmependwa huwa kuna vitu mnafanya makusudi sababu mnajua hamuwezi kuachwa
Hivyo kuna wanaume wengine wanautumia huo udhaifu na wanawaambia wanawake wao wawazalie watoto ndiyo watawaoa na wakikataa basi wanaachana sasa kwa mwanamke ambaye kapenda kweli lazima akubali tu hata kama ni kishingo upande na shida ndiyo inaanzia hapo
Hakuna anayependa ila ndiyo inatokea na hauwezi kubadilisha hilo pole sanaDefend yourself at all times! Yaani niache wanangu na niwapendao wanaangamia hivihivi? Big NO!
Inaonekana haujui binadamu walivyo wewe haya endelea kukariri tuWa kusingizia atajulikana tu, njia ya mwongo ni fupi.