Wako wapi waliodai Tume ya Katiba haina weledi na wala si huru!??

Wako wapi waliodai Tume ya Katiba haina weledi na wala si huru!??

Nape Nnauye

Professor Baregu amewavua nguo CHADEMA na katibu wako mkuu......


Professor Baregu once said

“If I told to choose between my country and my party (CHADEMA), I will choose my country,” akiwa na maana kwamba kama angetakiwa kuchagua kimoja kati ya nchi yake na chama chake cha CHADEMA, angechagua nchi yake kwanza.
Sasa amewavua nguo vipi? hebu acheni mambo yenu ya vyama hapa!,wengine hatuna vyama, tumekaa miaka 50 wachache tu wanafaidi keki ya taifa, wakiulizwa wanasema haya ni vyeti hayazungumziki, wimbo ukawa ujamaa huku wao wakifanya uporaji na ujimbilikizaji mali uliokithiri, watu wakadai mgombea binafsi, kikatiba ilikuwapo lkn ilizimwa kwa sababu wakamata minofu wachache walikua na hofu ya kupunguza nguvu zao chamani, huyu Nape tu alikua ni victim wa mchezo ule mchafu bila kuwasahau ekina Malecela, Mpendazoe na Shibuda, Kipi, vigezo gani vilitumika kuwaengua kama haukua UBABE? , eti utaratibu tuliojiwekea, utaratibu upi unakinzana na katiba? kama si haikua kulinda waporaji wachache ilikua ni nn?, Kwa kiasi kikubwa itaondoa UMANGIMEZA wa CCM, jana ni kama muongozo wa Tanzania huru umetoka, watu wa nchi hii wametabika vya kutosha.
 
Stop being the captive of your own ignorance
 
Hakuna mjumbe wa baraza la katiba atakaye pinga serikali tatu, huo ni ushindi mkubwa, kufanikiwa kwa hilo kunamaana ya muungano kufa kwa sababu serikali ya shirikisho itakuwa haina nguvu yoyote , kwa maana hiyo hakuna haja ya kuwako serikali ya shirikisho kwa sababu kila Nchi soon tutaingia katika serikali moja ya shirikisho la Africa mashariki ambayo, mambo ya ulinzi na usalama yatakuwa ndani ya shirikisho hali kadharika ulaia na uchumi, sioni haja ya Zanziber kuingia kwenyeshirikisho ikiwa ndani ya shirikisho jnine iingie moja kwa moja kama Nchi ya 6. Katika hili niwapongeze G55 walioyaona haya zaidi ya miaka 25 iliyopita wakaitwa wasaliti wa muungano. wale mliofariki Mungu awazawadie stahili zenu wale mlio hai tutawapa nishani za kutukuka na mtaandika katika kitabu cha kumbukumbu ya histolia ya Taifa kama watu mliopuuzwa kwa kutetea angenda ya uponyaji wa Taifa. Pole Nyerere Muungano wako umekufa.
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

ha ha wale waliomtaka mzee Baregu ajitoe wako wapi leo ha ha ha kumbe wao kazi yao kubwa ni kuongoza fujo na sio mageuzi ya kifkra na muelekeo wa Taifa kama ambavyo Rais Kikwete na CCM ambavyo inafanya sasa tusubiri tusikie singo gani wanaitafuta kutoka nayo
 
Akili za kibavicha hizi, mwenzako kakujibu kistaarabu wewe una mtusi, nyie ndio munao chafua hadhi ya jukwaa. Waombe Mods wafungue jukwaa lamatusi uweze kujimwaga vizuri nasisi wastaarabu tusipate kuuona huo Ubavicha wako.

Huyo sio "mwenzangu" siwezi kuwa na affiliation na mtu ambaye anauza utu wake kwa 7,000 ili maisha yaende.

Narudi kwako. Hakuna sehemu niliyojitambulisha kuwa mimi ni BAVICHA, mimi niko NCCR, naona unarukia wanaume kama Juliana alivyojipeleka kwa Mwigulu.... Je, wew ni S/HE???? Kama SHE you are welcome, kwa kuanzia nitakupeleka Zenji....
 
Watu wengine ni wa ajabu sn sasa nape unapoishangilia hii rasimu na we ni kiongoz wa chama unataka si tukueleweje? Kwamba mmeipiga bao cdm ama? I.D.I.O.T
 
tatizo baadhi ya wanachama wa chama flani cha siasa walidhani katiba ni yao na inakuja ili kuwaondoa chama fulani ndio maana walikua wanapiga kelele lakini mimi naona rasimu iko very fair
 
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!

Nape Nnauye; acha kudanganya watu kuwa Rasimu imekuwa nzuri na imetengenezwa na watu wenye weledi. nakutaka ufuatilie kwa makini na utagundua madudu mengi kwa leo nakuashauri fuatilia sura ya sita na utagundua kuna bomu mnalotaka kuwaandalia waTANGANYIKA. Fuata link hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-ya-sura-ya-sita-katika-rasimu-ya-katiba.html
 
Ningetoa matusi ila jana leticia nyerere katuasa tusitukane, kwa kuwa nawaheshimu kina mama basi nakusitahi ila nape una akili za kitoto, hayo waachie kina shonza
 
Sikutegemea kusikia kauli hiyo kutoka kwako, nilitegemea ungepongeza tume na kidogo kujaribu kufanya analysis yako kujua wapi wameweza na wapi wameshindwa. Nilitegemea pia ungeomba waendelee kuwasimamia wananchi na kuhimili pressure kutoka kwa wasioitakia mema nchi yetu. Pia nilitegemea ungetoa rai kwa watanzania kuungana katika kuhakikisha yaliyomo yanasimamiwa na kushirikiana ili kuifanya iwe bora zaidi. Kauli za majungu na kujenga mazingira ya mgawanyiko nisingetegemea zitoke kwa kiongozi mkubwa kama wewe ndani ya chama chako. Umekua mtu mzima siku hizi, jaribu kufanya au kuongea mambo yanayoendana na hadhi yako na umri wako.

Well done mkuu, hyo ndo stahili yake anatakiwa kujadili issues na cyo watu, he should grow up, siyo kila kitu ni propaganda
 
Dah ! Kama Nape ameweza kuwa Katibu Mwenezi wa CCM , basi bila shaka Mimi kwa uwezo nilionao nadhani ninastahili hata kuwa Kiongozi wa UN aisee ! Uongozi siyo Mgumu bhana !

kweli JF tamu sn yaan umenichekesha mpaka basi. Real you have made ma day na umenifanya nisaau kidogo machungu ya kupigwa chin na demu wangu
 
Mkuu Nape Nnauye,
Unajua Hata Shetani Pia ameumbiwa Haya, Mkuu Kwanini hujifunzi kutoka kwa Wenzako akina John Mnyika.
Asilimia zaid ya 99 ya waliochangia wote wanaonesha ni Jinsi gani ambavyo Bado Hujakomaa.
Wenzako wakiamua ku post kitu JF basi hiyo Topic huwa Very Hot na Kuvutia Wachangiaji Mbali Mbali.
Ona Sasa ulichopost, Hata Vijana wako wa Lumumba wanaona Haya kuja Kuku Support Hapa.

Mkuu ifikie Kipindi uwe unaona Haya na wewe basi
 
Last edited by a moderator:
Dah ! Kama Nape ameweza kuwa Katibu Mwenezi wa CCM , basi bila shaka Mimi kwa uwezo nilionao nadhani ninastahili hata kuwa Kiongozi wa UN aisee ! Uongozi siyo Mgumu bhana !

Mkuu, yaani ni Full Vituko, yaani kama Watu dizain ya Nape na Mwigulu wameweza kupewa wadhifa Mkubwa hivyo Ndani ya Chama, Aisee mie kwa Uwezo wangu Nastahili kuwa Rais wa Dunia
 
hizi tambo za chadema zinamwisho na mwisho wake upo karibu sana.
 
ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa tume ya mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!
ndugu nape kama hiyo rasimu itapita ivyo kama ilivyo ama mabadiliko yakawa madogo ndipo nitawa prove wrong waliosema hivyo mana waswas mkubwa upo kwenye mabalaza ndipo wanapolalamikia kuwa mmeodhi.
 
Sikutegemea kusikia kauli hiyo kutoka kwako, nilitegemea ungepongeza tume na kidogo kujaribu kufanya analysis yako kujua wapi wameweza na wapi wameshindwa. Nilitegemea pia ungeomba waendelee kuwasimamia wananchi na kuhimili pressure kutoka kwa wasioitakia mema nchi yetu. Pia nilitegemea ungetoa rai kwa watanzania kuungana katika kuhakikisha yaliyomo yanasimamiwa na kushirikiana ili kuifanya iwe bora zaidi. Kauli za majungu na kujenga mazingira ya mgawanyiko nisingetegemea zitokaka hii nmeipenda sana.good answer at a right time
 
Nape Nnauye , Habari za siku mkubwa.

Kwanza hakuna aliyesema unnayoyasema hapa, ila malalamiko ni mabaraza ya katiba yaliingiliwa na makada wa CCM mmoja wapo ni mama yangu, dada yangu Asha rose Migiro na wewe. Mliwatengeneza watu wa kuingia kuyapigia kura haya maoni. Naomba utafute matamko ya wote waliopinga utajua wapi walipinga. Mpaka sasa tunapinga upatikanaji wa watu watakao jadili na kuyapitisha haya maoni. Je kweli watayakubali wakati wengi ni makada wa kuingizwa wa CCM?

Tutafurahi wengi kama mtawaelekeza makada wengi kuzingatia maoni ya watanzania.

Maoni yangu binafsi sikubaliani na uwakilishi wa wanaume na wanawake kwenye majimbo utaongeza gharama kubwa sana za kuendesha bunge. Kama nimeelewa vyema yaani kuwe na wawakilishi wa kike na kiume kwenye jimbo moja. No huu utakuwa ni mzigo kwa walipa kodi. yaani majimbo 239 yatoe wabunge 478??? come on haiwezekanai. ni wengi mno ukilingisha na uwezo wa nchi. Nilitegemea tume ingepunguza majimbo ya uchaguzi na kufikia walau 70 au 100. ya kudumu.

Nape tujadili hizi rasimu Tanzania ni yetu wote, wewe utapita, Jk atapita, Lowasaa atapita , Membe Atapita ila Tanzania bado tunayo sana, msifikiri ninyi viongozi wa sisasa mna maana sana zaidi ya maisha yetu la hasha ninyi mnatetea ajira tu hamna la maana mnalilifanya, hamtetei taifa, wananchi wala ustawi wa tanzania. hamna uchungu na uhalisia wa maisha magumu ya Mtanzania.

ndio maana hamjali kushuku kiwango cha elimu manapendekeza utumbo wa kuwaongezea wanafunzi alama. Tukishindwa kuwaandaa vijana wetu leo kwanini kesho tulalamike kuhusu huduma za afya, barabra, mahakama , waalimu wabovu?? Kama leo tunashindwa kuandaa wataalamu kwanini kesho tushangae ghorafa zikituangukia ?? Nape serikali yenu imeshindwa vibaya sana. Na ninaomba miradi yote ya viongozi walioshiriki kuuwa elimu ya nchi ife kwa ukosefu wa utaalamu labda mtajifunza. Nape leo mnafurahia kutibiwa nje na kuiuwa Muhimbili na hospitali zote za ndani, ila ukumbuke kesho mnastaafu uwezo wa kwenda nje kwa fedha za walipa kodi masikini mtakuwa hamna. Najua wote mnapigana vikumbo kutuibia ili kujaza mafedha ya kesho mkiwa nje ya siasa za kibazazi.

Ila Iko siku watanzania watadai fedha zao kwa nguvu.

Well said
 
Ungekuwa timamu "upstairs" ungekuja na uchambuzi yakinifu wa rasimu ya katiba kwa mustakabali wa taifa letu. Lakini kutokana na hitilafu "upstairs" umekuja na maneno ya kwenye kanga. Think wider we kijana
Ninasubiri kwa hamu kubwa kuwasikia waliosema kwa sauti kubwa nahadharani kabisa kuwa Tume ya Mabadiliko ya katiba nchini haina watu wenye weledi kwa kazi hiyo tena wakaenda mbali kuwa haiko huru tume hiyo kufanya kazi wanayotakiwa kufanya. Sasa baada ya rasimu hii natamani kuwasikia tena wakisema nakurudia maneno yale na pengine kwa kuyapigia mstari mkubwa!!
 
Una tatizo moja tu
Nalo ni kushindwa kufunga mdomo wako

Hii taarabu ilikuwa na umuhimu wowote kipindi hiki??
 
Back
Top Bottom