Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Habari zenu.

Nasema hivi. Mwanaume yeyote rijali hawezi kuoa mwanamke single mother. Ninaposema single mother namaanisha wewe mwanamke uliyezaa kabla ya kuolewa.

Na ninaposema rijali namaanisha mwanaume mwenye akili sawa sawa au bara bara anayefikiri kwa usahihi asiyeendeshwa na mihemko bali hutumia akili yake kutafakari mambo. Hii ina maana mwanaume chizi au mwenye ugonjwa wa akili sio rijali. Ili uwe rijali ni lazima uwe na akili timilifu. Ushahidi ni kwamba mwanaume hanithi anapungukiwa pia akili. (Sitaki kulizungumzia hili) na ukishapungukiwa akili wewe sio rijali.


Ukweli ni kwamba mama zetu ( sisi wanaume) wanafurahi zaidi kama utampa taarifa kuwa unamuowa bint ambaye hajawahi kuzaa. Achilia mbali bikra ambayo hata hivyo wanatamani uwaambie unamuowa bikra. Ni heri uwaambie unamuowa bint uliyezaa naye wewe mwenyewe mtoto wake wa kwanza kuliko kuwaambia wamama eti....eti...unamuowa Lilian single mother!!! Nyoyo husononeka ingawa hawawezi kusema wazi wazi. Utasikia tu mama akisema "Kama umempenda na mnapendana sawa" Tafakari sana haya maneno kijana unayetaka kumuowa single mother.

Ni uzembe wa hali juu sana kuzaa kabla ya ndoa. Ni mwanamke ndiye unayeamua ushike mimba au usishike. Sisi wanaume huwa tunatandika tu.....sasa kama you don't take care about yourself....who else will? Halafu unamlaumu mwanaume kakutia mimba na hajakuowa.

Asikulaghai kwa maneno matamu yoyote yale eti beba mimba kabla hajakuowa. Usikubali. Na mwisho wa siku uamuzi unao wewe wa kubeba mimba au lah. Sasa mnakwama wapi?

"Asiponioa ntalea mwenyewe!" Huo ni uzembe.....tunajua mna vipato vyenu....mna pesa zenu, mnayamudu maisha....mnaweza kulea watoto wenu. Nikuulize, hivi kuna raha gani kulea mtoto peke yako? Mnapojitosheleza kiuchumi na kijamii (kutokuwa single mother), machaguo yanaongezeka. Hamuoni? Basi someni. Baadaye mnasema kuolewa bahati. Kuolewa sio bahati. Kuolewa mna haki wala msiite bahati....we unadhani wanangu mi ntalea na nani? R.I.P Ngwea

Jamaa akuzalishe huko halafu mi nije nikuoe? Acheni masihara nyie. Mi hakuna niliyemzalisha bila ndoa nikampiga chini sina sababu ya kuowa single mother.

Hakuna mwanaume RIJALI anayeweza kuowa single mother. Period.


Meraki
Umri wako tafadhari,,msichana wako kapewa mimba nini?
 
Sijazungumzia issue ya kuchepuka hapa. Kuchepuka hata bint aliyeolewa bikra anachepuka.
Ndo hivyo sasa, swala ni kupata mke mtakayependana na kuendana kuoa mwali si kigezo kwamba ndoa yako itakuwa sustainable. Kuna complications nyingi kwenye hizi mambo, punguza kukurupuka na kuanza kutoa kufuru
 
Unawasema single mother si kazi umelelewa Na baba Wa kambo au umezaliwa nje ya ndoa,pole Sanaa..

Kuna jamaa alikuwa anakazia kama wewe ingalia Kalelewa na baba Wa kambo hadi anajitambua.
Kwa hiyo kama amezaliwa nje ya ndoa na yeye ndo azae nje ya ndoa? Kama alilelewa na single mother na yeye ndo aoe single mother?
 
Well said
Hata kama mleta mada atapigwa mawe lakini kaeleza ukweli mtupu. Hasa aliposema wazazi wa mtoto wa kiume huwa wanasononeka, hili ni kweli maana hata Mimi liliwahi kunikuta. Nilimpata single mother mmoja mkali kwa sura, nikachukua picha yake kwa mbembwe hadi kwa mama. Lahaulah!!
MAMA: Mbona kama alishazaa na MTU
Mwingine?
MIMI: Ah! Mama? Kwani hilo ni tatizo?
Kikubwa upendo tu.
MAMA: Umechunguza kwa nini aliyezaa
naye hakumuoa?
MIMI: Nadhani ni tabia za vijana wa siku hizi kutopenda kuoa, lakini mbona ana tabia nzuri sana?
MAMA: Hayo unajaribu kupamba, lakini
Mbele ya safari utakutana na
hali halisi ndo utajua kwa nini
Aliyemzalisha hakumuoa.
MIMI: Kimyaaaaaa!
 
Back
Top Bottom