Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Hapo umesema kweli, wanawake wamegeuka mawakala wa shetani. Ndio wanaotumika kumjaribu mwanamume, wakitoswa wanaliiiia wakati walikuwa wanatumikia matakwa ya bwana wao.

Andiko? Hili hapa:

1 Timotheo 2
Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―Β―
⁹ Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
¹⁰ bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
 
Mwanamke mcha Mungu na asiye mcha Mungu wote wana bikira. Wakiteleza tu kwenye uzinzi wataingia kwenye daraja ya single mother, hawatafaa kwa ndoa
 
Thatdumbgirl,

Ndugu mimi sio wa mtazamo finyu hivyo. Kwanza fanya toba, Mariamu mama wa Yesu hakuwahi kuwa single mother kiasi cha kuhitaji rehema za Mungu. Ni neno baya kabisa kuwahi kulisikia.

Kukemea dhambi hakuhitaji kubembeleza, ni neno moja kwa moja. Sipo hapa kukufurahisha, nipo kuisema kweli na kama unadhani unazo hoja za msingi, jibu kwa hoja sio maneno ya ujumla tu. Na hapa tambua sijashawishi mtu, nimeeleza matokeo ya mahusiano hayo. Ukipenda chukua ukipenda acha. Ni vema binti zetu kuepuka zinaa na kujizuia kww ajili ya ndoa, hiyo injili jumuishi piga wewe, mimi nasema kweli ya Mungu tu.

Halafu unasema ninayemhukumu ni mtoto, mimi nahukumu? Nimesema madhara ya kuoa single mother kwa vijana, sijaongelea mtoto. Mungu ameagiza tujitunze mpaka ndoa, sasa binti akiruhusu kuzalishwa nje ya ndoa atalipa gharama kubwa, upende usipende. Ukweli utawaweka huru, na ndio njia pekee ya kukinusuru kizazi kinachopotea.
 
Nyenyere, Kama ulivyoniletea hili andiko niletee na andiko lililosema mwanamke ndiye anayetakiwa ajitunze ili kumuokoa mwanaume, nasubiri.
 
Huna ujualo, unabaki kulalama tu
Wewe ndiyo hauna ujualo kwa sababu wewe mwenyewe umesema unaongea kweli ya Mungu tu ila nikikuambia uniletee andiko linalothibitisha hayo yote unayoyasema hauleti sasa hauoni kama hayo yanabaki kuwa maneno yako ya kutunga tu?? Labda utuambie unaongea kweli ya mungu yupi maana miungu iko mingi!!
 
Na wakifanikiwa hao wanaume ndiyo wakwanza kupeleka videvu vyao kulia lia kwa watoto nakusema mama yake kamlisha sumu asinikumbuke Mimi Baba yake,huwa najiuliza hivi Baba anayejitambua anahitaji kujitambulisha kwa mtoto? Au mtoto anakuona Baba kwa matendo na kujua huyu ndiye Baba! Shida sana hii dunia
 
Wanaume huwa wanajiona wako innocent kwenye kila kitu yaani wao hawakosei kabisa na hiyo ndiyo shida yao kubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…