Kwanza Nakupongeza kwa kuwa hukutoa mimba..! Ubarikiwe sana.
Ila, usimlazimishe mwanamume kulea mtoto, kama hataki muache tu.
Lea mwanao atakuwa msaada mkubwa kwako baadae.
Usikubali awe kichwa cha habari cha media kuwa "MTOTO AMETELEKEZWA" wakati wewe Mama Uliembeba kwa Miezi 9 tumboni upo HAI na Una Nguvu na Akili,
Vaa ujasiri, muombe Mungu msamaha kwa lililotokea, Songambele.Usiuze Utu..
Uza mbogamboga,Uza Karanga fanya chochote kilicho halali ili mwanao akue...
Atakupenda na akikua atajua kabisa kuwa wewe ndiye uliyemlea bila baba.
Hapo ndipo baba atakapoanza kujipendekeza baada ya mtoto kufanikiwa na kuwa mtu mkubwa.
Nani ajuaye? Huenda Mungu kakuweka mbali na huyo baba ili akuokoe na kitu kibaya mbele,
Hivi mnajua kuna watu wanazaa na mtu ili atakayezaliwa aje kuwa mbuzi wa kafara?
Yes, anaona biashara zinayumba anaamua azae na wewe ili apate cha kutoa.
Tulia mama Lea mwanao, muombee kila siku, Mungu atanyoosha mkono wake.
#SikuNjema.
Sent using
Jamii Forums mobile app